The Chant of Savant

Wednesday 13 July 2016

Kijiwe: Makufuli tukumbuke kwa maburungutu


            Baada ya kijiwe kushuhudia ukarimu wa rahis Joni Kanywaji Makufuli, kimeamua kumbipa mzinga lau nacho kifaidi utukufu wake.
Mgosi Machungi analianzisha, “Jamani mmeona jinsi rahis Makufui aivyomwaga njuuku kwa Bakuata? Kwanini nasi tusimtwishe mzinga hata kama hatiendi hijai? Maana, jamaa anaonekana anazo; hacheei kukata mshiko.”
“Kweri tunahitaji njuruku kujikimu hasa ikizingatiwa hatuna miladi wala kuripwa mishahala kama hao, ira napinga hii tabia ya munene kumwanga mabulungutu badara ya kuandika cheki,” anachomekea Mbwamwitu huku akimuigiza munene Kanywaji kwa lafudhi yake ya Kizinza.
Kapende anamchomekea, “Hivi kama rahis–anayepaswa kuwa mfano anafanya hivi–sisi akina yakhe tutafanyaje? Hii maana yake ni kwamba jamaa haweki njuluku benki jambo ambalo ni mfano mbaya kiuchumi. Nadhani hata yeye analijua–na kama halimanyi–washauri wake wanapaswa kulijua na kumuonya mfano anaoonyesha. Kumbuka; jogoo aliwafundisha vifaranga kunonihiii ndani.”
“Unashangaa hilo siyo! Mbona jamaa amekuwa akifanya mambo kama vile yeye muungu pamoja na kuwa na shahada ya uzamizi? Rejea anavyosema ‘silikali yangu na si ya wabongo’; au anavyosema ‘nataka si wanakaya wanataka vile na hivi.’ Hapa maana yake ni kwamba jamaa yuko juu ya kila kitu na kila kitu ni mali yake binafsi. Hukuona alivyowakingia fua wanene wa zamani kana kwamba kaya ni mali yake binafsi?” anazoza Mipawa huku akibusu kombe lake la kawaha.
Mpemba anakatua mic, “Yakhe hata mie nshangaa sana. Jamaa yu afanya mambo kama vile tuko kwenye ile miaka ya utwahuti ya 60 ambapo kila mnene alijiendeshea kaya alivotaka. Wallahi huyu jamaa ankumbusha Karumekenge wa kwanza alivogeuza Zenj mali binafsi.”
“Jamani nyinyi taka yeye fanya nini nyinyi. Veve naweza kata shiko kuba kama ile nakata Kufuli? Kwanini hapana kubali juluku nakosekana sipokuwa kwa ile mizi naiba milioni saba kwa dakika,” analalamika Kanji.
Mheshimiwa Bwege hamkawizi; anaramba mic, “Kanji najua nyinyi huabidia ng’ombe na njuluku bila kujali kama zinatolewa kwa utaratibu au la. Tuwe wakweli. Kama rahis haweki njuluku benki, hao wauza bwimbwi si wataijaza kwenye mashimo kiasi cha kuathiri uchumi? Tusiongee kama hatujui uchumi tena wa karne ya 21.”
Mzee Maneno anakula mic, “Mie simlaumu mtani wangu. Hamjui kuwa jasiri haachi asili? Sitegemei Msukusi aweke njuluku benki,” anamalizie akiwaangalia Mijjinga na Mipawa wanaotabasamu; kwa vile ni mtani wao Mzaramizi.
Msomi anapoka mic, “Mimi sikushangaa hasa ikizingatiwa kuwa huku uswekeni viongozi hufanya kama jamaa yule wa kwenye Biblia aitwaye Paul aliyesema, ‘fuateni niwaambiayo lakini siyo nifanyayo.’ Kwani hamuoni anavyotumbua awatakao na kuwasaza awatakao? Hapa hujagusia kutoa maagizo yanayokinzana na sheria kama kuwaagiza wakubwa wa wilaya watumie ulaji wao watakavyo kuwakomesha wabaya wao. Hujagusia namna alivyowahimizi wazee wa mabao kuiba vipuri vya mikangafu watakayokamata na kuamuru ipelekwe kituoni ikakongorolewe. Ama kweli ukishangaa ya Njaa Kaya utaona ya Kanywaji! Hatuwezi kuendesha kaya kama mali ya mja binafsi. Lazima tufuate sheria tulizojiwekea kwa hiari yetu tena kwa usawa bila huba, ubaguzi wala upendeleo au vipi?”
Anabwia gahawa yake na kuendelea, “Kama jamaa hatabadilika, nadhani huu ni mwanzo tu; mtaona mengi. Maana, kwa hali ilivyo, waliomzunguka jamaa wanamgwaya ili wasipoteze kitumbua chao usawa huu wa kuburuzana.”
Da Sofia Lion aka Kaunungaembe anakula mic, “Kaka Msomi usemayo kweli tupu. Kama watani zake walivosema, jasiri haachi asili. Kwani, kabla ya hili la kumwaga miburungutu, tulishuhudia bi mkubwa wake akimwaga misaada kwa wazee ambayo alivyoipata ajua yeye na Mungu wake. Wengi tulimsifu tukidhani asingeanzisha NGO kama dada zangu kina Ana Tamaa na Si Salama. Kumbe tuliingizwa mkenge. Anayo NGO japo hajaitangaza rasmi. Matendo yake yamekaa Ki-NGO, NGO.”
Mchunguliaji anakula mic, “Naungana na brother Kanji kumuunga mkono Dk Kanywaji japo si katika kila jambo. Ni nani–kati ya watangulizi wake–aliyewahi kufanya hivi pamoja na wengine kuiba sana? Usawa huu ukiona mtu anakupa neema kama alivyowafanyia jamaa wa Bakuata, lazima ushuru; tena bila kuuliza amepataje au ametumia utaratibu gani. Hili la bi nkubwa wake kusaka misaada hata kwa wanigeria halinipi taabu kama hatachukua kikubwa na kutoa kidogo kama walivyofanya akina Ana Tamaa na Si Salama.”
Mheshimiwa Bwege anarejea kwa hasira kidogo, “Ama kweli mkiambiwa mwaliwa msitunishe misuli. Hatuwezi kujigeuza mashimo kumeza kila kiingiacho bila kuhoji hata kugoma japo kidogo. Lazima sheria zifuatwe; vinginevyo tutaendelea kutumiwa na kuliwa tena kwa hiari yetu. Angalia jamaa alivyowaziba midomo wapingaji ili wasimghasi atembeze undavandava kama rafiki yake Ka-Game ambaye anaonekana kumhusudu bila kujua kilichoko nyuma ya pazia. Siku atakapogeukwa kama alivyofanyiwa M7 atakumbuka maneno yangu ya busara ambao–bila shaka–mzee Mpayukaji utayaanidika ili wote wasome na kuwa mashahidi wa unabii huu.”
Mbwamwitu anarejea, “Jamani acheni rongo rongo zenu. Kwanini–kama kijiwe–tusitume ujumbe kwa munene atukatie iwe kwa maburungutu au macheki. Sisi tumepigika; tunahitaji njuluku kwanza. Mengine yatafuata baadaye baada ya kuhomola. Kwanini tusijifunze toka kwa Bakuata ambao sasa wamemmezea ili baadaye wamuwashe akiwachemshia kwenye ajenda zao za siri?
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita manzi aliyejazia kiasi cha kutufanya tuache kila kitu na kumukodolea huku tukila kwa macho!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

No comments: