The Chant of Savant

Saturday 13 February 2016

Mlevi kupambana na wabaguzi wa kigabacholi


            Baada ya kuzinyaka kuwa binti wa kilevi amefanyiwa kitu mbaya kule ugabacholini, Mlevi anatishia kuingia kwa fosi Bangalole ili awasake wabaguzi waliomfanyia kitu hii na kuwatia aibu.  Nilipopokea habari hii chafu na mbaya, kwanza nilipiga misokoto kama mitatu bila kupumzika halafu nikaanza kupiga mahesabu ya kutafuta pa kulipizia kisasi. Nikiwa napanga kurudufu lile zoezi uswazi ilibidi kwanza nipate kanywaji. Nilipokwenda Uwanja wa Hyena kupata tugongo kidogo si ndiyo nikabadili mawazo kuwa lazima niende kule kule nikafanye kweli kule kule ili kila ngurumbili aone mwenyewe na kuamua mwenywe kama ubaguzi wa rangi unalipa. Hakuna kitu kimemuudhi kama migaendaeka tunayofuga kutubagua na kututenza kama si wana wa Adamu. Inadhani tumesahau kuwa ilikuwa imported na wakoloni wa kiingilish walioileta hapa kuja kutunyonya kwa kununua mazao yetu kwa bei ya kutupwa na kumuuzia bwana wao? Hata hivyo ina hasara gani kama iliweza kuwageuza ndugu zetu Wajarawa manyani inayotumia kufanyia utalii kwenye visiwa vya Andaman huko ugabacholini na viongozi wa kimakonde kwenye AU bado hawaulizi ni kwanini nasi tusiwafungashie vilevi kunguru wao?
            Kwa vile ubaguzi wa rangi ni kosa la jinai lazima tulaani kitendo hiki tena kwa herufi kubwa.  Jamaa mmoja ambaye kitegemezi chake kinasoma huko ugabacholini alinitonya kuwa binti wa Kibongo alifanyiwa kila dhihaka, kuvuliwa nguo, kupigwa na kuchomewa mchuma wake simply because Mswahili wa Kisudan ambao wengi wao hupenda kujiita wamanga wakati ni wamakonde alimgonga mama wa kigabacholi.
            Baada ya kuzinyaka, haraka haraka nilimkumbuka marehemu Kris Mtikisa. Nilichukua hadi nikaanza kumpenda Idi Amini kama alivyofanya askofu Festo Kivengele aliyeandika kitabuc ha I love Idi Amin.  Kama brother Mtikisa angekuwa hai bila shaka tungeingia mitaani kuonyesha hasira zetu na pia kunyesha hata mmakonde ana thamani. Mipuuzi mingine bwana, mbona kuna magabacholi weusi kama wasomali lakini nao bado eti wanatubagua? Kama mnaona hatufai si mtwambie tusije kwenu ili nasi tuwambie wa kwenu watoke kwetu warejee kwao hasa ikizingatiwa kuwa waliletwa kinyume cha sharia?
            Hata hivyo,mijamaa hii ni mibaguzi ya kutupa. Hebu nionyesha mlevi yoyote aliyeoa au kuolewa na mgabacholi basi nitakupa ubavu wangu wa mbwa nilioridhi kwa wazazi wangu. Mingine tunajua jinsi inavyowatesa wafanyakazi wao wa majumbani kwa kuwabagua na kuwafanyia kila ushenzi huku lijiserikali likiangalia tu.
            Kwa vile walevi ni watu, tunapaswa kujitetea kwa jino kwa jino na jicho kwa jicho vinginevyo hawa gendaeka wataendelea kutudhalilisha na kutubagua wakati sisi hatuwabagui pamoja na kuletwa na mkoloni kufanya kitu mbaya kwetu.
            Pia lazima tumwambia rahis Kanywaji abadili hii hali ya kaya kutegemea ugabacholini. Pamoja na kutuma wachovu kwenda kule kutibiwa baada ya kuinyonga Muhimbili, bado hii mijitu haioni tunavyochangia uchumi wao! Pamoja na kupeleka vitegemezi vyetu vikapate elimu feki kule bado hawaridhiki? Kama haitoshi, pamoja na kuendelea kutorosha wanyama wetu bila kusahau tanzanite bado hawaridhiki na kutuheshimu! Pamoja na kuruhusu wakimbizi wao wa kiuchumi bado ugabacholini hawatuheshimu na kututhamini! Pamoja na kuingiza bidhaa zao feki kwenye kaya yetu iliyogeuzwa shamba la bibi bado hawatuthamini! Pamoja na kuwatajirisha ndugu zao bado hawatuthamini! Je ni mabilioni mangapi ya njuluku ndugu zao wameishatoroshea ugabacholini tangu kuja kwa mkoloni muingilish? Pamoja na kuwaachia houses za Asajile Mwaijumba bado hawajatutambua tunavyowasaidia? Sijui kuna walevi wangapi ugabacholini waliokwenda kule kubangaiza zaidi ya kwenda Apollo na kwenye mavyuo huku wakiwajaza mafweza kama yule jamaa yangu wa zamani aliyewatapeli walevi kuwa angewajaza mafweza kumbe alikuwa kopa kopa asiyelipia hata hekalu lake. Sijui naye kaishia wapi?
            Hata hivyo, wakati mwingine walevi wanapaswa kujilaumu kwa ujuha wao. Leo wao wanazuiana kuwa na uraia wa kaya mbili lakini magabacholini wanakuwa nao wa kaya moja wala mbili. Kwanini wasitudharau? Kama tunawashobokea hata kuwaruhusu waendesha uchumi wa kaya unategemea watashindwa nini kutuona kama kuku ambaye pamoja na mwanadamu kula mayai na watoto wake hata yeye mwenyewe bado huogopa kukitoa na kwenda kuishi kwa uhuru mwituni kama kanga.
            Hata hivyo, nani atawashughulikia gendaeka na wajalaana hawa wakati wakubwa wetu wengi wanakula nao? Mara hii tumesahau majambazi kama Singasinga wa Esrew, Chavda wa mashamba ya mkonge bila kusahau Visirani wa rada na ndege mkweche ya rahis. Kwanini wasitudharau na kutubagua pamoja na kwamba ukienda majuu watasha huwaita waswahili jamaa hawa wabaguzi. Hapa lazima rahis Kanywaji atumbue hili jipu la hawa jamaa ambao wametokea kuwa na ukwasi wakati walevi wakiendekea kupigika. Lazima kutakuwa na kitu wanafanya ambacho kinawazalishia kuliko hata jamaa zangu akina mbee na arawa.
            Pia tunamshauri rahis Kanywaji afufue mahospitali yetu na vyuo vyetu ili kuepuka walevi kwenda kubaguliwa na viumbe maskini wa kila kitu kuliko yoyote duniani.
Namalizia kwa kutoa onyo kuwa naweza kufanya kitu mbaya kwa gabacholi anywhere anytime in any manner.
Chanzo: Nipashe Feb., 13, 2016.

No comments: