The Chant of Savant

Thursday 29 October 2015

UKAWA walaumu pupa, upogo, ubinafsi kushindwa vibaya

  • Tunapompmgeza Dk John Magufuli... wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Joseph Magufuli
Kushindwa vibaya kwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kunaweza kufupishwa kirahisi kwa kuangalia yafuatayo:
Realpolitik za Tanzania na historia ya UKAWA
Wananachi kuichoka CCM lakini wakanyimwa chaguo na UKAWA
Kumleta Edward Lowassa na kumpitisha kuwa mgombea wa UKAWA
Kutokuwa na hoja kwa UKAWA
Kujipiga mtama na kuondoka kwenye misingi iliyosimamia UKAWA
Lowassa kuwa bubu na kushindwa kuinadi na kuitetea UKAWA
Uchapakazi wa Magufuli nao ulikuwa kikwazo kwa UKAWA

Nguvu ya CCM kifedha na kimkakati ikililinganishwa na UKAWA
Hivi UKAWA wangemsimamisha Dk Slaa tungekuwa tunaongeaje sasa?
Kinachoshangaza ni ile hali ya wakuu wa UKAWA kushindwa mambo rahisi kama haya. Wengine tena ni maprofesa. Ni bahati mbaya kuwa wote walikuwa kama vipofu walioamua kumchagua kipofu mwenzao awaongoze.
Sina shaka kama UKAWA ingemsimamisha Dr Slaa kazi ingekuwa kubwa kutokana na sifa walizokuwa wameishajizolea. Ni wakati muafaka kwa CCM kujipima na kujirekebisha. Maana inavyoonekana imepigiwa siyo kubeepiwa. Kwa mchapakazi kama huyu na asilimia walizopata, hivi kama Magufuli angegombea na mtu mwenye udhu na uwezo hali ingekuwaje? Je CCM miaka kumi ijayo itakuwa na Magufuli mwingine kweli?
Hongera Magufuli. Sasa kazi kwako kutimiza ahadi zako na kukidhi matumaini makubwa ya watanzania kwako.

No comments: