The Chant of Savant

Monday 31 August 2015

Kwanini Mkapa anakataa kukua?

Image result for photos of benjamin mkapa 

          Matusi yaliyoporomoshwa na rais mstaafu mwenye kashfa ya kujitwalia Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira Benjamin Mkapa hivi karibuni kwenye kufungua kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) yameacha wengi vinywa wazi.  Mkapa alikaririwa akiwaita wapinzana malofa na wapumbavu asijue alikuwa akijichamba asijue? Hatutachambua maneno malofa na wapumbavu kutokana na urahisi wake kueleweka. Je tukiangalia hawa wapinzani na Mkapa aliyekwisha achia dola tena kwa aibu ya wizi wa kijinga nani lofa na mpumbavu? Ngoja tuache wasomaji waamue wenyewe. Kwani hatutaki kumlaumu Mkapa kwa kurudia alichofanya.

          Pili, kwa rekodi ya Mkapa kisiasa, wengi hawakutarajia kama angepata mshipa achia mbali jeuri ya kutukana wenzake hadharani tena bila sababu. Wapo wanaoona kama Mkapa alipaswa abwate ili kuwaridhisha watakaoingia madarakani wamkingie kifua kama alivyofanya rais anayeondoka Jakaya Kikwete baada ya kubainika yeye marafiki na familia yake walivyotumia uwekezaji kulihujumu taifa. Ni aibu kiasi gani kwa mtu anayetegemewa awe mfano wa kuiga anaongea kama wahuni na wapiga debe wa vijiweni.

          Tatu, kwa hadhi ya Mkapa kama rais wa zamani–hata kama ana madudu na mazabe yake aliyotenda kutokana na upogo na tamaa–hakupaswa kuwa bingwa wa matusi na mipasho jambo ambalo linaweza kufanya wenzake wamuite mtu mzima hovyo.

          Nne, kwa umri wake alipaswa awe ameishajua jinsi ya kuchagua maneno ya kuongea na ya kutoongea. Si jambo la maana kwa mzee tena wa hadhi ya Mkapa kuongea kama watoto wa vijiweni au wale wazee waliokataa kukua. Sijui kwa matusi ya Mkapa ametufundisha nini kama jamii aliyowahi kuitawala baada ya kushindwa kuiongoza?

          Tano, Mkapa alipaswa kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kutenda makosa ya jinai mojawapo likiwa ni matusi na kutumia lugha za shari. Sijui Mkapa amekumbwa na nini? Maana huko nyuma hakuwa hivi! Hata mwl Julius Nyerere aliyempigia kampeni baada ya kugundua kuwa alikuwa hauziki bila kubebwa, hakutumia lugha za hovyo na aibu kama hizi anazotumia Mkapa.

          Sita, Mkapa anapaswa aambiwe kuwa lugha aliyotumiwa licha ya kutokuwa saizi yake si ya kistaarabu wala haina cha maana cha kulifundisha taifa zaidi ya kumvua nguo na kumuonyesha kama mtu muhuni na mpayukaji asiyejua jinsi ya kuzuia ulimi wake. Kama hakuwa na la kusema si angejinyamazia kuliko kumwaga upupu.

          Saba, kama Mkapa atataka asiendelee kueleweka vibaya, basi awaombe msamaha wapinzani aliowatukana na watanzania aliowanyosha utovu wa nidhamu tena hadharani. Hivi kama ni ulofa na upumbavu, kuna ulofa na upumbavu kama kuingia kwenye mikataba ya kijambazi ya uwekezaji ambayo haina maslahi kwa taifa? Je kuna ulofa wa kisiasa kama kutumia matusi na maguvu kama ambavyo inaanza kubainika bila sababu ambapo wahusika wameishaanza hata kutumia polisi kuwahujumu wapinzani? Ama kweli mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi. Sijui kama wapinzani ni malofa na wapumbavu kama anavyowaelezea Mkapa wakati wameizidi CCM yake kete wakawasomba mawaziri wao wakuu wawili kwa mpigo akiwamo mshirika , rafiki na waziri mkuu wa pekee wa Mkapa Fredrick Sumaye ambaye ameamua kujitenga na dhuluma na kushindwa kusoma alama za nyakati.  Hivi ikitokea wapinzani wakashinda Mkapa ataweka wapi sura yake? Tulitegemea wazee aina ya Mkapa wahubiri haki ,upendo, amani, heshima, maadili, haki, kumbe wapi. Badala yake wanahubiri maangamizi, matusi, uchokozi na vurugu. Tunamshauri Dk John Pombe Magufuli ajitenge na watu wa namna hii asionekane yu sawa na wao au ni kikaragosi chao. Hatudhani kama Magufuli ni mchovu hivi kiasi cha kuhitaji kubebwa na wale waliobebwa.

          Namheshimu sana mzee Mkapa ila kwa hili alilofanya, kwa mapenzi yangu makubwa kwake, sitamuogopa wala kumdanganya, amechemsha tena vibaya sana. Hata huyu aliyempigia kampeni kwa lugha za mipasho, kashfa, matusi na ukosefu wa busara hamsaidii zaidi ya kumuumiza. Badala ya kujifunza kwa Nyerere aliyewahi hata kuambiwa amebeba kinyago cha mpapure bila kurusha ngumi wala matusi, Mkapa anazidi kujivua nguo tena hadharani. Hakika hii siyo saizi yake.  Hata mzee Jangala kwenye maigizo yake hawezi kufikia uhovyo kama alioonyesha Mkapa.

          Tuamalize kwa kumtaka Mkapa aombe msamaha yaishe. Maana waingereza wana msemo kuwa ukiishi kwenye nyumba ya vioo usiwachokoze vichaa. Bado watu wanajua madudu yake ya NBC, Kiwila, EOTL na mengine mengi. Ashukuru Mungu tuna siasa za kulindana tokana na wote kuwa waovu. Vinginevyo angepata wapi hiyo jeuri mtu kama yeye.  Wapinzani wanaweza kuamua kama mbaya mbaya wakamjibu kizembe kama alivyofanya akaumbuka zaidi. Tunawashauri wasimjibu Mkapa kwa vile lugha aliyotumia siyo saizi yao. Sana sana walipaswa kwenda mahakamani kuweka katazo Mkapa asishiriki kampeni kwa vile hana udhu wala uwezo wa kufanya hivyo bila kuvunja sheria.
Chanzo: Dira Agosti 31, 2015.

Sunday 30 August 2015

Is it the beginning of the end of CCM?


          It is official now that former Big Minister Freddie Sumaye has taken hard decision. Sumaye is now out of the fold and Chama Cha Maulaji (CCM) once again is caught off guard.  Will Sumaye’s cross over shake and injury CCM? Anything is possible in this game of deceit known as politics. Given that boozers have no stake in this game of deceit, theirs is to drink heavily and smoke joint to see what will transpire after odd bedfellows abandon each other at the eleventh hour.
           I feel bad for my friend Joni Kanywaji Makomeo. I thought it would have been easier for him to claim residence in Magogoni posh mansion. What a goof!  Does it mean that those who said that CCM will die in the hands of Jake Kiquette saw the future? Who knows? Again, do you know who made such a prediction? You’ve the answer. It is me not anybody else. I saw this because I knew it and I’d see it coming. However, CCM didn’t get it. Now they are caught off guard. What’ll they do to alleviate or mitigate the looming danger? I see red. Wait a second. Let me make another prediction. Tomorrow or soon after, mzee Kimdunge Ngumbalu Mwehu will follow suit and many others I am telling you.
          What a calculated move however latent it has come! Again, does Sumaye have what it takes to tip the balance? Is the beginning of the end of CCM–at last–kicking in? Although it is early to tell, shall other bigwigs follow suit, believe ye me, this is but the end of CCM whether they like it or not. If CCM wins the coming elections without rigging, it will be a miracle. If it wins by rigging, believe ye me, some bigwigs will end up in The Hague. I am now convinced that–at last–change has come. We need to welcome it. Again, will there be any meaningful and substantial changes or just changing guards after crossing over? This imbroglio busies me the most. For, if you look at those who champion changes through crossing over and who they actually are, you end up confused. Again, do we need to keep the same kit and caboodle of swindlers in the same outfit or have they in a different one?  You know what I mean even though I am stony after swallowing and burning something.
Let me quote some nuggets from Freddie. He’s quoted as saying, “I believe Ukawa will win this year’s elections because people are fed-up with empty promises and all they need is change.” Freddie is right save that he is one of those who enacted those vices is complaining about. Will boozers take him seriously or barbecue him with his own words?  When did Freddie see the light? Is he abandoning the boat simply to revenge? Where would he be and what would he be saying had he been chosen to a CCM flagbearer? This is why I doubt if such defection will cause any danger to CCM. Essentially, some of our politicos –especially those defecting from the ruling party –have portrayed themselves as opportunists.  I am not making this up. If you read Sumaye’s reasons for defection between the lines, you’ll find that he’s defected simply because he believes “Ukawa will win.” Such a person can shake a party that’s in power for decades shall it uses his words wisely and skilfully.
          If CCM would seek my expert opinion on how to deal with Sumaye and others, I’d tell it: Don’t attack them. Just use their words. I remember. Sumaye once said that he’d defect shall CCM appoint a fisadi (Luwasha). Now that CCM didn’t why is he defecting?  Again, given that Freddie has rocked the boat, anything can happen. It is too early to tell. However, when you look at two opposing fellas, you see no difference except the dilemma for boozers. There's nobody that cares for their maslahis except using them to get into ulaji. Should we boycott the coming elections? Again, is it the beginning of the end of…” fill in the gap. Again, if the UKAUA loses to …. Or if CCM loses to …” What an aw-cum-wow situation! Should we aw or wow? Time’ll accurately tell.
Source: Thisday Aug., 30, 2015.

Saturday 29 August 2015

Je ahadi za CCM zinauzika?

Uchaguzi mkuu uko mlangoni kwa sasa. Wanasiasa na vyama vya siasa nchini wamo tena uwanjani wakijinadi kwa mbinu hizi na zile. Wapo wanaotumia–au tuseme–wanaokuja na mapya wakati wengine wakija na wimbo ule ule wa jogoo. Mojawapo ya vyama vilivyokwisha kutoa ahadi zake katika uchaguzi ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kimetoa ahadi kuu nne kinachodhamiria kutekeleza kama kitapewa ridhaa ya kuongoza tena.
Ahadi ambazo CCM inalenga kuzinadi –na hatimaye –“kuzitekeleza” ni pamoja na kupambana na umaskini, ajira, ulinzi na usalama na kupambana na rushwa.
Ahadi hizi ni nzuri na zinaingia akilini hasa kipindi hiki ambapo nchi yetu inakabiliwa na umaskini wa kutisha kwa walio wengi. Pia nchi yetu inakumbwa na uhaba mkubwa wa ajira kutokana na serikali inayomaliza muda wake kuahidi kutengeneza ajira isifanye hivyo wala kutoa sababu za msingi za kushindwa kufanya hivyo. Kadhalika, wananchi wetu wengi ni maskini hasa kutokana na serikali inayomaliza muda wake kufumbia macho ufisadi ambao umeligharimu mabilioni ya shilingi huku wahalifu waliotenda jinai hii wakiachiwa waendelee kutanua na kutumia chumo lao la wizi. Pia hali ya usalama nchini ni tete hasa kuzidi kuwa tishio la ujambazi na jinai nyingine kama hizi ukiachia mbali migogoro kwenye nchi jirani na kitisho cha ugaidi. Kadhalika, kuzidi kuzoeleka na kufumbiwa macho kwa vitendo vya rushwa.
Kwa vile CCM ndiyo imekuwa madarakani tangu kupata uhuru, wengi wanajiuliza: Kwanini sasa? Hii maana yake ni kwamba CCM inakiri kuwa kwa kipindi chote ambacho imekuwa madarakani imeshindwa vibaya hasa pale ilipoamua kufumbia macho rushwa au kuiacha itanue kwa kipindi chote ilichokuwa madarakani. Je wapiga kura watafanya kosa jingine kuiamini serikali hiyo hiyo iliyokiri kushidwa? Je CCM ina mipango madhubuti inayotekelezeka na kuingia akilini ya kupambana na majanga haya kweli au ni ahadi za uchaguzi? Yako wapi maisha bora kwa watanzania iliyoahidi miaka kumi iliyopita?
Kuko wapi kufumua na kusukua mikataba ya uwekezaji upya ambayo, kimsingi, iliingiwa kutokana na kuwapo mianya ya rushwa tena kubwa tu.
          Kwa vile ushahidi unaonyesha kuwa CCM ilizembea kwa muda wote iliokuwa madrakani, wapo wanaohoji: Nani anamdanganya nani hapa? Je wapiga kura na wananchi nao wataingia mkenge na kusikiliza porojo hizi zinazolenga kuwatoa kura na baadaye watelekezwe kama ambayo CCM imefanya tangu mwaka 1985? Je watapambana na majanga haya vipi? Hawaelezi zaidi ya kutoa ahadi tamu tamu!
Huwezi kuondoa majanga husika ambayo ahadi za CCM ni kukiri wazi kuwa yapo kwa maneno. Ni vizuri wananchi wakaiuliza CCM ilikuwa wapi muda wote huo na imeona mwanga lini na kwanini kama siyo kusaka kura?
          Laiti kungekuwa na upinzani makini, nadhani hapa ndipo ungeanzia kuisambaratisha na kuimomonyoa CCM vilivyo once and for all kama wasemavyo waingereza. Maana imeshindwa vibaya sana. Ukitaka maelezo na sababu za msingi kwa majanga tajwa kuendelea kuwepo wakati CCM iliahidi kuyaondoa hupati jibu. Hii maana yake ni kwamba CCM wanatoa ahadi juu ya ahadi ili kupata kura wakijua wazi hawatazitimiza. CCM wangekuwa na dhamira ya kutekeleza wanayoahidi, angalau wangekuja na mikakati na sera ya kutekeleza ahadi ambazo waliahidi kwenye chaguzi zilizopita wasizitekeleze. Wengi –kabla ya kuchangamkia ahadi hizi mpya –walipaswa kuhoji ni kwanini ahadi za awali hazikutekelezwa.
          Tumalizie kwa kuwashauri wapiga kura na wananchi kuhoji ukweli, udhati, usayansi na utekelezekaji wa ahadi mpya zinazotolewa na CCM.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 30, 2015.

Friday 28 August 2015

Leo mlevi anachonga na CcM


          Wiki jana tulichonga na muishiwa, sorry, mhishimwa Eddie Luwasa baada ya kutupiga changa la macho kuwa angewajaza mafweza wachovu hadi wajihisi wako Uswizi. Punde si punde, si Chama cha Maulaji (CcM) kikarudia ujinga, sorry, mchezo ule ule! Hii–kwa kitasha–huitwa counterstrategical approach. Sijui ni kwa sababu Luwasa na CcM wote ni dugu moja. Mie sijui.
          Baada ya kumsikia Luwasa akitishia kuifanya Bongolalaland Uswizi, CcM wamejivuvumua kuja na hoja kubwa nne ambazo ni kupambana na uchovu, kutengeneza ajira, ulinzi na usalama na kupambana na rushwa.
          Niliposikia ahadi hizi ilibidi kwanza nipate kanywaji na bangi kidogo ili kutuliza mshangao niliopata.  Sasa–kama bado kuna umaskini tena wa kunuka–ina maana ile sera yenu ya Best Life for All (BLA) ilibuma nini?  Je hamuoni kuwa mnakiri kuwa kwa muda mliokuwa maulajini mkitanua na kutanuka mlieneza umaskini?  Mlitegemea nini mlipoachia majambazi kama wale wa Escrow wakahomola kana kwamba kaya hii ni shamba la bibi? Nadhani kama ni kufuta umaskini basi mngewapitisha Jimmy Rugemalayer na Singasinga waliomtajirisha Anna Kajuamlo Tiba-Ijuka akachanganyikiwa; akasahau dhamana yake.
          Yote tisa. Kumi, mliniacha hoi pale mliposema eti mna mpango wa kupambana na ufisadi wakati kwa kipindi chote kilichopita mlihulalalisha karibu katika kila kona. Yupo mlevi mmoja–jina kapuni–aliyesema kuwa kweli nyinyi na chata la sanaa, mizengwe na ahadi hewa. Maana haiingii akilini kusema eti mnapambana na umaskini wakati mliueneza kwa kuushiriki na kuupamba ufisadi hadi wachovu wakaendelea kupigika wakati nyinyi mkipiga mabilioni.
          Hili la ulinzi na usalama limeniacha hoi hadi kuongeza dozi ya kanywaji na bangi ili kuepa kunyotoka roho (kufa) kwa mashambulio ya ugonjwa wa moyo. Je waandishi wa umbea nao wamo? Je akina Ulimboka na Kibanda nao wamo kwenye mpango wenu huu wa ulinzi na usalama wakati ndiyo sheria za kuwabana na kuwang’oa meno na kucha zinazidi kupeta huku tukiona watuhumiwa wakipelekwa majuu kuula kama mabalozi? Hivi Rama Ighon-du aliyemsulubu Ulimboka yuko wapi siku hizi?
          Je katika ulinzi na usalama wenu utahusisha wachovu wote? Nashangaa sana. Hasa nikizingatia kuwa watu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe wanaendelea kunyotolewa roho ili viungo vyao kutumika kutengeneza utajiri baada ya ufisadi na ujambazi kubarikiwa. Mbona hamkuongelea kukuza elimu ambayo akina Dk Shukrani Kawa-dog walinyotoa huku wakipelekea vitegemezi vyao kupata elimu ya haja ughaibuni ukiachia mbali kughushi tena kukifanywa na wazito kukihalalishwa? Hivi mnaweza kunipa sababu japo moja ya wale wazito waliotuhumiwa kughushi kuendelea kushika nyadhifa kwenye ofisi za umma?
          Mliposema mtatengeneza ajira mmeniacha hoi. Je hizi ajira hewa mnazopanga kutengeneza ni kwa ajili ya wachovu au washikaji na vitegemezi vyenu? Ajira gani wakati mmeruhusu wachukuaji mnaowaita wawekezaji kuendesha biashara bila kulipa kodi ukiachia mbali kutujazia wamachinga toka India, China, Uturuki na kwingineko? Mnadhani tumelewa sana kiasi cha kutowaona machinga wa kigeni wakijaa mitaani na kuwatupa nje machinga wazawa? Je mna mpango wa kutumia Ben-Tunituni Makapi strategy ya kuwapa laivu wachovu kuwa nguvu ya maskini ni mtaji wake? Je mtaji wa wajinga ni nini hasa wale watakaoingia mkenge na kuona kuwa sasa mambo mswano wakati ndiyo mabalaa yanaongezeka kutokana na kubadili walaji?
          Kwa vile simo kwenye kuingizwa mkenge huu, siamini mnayosema ndiyo mtakayotenda. Najua wazi.  Mtasema msiyotenda na kutenda msiyosema kama mlivyozoea.
          Message sent. Insh’Allah tukutane wiki ijayo. 
Chanzo: Nipashe Agosti 29, 2015.

Thursday 27 August 2015

Je ni mwanzo wa mwisho wa CCM?


          Si uvumi tena. Waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye ametua kwenye upinzani akimfuatia waziri mwingine wa zamani Edward Lowassa. Haijawahi kutokea kwenye nchi yoyote duniani!  Sasa Sumaye yuko nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Bila shaka CCM hawakulitegemea hili sawa na la kuondoka Lowassa. Je kuondoka kwa Sumaye kutaleta mtikisiko au kubakia kuwa unyasi mmoja kwenye msonge? Je CCM itatikisika au kuendelea kujikaza kisabuni wakati mambo yakizidi kuwa mabaya? Ama kweli kwenye mchezo wa siasa hakuna anayeweza kutabiri lolote kwa ukamilifu tokana na wachezaji kusifika kwa uongo wao. Kwa waliomsikia Sumaye akisema kuwa kama CCM ingeteua fisadi angejitoa, hawakutegemea hili hasa ikizingatiwa amemfuata fisadi yule yule aliyempinga! Je kuondoka kwa Sumaye kutaiathiri CCM? Je amefanya hivyo kwa sababu na hoja au kulipiza kisasi kwa kutopitishwa kupeperusha bendera ya CCM? Je Sumaye amesoma vizuri alama za wakati? Ama kweli, ukishangaa ya Musa utaona ya Firauni!
          Alipojiengua Lowassa mengi yalisemwa kubwa likiwa ni tamaa yake ya urais. Je Sumaye ambaye amejiengua baada ya zoezi la kusaka urais kufungwa naye watasemaje? Majibu anayo Sumaye mwenyewe aliyekaririwa akisema, “Naamini Ukawa watashinda uchaguzi huu, CCM wamezubaa wakidhani watashinda wakati wananchi wamewachoka, wanahitaji mabadiliko.” Sasa tunajua kuwa kumbe Sumaye amefuata ushindi na siyo sera wala nini. Je Sumaye amesoma alama za wakati au kufuata ushindi?
          Japo waliotabiri kuwa CCM ingefia mikononi mwa rais Jakaya Kikwete waliposema hivyo walibezwa, lolote laweza kutokea kuanzia sasa. Maana haiwezekani chama ambacho kimehimili kufutika kashfa kama vile Escrow, EPA, utoroshaji wa pembe za ndovu tena ukiwahusisha wakuu wake kikakubalika na kupendwa na wananchi.  Je CCM itatumia miujiza gani kuzima upepo huu unaoielekeza kuzimu kisiasa ambapo vigogo wake wanazidi kuitupa mkono? Sitashangaa nikisikia wakongwe kama Kingunge Ngombale Mwale, Joseph Bukuku, Joseph Walioba na wengine wameipiga teke. Maana, imekuwa kichwa ngumu hasa pale ilipoua katiba mpya na kuendelea kuwalea, kuwaendekeza na kuwakumbatia mafisadi. Hata hivyo, kwa kushika dola muda mrefu, CCM bado ina nyenzo ukiachia mbali kuwa na roho ya paka. Je kama itatumia mabavu na kushinda na upinzani ukaamua kukomaa watu watashindwa kuishia The Hague kama jirani zetu wa Kenya?
          Hata hivyo, wapo wanaohoji kama Sumaye ana jipya ikizingatiwa kuwa haya yaliyowachosha watanzania kama anavyodai mengine ameyaasisi na rafiki yake Benjamin Mkapa? Hawa ni wale wanaosema: Lao moja. Kimsingi, hawa wanashindwa kumtofautisha Sumaye na Lowassa na mgombea wa CCM Dk John Magufuli kwa sababu wote walikuwa kwenye chama hicho hicho kinacholaumiwa. Je kuondoka CCM kutaleta nafuu na kubadilisha mambo?
          Tukiangalia upande wa pili, CCM imekuwa ikijiridhisha kwa kuwaita wanaoihama kuwa oil chafu. Je wataendelea na jeuri hii au kubadilika? Maana, oil chafu inazidi kuchafua hali ya hewa huku injini ilimotoka ikizidi ku-knock. Je kweli wanaotoka ni oil chafu au oil chafu ni  ile iliyobaki kwenye injini husika? Hili swali ni muhimu hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wanaamini kuwa mageuzi yanaweza kuja kupitia upinzani huku ukale ukiendelezwa na CCM. Je hapa oil chafu ni ipi kwenye macho ya wananchi ambao kimsingi ndiyo waamuzi kwenye uchaguzi ujao?
          Ingawa CCM wameendelea kujikaza na kuona kama hili ni wingu la kupita, ukweli mambo ni tofauti. Na kama CCM wataendelea na dharau hizi watastuka wakiwa nje ya ulaji waanze kulaumiana. Tumeyashuhudia kama haya kule Malawi, Kenya, Zambia na kwingineko. Je wakati wa kaundika waraka wa mwisho kwa CCM umefika? Je kinachoendelea kutokea ni mwanzo wa mwisho wa CCM au mwanzo wa mwanzo wa upinzani kuchukua nchi?  Kwa vile waamuzi ni wananchi na wapiga kura, yetu macho japokuwa–kwa hali ilivyo–unaweza kutabiri kitakachotokea. Hata hivyo wahenga walisema; Hakuna marefu yasiyo na ncha na kila chenye mwanzo sharti kiwe na mwisho. Je ni mwanzo wa mwisho au mwisho wa mwanzo? Oktoba itatuambia.
Chanzo: Dira Agosti 27, 2015.

Tuesday 25 August 2015

Migrants: Europe Needs to Go Back to History


Many desperate people from Africa, Asia and Middle East are now making perilous journeys in thousands in their attempts to reach Europe seeking green pastures. They are risking everything to cross the Mediterranean.  Italy’s ports have become modern-time Kilwa, Mafia, Dakar or Lamu for Africans to enter Europe as it was for Europeans to enter Africa landing in the above mentioned city states. Europe is grappling with the heavy load of invaders just as Africa did when Europeans invaded and colonized her in the seventeenth century. Those poor but energetic and ambitious Africans, Arabs and Indians are called a calamity there due to the danger they pose to the economies and cultures of European countries.
          Nevertheless, it is sad that Indians and Arabs are not seen with the same lenses as Africans are. Is it because of racism or ignorance? Why don’t they feel pity for them after considering how dangerous and adventurous their voyages are?  Is the history repeating itself or is the law of reciprocity based on times displaying its nature? It is time to tell Europe to stop worrying for no reasons.These folks are heroes who want to help poor relatives made poor by black colonialists that are always in bed with Western ones. Africa’s economies can’t support their population thanks to playing a service role to Western economies. If the situation remains the same, Europe must brace itself for even more. Maybe, this is the new way of deconstructing the archaic system of exploitation enacted by the same European countries under colonialism, slavery and imperialism. This is why I fully endorse it. For I know. It will help all of us to see the problem as ours not Africa's or/and third world's as those who created such a dichotomous schema have always wrongly maintained for many years. Importantly, Europe needs to open doors, borders and hearts the same Africa did when first Europeans inundated Africa seeking spheres of influence that later became colonies.
          Again, Europeans seem to have forgotten a simple fact that they once gone to Africa  thereby colonizing her and destroying her economy and her ways of life. What did they expect out of an unequal and inequitable trade relationship the world evidences today? When they invaded to Africa, they did not have passports the same way our people are doing now. They’re called floods that’ll wipe out European good life standards. So be it; if they wiped out our own life standards before introducing slavery and colonialism. Swahili sages have a saying kula na kulipa. You eat and pay for what you’ve eaten. Or when you eat expect to be eaten. Aren’t we eaten by bacteria after our dead bodies undergo rigor mortis, chemical changes, when we die? The Europeans came to Africa and robbed her everything. Fortunately for them, Africans are not going there to rob or colonize them. But they’re going there to work because they’re good and hard workers. They are honesty and innocent victims of manmade exploitation in their continent.  Again, the Europeans are the same humans who created the exploitation that is forcing Africans to flee their countries. That’s why they are not aiming at colonizing anybody. If Europeans flooded Africa in the seventeenth and  the eighteenth centuries, what’s wrong for Africans to flood Europe in the twenty first century as the sign of reciprocity?

           I think European countries honestly need to learn about globalization they introduced to the world. They must do so by using the waves of economic immigrants. They need to learn that when you leave a thorn back in the farm, the same will hurt you one day. Time for colonial monsters to pay what they ate is now. European countries need to understand that what’s going on is, essentially, the real product of their plundering policies championed by capitalism. Africans have a saying that the capital of a poor person is his or her energy. This is why Africans are looking for good life and jobs in Europe after colonial monsters conspired with black ones to deny them works at home. These folks are looking for the means to live dignified and meaningful lives. Invest in Africa and create jobs. You won’t see the assemblages of Africans coming to your doors to destroy and infringe on your cultures and standards the way you destroyed theirs.
Source: African executive Aug. 26, 2015.

Kijiwe chastukia janja ya CcM


          Baada ya msimu mwingine wa kusia uongo na kuingizana mkenge kuanza, tunaanza kusikia mambo ya ajabu ajabu. Ajabu ya maajabu ni kwamba wanaoyasema haya wanawageuza wachovu hamnazo au wasio na kumbukumbu.
          Mgosi Machungi baada ya kurejea kutoka Ushoto kupiga kura ya maoni analianzisha. Akionyesha gazeti la Danganyika Daima anasema, “Jamani mimeona ahadi mpya za CcM na jinsi waivyoenga kutiingiza mkenge mwingine?”
          Kapende anadakia, “Hawana jipya hawa wala hawana dola zaidi ya rongorongo za kusakia kura ya kulia bure tu. Hata hivyo, naona Eddie Luwasa amewashika vibaya kipindi hiki.”
          Mbwamwitu anachomekea, “Hebu fafanua tu-understand. Wameshikwa pabaya wapi na vipi?”
          Mpemba anakatua mic, “Yakhe tuache utani wallahi. Hawa jamaa wa CcM walozoea vya kunyonga vya kujichinja wasiweze kweli wamenasa muhula huu. Hivi mmeona wanivyohaha kuwahadaa wachovu kwa kuja na ahadi tamu mpya wakati zile za awali hawakutekeleza hata moja?”
          Mijjinga anakwanyua mic, “Hawa tulishawazoea. Ukifika wakati wa uchaguzi wanajifanya kujali maslahi ya umma wakati wao ndiyo kikwazo kikubwa cha mstakabali na maendeleo ya umma  husika. Nashauri kupindi hiki tuwapige chini kwa kuwajaribu wapingaji au vipi?”
          Sofia Lion aka Kanungaembe anakamua mic, “Wapingaji wapi wakati wote ni wana CcM? Mnadanganywa na Luwasa kuingia upinzani wakati hana sera zaidi ya za CcM? Ama kweli wajinga ndio waliwao! Nyie hamjui mchezo unavyokwenda siyo!”
          Kapende anakatua mic, “Japo siwapendi wapingaji, angalau wamethubutu kwa kuonyesha ujasiri wa kumchukua Luwasa na kumpitisha agombee urahis. Dawa ya moto ni moto. Kwa vile huyu alikuwa nao kitanda kimoja kwa muda mrefu basi tumtumie huyu huyu kuwamaliza mahabithi hawa.”
          Mheshimiwa Bwege anakatua mic, “Mheshimiwa Kapende nakuunga mkono. Wahenga walisema mchawi mpe mwana alee. Isitoshe, kama upingaji ungemkataa Luwasa ungepata hasara kuliko hatari ya kumtumia kupambana na joka kuu. Nakubaliana na wanaosema adui wa adui yako ni rafiki yako.”
          Kanji naye hajivungi. Anakatua mic, “Lakini pinjani siku mingi iko sema Luwasha iko fisadi papa. Sasa naingia pinjani nageuka malaika?”
          Msomi Mkatatamaa anaamua kutia guu, “Mheshimiwa Kanji usemacho ni kweli. Ila unapokuwa vitani akatokea mwanajeshi au wanajeshi pinzani wakaasi huwezi kuacha kuwachukua lau wakusaidie kupigana kwa kukupa siri za walikotoka ili ushinde kirahisi vita hii. Nadhani haya ndiyo mantiki waliyotumia wapingaji kumpokea na kumpa tiketi Luwasa. Najua wengi hawakubaliani na hili na wanalaumu sana upingaji. Tunapaswa kujua kuwa wakati wa vita haukupi fursa kubwa ya kuchagua zaidi ya kuchukua maamuzi magumu kama walivyofanya upingaji. Wale wanaopinga Luwasa kupokelewa na kuteuliwa walitaka aende wapi kama siyo upingaji?”
          Mzee Maneno anapoka mic, “Msomi hapa nikukubali. Luwasa ni bonge ya silaha dhidi ya CcM. Tunajua ana mapungufu yake.  Lakini ukiangalia hali halisi, mapungufu yake ni rahisi kuyashughulikia kuliko kukosa dola na kuendelea kuliacha kwenye mikono ya manyang’au.”
          Mgosi anarejea, “Hebu tiangaie ahadi za CcM za muongo huu. Wanasema eti watatengeneza ajia. Je ajia hizi ni kwa ajii ya wachovu au vigogo, vigemezi vyao na maafiki zao? Wanaendeea kusema eti watapambana na ufisadi, mbona hawajakama wezi wa Escoo?”
          Kabla ya kuendelea Mijjinga anakatua mic tena, “Hakuna waliponiacha hoi kama kusema eti watapambana na umaskini wakati ndiyo mtaji wao wa kuwatumia wajinga kuwapigia kura ya kula. Ama kweli akutukanaye hakuchagulii tusi. Sijui wachovu wafanywe nini au watukanwe tusi gani ndiyo wachukie na kufanya kweli mwaka huu?”
          Mgosi anachomekea, “Iko wapi ahadi ya kuandika katiba mpya ya wananchi? Upuuzi na uongo mtupu.”
          Msomi anaendelea, “Wasingeweza kuongelea katiba mpya. Kwani wanajua fika wakiigusia, wataumbuka. Wakisema iandikwe ile ya jaji Waryuba ndiyo watakuwa wamekufa kwa vile baada ya kuongopa itawawajibisha. Hivyo, kinachoendelea ni usanii ule ule. Hakuna la maana wala jipya. Heri tuwape wapingaji lau nao tuone vitu vyao chini ya Luwasa au vipi?”
          Sofi haridhiki. Anarejea upya, “Hivi mnaposema Luwasa ndiye apewe kaya mnajua mipango yake ya sirini?”
          Mbwamwitu anakatua mic, “Acha da Sofi nikuchomekee. Unakumbuka wewe ndiye ulikuwa mtetezi wake kabla ya kuwapiga teke? Basi tupe hiyo mipango yake ya siri ambayo umeijua wakati huu au ule lakini ukaificha. Nadhani huu ni unafiki kumuona Luwasa mbaya baada ya kuondoka kwenu wakati wewe mwenyewe ulikosana na watu wengi ukimtetea lakini leo unapiga madongo. Hivi umeingiliwa na nini dada yangu mbona huko nyuma hukuwa hivyo?”
          Mpemba anakatua mic tena, “Nyie hamuwajui hawa sisiemu. Wao mabingwa wa fitina ati. Na ni fitina na ghilba hizi hizi wanizotumia kuendelea kufanya mauza uza yao miaka nenda rudi wasiochelee lolote. Naunga nkono mwaka huu tuwape wapingaji potelea kote.”
          Mipawa anakatua mic, “Nami nakuunga mkono ami. Hizi ajira wanazoahidi kama si hewa basi zitakwenda kwa washikaji na vitegemezi vyao. Kuhusu usalama hiyo sahau. Usalama ni wao kuendelea kuula wakati sisi tukiliwa. Hili la kupambana na ufisadi nadhani wanamaanisha kuupamba zaidi nasi kupoteza njuluku zaidi. Ama kweli akutukanaye hakuchagulii tusi!”
          Kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga si lakipita shangingi la Nipe Mapepe. Acha tulitoa mkuku!
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 26, 2015.

Mchwa Kipanya na Wagombea Ulaji

Monday 24 August 2015

Mjue mke na mama wa rais aliyegeuka mwanamuziki

Patience Dabany ni mama wa rais wa sasa wa Gabaon Ally Omar Albert Bongo Ondimba na mke wa rais Omar Bongo Ondimba. Alikuwa first lady kwa takribani miaka 30 kabla ya kuachika na kujiingiza kwenye muziki. Amepiga nyimbo nyingi na anaendelea kupiga muzika kama kawaida. Anasema muziki umo kwenye damu yake. Kwani baba yake alisifika kwa upingaji ngoma  na mama yake alikuwa muimbaji.

Sunday 23 August 2015

I predict: Many political nuptials will hit the rock
















Source:Guardian Aug., 23, 2015.

Dk Bilal hana sababu kujitoa CCM
















              Kuna uvumi uliokuwa umezagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa makamu wa rais Dk Gharib Bilal angejitoa kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM). Baada ya uvumi huu kuzagaa, ofisi ya Makamu wa Rais iliwahi kuzikanusha jambo ambalo ni jema na lenya nafuu kwa mhusika.
          Jambo ambalo ni vigumu kuelezea ni kwanini uvumi huu umemlenga Bilal na si waziri mkuu anayemaliza muda wake, Mizengwe Pinda, waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye au vigogo wengine? Je ni wapinzani wake aliowahi kuwapa hali ngumu visiwani hadi akapewa umakamu wa rais au system iliyompa ulaji huo bila kutaka walioanzisha uvumi huu ili kupima maji au kuzidi kumbomoa mhusika? Je kuna chembe za ukweli kwenye uvumi huu? Je ni vyama vya upinzani ambavyo hivi karibuni vimevuna baadhi ya vigogo wa CCM baada ya kumaliza kwa mchakato wa utafutaji atakayepeperusha bendera yake?
           Kama utamuangalia Bilal kwa makini sana kufuatana na historia yake kisiasa, walioanzisha uvumi huu walipoteza muda wao kwa vile–kama ni kuleta changamoto mpya Visiwani kama alivyofanya kabla ya kunyamazishwa kwa kupewa umakamu wa rais–ameishazidiwa kete; au tuseme kuwekwa sawa. Kwani mchakato wa kumtafuta atayepeperusha bendera ya CCM visiwani ulishakwisha.       Kumbuka, Bilal aliteuliwa–si kwa sababu ya kupendwa–bali kuepusha balaa Zanzibar. Kwa wanaokumbuka sekeseke alilozua Bilal –akiungwa mkono na rais wa zamani Salmin Amour na alivyotaka kuipasua CCM –wanajua fika alivyokuwa mwiba kwa CCM pamoja na kupewa umakamu wa rais ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Kwa vile Bilal alikubali kuwekwa sawa, hana tena ubavu wa kufanya lolote kisiasa hasa ikizingatiwa kuwa umri nao umeishamuacha. Uzuri ni kwamba Bilal na wapambe zake wanalijua na kulikubali hili. Hata yule aliyempa nguvu na support, hana tena ubavu zaidi ya kuuguza mavune ya ugonjwa na uzee ukiachia mbali kuondoka kwenye hadhira kisiasa.
          Pia Bilal anafahamu kuwa kwenye siasa za Tanzania ni mtu mmoja tu aliyekuwa na ubavu na ushawishi wa muda mrefu yaani Mwl Julius Nyerere.  Hivyo, kubebwa kwake na Amour–aliijua fika–lilikuwa ni suala la muda kabla ya historia kumweka kwenye kapu lake la sahau.
           Wapo wanaoona kuwa Bilal bado ana ubavu wa kuweza kulianzisha kama alivyofanya awali kiasi cha kuilazimisha CCM kumtengenezea ulaji wake wa miaka mitano.  Je ukweli na hali halisi ikoje? Hata akirejea Zanzibar, hana tena ule mvuto aliokuwa nao dhidi ya rais Dk Ali Mohamed Shein ambaye alichomolewa kwenye Muungano na kurejesha Zanzibar ili asiwavurugie wapakwa mafuta wa upande wa bara.  Sasa wakati wa kukaa kando umefika sawa na wengine kama vile Pinda na wengine wengi ambao walitemwa kwenye mchakato uliomuibua John Pombe Magufuli huku CCM ikimpoteza Lowassa na wapambe zake.
           Hata ukiangalia muda wote aliokaa ofisini, alibanwa na kuwa mtu wa kufungua makongamano na matamasha. Haijulikani kama ni kwa makusudi au bahati mbaya, Bilal hakujijengea umaarufu kama aliokuwa ameujenga makamu wa rais wa zamani marehemu Dk Omar Ali Juma aliyekufa kwenye mazingira ya utata kutokana na mitandao ya urais kumuona kama tishio.  Kwa muda wote aliokaa madarakani, alijiandalia hili. Kwani, hakuonyesha wala kuruhusiwa kuonyesha makeke. Je Bilal alijua na kulikubali hili hasa baada ya kujua kilichompata marehemu Dk Juma baada ya kuonyesha makeke ingawa hakuwa na nia mbaya?
          Hata hivyo, kwa wanaojua siasa za visasi na kuviziana, ilikuwa dhahiri kuwa Bilal alikuwa mtu wa kuja kwenye ofisi ya makamu wa rais aliyewekwa pale kwa lengo maalumu ambalo wengi wanalijua kuwa ni kutaka kuepusha shari ambalo kuendelea kwake kutaka kusimama dhidi ya Shein, chaguo la Dodoma kungesababisha visiwani na kwa muungano mzima. Nani angeendelea kumzawadia kwa ujeuri wake huo hata kipindi hiki alichochukua fomu za kugombea urais? Sioni tofauti ya Bilal na Augustine Ramadhani au Augustine Mahiga waliogombea wakiwa watu safi lakini wakabwagwa kwenye awamu ya kwanza huku hata watoto wa jana kwenye siasa wakipitishwa jambo ambalo ni aibu kwa wakongwe hawa.  Inashangaza ni kwanini wakongwe hawa kwenye fani zao hawakuliona hili sawa na ambavyo Dk Bilal hakuliona.
           Kwa kuzingatia ujio wa Bilal kwenye siasa za bara kama makamu wa rais, ingekuwa jambo la ajabu kama CCM wangempitisha kumrithi Kikwete. Pia litakuwa jambo la ajabu kama Bilal bado ana ndoto ya kulianzisha ima akiwa CCM au nje. Anachoweza kufanya –kama anahisi alitumiwa ili kuzuia mbio zake baadaye –ni kijiunga na upinzani kuongeza nguvu kwa Lowassa ambaye pia naye anatisha shaka kama atafikia malengo yake ya kuiadhibu CCM kwa kukataa kutumika kumfikisha kwenye malengo yake binafsi.
          Tumalizie kwa kusema wazi kuwa–kwa sasa–Bilal hana mvuto wala ubavu wa kuweza kufanya lolote kisiasa. Hivyo, wanaozusha kuwa ana mpango wa kuhamia upinzani–hata kama anao–wajua hautayumbisha CCM.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 23, 2015.

Saturday 22 August 2015

Kujiondoa CCM Sumaye mwanzo wa mwisho?

  • Edward Lowassa na Frederick Sumaye

Taarifa tulizo nazo ni kamba waziri mkuu mwingine wa zamani Fredrick Sumaye amefanya maamuzi magumu na kujivua gamba. Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Sumaye kujiondoa CCM si fununu wala uvumi tena. Laiti na akina Jaji Augutine Ramadhani, Dk Augustine Mahiga, Ali Karume na wengine walioona kama hawakutendewa haki wangechukua maamuzi magumu, hakika huu ungekuwa mwisho wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Je kuondoka kwa Sumaye ndiyo mwanzo wa mwisho wa CCM? 

Mlevi ambeep Luwasa


Bwana Eddie Ngonyani Luwasa,
Kwanza, nakusalimu. CCM hoyee sorry, CHANDIMU, sorry, UKAUA hoyeee! Kaka, usidhani nakusanifu au kukuchulia. Unajua mtu akivaa magamba, sorry, magwanda mengi anachanganya kidogo. Mbona huu ulabu na bangi vimenichukua mapema hata kabla ya kusend message? Tuyaache. Kwa vile nimeishawabeep, kuwatweet hata kuwatwangia mkuu na Dk Joni Kanyawaji Makufuli, sasa nimeona ni zamu yangu kuchonga nawe juu ya masuala mbali mbali.
          Mheshimiwa mtarajika, nilikusikia juzi ukiwa kwa akina twambombo tununu kuwa una mpango wa kuibadili Bongo kuwa kama Uswizi wazito wanakoficha mishiko. Nilioposikia hivi nilishangaa kidogo ila nikasema nikiwasiliana nawe utanipa jibu. Naunga mkono mpango wako japo niliwahi kufanya hivyo mara mbili na walevi wenzangu tukaishia kuumia. Mara ya kwanza tuliingizwa mjini na jamaa moja tapeli wa kisiasa aliyejipachika jina la Bwana Mafweza wakati alikuwa msanii na kopakopa wa kawaida. Baada ya kugundulika kuwa kumbe hekalu alilokuwa akiishi lilijengwa kwa mkopo ambao alishindwa kuulipa nilidharau.
           Mara ya pili nilitapeliwa na mtu ambaye unamjua sana. Si walevi tuliahidiwa Maisha Bien kwa Wote Apeche (MBWA) chini ya ANGUKA. Hatukujua kumbe tungeishia kuangushwa na kuwa mbwa kama kifupi kilivyo. Hayo tuyaache.
          Nilivyokusikia juzi nilishangaa na kujiuliza kama nawe hutafanya kama hao matapeli wengine. Je kipindi kile mkipunyua ule uchache wa Richmonduli ndiyo mlikuwa mnaanza sera hii ya kugeuza kaya kuwa Uswizi ama vipi? Maana kuna kipindi nilisikia ukisema kuwa chini ya Richmonduli mliokoa njuluku nyingi wakati waliofaidika ni akina Kagoda na wengine au vipi? Je bado unaweza kusimama mimbarini ukasema kuwa dili la Richmonduli lilikuwa la maana kwa kaya au ni yale yale ya kusema kuwa uhusiki isipokuwa bosi wako aliyekuzuia kuvunja mkataba. Je ni kweli kuwa –kwa usongo wa kaya –ulitaka kuuvunjilia mbali ule mkataba au kamba? Wapo wanaosema kuwa kama ni kweli ulitaka kufanya hivyo, ni kwanini uliendelea kumtumikia njemba mliyepingana badala ya kukitoa na kumchomea utambi kwa walevi au kuna kitu unaficha mkuu?
          Pia nilikusikia ukimkandia swahiba yako ambaye hamjakutana uchochoroni kuwa amebemenda uchumi. Je ulimaanisha nini wakati ulipokuwa Washington kwa Joji Kichaka ukihojiwa ulimwagia ujiko kuwa amejenga barabara na ameweza kuvutia marais wa Uchina, Marikani hata Joji Kichaka mwenyewe? Je wakati ule alikuwa anaonekana mzuri kwa vile mlikuwa timu moja na sasa umejiondoa na kuanza kumtupia mawe. Je unadhani utafanikiwa? Je unadhani walevi watakuamini au watakukaanga kwa maneno yako?
          Juzi nilikusikia ukisema kuwa hutaki mchezo. Ulidhani CCM na Dk Kanywaji wanacheza makidamakida kama yule binti Microphone wa mjengoni? Hebu nimegee kidogo. Hivi yule kitegemezi wako alifanyafanyaje hadi akaukwaa ubalozi? Je yule kitegemezi wa Belly of Tembo (BoT) bado anaendelea kupiga mzigo pale? Mbona hugusii ufisadi kwenye sera yako ya kufanya kaya iwe Uswizi kama siyo Uswazi? Je bado mnawasiliana na kuchat na swahiba yako Njaa Kaya? Juzi nilisikia hata akina Ngeleza na washirika zako wengi wa zamani wakikucheka huku wakimuunga mkono mpinzani wako. Je hili limekustua au umeamua kuwapuuzia kama walivyokushiti?
          Muishiwa, sorry, mhishimiwa, kabla sijasahau, hivi ulimsikia Mapepe Ninaye juzi akitetea uamuzi wa kufyeka jina lako kuwa ulitumia mabilioni kuusaka urahis? Je ni kweli? Kama ulitumia mabilioni je uliyanyakaje kaka? Kama ni rongorongo, unajitetea vipi?
          Kwa vile utanijibu, naomba niishie hapa nikiongoja majibu yako.
Ubarikiwe sana muishiwa.
Chanzo:Nipashe Agosti 22, 2015.

Friday 21 August 2015

Je kampeni umeuona mtego uliomo?


          Japo tunaambiwa kuwa muda maalumu kisheria wa kuanza kampeni za uchaguzi mkuu ujao hazijaanza, sidhani kama hili ni kwa wote. Hivi karibuni, mgombea wa upinzani, Edward Lowassa ameonekana kwenye miji mikubwa mbali mbali akivuta umati wa watu huku akijisifu kuwa anakubalika.
          Kwa vile muda maalumu wa kuanza kampeni haujafika, wengi wanajiuliza, anachofanya Lowassa ni nini kama si kampeni tena kabla ya muda muafaka kufika? Je anachofanya Lowassa kingefanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wapinzani wangenyamaza kama ilivyofanya CCM? Je ni kwanini CCM imenyamazia uvunjaji huu wa kanuni? Wapo wanaoamini kuwa CCM imeamua kunyamaza ili wapinzani waseme wamalize yote halafu ije kwa kustukiza na kuwazima kama kibatari. Sijui kama wapinzani wameishaling’amua hili.
          Hata hivyo, wengi hawashangai wapinzani kuendelea kuingia mtego huu wa kufanya kampeni kabla ya wakati hasa ikizingatiwa kuwa maamuzi ya kumpokea na kumpitisha Lowassa hivi karibuni yamewaonyesha kama watu wasio makini na serious.
          Sijui kama wapinzani wanaliona hili. Ukiangalia walivyompwakia Lowassa kwa imani kuwa watachukua nchi, huenda ni dhana hiyo hiyo wanayotumia kuwa wakianza kampeni kabla ya wakati watazoa wapenzi, wafuasi na wapiga kura wasijue siyo. Si kawaida kwa chama kikongwe kama CCM kunyamazia rafu hii kama hakuna faida kwake.
          Kunyamaza kwa CCM kunaweza kutafsiriwa kama janja ya kutathmini ufuasi wa upinzani na madhara ya kisiasa unayoweza kuisababishia CCM. Pili kunyamaza kwa CCM ni njia ya kisayansi ya kubaini maeneo ambapo upinzani una nguvu.
          Tatu, ni fursa ya kujua mbinu na mikakati waliyopanga kutumia wapinzani ukiachia mbali kuorodhesha hoja za wapinzani na kuzijibu. Siasa hasa za uchaguzi ni kama mchezo wa ngumi. Mhusika hapaswi kutumia nguvu zote mwanzoni. Kwani kufanya hivyo humfanya achoke mapema na hivyo kutwangwa kwa knockout kirahisi. Au tuiweke hivi. Harakati za uchaguzi ni sawa na mbio za marathon ambapo mkimbiaji mahiri huanza taratibu ili kutunza nguvu ambayo huionyesha anapokaribia mstari wa ushindi.
          Ukiangalia Bara na Visiwani, CCM inacheza mchezo ule wa wait and see yaani ngojea na uone. Inashangaza kuona upinzani –pamoja na kuwa na viongozi wengi wasomi –unaingia kwenye kile ambacho wataalamu wa vita huita booby trap yaani mtego shutukizi. Japo ni mapema kusema, mikiki mikiki ya uchaguzi itakapoanza kwa upande wa CCM itawastua wengi kwa namna watakavyowamaliza wapinzani.
          Wengi walitegemea wapinzani wangekaa kimya huku wakisoma na kujifunza udhaifu ambao CCM itatumia kuwakabili. Lakini si hivyo. Wapinzani wameishaanza hata kujitangazia ushindi wasijue ngoma bado mbichi!
          Ukiachia mbali kukurupuka, upinzani una kibarua kingine kikubwa ambacho ni kuonyesha kuwa ukweli wao wa awali ni uongo na uongo wao wa sasa ndiyo ukweli. Kwa kumpokea na kumsimamisha Lowassa ambaye wapinzani walimuonyesha kama mtu fisadi watakuwa na kibarua kigumu kumsafisha. Je wataweza na kufanikiwa? Je hili ndilo linalowahangaisha wapinzani kuanza kampeni mapema ili kumsafisha mtu wao waliyemchafua wenyewe pamoja na kuwa naye pia alijichafua hata kabla ya wapinzani kumuanika?
          Ukiachia mbali Lowassa kama mtu binafsi,je ana sera gani zinazoweza kuwavutia wapiga kura na wananchi waliokwisha choshwa na ufisadi?
          Wengi wangetamani kusikia mipango ya Lowassa hasa namna ya kupambana na ufisadi. Pia hata matamko machache aliyotoa kuwa anataka kuifanya Tanzania iwe tajiri bado hayaeleweki hasa ikizingatiwa kuwa haelezi ni sera gani atatumia kulifanikisha hili. Wengi watataka awaeleze ni kwanini alishindwa kulifanya hili alipokuwa madarakani na badala yake akafanya kinyume. Sijui kama kuingiza Richmond na kutumia fedha za EPA kutafuta urais ilikuwa ni sera nzuri ya kutajirisha zaidi ya kufilisi nchi. Lowassa ana mengi ya kujibu ukilinganisha na mgombea wa CCM Dk John Magufuli ambaye rekodi yake ya utendaji kazi haina shaka yoyote. Je Magufuli na CCM wanajivunia hili kiasi cha kuwaacha wapinzani wahangaike ili waje wawamalize mwishoni ambapo hawatakuwa na muda wala fursa ya kujibu mapigo? Je CCM wanawaacha wapinzani watumie raslimali zao kabla ya wakati muafaka ili wakati ukifika wawe wameishafilisika kimkakati na kulhali? Yote yanawezekana hasa ikizingatiwa kuwa si mara ya kwanza kwa CCM kushiriki uchaguzi mkuu ikilinganishwa na wapinzani wanaposhiriki kwa mara ya kwanza wakiwa na mgombea wa CCM tena mwenye kutia shaka.
          Kitu kingine kinachofanya wachambuzi waone ni kwanini CCM imeamua kukaa kimya kwanza, ni ile hali ya uzoefu walioupata mwaka 1995 wakati waziri wake wa mambo ya ndani Augustine Lyatonga Mrema alipojitoa chamani na kujiunga na upinzani akaishia kushindwa na kuzama nao. Kwa wanaojua hasara iliyotokea kwa upinzani mwaka huo, wanasikitika kuwa kishindo cha anguko mwaka huu kitakuwa kikubwa hasa ikizingatiwa kuwa Lowassa anaweza kushindwa na kuzama na vyama vikubwa vinne vilivyokuwa vinaonekana kuwa tegemeo kitaifa. Hata hivyo, wengi wanahoji ukubwa na ushawishi wa vyama husika iwapo vinazidiwa na mtu mmoja kiasi cha kumpokea, kumnyenyekea na kumwachia aamue atakacho hata kama hakiingii akilini kama kupeperusha bendera ya upinzani. Ingawa ni mapema kutabiri matokeo ya uchaguzi ujao, mshindi anajulikana hasa kutokana na sifa na mikakati ya wagombea.
Chanzo: Dira