The Chant of Savant

Saturday 6 December 2014

Hii imenichefua na kunichafua


Kama wangetaka kututendea haki basi wangehukumu na wote waliowezesha dili hili kuanzia serikali iliyojifanya kutojua wakati wakubwa zake walishiriki kikamilifu.. Huu ni uchavda mwingine. Mnakumbuka skandali ya Chavda alipopewa mashamba akaishia kuyatumia kuchukua mamilioni toka Benki bila kuyaendeleza? Alipobainika wakubwa walifanya nini zaidi ya kumfukuza nchini ili asiwataje? Nalo hili mmelisahau?”

2 comments:

Anonymous said...

Eti sasa tunaunda kikosi maalumu kupambana na utoroshaji madini ya Tanzanite, iwapo tumeshindwa kuwaona Twiga mnyama na mpaka kusafirishwa kwa machine zetu za scanner pale KIA, na Dege la kijeshi la serikali ya Qatar kuwapo pale uwanjani kwa zaidi ya majuma mawili pia hiyo Dege halikuonekana.

Basi nafikiri tuendelea na na utaratibu wetu wa kupiga ramli nafikiri ndiyo njia sahihi kwa kurudishwa nyuma maendeleo.

Iwapo tupo makini basi tumrejeshe mkoloni maana sisi wenyewe tumeshindwa kujiongoza.

Iwapo kama uamuzi huu wa kumrejesha mkoloni utaonekena ni fedheha basi tujifunze kwa wananchi nchi zingine walivyo wazalendo kupambana na wanafiki kwa wavurulumisha mpaka kukimbia nchi.

Na hivi sasa wazalendo wameanza kufufua pia zile kesi Tata kama kuuwawa kwa Komradi, Mzalendo, Mwanamapinduzi, Mpenda Maendeleo,Shujaa,Mpiganaji, Thomas Sankara.

Hizi sifa zote angalia hakuna hata cheo cha madigrii hapo lakini kila kitu kinajieleza kuhusiano na elimu na madigrii yake huyu mpendwa wetu mungu amlaze pema peponi. na vilaza wote wahuugue magonjwa kwa muda mrefu kabla vifo vyao ilie wasikie raha ya maumivu kunyang'anya haki za wanyonge

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon ujumbe wako licha ya kufikirisha na kuchochea hasira unafikirisha sana. Umemwaga usongo wako wote kuhusiana na ushamba na ujambazi tunaofanyiwa na wezi wetu wenye madaraka. Nisingependa kuongeza kitu kwa kuhofia kuharibu. Isitoshe umaliza yote. Ubarikiwe na uendelee kupita hapa na kuwasha moto kama ulivyofanya.