The Chant of Savant

Thursday 31 July 2014

Kwani tuzo za Kikwete zina nini na wanigeria?

Habari iliyosambazwa kwa vyombo vya habari ni kwamba rais Jakaya Kikwete amepewa tuzo nyingine ya  The Icon of Democracy. Ajabu pamoja na wahusika kujisifu, ukichunguza sana unagundua kuwa nyuma ya tuzo hii kuna wanigeria. Kulikoni? Je kuna matapeli wanaomzunguka Kikwete na kusuka apewe upuuzi huu ili baadaye wahusika waje kumtoa upepo au kutafuta fursa na kuchukua kwa njia za uwekezaji uchwara kama ilivyokuwa kwenye tuzo nyingine ya kutia shaka ya The Most Impactful Leader of Africa iliyotolewa na Jarida lenye uhusiano na wanigeria? Maana tunaambiwa yupo Mwandishi wa habari ambaye pia ni pastor Elvis Ndubuisi Iruh kwenye tuzo ya sasa sawa na  African Leadership Magazine ambalo makao yake makuu ni 13 Mambilla street,Off Aso Drive, Asokoro.P. O. Box 9824 Garki – Abuja, Nigeria.

Wednesday 30 July 2014

HAVE IMF AND WB REACHED THEIR PEAK?

After World War II the world experienced economic change resulting from what came to be known as Marshal Plan thanks to its initiator Secretary of State George Catlett Marshall, Jr. (December 31, 1880 – October 16, 1959). Under Marshal Plan, America loaned Europe $ 13 bn to rebuild its economy that's destroyed by the war. Ever since, the world's nary turned back as far as economic survival is concerned.  He who pays the piper calls the tune. Those providing financial lifeline have become what one can call neo-colonialists. As it was Marshal Plan for Europe, the World Bank (WB) and International Monetary Fund (IMF) otherwise known as Bretton Woods Institutions, are the creatures of one person, John Maynard Keynes (5 June 1883 – 21 April 1946), which instead of helping the world to recover from economic doldrums; they cause mayhem to some poor countries. These two bodies, for long, have dictated almost every aspect of poor countries’ economies. Their stingy and tormenting policies left many poor countries suffering without having anywhere else to go. The difference between Marshal Plan and IMF and WB is that there were few strings attached to the loan that Europe received as opposed to many that poor countries have received.
Recently, there's born new international initiatives whose vision is likely to change the economic landscape of the world. This is none other than BRICS which is an ellipsis for Brazil Russia, India, China and South Africa. According to BRICS just ended conference, it decided to form its own Financial Institutions that’ll help member countries and other countries to get financial support whenever their economies face a slump. For the first time, Africa’s among the movers and shakers in this new kid on the block thanks to the presence of South Africa. If anything, something’s to be said. This move’s likely to help poor countries as it threatens the existence of IMF and WB whose strength’s always depended on exploiting poor countries to which they give loans with high interest rates not to mentions superimposed policies.
So, to do away from IMF and WB taking advantage of others, BRICS decided to form its own Development Bank with the capital of $50 bn plus Currency Pool with the same amount as its capital. Every member country'll contribute $ 10 bn and the Bank’s headquarters will be in Shanghai China.  The Currency poor aims at helping countries forestall short-term liquidity pressures.
Russia’s Foreign Minister said that BRICS members, while speaking against unilateral actions in the world economy and politics, are not seeking confrontation but propose working out collective approaches toward the resolution of any problems.
Many still wonder even doubt if BRICS will succeed in awkwarding longtime western Financial Institutions that, for many poor countries, have become another scalawag. Chances of success are obvious given that currently, BRICS countries have fast growing economies compared to western countries.
When she's asked if BRICS Development Bank aims at countering IMF and WB, Brazil’s president Dilma Rousseff had this to say, “It is a sign of the times, which demand reform of the IMF.” On his side Russia’s president, Vladimir Putin, hailed the Bank saying, it was “a very powerful way to prevent new economic difficulties.” Power indeed so much that it is going to scale down the power of Breton Woods Institutions. Putin got another source of influence after being kicked out of G8 due to his involvement in Ukraine crisis.
Also, the policy they've embarked on is likely to help them to get a lot of countries supporting this project. Hence, make it successful. So too, BRICS will learn from the mistake of the west especially financial liberalism that enabled some companies in the US to offer money to mortgage knowingly that those receiving the money were unable to pay thus causing credit crunch.
Shall BRICS meet its obligations and plans chances or ushering the end of IMF and WB are so high that the world may experience a new economic order just soon. This being the case, BRICS needs to avoid repeating the mistakes that the west made to find itself in this situation. Again, nothing’s for good. Time for capitalistic institutions even pillars to be phased out is coming. What BRICS needs to avoid for all costs is war. History shows that Europe, especially, Britain and Germany, lost the baton after being engaged in wars. So too, the US soon will lose its superpower crown due to being engaged in wars in Afghanistan and Iraq. Therefore, the creation of BRICS Development Bank and Currency Pool is just the beginning of many things in the pipeline.
In sum, given that BRICS Development Banks stands to help poor countries out of the tentacles of Bretton Woods Institutions, poor countries need to make use of this opportunity. Again, have IMF and WB reached their climax? Time soon will tell.
Source: Business Times July 28, 2014.

UKAWA wasibebeshwe zigo la Kikwete na CCM


          Kwa hali inayoendelea kuhusiana na majaliwa ya katiba mpya, kama busara haitatumika, yako mashakani. Kama ujanja ujanja, ubabaishaji, visingizio na urushi, kusukumiziana na kubebeshana lawana vinavyoendelea visipoachwa, kinachoonekana kama jitihada za kupata katiba mpya kitabakia kuwa kiini macho. Je nani alaumiwe kwa zengwe na mkwamo huu?
          Historia ya uandikaji katiba nchini inaanza pale rais Jakaya Kikwete alipounda Tume ya kukusanya maoni iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba. Tume hii ilipewa jukumu la kuandika kielelezo katiba (Draft constitution) ambacho kingejadiliwa na bunge la katiba (Constitutional Assembly) na kupitishwa kisha kupelekwa bungeni na kujadiliwa kama mswaada na hatimaye kupelekwa kwa rais kuusaini kuwa sheria. Mwanzoni, Kikwete, kabla ya kulishwa maneno na wahalifu fulani wenye woga kuwa katiba mpya ingefichua maovu yao, alikuwa kwenye mstari.
          Kama ilivyodaiwa mara nyingi bila kukanushwa na wahusika, inasemekana kuwa Kikwete aliitwa na watangulizi wake wakamtisha, wakamwongopea na kumshawishi hadi akaamua kuanza kujipinga na kuvuruga kazi njema iliyokuwa ikiendelea vizuri.  Hakika ni aibu.
          Mwanzoni Kikwete akiwaaminisha watanzania kuwa moja ya watakayomkumbuka kwayo ni kuwapatia katiba mpya itokanayo na wananchi na si watawala kama iliyopo.  Hata hivyo, tarehe 21/3/ 2014 itaingia kwenye vitabu vya historia ya Tanzania kama siku ya kiza ambapo Kikwete, kwa makusudi mazima na kinyume cha taratibu, alilihutubia bunge maalum baada ya jaji Warioba kufanya hivyo na kuamua kuvuruga kazi ya tume. Alichofanya Kikwete ni kuonyesha wazi mkengeuko uliojitokeza kwa kutoa msimamo wa chama chake. Heri angeishia hapo. Kwani, alikwenda mbele akaishambulia, kuizushia na kuidhalilisha tume aliyoiteua mwenyewe bila kulazimishwa wala kushawishiwa. Wengi walipigwa na butwaa na kujawa na simanzi wakijiuliza: Kulikoni, kipi kimemsibu rais? Tangu siku hiyo ya kiza Kikwete hakurudi nyuma. Ameendelea na mbinu za kichinichini kuhakikisha inaandikwa katiba aitakayo na si itakiwayo na wananchi.
          Hivi karibuni, Kikwete na CCM waligundua kuwa umma umestukia janja yao.  Hivyo, waliamua wakuwatwisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) lawama wanazopaswa kutwishwa CCM na Kikwete. Badala ya kukubali kuwa kitendo rais cha kumvizia jaji Warioba, kumshambulia, kutoa msimamo wa chama chake na kutokuwa tayari kukiri kuwa alikosea na kuomba msamaha, ndicho chanzo cha yote, wameanza kulalamikia UKAWA ili uonekane ndicho chanzo cha mkwamo wakati siyo. Je watanzania watakuwa wajinga na wasahaulifu kiasi hiki kukubali matusi ya nguoni kama haya? Je Kikwete na CCM watafanikiwa katika kutapatapa kwao hadi wakafikia kutoa vitisho kuwa kama UKAWA hawatarejea bungeni watabadili katiba waendele? Bahati nzuri, tofauti na Kikwete aliyetishwa na woga wa kuwajibishwa, UKAWA wameshikilia msimamo wao. Wamesema wazi hawako tayari kurejea bungeni na kujidhalilisha. Huu ni msimamo safi wa kupigiwa mfano unaoweza kusaidia kufanikisha mambo kadhaa muhimu.
          Mosi, kuinyima CCM fursa ya kuwatumia kuandika katiba chafu itakayoendeleza matakwa yake machafu.
Pili, kuzidi kuanika unafiki na kigeugeu cha Kikwete kiasi cha kumweka kwenye hatima ya kuweza kuachia ngazi akiwa na rekodi ya kuvuruga mchakato wa katiba mpya na kutumia vibaya fedha za umma na ofisi ya rais.
Tatu, umma kutopata katiba chafu na hivyo kuwa na hasira na wale waliozuia kupatikana kwa katiba wanayoitaka wenyewe iwatawale.
Nne, kuchochea hamu na hamasa ya kutaka katiba mpya baada ya Kikwete kuondoka ili itumike kufumua yote yaliyomsababishia kujipiga kujipinga asijue kesho hayo yatakuwa kichocheo cha kutekeleza kile alichotaka kukiepuka.
Tano, msimamo wa UKAWA utadhihirisha busara au ukosefu wa busara wa CCM na Kikwete kutokana na watakavyoamua kulimaliza tatizo hili. Baadhi ya wana CCM tena wasomi wa sheria kama Spika wa bunge maalum Samuel Sitta na waziri mkuu Mizengo Pinda wameishaonyesha uhovyo wao kwa kutishia eti kubadili sheria na kupitisha katiba chafu.
Sita, kuzidi kuichanganya CCM ikitaptatapa na kufichua ubovu zaidi ambao wananchi hasa upinzani unaweza kutumia kuunyesha umma wa wapiga kura jinsi ilivyoisha na kuishiwa.
Saba, CCM itazidi kuumbuka kwa hofu kuwa katiba isiyoitaka inaweza kupita. Hivyo, wahusika watatumia muda mwingi ima kujaribu kuficha madhambi yao au kutafuta nguvu ya kuendelea kuwa madarakani kwa gharama zozote. Hapa lazima tutegemee wizi wa fedha za umma kuongezeka kama tulivyoshuhudia wizi wa ESCROW hivi karibuni uliowachanganya CCM kiasi cha makada wao kujifichua walikokuwa wamejificha na kutaka kuzipiga bungeni.
Nane, mwitikio wa hovyo wa CCM utazidi kuwapa UKAWA hoja na hamasa ya kuhakikisha ufisadi huu wa kimawazo unakomeshwa.
Tisa. UKAWA watazidi kuona faida ya kuungana kama upinzani jambo ambalo wakiliendeleza hadi kwenye uchaguzi ni mwanzo wa kuizika CCM.
Mwisho, tutoa ushauri kuwa kadri CCM na Kikwete wanavyozidi kutumia mbinu za mwituni, wanazidi kufanya mambo kuwa magumu kwao.  Watumie busara ya kukubali kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu. Hivyo, hata wangewatishwa UKAWA lawama na zigo lao vipi, hawatafanikiwa kwa vile watanzania si majuha na mataahira kama wanavyowachukulia. Hakika, huu ni mwanzo wa mwisho wa CCM. UKAWA lazima wajue hili na kushikilia msimamo wao ili kuwaumbua wanafiki na mafisadi wanaotaka kuhujumu na kuzuia kupatikana kwa katiba mpya.
Chanzo: Tanzania Daima Julai, 2014.

Kijiwe chakaribishwa futari

 Baada ya kufuturisha kugeuzwa fasheni kiasi cha kukosa maana, juzi wana kijiwe walipata mwaliko kwa ajili ya kupata futari na stafutahi toka kampuni ya Fiction inayosifika kwa kukwepa kodi na kutoa huduma aghali na mbovu ili kuwaweka sawa kwa kutumia makulaji.
          Mwaliko huu ulizua utata, ubishi, kupishana hata lugha na nusu kushikana mikono sisi kwa sisi. Kabla ya kwenda au kutokwenda mjadala mkali ulizuka kiasi cha kuacha sintofahamu isiyo ya kawaida.
          Kanji ndiye aliyeleta mwaliko huu. Alianza kwa kusema, “Dugu zangu, iko furaha kubwa alike veve kwa futari kesho kutwa.”
          Mzee Maneno anajibu, “Ama kweli huu kweli mwezi mtukufu ambapo kila mwenye nazo hujitahidi kuwa mkarimu. Shehe Kanji twashukuru kwa mwaliko wako mwanana.”
          “Yakhe huwezi ongea kwa ajili yetu sote kana kwamba umetuuliza na kupata mawazo yetu kuhusiana na huu mwaliko wa futwari.” Mpemba anadakia akionekana kuudhika.
“Sasa veve karibisha jambo heri wakata siasa nini? Mimi ona hapana mtu kataa futari dugu yangu.” Kanji anamjibu Mpemba.
Mijjinga aliyekuwa ndiyo kamaliza kunong’ona na Kapende anakula mic, “Kanji hujamwelewa ami pale. Shida hapa si kukubali au kukataa bali kupata ridhaa . Kama mzee Maneno kishaamua kwenda basi ajisemee badala ya kutusemea wote au vipi?”
“Shehe Mpemba usemayo ni kwei. Mimi muumini ati. Siwezi kukubai kila mwaiko kwa vie nimeambiwa kuna futaai. Futai nyingine haziswihi ati. Hei niende kwetu Mashindei nikajichimbie viunga vya futai kuiko hii futai mauzauza.” Mgosi Machungi anaamua kumpa kampani Mijjinga.
Kapende naye hataki kuachwa nyuma kwenye mechi hii. Anakula mic, “Shehe Mgosi na Mpemba mna hoja tena yenye mashiko. Siku hizi kufuturisha imegeuka fasheni kiasi cha hata mafisadi, maafisa wa serikali hata marais na mabalozi kutumia fursa hii ima kujipigia kampeni au kuibia umma kwa kisingizio kufuturisha. Nani anataka futari ya kijambazi kama hii kama tutasema ukweli?”
Msomi aliyekuwa ndiyo anampa gazeti Mchunguliaji anachukua mic, “Wote mnaoshuku mialiko hii ya kinamna mna hoja kubwa sana. Hivi jiulize: Haya makampuni mabingwa wa kukwepa kodi, kulangua wachovu na kuwapa huduma mbovu yanafuturisha kweli au yanawageuza watu mabwege na kuwasanifu kwa kisingizio cha kufuturisha? Mbona wanaona wepesi kufuturisha lakini si kufunga angalau kukwepa kulipa kodi?”
Anakunywa kahawa yake na kuendelea, “Juzi kwenye gazeti la the News nilicheka sana nilipomuona mwana mama mmoja balozi kwenye nchi moja ya jirani akiwaalika mashehe kufuturu. Ajabu ya maajabu, mjivuni huyu pamoja na kujifanya kufuturisha, hakuvaa hata ushingi lau kuheshimu mila za wenzake. Ajabu ya mwaka, hata waalikwa walipwakia futari bila kuangalia kama ni halali au haramu.”
Mbwamwitu anaamua kuchomekea kabla ya Msomi kuendelea, “Kaka siku hizi haramu ni halali na halali ni haramu. Maendeleo ati. Huoni wezi wakubwa wanavyoandaa mifutari kibao na watu kuifakamia bila kuuliza. Sijui tunakwenda wapi yarabi?”
“Usemayo shehe ni kweli tupu. Hebu tuwe wakweli japo kwa nafsi zetu hata kama tuna shida. Hivi futari au msaada utokao kwa mafisadi na majambazi nayo ni futari au haramu? Juzi nimeshangaa nusu kukata roho niliposoma gazetini kuwa fisadi wa IpTL naye anatoa misaada ya kujenga vituo vya ndata na mahekalu. Sitashangaa kusikia mafisadi kama bwana Richmonduli, Kagoda na ANBEN wakifuturisha.” Anaongezea Msomi.
Mipawa hataki kuachwa nyuma. Anakwanyua mic, “Nyie mwashangaa hayo. Mbona nimeshashuhudia watu ambao njuluku zao zinatokana na biashara ya mihadarati, nguruwe na ulabu nao wakifuturisha?  Usishangae hata madada poa  sijui makaka poa nao wakafuturisha.”
Muishiwa Bwege anapoka mic, “Tukubaliane mabwana. Huku tunakoambiwa ni kufuturisha siyo bali hongo ya kibwege tu. Mbona wakati wa mzee Mchonga sikuwahi kumuona akiandaa futari patakatifu pa patakatifu kama hakuna namna? Hii imani na mapenzi vimetoka wapi kama si watu kutumia ujinga na umaskini wetu kutulisha haramu zao?”
“Yakhe mie siweziharibu swaumu yangu kwa kupwakia vitu haramu hata kama vyatolewa bure ati. Kidini, futari itokanayo na fwedha haramu nayo ni haramu pia. Hii ni fatwa natoa kama msomi wa dini wallahi.” Mpemba anazidi kuongeza utamu.
Kijiwe hakina mbavu jinsi Mpemba anavyotoa fatwa kijiweni.
Sofia Lion aka Kanungaembe aliyekuwa anaonyesha kukereka wazi anakamua mic, “Wahenga walisema kutoa ni moyo usambe ni utajiri. Kama hutaki kushiriki futari acha wenye kutaka wafuturu. Kwani unahukumu wewe Mungu? Ukimchunguza kuku alacho hutomla.” Anamgeukia Kanji na kusema, “Kaka Kanji wala usikatishwe tamaa na wale wanaotaka kufanya mambo rahisi kuwa magumu. Hebu twambie futari hii inafanyika wapi tukuunge mkono.”
Kabla ya Kanji kujibu Mbwamwitu anachomekea, “Je ustaadh Kanji hii futari italiwa jamatini au hotelini au tuseme baa?”


Kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga likaja kundi la watoto na vigoma vyao vya kuarika watu kwenye futari. Kila mmoja aliendelea kushangaa aina hii mpya ya dini. Tieni akilini msijeliwa mwajiona.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 30, 2014.

Monday 28 July 2014

Mkono wa Idd unapogeuka rushwa ya Idd!

Pichani ni mbunge wa Temeke (CCM) Abass Mtemvu akitoa box lenye zawadi za vikombe, vijiko. chupa ya chai na upuuzi mwingine kama mkono wa Idd. Unajiuliza, zawadi gani ina picha ya rais kama siyo rushwa ya Idd? Hata ukiangalia kinachoitwa zawadi ni udhalilishaji na umaskini mtupu. Viongozi wetu na wanasiasa wataacha lini kutukana dini kwa kuzitumia kisiasa?

Is Islamic Banking System the saviour of our economies?

          Unequal and exploitative economic relationship between rich and poor countries is one of the reasons that made African economies redundant and poor. Since they attained their independence, African countries have always depended on western mode of economy which has always exploited and dwarfed them. For instance, many African governments depend of loans from rich countries. These loans have always been offered after strings were attached on them. One of the major blows that make African economies dependent is the whole issues of high interest rates.
Apart from imposing high interest rates on the loans African countries secure from rich countries and International Financial Institutions (IFI), conditions on how to spend the loaned monies, are hard and exploitative. Take for instance; the conditions the World Bank (WB) and International Monetary Fund (IMF) levy on loaning countries.  These conditions are always changing to favour rich countries. In this piece we’ll briefly examine how Islamic Banking System may help African countries to do away from exploitation by IFIs.
Under Islamic Banking System, no interest rates (riba) are required to be paid at all. If anything, multinationals corporate and other international financials have kept the economies of poor countries in doldrums simply because they offer them conditional loans whose interest rates are exorbitantly higher. Such countries can do away from such exploitation by taking interest-free loans from Islamic banks all over the world.
If developed economies do somewhat depend and take loans and trade with Islamic Financial Institutions why not us? If poor countries would take long term loans from Islamic Banking Institutions chances are that their economies are likely to get a reprieve. Again, why have African countries become adamant of taking such helpful loans? Is it because there’re no kickbacks involved or just sheer ignorance and fear?
Islamic doctrine of trading is based on moral philosophy that regards riba as an evil thing. One academic once wrote, “Credit is a Human Right, the best of People are those who are most Beneficent to others, we should not rent money and we should not do business with socially irresponsible activities and entities (e.g. liquor Stores, unfair businesses, pornography, polluters and the like.).”
He goes on, “Making money on money without investing in a tangible asset may border on speculation and gambling. Money is a measuring device, it is a thing. The use of money cannot be rented.” Are our countries afraid of taking loans from Islamic Institutions because of being irresponsible in running the business of their countries? I wonder. Why Kenya, for instance, would take loans of billions of dollars from China to build a railway instead of taking it from Islamic Financial Institutions. If responsibility and morality are the conditions Islamic Banking Institutions offer, indeed, they're reasonable conditions to be met.
There are counterparts in almost all forms of Islamic banking in Western banking.  If anything, Islamic banking is verily, pushing the envelope as far as modern economics is concerned. IMF and WB have always exploited poor economies by levying many conditions on them pointlessly. They destroy the economies of poor countries under the pretext of helping them. Once things go awry, the same institutions blame poor countries while their conditions are the very cause of the failure.
Beware. While African countries are sweating about whether to take such safe money and do business, rich countries have nary bothered to worry. If you ask how Dubai was built and who built you’ll be told it is western companies. America doesn't worry to do business with Saudi Arabia. Why should we? To me, Islamic banking is safer and more reliable than Chinese cash offered easily without those receiving looking at strings attached to it especially high rates and long term impacts on their economies.
When Asian migrants took advantage of Islamic banking and prospered the US Today had this to say, “Islamic finance is booming worldwide, fueled by the windfall from sky-high oil prices and a return to a more strict interpretation of the holy Koran across the Islamic world.”
People or countries shouldn't be afraid of Islamic banking system especially interest-free loans. They’re likely to fear the conditions that the said money shouldn't be employed in things like alcohol gambling and charging interests. Again, there is another way of making profits out of such interest free loans as US Today says, “For instance, the German state of Saxony-Anhalt, which issued the first Islamic bond in 2004, sold government property to bond investors and then leased it back from them. The investors technically earned money from the rent, not interest.” This is obvious, especially, for mortgage. If, for instance, the country takes a loan from Islamic banks and builds a university or a hospital, it will make more money without breaking Islamic law, and it will benefit both sides namely the bank loaning and the country taking the loan.
Furthermore, there are top Islamic banks in America which contribute to the economy of the US. These are LARIBA- The American Islamic Finance House, University Bank, Harvard Islamic Finance Program, Guidance Financial Group, and samba. Do we have the same in Africa? Nope! Why?
Islamic financial institutions ‘contribution to the world economy can’t be gainsaid. In 2008 Islamic Financial Institution s had a humongous amount of money in assets as expressed, “Total assets of Islamic banks worldwide are estimated at about $250 billion, and are expected to grow by about 15 percent a year,” (Choong and Liu, 2006; Ainley and others, 2007). The figure skyrocketed within no time as observed, “It is estimated that the size of the Islamic banking industry at the global level was close to US$820 billion at end-2008,” (IFSB et al, 2010).
Suffice it to say that African countries have a future in Islamic Banking system. Thus, we need to change and take advantage of this economic friendly system.
Source: Business Times Friday, 11 July 2014 08:39.

Picha ya mwezi ya blog hii

Tulitoa picha hii katika maadhimisho ya ndoa yetu hapo Julai 18. Katika kuangalia picha za mwezi huu, tumeona tujipendelee angalau turejeshe picha hii kwa vile ilionekana kuwa picha nzuri ya mwezi huu.

Sunday 27 July 2014

What a generous-cum-religious hunk!

 
          I must say it clearly, loudly and openly before I jolt it down. I’m against the tendency that’s become an in-thing in our society whereby biggies, companies and who've duped boozers pretending they love them while they actually hate and use them.
To begin with, public figures have been in the forefront when it comes to generously and oft-preparing iftar for boozers. Such show-offs can be seen everywhere in the hunk especially at this time of holy Ramadan. It’s reached a stage at which even sinners do offer iftar.
Offering iftar isn't a crime or a bad thing if a person doing so is spending his legally-gotten dosh. When such a person misspends public or ill-gotten monies, it becomes a whole new ball game.
The other day I heard it with my two ears. One boozer who’d enjoyed the iftar prepared by Jake Kiquette saying that he’s molesting the office plus misappropriating their dosh! Kweli binadamu hawana shukrani. You ate his yummy food and still accuse him of fiddling your dosh!
 The boozer who happens to be my best friend who looked yum-yum after munching Jake’s gourmet, wanted to know where Mr. Big gets the dosh for preparing iftar for unwanted eaters like boozers who observe no religion except kanywaji.  The boozer went on saying, “I think apart from promoting his religion, he uses this opportunity to bribe religious leaders.” To prove his point that this is a conduit for some biggies to bribe poor wananchi, the boozer said, “You can now see how companies are spending millions in this business of offering iftar. Muslims do not need this iftar given that when they fast they do so knowingly how they're capable of getting iftar legally. I'd like to know where Jake gets this money he squanders on iftar every year. Mzee Mchonga’d nary squandered our dosh in such hoo-ha.”
Given that I love Jake, I wanted to teach this guy a lesson save that given that he’s my best buddy, I found myself between a rock and a hard place. I, thus, decided to jolt this down so that others can muse on it.
I somewhat wonder to evidence companies known for swindling our dosh preparing iftar for boozers. If you truly love us why don’t you stop stealing our dosh or avoiding paying tax? The other day I saw IpTL guy donating monies to churches and police stations. Wow! If you truly love us why then have you stolen our ESCROW dosh?  Astonishingly, those institutions to which this dirty dosh is donated do keep mum. They don’t want to query the cleanliness of the dosh. Ukimchunguza kuku ati.  We all know how IpTL, for instance, has destroyed our lives for over ten years of its theft and illegal biz. We've borne the blunt of its dirty biz as we evidenced the death of our Tanesco not to mention power cut and power hike. Let’s face it. Don’t those who receive such dirty dosh condone theft in the first place? Baniani mbaya!
What’s more, history shows that fisadis and thieves like to use our institutions especially religious ones.  Who has easily forgotten how one mega thief used one Kinondoni church to clean his dosh? Wonder not to find that those whose dosh is made by means of selling pork, alcohol even drugs preparing iftar. Is this iftar really? Dosh cleaning using paupers and their hyena-like institutions has become an in-thing. Many tainted politicos use this loophole to even bribe and dupe voters. I still remember my friend Eddie Luwasha who throws dosh to every organization to see to it that he wins support from them come next general elections. I recently witnessed one son of big offer a lot of mattresses to some schools as he prepared his way back to ulaji.
Methinks. Our boozers need services and means of making them live respectable lives instead of depending on handouts by those who rob them and their hunk. The sage’s it that blessed is the hand that giveth than the one that taketh. Is there anybody who doesn't want blessings? Why’d blessings and power go to the same kit and caboodle of swindlers? Why should boozers give their blessings to criminals and sinners? Aren't themselves sinners as well for accepting dirty dosh?
Though generous as we might think and daydream we’re, slowly and systematically, we’re becoming nchi ya kitu kidogo. Like rats, we’re falling in the trap because of just small things like a groundnut that ends up costing the rat its dear life. Again, we’re bin-Adams. We’re supposed to use our heads in lieu of our stomachs.
Guess what. The other day I heard that Mr. Richmonduli is preparing iftar for boozers. If you ask him of his religion he’ll answer, “Graft and dosh.” How can such a creature know God at all? Who is fooling who in this megalomaniac generosity next to suicide for hoi polloi?
Source:ThisDay

"Shehe" Peter Kayanza Mizengo Pinda aandaa futari akimbia swalat!

Waziri mkuu Mizengo Pinda akifurahi na wasanii
Rais Kikwete akiwasili kwenye makazi ya Pinda
Wala pilau wakiswali baada ya futari aliyoandaa Pinda.

Waziri mkuu Mizengo Pinda akifurahi na wasanii waliokuja kula futari kwake ambayo ilihudhriwa pia na shehe mkuu mufti Shabaan Simba na rais Jakaya Kikwete. Pinda amesaidia kufumbua kitendawili kuwa hizi futari tunazoona si futari chochote bali usanii. Futari gani inaandaliwa na mtu asiye wa dini ile? Mbona huko nyuma hatukuwahi kuyaona haya au uislam nao umebadilika?

Friday 25 July 2014

Seriously, Mlevi kugombea urais

Baada ya kila msaka tonge kutangaza nia ya kugombea urais ambao unaanza kugeuka urahisi yaani ulaji rahisi, mlevi japo alishabainisha kuwa anaweza akatia timu, sasa anatangaza rasmi kuwa atagombea urais. 
Kwanini nisigombee iwapo naona watu wanaotegemea majina makubwa ya wazazi wao na umri mdogo unaoonyesha ukosefu wa uzoefu kuwania urais? 
 Kwanini nisitangaze iwapo urais umegeuzwa urahisi tena wa kuhomola na kuibia kaya? Kwanini asigombee iwapo urais ni kijiko cha kuchumia utajiri wa haraka kwa rais na ukoo na marafiki zake? 
Mlevi anapanga kufanya yafuatayo ili kuikomboa kaya toka kwenye mikono na midomo ya mafwisadi na mafisi. 
Mosi, atakuza uchumi kwa kutosafiri nje kwa vile ameishi nje sana. Hivyo, si mshamba wa pipa wala wa miji mbali mbali duniani. Nitapiga marufuku hata mawaziri wangu kupoteza fedha na muda kwenye uzururaji usio na tija kwa taifa. 
Wasaka’ per diem’ jiandaeni. Lazima niwashukie kama mwewe ashukiavyo vifaranga. Pia nitahakikisha najenga uchumi wa kizalendo unaotoa kipaumbele kwa wazawa katika uwekezaji badala ya huu uliopo ambao unapendelea wageni ukiwakomoa wazawa kutokana na kuwa wagumu kutoa ten percent. 
 Nani anataka uchumi unaoendeshwa na magabacholi kumi tu? Nitahakikisha najenga uchumi wa kutumainiwa badala ya uchuuzi na ufisadi unaoendelea ambapo kaya inasifika kwa kuwa na rasilimali nyingi lakini bado inaombaomba na kukopakopa kichizi. 
Pili, vitegemezi vyangu wala mke wangu hawataruhusiwa kujihusisha na siasa nikiwa madarakani. Hata hivyo, vilishasoma na kupata kazi vinavyoridhika nazo ughaibuni.  
Hivyo, msitegemee kuona wanangu wakijifanya marais wadogo wala mke wangu kujifanya rais wa kike kwa vile mumewe ni rais. 
Wakifanya hivyo nasweka ndani bila kuwatazama usoni. Ukitaka kuua nyani..? Nitatawala kama Mchonga kwa kuhakikisha urais haugeuki mali ya ukoo wala marafiki. 
 Urais wangu hautakuwa wa ubia kama wale waliosema kuwa urais wao si wa ubia wakimaanisha kinyume.  Kuepuka kujichanganya, lazima nitangaze mali zangu kila mwaka tena bila kukumbushwa wala kutafuta visingizio. Kutotangaza mali kwa kiongozi kama rais ni ushahidi kuwa ni mkwapuzi wa kunuka. 
Tatu, Bi mkubwa wake ni msomi wa kupigiwa mfano aliyesoma na Michelle Obama. Hivyo, hataanzisha NGO wala kugombea vyeo vidogo vidogo kwenye chama cha mlevi. Hata hivyo, nitaamuru katiba itamke wazi kuwa hakuna cha mke wala nani wa rais kutumia ofisi yake kwa namna yoyote kutengeneza njuluku. Enzi za akina Anna Tamaa na Shari zimepita. 
Nne, Mlevi ni msomi wa kupigiwa mfano ambaye hataingizwa mjini na vyuo vya kitapeli kwa kumpa shahada za uongo na ukweli halafu vije kumtembelea ili kumtoa upepo kama tulivyoshuhudia chuo kimoja cha kwa Joji Kichaka kikifanya. 
Tano, sera za mlevi ni usawa. Ndiyo maana analaani wale wanaotaka kutumia kete ya umri, jinsia, dini, maeneo ya bara au visiwani, mitandao uchwara, kujuana, kuhonga na jinai nyingine kutafuta urais. 
 Nichukue fursa hii kuwatahadharisha walevi na wapika kula. Yeyote mtakayemuona anakuja na sera za kibaguzi muogopeni kuliko ukoma. Hata kama hana mpango wa kugombea kwa sasa akijiandalia kugombea baadaye, muwekeni kwenye maweko ya kumbukumbu zenu na kuhakikisha hachaguliwi hata baada ya miaka 50. Ubaguzi ni ukaburu na anayeufanya ni kaburu mweusi anayepaswa kuzomewa hata na kunguru na wadudu. 
Sita,  kwangu urais ni utumishi wa umma na si njia yake na familia yake na marafiki zake kuuibia na kuunyonya umma kama ilivyo. 
Saba, lazima niweke wazi. Sigombei kwa vile eti kuna watu wanataka nigombee kama waongo wengi wanavyosema. Nagombea kwa vile nautaka urais ili niisafishe kaya kutoka kwenye uchafu huu na uroho wa watu kula kwa mikono na miguu tena bila kunawa wala kuomba. Ukisikia mtu anasema eti ameambiwa na watu agombee jua mbea na muongo wa kupaswa kupigwa mawe hadi kufa. 
Nane, nagombea urais si kwa kutegemea mitandao ya bibi wala babu yangu. Wala sitegemei ukubwa wa jina la wazee wangu ambao bahati nzuri ni marehemu ambao walikuwa malofa wa kawaida. Nagombea kwa vile naamini walevi wanajua vitu vyangu na lazima wavikubali kwa ajili ya ukombozi wao. Mimi ndiye yule aliyetabiriwa na manabii kuwa atatokea rais ambaye hamkumtegemea na atawaweka huru. 
Tisa, kampeni zangu zitakuwa za uwazi na ukweli kwa maana kwamba walevi wasitegemee kuhongwa kanywaji kanga wala mabulungutu ya njuluku. Huku ni kuwanunua. Watakaowapa vitu kama hivyo wale na kuwaadhibu kwa kuwanyima kura.  
Kwani watu wa namna hii wanatafuta kura ya kula si kura ya kuwakomboa walevi.
Kumi,nitakamata na kusweka ndani wale wote waliouza kaya kwa wachukuaji kuanzia wale waliochukuwa Kiwila, IpTL, Richmonduli, Gesi, Tanesco, Net Group Problem, NBC, EPA, Kagodamn, Meremetuka, Mwananchi gold, SUKITA na ujambazi mwingine mwingi. 
Kumi na moja, nitahakikisha nawapa katiba mpya na safi ambayo itahakikisha kila jiwe linafunuliwa tangu kaya ipate uhuru kuhusiana na ufisadi. Hivyo, wanaozuia katiba mpya kuandikwa watakuwa wanapteza muda na kujipalia mkaa kama nitapata kuchaguliwa kuwa rais. 
Kumi na mbili, nitahakikisha urais unarejea kuwa urais badala ya kuwa urahisi kama ilivyo sasa ambapo unavutia majambazi na mafisi na mafisadi wengi ili wawaibieni wapendwa walevi wote.
Kwahereni tukutane nikianza kampeni!
CHANZO: NIPASHE 

Thursday 24 July 2014

Futari au aina mpya ya hongo na ufisadi?


Kumezuka utamaduni wa kutumia vibaya fedha za umma kwa maslahi binafsi. Siku hizi ni fasheni kwa viongozi hasa marais, mabalozi, makampuni hata mashirika kufuturisha. Je hii ni futari au hongo na matumizi mabaya ya fedha za umma? Kwa mfano rais anapata wapi fuko la kufuturisha mikoa karibu yote huku mabalozi nao wakifanya hivyo? Ajabu hata makampuni yanayosifika kwa kukwepa kodi na kutoa huduma mbovu kama vile ya simu nayo yanafuturisha! Inatia kinyaa kuona makampuni kama vile ya kuuza ulevi na upuuzi mwingine eti nayo yanafuturisha. Je tatizo hapa ni njaa au ujinga wa watu wetu? Yaani tumegeuzwa taifa la njaa lenye kuweza kufakamia kila upuuzi hata bila kuuliza kama ni halali au haramu?

Wednesday 23 July 2014

Kutupwa viungo vya waswahili ingekuwa India waswahili wakafanya hivyo ingekuwaje?

Makamu Mkuu wa Chuo cha International Medical and Technological University (IMTU), Profesa PV Prabhak Rao (mwenye koti la blue)  na viongozi wengine wakisindikizwa na polisi kuingia kwenye Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam jana, kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na upatikanaji wa viungo vya binadamu eneo la Mpigi Bunju. Picha na Rafael Lubava
Tukio la chuo chenye kutia shaka cha International Medical and Technological University IMTU cha Dar es salaam kuhusika na kashfa ya kutupa miili na viungo vya binadamu kwenye bonde la Mpiji  limeniachia maswali mengi mojawapo yakiwa: Je miili hiyo ingekuwa imetupwa nchini India na Chuo Kikuu cha Kiafrika hali ingekuwaje? Bila shaka moto ungewaka na wahusika huenda wangekuwa marehemu. Je kwanini chuo cha kihindi kitupe miili ya waswahili kama ya mbwa na hali iendelee kuwa shwari? Je nini mantiki ya kuwa na serikali ambayo inaonekana kuwa mfukoni mwa watu hawa ambao Idd Simba waziri wa zamani wa Biashara na Viwanda alisema wahindi kumi tu wanamilki uchumi wa Tanzania?
Hawa jamaa pamoja na ubaguzi na ufisadi wao wa wazi wazi wameendelea kututendea ukaburu huku tukichekelea kana kwamba sisi ni jamii ya nyani? Je akitokea kiongozi mwingine kama Mtikila akakumbushia yote haya kuanzia ujambazi wa Chavda, EPA, Rada, Ndege ya rais, ESCROW, ubaguzi majumbani na sasa kutupa maiti zetu kama mbwa hali itakuwaje? TAFAKARINI KWA KINA. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

Tuesday 22 July 2014

Did you know traffic jams kill?



        All those residing in Dar-si-salama (haven is no longer safe) that used to be Dar es Salaam or the haven of peace know what I’m trying to say. I recently spoke with a friend whose name is top secret.  Hot under the collar, the guy was complaining on the phone due to unnecessary traffic jam. This guy who lives in Tabata told me that his car and heart are worn out not just because he uses them roughly. Nay, pointed a finger on traffic jams. The day the vice president of China came to the hunk the guy spent over three hour on traffic jams. The other day the minister without head or tail nearly killed this gent when the roads at Mwenge were closed to let this spineless big pass.
Agonizing, sweating, swearing and marooned in his car, the guy told me of his predicament.  I asked him if those closing roads pay more taxes than those they crucified in jams. For my dismay, the guy told me that those guys don’t pay tax.  Instead, they even rob the same tax collected from paupers and boozers. I frowned, what? He said that this is the real situation whether I liked or hated it. Wow! I said sarcastically. If it were in Canada, such better than thou egoistic creatures would be kicked out of public offices mercilessly.
Jokes aside, did you know that traffic jams are ones of the reasons that send many people to grave early? If you don’t know you know now. How can one avoid this agent of early deaths? There are two sure solutions namely to boot those causing traffic jams or pretend that they don’t exist. You know what? These guys close roads so that they can pass speedily in order to avoid dying of heart attacks resulting from traffic jams which essentially cook you alive. I’m trying to imagine. How does it feel to be in a dala dala for hours in burning Dar? Methinks. This is no other than being baked alive so to speak. Shall our boozer use their brains well; such a situation would create mayhem for those torturing them so as to be too hot to handle. Thus, do the right thing, to stop traffic jams.
Again, when you’re baked alive so as to become an easy target of heart attacks, those baking you don’t care. For, they bake you to avoid being baked. Bake them. They’ll become responsible. Normally, they turn you into their beasts of burden pointlessly. To make these filthy rich beggars care, you need to bake them too so that they can experience what you experience. Heart attacks aside, I know Swahili ladies. When you come home late after such torturous traffic jams, brace yourself for the hot seat at home. From hot dala dala to hot seat! Wow! What a crisis!
Traffic jams kill both those at home and those at work. For, once one is late chances are some tend to worry not only about coming late but also about vibaka, vyangudoa, vyangupaka, wakware and whatnot. Again, there are those who take advantage of the situation to do their monkey biz such as visiting short time guest houses.  I know girls and boys, even men and women, who come home late after having an affair. Yet they blame everything on traffic jams. Such moves are deplorable and dangerous. So, be careful folks. Stick on the one you vowed to live with especially those whose moral laws obligate. Miwaya itawamaliza bure.
What’s nary crossed my mind is the rationale we use to embark on such loss-making show-offs. Does it mean that those ngurumbili who like to be escorted with convoy of unwanted motorcade don’t know this? First of all, apart from exploiting the paupers, they anger them. Secondly, they cause environmental pollution not to mention making our begging hunk poorer and poorer. They spend much money and time in begging while they actually can change their behaviour and make more dosh than the one they degrade themselves for. Again, who cares if their pop once said that if you see such traffic jams note that the economy’s grown? For, it can allow everybody to buy mkangafu and clog our narrow roads. If such a backward-looking thinking is the modus operandi on the top, what do you expect from such cold blooded sociopaths hidden behind power? With such creatures on helm the hunk is dead in the water.
What makes every observer sick is the fact that, despite all such brutality, nothing up and coming has ever seen coming out of suffering boozers. Beware. Make no mistake. Traffic jams kill!
Source: The Guardian.

January Makamba na falsafa ya ujana katika chama kizee

BAADA ya January Makamba kulianzisha akaungwa mkono na Jaji Joseph Warioba kuwa rais ajaye lazima awe kijana, wengi tumejiuliza mantiki ya vijana kutaka kuingia madarakani kwa kutumia chama kizee. Kwanini isiwe shehe mpya kanzu mpya?
Hivyo, bila kuzungusha, kitendo cha Makamba na wengine wenye mawazo na mipango kama yake kutaka kutumia vyama vizee kinawatoa kwenye ulingo hata kabla hawajaingia.
Huu ni ushahidi kuwa hawana maandalizi wala sera na mipango ya maana yoyote. Baya zaidi, kinachowapiga chenga ni ile hali ya kujifananisha na Rais Barack Obama wa Marekani ambaye hakuingia kwa ujana bali umakini na mchango wake katika chama chake na taifa lake.
Hata kauli ya Obama ya ‘Yes, We Can’ ilijengwa kwenye ‘Hope and Change’ yaani matumaini na mabadiliko. Obama alijikita katika kujenga hoja zinazoingia akilini na kuzitetea na zikaeleweka.
Mfano, aliahidi kurejesha majeshi ya Marekani kutoka Iraq jambo ambalo liliwavutia wapiga kura wengi waliokuwa wamechoka na utawala wa mtoto wa kigogo George Bush ambaye hana tofauti na January Makamba. Hivyo, kudai kuwa Obama aliingia kwa kete ya ujana ni upotoshaji na uongo wa makusudi. Hii si tabia ya kisomi.
Pia ifahamike, kudandia ujana ni ukosefu wa sera. Watanzania wanahitaji sera na mawazo mbadala hata yakitolewa na mzee wa miaka elfu moja. Nani anajali kama wewe ni kijana?
Hii inatukumbusha maneno ya baba wa taifa, Mwl. Julius Nyerere alipoambiwa eti Jakaya Kikwete alikuwa na sura nzuri. Alijibu tena kwa kukereka; “Kwani tunatafuta mchumba?” Sambamba na hili la kina Makamba, “kwani tunatafuta mchezaji mpira au rais?”
Pia kina Makamba wanapaswa kufahamu kuwa hao wazee wanaowaponda walikuwa vijana waliotumia ujana wao kujiandalia wanachotaka. Na isitoshe, ni hao hao wazee waliowazaa na kuwaandaa kina Makamba wanaojisahau hadi kuwabagua hao hao waliowaumba kimwili na kisiasa.
Ajabu vijana hao hao waliopendelewa na kubebwa kwa kutumia nyadhifa za wazee wao ndio wanaoanza ubaguzi.
Japo ni kweli tunahitaji uongozi mpya wenye sera na mawazo na staili mpya ya kufanya mambo, lakini hautokani na ujana bali sifa zaidi ya hiyo.
Makamba hawezi kuwa makini. Kama yuko makini, basi uwezo wake wa kufikiri unatia shaka. Huwezi kutaka mambo mapya kwa kutumia chama kizee kilichochoka na kuishiwa dira.
Ukiachia ujana, Makamba na wenye mawazo ya kibaguzi kama yake wana nini kipya zaidi ya utimbakwiri? Makamba amebebwa na jina la baba yake. Ndiyo sifa pekee iliyomfikisha hapo alipo.
Makamba kujilinganisha na Obama ni tusi la nguoni. Obama hakubebwa na baba yake wala vigogo kama anavyofanya yeye. Nadhani kama kuna matusi CCM imewahi kutukanwa mojawapo ni hili la Makamba kutaka urais kupitia mgongo wa ubaguzi na kubebwa na marafiki wa baba yake.
Kimsingi, akichaguliwa atakayekuwa akiongoza nchi ni Yusuf Makamba na si January Makamba. Nani anataka George Bush Jr Tanzania ambaye anaweza kuendeshwa kama Joyce Wowowo (Kikaragosi) na kina Donald Rumsfeld wa Kitanzania?
Taifa letu halijafilisika kifikra na kisiasa kiasi hiki. Eti anasema wana mazoea mapya, fikra mpya na maarifa mapya. Si kweli. Kama wana mawazo mapya basi ni ya kutumiwa na kujificha nyuma ya ubaguzi wa kiumri na majina ya wazazi wao. Makamba na wenzake ni wa kuogopwa kuliko hata ukoma.
Mbona haongelei uzoefu ili walau tumlinganishe na Obama ambaye alikuwa na uzoefu wa muda mrefu akilinganishwa na Makamba anayetaka kumtumia kutuingiza mkenge? Makamba anaweza kusema ana maarifa mapya. Je ameyapata kihalali? Mbona hataki kuongelea kutuhumiwa kughushi kuingia kidato cha tano?
Waziri mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, aliwahi kusema; ”Kuna vijana wenye mawazo ya kizee na wazee wenye mawazo mapya.” Hivyo, ujana tu si kigezo tosha wala cha kutuhangaisha kumsaka rais.
Tuna vijana wengi kwenye viwanja vyetu vya ndege wanaoruhusu mihadarati kupita na kuingia. Je, hawa ujana na maarifa yao ya jinai vinalisaidia nini taifa? Nadhani kwa sasa ukitaka kukosana na Watanzania, uje na ndoto na ngonjera za upya.
Jakaya Kikwete aliingia na gea hii hii ya ujana japo alikuwa mtu mzima na falsafa ya Ari mpya, Kasi Mpya, Nguvu mpya vyote vikiashiria ujana, lakini baada ya kuingia madarakani alivurunda kuliko wazee kama Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa ambao nao walivurunda, lakini ikilinganishwa na Kikwete wana nafuu.
Nani anataka fikra mpya za kifisadi, kasi mpya ya kuingia madarakani kutuibia na nguvu mpya ya kutegemea majina na mitandao ya wazazi? Si kwa sasa ambapo taifa letu limezamishwa kwenye umaskini na uongozi wa kujuana na kufadhiliana. Hatuhitaji rais atokanaye na ubaguzi uwe wa umri au jinsia.
Makamba na wasaka tonge wenzake wanajua wanachofanya wanapoongelea ujana na upya bila kuweka uzoefu. Wanashindwa kuelewa mazingira ya Tanzania ambapo mtu anapoomba kazi, mojawapo ya sifa anazotakiwa kuwa nazo ni angalau uzoefu na si upya wala ujana na ndoto zake.
Tulishaambiwa na wahenga kuwa ujana ni maji ya moto. Leo Makamba ana miaka 40. Mwakani atakuwa na miaka 41 ambayo inamtoa kwenye kundi la vijana na kumuingiza kwenye uzee. Makamba anaongelea ujana bila hata kufikiri kuwa anaweza akatokea kijana wa miaka 30 akamwambia, “mzee January hebu tuachie sie vijana” akaishia kukaangwa kwa dhambi hii hii anayoianzisha kwa tamaa ya ulaji. Ni kichekesho cha aina yake kijana kukana uzee akategemea kutumia chama kizee!
Chanzo:Tanzania Daima Julai 23, 2014.