The Chant of Savant

Wednesday 21 August 2013

Mama anapopenda pesa kuliko watoto wake!

Tulizoea kusikia watoto wakiua wazazi wao ili kurithi mali zao hata ndugu kwa ndugu kutoana roho wakigombea urithi. Mama mmoja nchini Afrika Kusini aliicha dunia kinywa wazi alipotafuta muuaji ili awafutilie mbali watoto wake. Mama huyu mroho na mwenye roho mbaya alitaka watoto wake wawili wa kiume wauawe ili adai fidia toka kwenye kampuni ya Bima. Pesa inatupeleka wapi jamani? Je ni wazazi wangapi walioingia ibada ya mali hadi wakawa kuwatoa kafara watoto wao ili wapate utajiri? Je watoto wa mama huyu wakiamua iwe jicho kwa jicho nani atamlaumu nani? Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

No comments: