The Chant of Savant

Tuesday 14 May 2013

Hatimaye nimepata video ya MPIGS wa Kenya yaani wabunge!

Je wabunge wanaolala bungeni, kutukana, kukwepa vikao, kuongopa, kwenda kwa ajili ya sitting allowance siyo ma MPIGS? Je wabunge waliotumia vyeo vyao kuhongwa na wawekezaji hadi kupata pesa za kuficha Jersey Island na kuanzisha wizi kama EPA, Kagodamn, Dowans, IPTL, Songas, Meremeta na mwingine si ma MPIGS? Je wabunge walioingia bungeni kupitia uchakachuaji na wizi wa kura ukiachia mbali rushwa wakisaka rushwa na kutumia ubunge kama mtaji wa kujitajirisha si ma MPIGS? Sitashangaa kusikia siku moja kuwa kuna PIG President kama PIG anawakilisha uchafu uroho ulafi na kutoridhika. Je watoto wa wakubw wanaotumia madaraka ya wazazi wao siyo PIGLETS au vitoto vya nguruwe? Je nguruwe aweza kuazaa kondoo? Naomba tutafakari pamoja hasa kwa kufanya kile ambacho kitaalamu huita contents analysis based on Ethos and logos but not pathos. Karibuni nyote tutafakari kwa pamoja na kwa busara na akili kwa ajili ya kutafuta jinsi ya kulikomboa taifa letu after it went to the dogs.
Dokezo: Wale wanaokerwa na mawazo yangu wanisamehe kwa vile naamini nimeumbwa na kupewa ubongo na vipawa ili nifikiri hasa kwa ajili ya ukombozi wangu binafsi na kuibadili dunia yangu na wenzangu pale ninapoweza. Hiyo ndiyo falsafa yangu binafsi niiwekayo kwenye matendo au hadharani.

No comments: