The Chant of Savant

Thursday 23 August 2012

Kuna watu wana hasira waking'atwa na nyoka huwang'ata nyoka pia!



Jamaa mmoja nchini Nepali ametoa kali baada ya kung'atwa na nyoka aina ya Cobra. Baada ya kung'atwa jamaa alipandisha hasira na kumfukuza nyoka hadi kumkamata. Wajua alifanya nini baada ya kumkamata nyoka? Jamaa alimng'ata nyoka hadi kumuua. Hiki ni kituko si cha kawaida. Maana tumezoea kusikia mtu aking'atwa na nyoka na mwenye kung'atwa kumpiga nyoka na kumuua lakini si kumng'ata kama ilivyotokea kwenye kisa hiki. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: