The Chant of Savant

Thursday 28 June 2012

Urafiki wa mashaka Pinda, Kikwete na Ulimboka




Wanasiasa wetu hawana tofauti na matapeli wengine wa kawaida. Ukiwaona hapa waziri mkuu Mizengo Pinda na Dk Steven Ulimboka utadhani kicheko cha Pinda hakifichi chuki na kiasasi cha ajabu. Kwa wanaokumbuka maneno ya Pinda, ni kwamba kama binadamu wangejua kutabiri wanachofikiria wenzao, Dk Ulimboka asingefikwa na yaliyomfika. Pinda alikaririwa siku za hivi karibuni akisema kuwa lolote laweza kumtokea Ulimboka. Je alijuaje kama siyo tamko na mkono wa serikali? Ama kweli sasa Tanzania inatawaliwa na serikali ya kihuni. Bila watawala wetu kuja na melezo ya kutosha hawataeleweka. Kikwete liko wapi tamko lako?

No comments: