The Chant of Savant

Thursday 7 June 2012

Kurithisha urais kwa wake kwaanza kuwa fasheni Afrika

Nana Konadu Rawlings with her husband. Photo | GOOGLE IMAGESKuna taarifa kuwa rais wa zamani wa Ghana Jerry Rawlings ana mpango wa kumuunga mkono mkewe  Nana Konadu Agyeman Rawlings (pichani) kugombea urais kwenye uchaguzi ujao nchini Ghana. Habari za rais wa Uganda Yoweri Museveni kutaka kurithiwa na mkewe si uvumi tena. Je huu mchezo wa kuanza kufanya urais kuwa mali ya familia unaanza kuwa fasheni kwa watawala wa kiafrika hasa wale wasiopenda kuacha madaraka kutokana na madhambi waliyotenda? Rawlings, tofauti na Museveni,  aliacha madaraka muda mrefu na hakabiliwi na tuhuma zozote za uabadhirifu na kama zipo bado serikali haijazishughulikia. Rawlings hata hivyo, hatumii mbinu chafu kama Museveni. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa..

1 comment:

Anonymous said...

Hata wewe ungelifanya hayo hayo