The Chant of Savant

Sunday 27 May 2012

Waswahili kwa kuigiza na utumwa wa kiakili!

The leader of Boko Haram Abubakar Shekau
Huyo hapo juu ni kiongozi wa kikundi cha kigaidi cha Boko Haram cha Nigeria, Abubakar Shekau akiwa na bunduki zake. Ukiangalia gaidi huyu uchwara anavyojiweka utaona moja kwa moja kuwa anamuigiza Osama bin Laden asijue kuwa mwisho wake si mzuri. Kijana huyu amejiingiza kwenye utumwa wa kiakili na kuhatarisha maisha yake akidai anapigania Mungu na dini. Tangu lini Mungu mwenye nguvu kuliko yeyote na vyovyote chini ya ardhi akawa dhaifu kiasi cha kupiganiwa na kiumbe dhaifu kama huyu na wenzake wenye mawazo mfu kama yake? Waafrika kwa kupenda kuigiza upuuzi, hakuna mfano. Watu wanashindwa kuigiza vitu vya maana ambavyo vingewakomboa wao na jamii zao wanaigiza upuuzi! Kwa habari zaidi BONYEZA hapa na HAPA ambapo limbukeni wa kiswahili eti wanataka kuanzisha serikali ya kiislamu kule Mali.

No comments: