The Chant of Savant

Thursday 24 May 2012

Tanzania nchi ya 'madudu'





Taarifa zinazoendelea kupamba kurasa nyingi za vyombo vya habari ni uoza wa ajabu uliogundulika katika idara mbali mbali zikiongozwa na Maliasili na Utalii. Ukiachia mbali waziri wake aliyetimuliwa, Hezekiel Maige, tunasikia na vigogo wa mikoa ni matajiri wa kutupwa.
Bahati mbaya sana tatizo siyo Maliasili na Utalii bali nchi nzima. Ukienda TRA madudu.
Nenda Uhamiaji, madudu, Mambo ya Ndani, Madudu, Ikulu Madudu. Kweli Tanzania ni nchi ya madudu. Maana hakuna mwenye nafuu kuanzia watawala hadi watawaliwa. Kwanini tunashindwa kuwawajibisha watawala mafisadi? Simpo, tunatamani kushika nafasi zao nasi tukafanya ufisadi.

No comments: