The Chant of Savant

Wednesday 29 February 2012

Africa Needs to Sign a New Social Contract

Jean Russeau wrote in Social Contract, “Man is born free and everywhere he is in chains.” To free himself, Russeau suggests that man must gain security and measure of freedom from action in exchange for surrender of rights and property to the general will. This is not the language of compliance or cowardice but of rebellion.


It is no exaggeration to assert that Africa, politically, socially and economically is in the 14th century. Many African countries are sitting on the vast resources which are abused by a cabal of people in power. While this is happening, the big population is dying in abject destitution.


When philosophers Thomas Donaldson and Thomas W. Dunfee coined a phrase, “Intergrated Social Contract Theory” (ISCT), they stated categorically that every right an individual enjoys also has corresponding duty. In business, this is sharing risk and reward. Whenever there is a risk, change, calamity or needs, the corporate as a big entity benefiting more from the business must help employees - who also benefit from the business but at a less magnitude comparably - in this period of transition.


Running a country is like running a corporation. The difference though is that the corporation employs a person because he/she has some qualities or qualifications the corporation needs to use to make profit and sustain it. When it comes to be a citizen in the corporate known as a state, the citizen qualifies by the right of birth or application for those who apply for citizenship of other countries. When it comes to men and women manning Africa, they enjoy rights of spending poor taxpayers’ money as they deem fit without the corresponding duty of delivering service.


The corporate-government is duty bound to deliver so as to enjoy the right of being a government. This is where the situation in African countries worsens more than even under colonialism in 1960s. If anything, Africa needs a jumping-off point from the 14th century style of management next to Caesars’, to the 21st century of responsible presidents or managers of the corporation known as state. It is high time for Africa to have responsible and accountable leadership championed by our academics.


We need advocates of a new social contract who can decisively interpret and champion ISCT. This will be possible if our academics will stand and take on dirty regimes instead of joining them to plunder the hoi polloi as it currently is in many countries. It is no longer shocking to see African ignorant rulers using academics in their governments to destroy their country as it once happened in the Gambia where President Yahya Jammeh used the minister of health who is a doctor professionally to claim he had discovered a cure for HIV/AIDS. Under the new social contract, this wouldn’t be possible given that presidents would be accountable for their word and deed.


Our rulers are prone and proud of being referred to as Excellencies and other fake homilies. They live in the heaven amidst the hell of miseries of their people. Who is wrong hither between them and the citizens who are in bed with such obnoxious and notorious vices?


Gandhi once remarked, “How can men feel themselves honoured by the humiliation of their fellow-beings?” In the same book by Louis Fischer: Gandhi: His Life and the Message to the World seems to have the answer. He wrote, “Some men loom larger by lifting up others and some by kicking and humiliating others.” If anything, this is the real situation between Africa and the developed world. How can for instance, DRC produce tonnes and tonnes of minerals and Nigeria oil alongside with tonnes and tonnes of poor people? The West, despite having fewer resources, was able to attain their development, among others, thanks to signing and ratifying a new social contract that empowers people and their governments. It through accountability of everybody that made western countries be ahead of us for everything.


Africa cannot forge ahead with the current mediocrity whereby academics are abused without resisting. Our academics should enlighten the hoi polloi so that they can take on their irresponsible rulers. This must be the war between hoity toity and hoi polloi spearheaded by academics. It does not make sense to see our rulers abuse our tax and donor monies while academics scramble to join politics so as to share the loot. Why are our rulers spending our hard-earned taxes on travelling abroad and recruiting private armies while we are dying wantonly? This is the question our academics need to ask and give the answer instead of being in bed with those who arrest the future of our continent and her innocent people.


For Africa to move forward, a new social contract that holds our ruler accountable and responsible for whatever they say and do must be signed. We can draw a lesson from academics such as Martin Luther, Conrad Grebel, Bathsar Hubmaier, Thomas Muetzer, Ulrich Zwingli and others who gave the Roman Church hard time so as to change the world despite being young guys. We need to start asking our rulers what have they have done for us as agreed in elections or constitutions.


We need to start enjoying the fruits of our freedom that turned out to be enjoyed by rulers and their henchmen. Academics must pull Africa from the 14th Century to 21st Century by advocating the signing of a new social contract that makes our rulers accountable.

Source: The African Executive Magazine Feb. 29, 2012.

Kupunguza ujumbe au kuchunguza ziara za Kikwete?

TAHARIRI ya gazeti hili ya tarehe 22 Februari si ya kupuuza. Suala ililolenga na kuliongelea ni muhimu sana kwa mustakabali wa uchumi wa Tanzania na watu wake. Kwa ufupi ni kwamba tahariri tajwa ilibeba kichwa cha “Msafara wa Rais nje upunguzwe.”

Mhariri alimuonea aibu Rais Jakaya Kikwete kwa kutaka msafara wake upunguzwe. Kimsingi, msafara wa rais Kikwete si wa kupunguzwa bali kuchunguzwa na kuwekewa masharti. Kama rais hana nidhamu ya matumizi wa chini yake wataipata wapi? Maana, pesa anayofuja na marafiki zake huko nje si zake bali za mlipa kodi maskini wa nchi hii. Hapa ndipo mzizi wa umaskini wa nchi yetu. Lazima waliomwajiri (walipa kodi) wajue aina ya watu anaoandamana nao na kwanini? Kwa nchi yetu ilivyooza, tusipozuia mchezo huu wa matumizi ya hovyo yasiyoangalia hali halisi ya kiuchumi, tutashtukia tukiwa tunalipia misafara sawa na ile ya akina Mobutu Seseseko iliyojazana marafiki, waramba viatu na wanafamilia ya mwizi huyu wa zamani wa DRC.

Niliwahi kuhoji ni kwanini msafara wa rais siku hizi umekuwa hata siri. ni juzi tu nilijua kuwa aliandamana na watu 40. Mara nyingi idadi ya anaoandamana nao inakuwa siri. Mbona wakati wa mwalimu Julius Nyerere licha ya kufanya ziara chache, ujumbe aliokuwa akiandamana nao ulikuwa ukitangazwa? Rais Kikwete amelalamikiwa mara nyingi ila ameziba masikio. Amefikia kuitwa majina ya ajabu ajabu kama mtalii, Vasco da Gama na mengine mengi kutokana na mapenzi yake ya kusafiri nje hata wakati akihitajika kutoa maelezo na uongozi nchini. Nani mara hii kasahau alivyokwenda kwenye mkutano wa uchumi wa Davos nchini Uswizi wakati wa mgomo wa madaktari uliosababisha vifo vya watu wengi?

Kwanini rais hataki kujua na kukubali kuwa ziara zake nje ni chanzo kimojawapo cha umaskini wa taifa letu na mfadhaiko wa uchumi? Je, ni kwanini rais anajali sana safari za nje badala ya watanzania wenye dhiki nyingi za kutengenezwa na utawala mbovu uliokumbatia ufisadi na matanuzi? Je, rais anafanya hivi kwa faida ya nani? Kwa wanaokumbuka shutuma zilizompata waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye alipotumia zaidi ya shilingi 500,000,000 kwenye ziara yake ya Marekani, wajaribu kufikiri. Je rais anatumia kiasi gani kwa ziara moja ughaibuni iwapo waziri mkuu zama zile wakati mfumko wa bei na gharama za maisha vilikuwa chini anatumia kiasi gani kwa sasa? Kwa mujibu wa taarifa za siri za kiuchunguzi, kufikia tarehe 9/9/2011 rais aliposafiri kwenda Kenya kwa ziara ya kikazi, alikamilisha ya 316 tangu aingie madarakani mwaka 2005! Hii maana yake ni kwamba tangu Rais Kikwete aingie madarakani mwaka 2005, amekwisha kusafiri nje zaidi ya mara 300. Hii ukigawanya kwa miaka sita ambayo amekuwa madarakani ni kwamba kila mwaka amekuwa akisafiri mara 50 sawa na karibia mara mbili kwa mwezi au tuseme kila baada ya siku 20. Je, rais kama huyu anayekaa nje ya ofisi na nchi zaidi ya ofisini anafanya kazi lini?

Mbona marais kama Ian Khama wa Botswana nchi yenye uchumi mzuri Afrika hawasafiri kila siku? Mbona hapa jirani yetu Rais Mwai Kibaki hatumsikii akiruka kila uchao? Kuna nini kwenye biashara hii ya ziara za ughaibuni? Kwanini Kikwete hataki kuona na kuukubali ukweli? Je, hajui kuwa baada ya kuondoka madarakani hiki chaweza kuwa kikwazo kwake? Inashangaza kuona taifa lenye bajeti tegemezi kwa wafadhili kwa kiasi cha 40% kuwa na rais anayesafiri sana kuliko hata wafadhili wake. Ukifuatilia ziara za rais Barack Obama nje au waziri mkuu wa Uingereza na Canada nje, utakuta hazifikii hata hamsini, kwa mfano tangu Obama aingie madarakani, ni kwa utajiri upi Kikwete anatanua hivi? Kufikia tarehe 19/11/ 2009 Rais Obama alikuwa amefanya ziara 24 nje ya nchi tangu aingie madarakani na hili lilipigiwa kelele na Wamarekani. Kwa miaka minne maana yake ni kwamba kila mwaka amefanya ziara nane kwa mwaka wakati Kikwete akifanya mara zaidi ya kumi na mbili ya ziara za Obama! Ziara za Obama si siri; zina hadi Wikipedia yake ili anayetaka kujua aweze kujionea. Huu ndiyo uchumi na uwazi na ukweli na si matanuzi na maangamizi ya fedha za umma.

Kufikia tarehe 23/10/2010 rais mwingine anayeitwa mtalii na watu wake Zuma alikuwa ameishafanya ziara 40 chini ya miaka miwili tangu kuingia madarakani. Hata hivyo, baada ya kupigiwa kelele na wananchi wake, Zuma amepunguza ziara zake nje tofauti na Kikwete anayeendelea kuongeza ziara zake. Kwa wanaojua tabia ya Kikwete hawatashangaa kutokujifunza kwake. Hatabadilika. Maana hata alipoingia madarakani aliahidi kupunguza ukubwa wa serikali hasa baraza la mawaziri. Alifanya nini baadaye? Licha ya kuunda baraza kubwa la mawaziri kuliko la mtangulizi wake, aliongeza idadi ya wilaya na mikoa wakati uchumi ukiendelea kuporomoka kutokana na usimamizi mbaya na ufisadi.

Anachofanya Kikwete sawa na mwenzake wa Uganda ni kutumia pesa nyingi kuliko hata wizara nyeti. Mwaka 2011 kulikuwa na kituko ambapo Ikulu ya Uganda iliomba jumla ya sh za Uganda 5,055,000,000 kwa ajili ya safari za rais kwa miezi saba tu huku Wizara ya Maji na Mazingira ikitengewa sh bilioni 2.44 kwa mwaka 2010 na bilioni 3.228 mwaka 2011 kwa ajili mishahara ya miaka miwili. Wakati Ikulu ikitaka bilioni hizo 5.055 kwa ajili ya matanuzi ya Museveni nje, Ikulu hiyo hiyo iliomba pia Ushs bilioni 3.497 kwa ajili ya matengenezo ya magari ya rais huku mafuta pekee yakigharimu Ushs 120, 000,000! Wachunguzi wa mambo wanasemea kuwa Museveni alitumia jumla ya Ushs bilioni 13.386 ambazo ni zaidi ya mara nne ya bajeti ya Maji na Mazingira. Je, kwa watawala waroho na wabinafsi kama hawa Afrika inaweza kusogea mbele? Je, hawa si chanzo kikuu cha umaskini wa watu wetu? Je, rais kama Museveni au Kikwete wanatumia pesa kiasi gani katika utawala wao wote? Trillions of shillings of course. Kuna haja ya kuchunguza bajeti inayotengwa kwa ajili ya matumizi ya Kikwete. Chanzo: Tanzania Daima Februari 29, 2012.

Wednesday 22 February 2012

Africa: Are Rip-offs Paying Off?

News from Uganda that two ministers resigned after allegedly misappropriating a cool $ 60,000,000 was shocking. When this sacrilegious theft by the high and mighty was reported, Ugandans as well as other Africans received it just as a normal thing especially for a begging country like Uganda!

The two were Gender Minister, Syda Bbumba who then served as finance minister and Prof. Khiddu Makubuya, a minister in the Office of the Prime Minister, who was attorney general when money was paid as compensation to one Bassajjabalaba by inflating amount of money at the tune of excess $60,000,000. This is according to the Parliamentary Accounts Committee which launched an investigation and unraveled such rip-off.

Those conversant with how Africa is ruined and plundered by her own were not shocked. In neighboring Tanzania in 2005, close to presidential and parliamentary elections, over $ 130,000,000 was stolen from the Bank of Tanzania. The trails directed to the then president Benjamin Mkapa and the then presidential candidate Jakaya Kikwete, the current president. Since then, this country has not jailed any culprit in this connection.

Remember the mother of all theft in East Africa, the ‘Goldenberg’ scandal in 1990 that saw Kenya lose over $ 600,000,000 ? Responsible con-people have never been convicted since then. The Goldenberg scam was estimated to have cost Kenya the equivalent of more than 10% of its annual Gross Domestic Product (GDP).

Many would argue: Where was government? In the two cases of Kenya and Tanzania, such huge amounts of money were stolen directly from the Central Banks of the said countries. The governments were there in the same business of plundering the hoi polloi.

Going back to Uganda, when the two ministers decided to resign, the general public saw it as a victory due to the fact that sacred cows in Africa are nary slaughtered. So for countries where accountability is a foreign vocabulary, people felt like wining against the venal officials without knowing that resigning after causing such a huge hole on the economy is nothing comparably if the law would be utilized reasonably.

When a person robs the public and the punishment meted out on him is resignation, this means many will steal so as to retire rich guys. With such megalomaniacs in power, can we really develop our countries? What agonises is the fact that donor countries are always shouting at the top of their voices that accountability, good governance and democracy are key to a country being aided.

Is it because much of the money stolen is ending up being stashed in western banks or it involves their nationals? It is because this business- plundering Africa- has always benefitted them due to the fact that many fat thieves end up investing there as it happened for Mobutu Sese-seko and other big thieves? In Africa, stealing public monies is not a crime apparently. Challenging or opposing a president is. Africa is in financial anarchy whereby a connected cabal of thieves can rob the public without being made to face the music.

If you want to die earlier in Africa, try to steal small money or chicken. You will be butchered in the daylight even in front of police officer. But when you steal big sums, no son of gun will touch you. Instead, you’ll become mightier so as to dine with the president. For money is always power. Those who remember, Kamlesh Pattni, the architect of Goldenberg, know what I mean. One thing is obvious. Every humungous theft in East Africa used to involve two people -government official and Asian businessmen. Why? Simple, it takes two to tango. However, Uganda’s case is an exception to the general rule. For the receiver was a Ugandan. May be this is revolution in stealing public money. Before this revolutionary theft, who’d trust the guy, who after being cornered, would spill the beans by revealing who is behind this theft by the high and mighty whereas Indian business men can pack and jump onto the plane and vanish to Canada India and UK?

Africa must fight by all means to stop such $ 60,000,000 resignation as the only punishment for such an offence. When one muses on this theft, let us quote one of the reports that implicated these two ministers as quoted by The Daily Monitor, “November 13, 2010. President Museveni writes to Makubuya, Central Bank Governor Tumusiime Mutebile and Ms Bbumba instructing them to oversee a speedy compensation for Haba Group’s claims.” By the way, who’s who in this theft?

Source: The African Executive Magazine Feb.22, 2012.

Ubunge wa viti maalum ni haramu kisheria


Tanzania inaweza kuwa nchi pekee yenye viti vingi vya ubunge utokanao na vitu vyenye kila aina ya ubaguzi hata udhalilishaji chini ya dhana ya viti maalumu-wabunge wasio na kazi yoyote bungeni zaidi ya kungojea posho na sifa ndogo ndogo magazetini.

Kimsingi, hakuna mantiki ya kumpa mtu eti kuwakilisha vijana kwenye bunge, huyu mbunge wa kawaida ambaye jimbo lake lina kila aina ya binadamu atawakilisha nani? Je vijana au wanawake wana nini cha zaidi hadi kuwa na wawakilishi zaidi ya mmoja?

Kimsingi ubunge uwe wa vijana wazazi, wanawake na upuuzi mwingine ni iwizi wa pesa ya mlipa kodi unaofanywa na wanasiasa. Bahati mbaya hata vyama vya upinzani vimeuingia mtego huu na kushiriki dhambi hii. Siku hizi kila sehemu zinasikika nyimbo na ngonjera za demokrasia na usawa baina ya mwanamke na mwanaume. Hivi kweli kumpa mtu kiti kwa kigezo maalum na jina maalumu kama viti maalum si kumtukana na kumdhalilisha? Kwanini, kama tunawapenda na kuwathamini wanawake, tunawatengea viti vichache tu? Kwanini tusijenge mazingira ya ushindani wa haki na uchaguzi huru ili wanawake na wanaume na wanawake wapambane na atakayeshinda awe mbunge? Kwanini kuwadhalilisha na kuwagawana vijana na wanawake ambao kimsingi ni wengi na wakiamua kutumia wingi wao kwa busara hawana haja ya kupewa upuuzi unaoitwa viti maalum.

Umefika wakati wa kuwaambia vijana na wanawake kuwa viti maalum si suluhisho wala ukombozi kwao bali nyenzo ya kuwapumbaza na kuwagawanya ili wasitumie nguvu yao ya wingi kuamua nani awe mbunge hata rais. Hakuna asiyejua kuwa, kwa mfano, wanawake wengi walioteuliwa kwenye viti maalum wengi wanaonekana kwa jicho baya. Wapo wanaowaona kama kupe waliobebwa na watu fulani na kupewa ulaji huku wengine wakifikia hata kuvidhalilisha viti hivyo kwa kuviita viti vya chupi. Tumefikia mahali hata spika wa bunge anachaguliwa kwa jinsi yake badala ya sifa! Huku si kumkomboa mwanamke bali kumdhalilisha.

Ukiachia kudhalilishwa kwa viti hivi maalum, wengi wa wanufaika wa nafasi hizi ni watu ima ambao ni watoto wa wakubwa au wenye kuwa karibu na wakubwa chamani jambo ambalo limeleta malalamiko mengi karibu katika vyama vyote. Wengine wanasemekana kupata nafasi hizi kupitia rushwa na jinai nyingine kama kujuana, ukabila hata ujimbo. Anayebishia hili ajikumbushe majina ya akina mama wengi wabunge wa kuteuliwa ambao waume zao au baba zao wana madaraka atajua tunachomaanisha. Huku si kumkomboa mwanamke bali kumnyonya, kumtumia na kumdhalilisha.

Kwa vijana na wanawake kilichofanyika ni sawa na kuwatupia mbwa mfupa halafu mwizi aliyefanya hivyo akapata upenyo wa kuiba toka kwenye lindo la mbwa hao hao. Kuna haja ya kuwaambia wabunge wa kuteuliwa na viti maalum kuwa wanachofanya licha ya kuwa kazi ya kutumiwa, wanahujumu uchumi wetu. Hawana kazi bungeni zaidi ya kuwakilisha matumbo yao na wale waliowapigia kifua. Kimsingi, hawa si wabunge bali wala vya dezo vya umma. Kuwaambia ukweli ndiyo njia pekee ya kuwakomboa kuliko hawa wanaowatumia na kuendelea kutafuta jinsi ya kuhami jinai hii iliyohalalishwa.

Ukiangalia nchi ombaomba kama Tanzania kuwa na utitiri wa wabunge hata majimbo ya uchaguzi na mikoa unashangaa uwezo wetu wa kufikiri. Badala ya kujibana na kusogeza nchi yetu mbele, tumeruhusu kundi la watu wachache kupeana ulaji tena kwa kulipana kodi zetu! Kimsingi, hata tukiamua kutumia sheria zilizopo hasa katika inayolaani ubaguzi wa aina yoyote na kuhimiza usawa, viti maalum ni haramu na wizi unaohalalishwa kwa vile unatendwa na wanaoitwa waheshimiwa. Kwanini kwa mfano jimbo la Lushoto kuwa na wabunge maalum wakati mbunge wa jimbo anawakilisha aina zote za watu kuanzia wanawake, wanaume, wazee, vijana, watoto na kadhalika?

Kisheria kuwapa watu ubunge au kazi kwa kuangalia umri, jinsi, watokako na kadhalika ni uvunjaji wa katiba na sheria uanopaswa kuwafikisha wahusika gerezani. Je kuwapa wanawake ubunge kwa kuangalia jinsia yao siyo kuwabugua wanaume na hata kuwadhalilisha wanawake wenyewe? Au kwa vile ubunge ni ulaji basi wanawake wameridhika kuhongwa, kudhalilishwa na kubaguliwa katika taasisi za nchi? Kama wao wameridhika na dhihaka na jinai hii sisi kazi yetu kuwastua kuwa wasidhani kwa kupewa viti viwili vitatu vya udhalilishaji wamepata. Badala yake wamepunjwa na kupatikana. Hii yote huenda inatokana na kuwa na malengo madogo na mafupi kisiasa na ile hali ya wenye vyama kuwagaawana na kuwadhoofisha kimawazo.

Kimsingi viti maalumu licha ya kuwa nyenzo za kuibia kodi yetu na kutuwekea viongozi wa kupandikizwa na vikundi vya watu, ni chambo cha kuwaziba midomo mbwa wasiwapigie kelele wezi.

Je kuwapa vijana ubunge kwa kuangalia ujana siyo kuwabagua wazee? Mwanzoni mwa mwaka huu kuliamriwa kesi ya kihistoria iliyotufanya wachambuzi wa mambo tuliangalie upya suala zima la ubaguzi.

Je mnapotoa viti maalumu kwa mfano kwa jumuia ya wazazi. Hii siyo kuwabagua wasiozaa au ambao wameishaacha kuzaa? Wazazi hawahitaji hata kuwa na jumuia maana hata wabunge wa kuchaguliwa ni wazazi au wana wazazi pia na kama ni wanawake na wengine ni wanawake na kama ni vijana na wengine ni vijana.

Chimbuko la viti maalum ni mfumo wa chama kimoja uliowatumia ukiwahadaa kuwa walikuwa viognozi wa kesho. kuepuka changamoto na wingi wa wanawake na vijana ilibidi uundwe uchochoro wa kuwazuga, kuwagawanya ili wasikengeuke na kudai wao ni taifa la leo. mfumo wa chama kimoja uliona hatari ya vijana na wanawake kama wangeachwa bila kupewa kitu cha kuwahangaisha huku wakijenga chuki miongoni mwao kama ilivyo sasa ili kutotishia nafasi za wakubwa ambao mara nyingi waliwatumia vijana kwenye kila aina ya miradi na kampeni zenye faida kwao.

Sababu nyingine ya kuundwa jumuia za vijana ilikuwa ni kuwezesha kuwafuatilia na kuwadhibiti. Ukichunguza, kwa mfano, jumuia za Chama Cha Mapinduzi (CCM), kabla ya kuingia mfumo-zengwe wa vyama vingi vinavyoendeshwa na katiba ya chama kimoja, zilikuwa kama taasisi za ujasusi ya kuchunguzana baina ya vijana kwa vijana ndani ya chama.

Makala moja haitoshi kueleza ubovu na sababu za kuwapo ubunge wa aibu wa kudhalilishana. Tukipata muda siku nyingine tutauchambua tena. Kimsingi, kuna haja ya kubatilisha haraka ubunge huu haramu.
Chanzo: Dira Februari, 2012.

Mlevi aanzisha kampuni ya simu

KAMPUNI hii inaitwa TapelitelCOM. TAPELITEL au kwa urefu Tanzania Affordable and Preferable and Economical long-distance and Internal Telephone ni kampuni mpya iliyoanzishwa na mjasiriamali mie.

Ujasiriamali wangu ni tofauti na wa wale walioamua kujitwalia mali za umma wao wake zao watoto wao hata wakwe zao. Nadhani bado mnawakumbuka ingawa hamkuwapa discipline kwa ujambazi na udokozi huu.

Kwa vile mie si kibaka wala fisadi, nimeamua kuanzisha kampuni halali na ya kisasa isiyo ya kisasi kama ya wale.

Mie siyo kama wale walipopewa ulaji waliamua kugawana hata raslimali za umma. Nenda kwenye miraba ya uwindaji huko maporini utajua nimaanishachoa. karibu kila mahali ni ulaji ulaji ulaji mtupu. Na hii ndiyo maana mafisadi na mafisi hawashughulikiwi kwa vile huwezi kujua nani ni nani. Usijekuta unayetegemea amkamate mwizi ndiye mwizi mwenyewe. hayo tuyaache.

Nilitaka kuita kampuni yangu ya simu WALEtel au World Airphone Longdistance and Abracadabra Telephones baada ya kugundua kuwa kumbe uwekezaji kwenye makampuni ya simu una ulaji usio wa kutoa jasho, Mlevi nimesukuti kuanzisha kampuni ya simu. Ingawa sawa na makampuni ya simu ya ulaji yaliyojazana Danganyika, kampuni ya mlevi imebeba neno tel na com kwa shingo upande.

Maana uzoefu umeonyesha kuwa makampuni yenye majina ya tel mwishoni ni tel kweli kweli. Unajua maana ya tel? Tell Everybody Lies kwa Kiswahili mwambie kila mmoja hasa mteja uongo. Hamjasikia ukipiga simu unaambiwa mara: namba unayopiga haipo, huna salio la kutosha hata kama unapiga kwa dola, mara utasikia: jaribu tena mwaka ujao, namba yako imerongwa, namba unayopiga ni ya mzito na anaogopa kupokea, mara unayempigia yuko chooni na upuuzi mwingine mwingi. Wajua maana ya Com? com imewekwa kuficha ukweli wa neno lenyewe yaani Con or tapeli.

Tapelitel haitakusumbua na nyimbo za dini wala rafu ili kukuibia maana hazitolewi bure. Maana unaburudishwa ili kupumbazwa uibiwe. Pia mchezo wa simu kupokewa na secretary ndani ya gari la bosi unaambiwa bosi katoka nje kamuachia secretary usukani na simu hakuna.

Mambo ya bosi yuko mkutano wakati yuko pembeni mwa secretary ni noma sana. Pia kampuni ya Tapelitel haitaruhusu ukupe wa watu kubeep beep au kupiga haraka na kusema naomba unipigie. Maana uzoefu umeonyesha kuwa wanaobeep au kupiga na kuongea kama machizi kuwa uwapigie huwa na shida zao wanazotaka kukwambia lakini kwa kutumia pesa yako.

Wao wanajiona wajanja huku wakikuona wewe juha. Siku moja mlevi amewahi kupigiwa simu na jamaa akaomba ampigie. Alipompigia alishangaa kusikia kupe huyu akisema alitaka kumbomu fedha! Yaani unibomu halafu kufanikisha kunibomu eti mie ni kupigie? I am not mad and stupid that way. Sorry saana.

Kwa wale wanaishi nje wanajua adhabu wanayopewa kwa kukatwa pesa nyingi kwa kuunganishiwa simu bila kuongea. Yaani inakuwa pale kugundua kuwa mtu anakatwa pesa simply because kusikiliza upuuzi na uongo uliorekodiwa kwenye memory ya kompyuta. Jamaa washenzi kweli. Wanaunganisha simu ukianza kuongea wanakata na kuishia na pesa yako. Utasikia kuwa huna salio mara simu imeugua na upuuzi mwingine.

Kampuni ya TAPELITEL inawaahidi huduma mulua na za kisasa na si za kisasi kama hizi za sasa. Tutahakikisha wenye makampuni yote ya kijambazi na kisanii yanayowaambia upuuzi kila mnapopiga simu yatafunga madudu yake na kurejea huko ushenzini yalikotoka.

Kwa vile taifa linataka mkombozi katika mawasiliano, Tapelitel mkombozi aliyesubiliwa miaka mingi inawaahidi huduma siyo hujuma bora kama ilivyo. Kwanza tutatoza kiwango kidogo cha kuunganisha simu kwa walioko nje. Hawana haja tena ya kupiga simu zao kupitia kaya jirani.

Kwa walio ndani ya kaya, mambo ya kuwa na mitandao elfu katika simu moja sahau. Tutawapa huduma bora karibu na bure. Ila kwa wale wanaotumia simu kusema uongo na kutongozatongoza hovyo wanafunzi, wake na waume za watu wajue ima watapandishiwa gharama au simu zao kukatika hovyo hovyo kama hizi za sasa.

Kadhalika Tapelitel haitawasumbua na matangazo ya kijinga au kampeni za kifisadi kwa kuhongwa pesa na wanasiasa kuwatumia ujumbe wa kipuuzi. Sisi tutahakikisha mnaongea mnavyotaka wakati mnaotaka na kwa mnaowataka mradi msivunje kanuni tulizotoa hapo juu.

Pia Tapelitel haitashiriki kwenye kamari ya jishindie hiki wala kile. Sisi badala ya kuwapa zawadi zitokanazo na kuwaibia tutawapa huduma mnayostahili. Tutalipa kodi ipasavyo na wala hatutabadili jina hovyo hovyo ili kukwepa kodi.

Kitu kingine tutakachofanya tofauti na makampuni mengine ya kijambazi ni kuhakikisha tunaajiri wazawa kwenye kila idara ya kampuni. Tuna shida gani kuajiri wakimbizi wa kiuchumi wakati kaya ina maelfu ya watu wanaomaliza vyuo vikuu ndani na nje?

Kwanini kuajiri watu wa kuja kuiba na kulia kwao huku wakiwaacha walevi wakiadhirika kwa umaskini? Kitu kingine, Tapelitelcom haitaruhusu wakubwa wenye uroho, wake zao au watoto na wapambe zao kuja kununua shea kwenye kampuni hii adhimu.

Kwa ufupi ni kwamba kampuni hii mpya inaahidi kuwakomboa walevi kutoka kwenye makucha ya wezi wanaoitwa wawekaji wakati ni wachukuaji. Tunaahidi mapinduzi ya hali ya juu kuhakikisha kuwa kaya yetu inakuwa mojawapo ya kaya zenye huduma bora za simu. kitu ambacho tunapaswa kuwaambia mapema ni kwamba, sisi hatuna mshikamano na wanasiasa.

Hatuhitaji msaada wa wanasiasa kwa vile hatuna mpango wa kuhujumu uchumi wa kaya kama wao kwa kuwahonga wenye mamlaka ili waendelee kututia umaskini. Kimsingi, Tapelitelcom ni simu ya kila mtu.

Ni simu ya jamii na mali ya jamii. Tuungeni mkono tutokomeze huu ujambazi wa mchana unaofanywa na watu wenye mtindio wa ubongo kwa kukubali kutumiwa kuwahujumu watu wao.

Ngrrrrrrr! ngrrrrrr! Nani huyu kanideep? Ngoja nimtwangie. Pwi,pwi,pwi, ngrrrr ngrrr. “Simu unayopiga ina mafua.” Kwaheri.


Chanzo: Tanzania Daima Februari 22,2012.

Sunday 19 February 2012

Pesa ya Lowassa na marafiki zake ni safi na halali?


Hakuna shaka kuwa Edward Lowassa waziri mkuu aliyetimka madarakani kutokana na kuingiza kampuni feki ya Richmond iliyoishia kuleta maafa kwa taifa, ni mtu ambaye amegeuka kuwa mkarimu hata kupita kiasi.

Hivi karibuni akiwa Kigoma akichangia shule ya Sekondari ya FPCT Bigabiro, Kigoma, alitoa mchango wa shilingi 60, 500,000 cash ukiwa ni mchango wake na marafiki zake ambao hawatajwi kwa majina. Huu si mchango mnono wa kwanza wa Lowassa hasa baada ya kuondoka madarakani. Wengi wanajiuliza: Kama ana uchungu na taifa hili kiasi cha kulitakia maendeleo na mengine mema, mbona alitumia nafasi yake kujinufaisha kwa kuingiza kampuni feki iliyoliingiza taifa kwenye zahama? Mwaka 2006 alichanga jumla ya shilingi shilingi 60, 000,000 kati ya sh 88,340,000 kwa ajili ya shule ya sekondari ya michezo ya Kigamboni. Hapa bado hatujaorodhesha michango mingine ya kuanzia shilingi 10,000,000 kwenda juu ambazo Lowassa ameishachangia kwa vituo vya yatima, kuzindua album, makanisa na mingine mingi.

Je hii pesa inayochangwa imepatikana kihalali au ni matunda ya tuhuma zake za Richmond na nyingine za zamani za marehemu baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyedai mwaka 1995 kuwa Lowassa amejilimbikizia utajiri mwingi ambao hautokani na kipato halali-asioweza kuutolea maelezo ulivyopatikana. Na kweli, tangu mwalimu alirushe kimondo hicho, si Lowassa wala familia yake walikuwa tayari kuelezea walivyochuma huo utajiri!

Baada ya Lowassa kulazimishwa kuutema uwaziri mkuu, alijikuta akikabiliwa na pigo jingine takatifu. Pigo hili ni pale chama chake Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilipomtuhumu kuwa gamba au mtuhumiwa mkuu wa ufisadi kiasi cha kumtaka aachie hata nyadhifa chache alizokuwa amebakia nazo. Lowassa hakukubali kutupwa nje ya uringo wa siasa hasa ikichukuliwa kuwa anatajwa tajwa kutaka eti kumrithi rais Jakaya Kikwete hapo 2015 jambo ambalo wanaojua alivyochafuka sana wanaona ni kama tusi na kejeli kwa taasisi ya urais na wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

Ili kufanikisha azma yake hii, Lowassa, bila kujali kuwa watu wana akili za kuhoji na kuchambua, amekuwa akimwaga pesa kwa njia ya michango ili kujiweka karibu na wapiga kura akiwaaminisha kuwa anaweza kuwafaa wakati nafasi ya kufanya hivyo aliishaipoteza kwa kuitumia vibaya na kuliacha taifa kwenye zahama ya kiza na kulanguliwa umeme.

Je haya mamilioni anayotoa Lowassa yanatokana na malipo ya marupurupu ya ustaafu anayopewa kinyume cha sheria? Maana, Lowassa hakuwahi kustaafu zaidi ya kulazimishwa kuachia ngazi. Wengi wanashangaa ni kwanini Lowassa anaendelea kutanua bila kufikishwa mahakamani. Pia wengi wanashangaa jinsi CCM inavyomgwaya kiasi cha kumtishiatishia bila kumchukulia hatua. Kuko wapi kutekeleza dhana ya kujivua gamba ambako kumekuwa kukiahirishwa baada ya Lowassa kutishia kumwaga mtama? Je Lowassa kwa kukikamata mateka chama chake na serikali yake anaweza vile vile kuwakamata mateka watanzania akaishia kuwa rais wao hata kama ataingia kwenye vitabu vya historia kuwa anaweza kuwa rais mwenye kuchafuka kuliko waliowahi kumtangulia? Je watanzania ni wa hovyo kiasi hiki? Je wanapopokea mamilioni yake wanategemea kumpa kura wakati ukifika au kuyatumia kama ushahidi kutaka aeleze aliko na alivyoyapata huku pia wakimlazimisha atoe maelezo kuhusu shutuma zake?

Wengi pia wangetaka kuwajua hao marafiki wa Lowassa wenye uchungu na taifa letu kiasi cha kumwaga mamilioni kama wameyapata kihalali au ni watu wa kuaminika au kutisha shaka. Lazima kujiridhisha isijekuwa wananchi na michango ya maendeleo vinatumika kusafishia pesa chafu itokayo kwa magenge ya watu wachafu. Hata hivyo, kwa wanaokumbuka adha alizowasababishia Lowassa kwa kubariki na kuingiza kampuni ya Richmond na hatimaye Dowans, hata awape nini hawawezi kumsamehe. Kwa wanaokumbuka ni mabilioni mangapi ya shilingi yaliteketezwa na mradi huu ambao waziri wa zamani wa Nishati na Madini Ibrahim Msabaha aliwahi kusema ni waziri mkuu yaani Lowassa na mhindi wake yaani Rostam Aziz, hawezi kupumbazwa na misaada ya mamilioni wakati wao walichuma mabilioni ukiachia mbali kuendelea kuchuma ya ustaafu wakati Lowassa hakustaafu.

Kama michango yote ambayo Lowassa ameishaitoa ingefanyiwa mahesabu, ni pesa nyingi kuliko hata mishahara yake yote ya utumishi wake serikalini. Kwa mfano mifano miwili hapo juu ya michango ya Lowassa ya shilingi 120,000,000 ni zaidi ya mshahara wa mbunge wa mwaka mzima. Hapa hajala wala kulisha familia yake kuvaa na kufanya mambo mengine. Kama Lowassa akifanyiwa ukaguzi wa kimahasibu tangu aanze kazi na marupurupu yake yote vikalinganishwa na misaada aliyowahi kutoa na mali anazomiliki itagundulika kuwa maneno ya baba wa taifa yalikuwa ya kweli. Na hivyo, yasipuuzwe wala kusahauliwa hasa wakati huu ambapo nchi inahitaji uongozi adilifu na mpya.

Tumalizie kwa kumtaka Lowassa awataje hao marafiki zake na jinsi walivyopata hayo mamilioni. Lazima tujue kama wanafanya biashara au kazi halali, wakilipa kodi na kama ni watumishi wa umma akiwamo naye na Lowassa, je wametaja mali zao kama wanavyotakiwa na sheria? Kujua ukweli kuhusu jinsi wanavyopata pesa hii wanayotoa kwa jina jema la kusaidia jamii ni jambo jema. Lazima kila kitu kieleweke ili kuepuka jamii kugeuzwa kama fisi kulishwa nyama yake nayo ikaifakamia kwa uchoyo. Ni wakati muafaka kuangalia nani anatoa kuliko kuangalia nini kimetolewa. Hapa tuepuke cha baniani mbaya kiatu chake dawa.
Chanzo: Dira Februari, 2012.

Wednesday 15 February 2012

Rais huyu mstaafu anatufundisha nini kwa anavyoadhirika?

Nani angeamini kuwa baada ya rais kuitumikia nchi kwa miaka minne na kuweka miundo mbinu ya demokrasia bila kuiba hata shilingi moja angejikuta akifadhiliwa na mama
yake kwenye mabanda? Huyu simwingine bali rais mstaafu wa Sierra Leone, Valentine Esegragbo Melvine Strasser aliyetawala tangia mwaka 1992 hadi 1996 baada ya kunyakua madaraka kwa kuangusha Jenerali Joseph Momoh. Je hali hii inatufundisha nini? Je kwanini tunakuwa wepesi kufadhili mafisadi ilhali tukiwasulubu waadilifu? Huyu angekuwa amekwapua asingeteseka. Je nafsi yake ingekuwa huru? Inachanganya na kukera God knows. Kwa habari zaidi,BONYEZA HAPA

CCM ianguke mara ngapi?

KWA wanaofuatilia taarifa za vyombo mbali mbali vya habari walishtuka kusikia Rais Jakaya Kikwete akinakiriwa akisema kuwa kama Chama Cha Mapinduzi ambacho yeye ni mwenyekiti kinaweza kuanguka kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Wengi walishangaa kusikia kuwa kumbe Kikwete hajui kuwa CCM kilianguka miaka mingi iliyopita sema imeinuliwa na mbinu chafu kama vile kuchafuana mingoni mwao kumpata mgombea wa urais kama ilivyotokea mwaka 2005.

Kitu kingine ambacho inaonekana Kikwete amesahau ni ukweli kuwa CCM kama si kuokolewa na tume yake ya uchaguzi kwa kuiruhusu ichakachue uchaguzi na matokeo yake, ingekuwa historia kama UNIP (Zambia), KANU (Kenya), NP (Afrika Kusini) na MCP (Malawi).

Je, ni kwanini rais wa nchi na mwenyekiti wa chama tawala anakosa habari kama hizi kiasi cha kujua kuwa kumbe chama chake kilianguka miaka mingi tangu kilipobinafsishwa kwa mafisadi na wasanii?

Hivi Rais Kikwete hajui kuwa chama anachokiongoza kilianguka tangu siku kilipozika maadili ya uongozi na kupwakia madili?

Hivi Kikwete hajui kuwa chama chake kilianguka siku kilipotoa ahadi lukuki kisitimize hata nusu?

Hivi kwanini Kikwete haambiwi na washauri wake kuwa CCM kilianguka zama zile kiliporidhia kutumia pesa ya wizi kutoka kwenye taasisi za umma kama BoT (ujambazi wa EPA) kuwahonga wapiga kura na kuchakachua matokeo?

Hivi kweli kujua haya kunahitaji shahada ya uzamivu kwenye masuala ya siasa? Je, Kikwete na wenye mawazo kama yake wanaishi nchi na dunia gani?

Ili kujionea rais anavyoishi kwenye dunia ya kufikirika, hebu angalia nukuu hii iliyomnukuu akipokea maadamano ya kuadhimisha miaka 35 ya CCM huko Mwanza.

Alisema: “Haiwezekani tukaendelea kuwa na watu wa hovyo, lazima chama kijipange na kujiweka sawa ili kisipoteze sifa kwa jamii,”

Hao watu wa hovyo zaidi anayewavumilia ni nani? Kwanini Kikwete awaone hao watu wake wa hovyo leo na si jana alipokuwa akitahadharishwa kuwa chama kinamezwa na mafisadi?

Tungeomba Kikwete atutajie hao watu wake wa hovyo kama kweli ameamua kuwa mkweli badala ya kupiga siasa kama kawaida yake.

Hivi kuna mtu wa hovyo kama aliyeahidi maisha bora kwa Watanzania wote akaishia kuwapa dhidi wote? Hivi kuna mtu wa hovyo kama yule aliyesimama jukwaani mchana kweupe kuwapigia kampeni watu wa hovyo kama watuhumiwa mbalimbali wa ufisadi ambao ni wabunge kwa sasa?

Hebu angalia janja ya Kikwete. “Hivi karibuni nikiwa na NEC hapo Dodoma, nilitumia kauli ‘Nyoka Kujivua Gamba’. Usemi huo ulienezwa tofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameona azimio moja tu la kujivua gamba.”

Kuna jambo baya kama kauli hii isiyo na hata chembe ya ukweli? Kwanini Kikwete hasemi ukweli kuwa baada ya kuambiwa kuwa naye ni gamba hakuona haja tena ya kujivua gamba kwa maana aliyepaswa kuvuliwa kwanza ni yeye kabla ya kuwaambia wengine wenye magamba mepesi kujivua magamba?

“Wito wa kujivua gamba haujapewa mwitikio mzuri. Tumetupa mpira huo kwa wanachama kuwawajibisha viongozi hao, maana tunawafahamu. Sasa kazi kwetu sote,” anaongeza Kikwete.

Hivi Kikwete anataka kumdanganya nani kwa kuwatupia wanachama mzigo wakati wanachama walisharidhia vikao vya chama viwawajibishe magamba ambayo hayakutaka kujiwajibisha? sasa ni nini mantiki ya kupoteza pesa ya umma kufanya vikao iwapo jukumu lenyewe liliachwa kwa wanachama wasio na mamlaka yoyote kikatiba kuwawajibisha viongozi wao mafisadi?

Je, huku ni kuchanganyikiwa au kuishiwa kiasi cha kusema vitu vinavyopingana kwenye jukwaa moja na kwa wakati mmoja? Je, hapa wa hovyo ni nani? Nikijibu watasema Nkwazi Mhango siku zote ni mchochezi.

Kwa vile lengo la makala hii ni kutaka kuthibitisha kuwa watu wa hovyo ni viongozi wa CCM, tunatoa nukuu ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, ili wasomaji wapime pale alipokuwa akiongelea tuhuma za kujivua gamba.

Alisema: “Hata Waingereza wana tabia moja. Wakiona jambo linawasumbua, wanaunda Royal Commission, jambo hilo litachunguzwa kwa muda mrefu. Wakimaliza, watu wameshasahau.”

Mukama aliongeza: “Kufukuzana si dawa, si unaona jinsi jamii ilivyowageuka NCCR Mageuzi kwa kumfukuza David Kafulila au kufukuzwa kwa Hamad wa CUF? Sisi tumesema, kufukuzana si suluhisho, utakuwa unashughulikia tu dalili wakati ugonjwa wenyewe haujaufikia,”

Kwanza ni vigumu kuamini kuwa Mukama anaweza kujipayukia bila kujua anachosema ni nini na kinaweza kutafsiriwa vipi.

Sasa kama njama ya CCM ni hii ya kufanya mambo kijanjakijanja ili wananchi wasahau, Rais Kikwete analalamika nini au kutoa ushauri wa nini juu ya kufukuzwa watuhumiwa wa ufisadi. Huu si unafiki? Maana kama uongozi wa juu umeunda CCM royal commission ili kuwasahaulisha wananchi halafu mtu anakurupuka na kusema eti wananchi wataamua, wataamua nini iwapo wakubwa wamekwisha kuamua?

Je, hapa kama wananchi tufuate ya nani hasa ikizingatiwa kuwa Kikwete ana tabia ya kujipinga?

Rejea juzi juzi waziri mkuu Mizengo Pinda na Spika wa bunge Anne Makinda waliporipoti kuwa alikuwa ameidhinisha kulipwa nyongeza ya posho lakini baadaye akawageuka.

Kwa wanaoona CCM inavyozidi kuchanganyikiwa wakati ikipitisha hili na kulipinga hana sababu ya kuhofia kuwa haitaanguka kwenye uchaguzi ujao.

Wakati Mukama akisema hivi vigogo wengine wanasema vile. Hebu tumalizie kwa maneno ya waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye aliyesema sambamba na Mukama: “Hatuwezi kuwa na chama imara kama hatukuondoa magamba, mwenyekiti wetu wa chama taifa lazima tuyaondoe magamba yanayokipaka chama matope.”

Kama kuna kitu kitaiachia makovu ya kudumu CCM si kingine ni dhana ya kujivua gamba ambayo iliuawa baada ya rais mwenyewe kutajwa kuwa ni gamba, tena nene, ukiachia mbali magamba mengine kujua udhaifu wake na kugoma kuachia ngazi kama yalivyotakiwa. Je, kwa namna hii CCM ianguke mara ngapi?


Chanzo:Tanzania Daima Februari 15 , 2012.

Mtaje kijana wa Nyerere aliyebaki na maadili

NATUNGA kitabu. Najua wengi wakisoma hapa wataanza kucheka na hata kubeua midomo. Watasema mengi hasa wasiojua Mpayukaji ni kiumbe gani.

Watasema natafuta umaarufu kama jamaa yangu mtunzi mwenzangu na swahiba yangu Pio Kuchekwa aliyezindua buku lake la kujilisha ujiko kuwa alipata ukomavu toka kwa mzee Nchonga mwana wa Musa wakati si kweli.

Kama kuna mwanafunzi mzuri wa Mzee Nchonga si mwingine bali mimi Mpayukaji Nkwazi Nkuzi Mhango mtoto wa mzee Waambie Waipate bin Message Sent aka Mnenahovyo.

Mie ni mwanafunzi msikivu, mkweli na jabali wa mze Nchonga kwa sababu ya nifanyayo na kusema.

Ushahidi wa kwanza ni kwamba licha ya kupayuka mie si fisadi wala kilaza kama wale. Ndiyo maana katika tabu langu nililotunga liitwalo Kuambiana Ukweli sikugusia popote nilivyokuwa mwanafunzi hodari wa mwalimu.

Maana huwezi kuwa mwanafunzi wa kweli wa Mwalimu Nchonga ukakubali kujirahisi kulala kitanda kimoja na mafisi, mafisadi na wasanii. Never. Never on my dead body. you cannot be in bed with blood suckers and all hellbent thieves and whatnot as far as corruption is concerned.

Samahani nikichukia huwa naongea kiinglishi. Hivyo, msomaji nisamehe kwa kuzobokwa ung’eng’e sina maana ya kujionyesha kuwa nimechimba sana. Hata hivyo, si vibaya kuongea umombo kuonyesha nilivyochukia kama mwalimu wangu alivyokuwa akifanya akichukia.

Wengi hawatakisoma kitabu changu kutokana na wadanganyika kutokuwa na utamaduni wa kujisomea vitabu zaidi ya vya udaku. Kitasomwa na wenye pesa kwa vile kitakuwa ghali.

Hakitafundishwa mashuleni kutokana na wizara ya elimu kuamua kueneza ujinga badala ya elimu kwa kupiga marufuku vitabu mbali mbali kutumiwa mashuleni kama zamani.

Kitabu changu hakitapendwa na wengi kutokana na kutumia lugha kali na ya wazi kuwalenga walaji wa kaya hii.

kitabu changu kitapigwa marufuku na kama si kununuliwa na wabaya wa kaya na kukichoma moto ili mawazo yangu yasijulikane kwa wale wenye ujasiri na ustaarabu wa kujisomea ingawa si wengi.

Najua kitabu changu kitachomwa moto ingawa mawazo yangu hayataungua. Pesa ya ufisadi itatumika kununulia kitabu hiki na kukichoma bila kujua wanachoma pesa yao na si mawazo yangu adhimu.

Watashindwaje kukichoma ili watu wetu waendelee kusoma udaku na si mambo ya kuwapanua na kuwakomaza kiakili ili siku moja wajikomboe. Baada ya kutoa tabu hili nililowatajia hapo juu, napanga kutoa kingine kiitwacho Saa Ya Ukombozi. Samahani, msidhani naiba jina kutoka kwa kitabu kingine kama hiki ambacho nilikiona sehemu fulani. Huko mie siko.

Kitabu changu kitazinduliwa kimya kimya na makapuku maana sina pesa nyingi ya kuwahonga wazito kuja kukizindua. Watakizinduaje wakati kinawavua nguo kwa kuuzindua umma kuwafanyia kweli.

Kitabu changu hakipendwi kwa vile kinafichua siri za uongo usanii na wizi wanaofanyiwa walevi na wale waliowaamini wasijue ni mbwa mwitu na majoka.

Mie sihitaji wazito kuja kukizindua kwa vile najua huwa hawana muda wa kusoma ingawa wana pesa ya kununua vitabu. Wangekuwa wanasoma wasingefanya madudu wanayofanya.

Maana madudu mengine yanayofanyika hayahitaji kuwa na digrii kuyajua bali tabia ya kujisomea na kujielimisha. Msiseme nawasingizia. Hivi kujua kuwa kinachoendelea kwenye kaya chini ya uchukuaji unaopambwa kwa kuitwa uwekezaji wakati ni ujambazi kweli kinahitaji kuwa na shahada? Mbona mikataba yote ya kijambazi imesainiwa mbele ya wanasheria tena wenye shahada na mawaziri wao wenye shahada pia?

Hivi kujua kuwa na miji michafu ni uzembe wa kupindukia kuna hitaji shahada? Hivi kujua kuwa kaya ina vyanzo vingi vya nishati lakini inazidiwa na vijikaya visivyo na vyanzo hivi nako kunahitaji shahada? Hivi kuwawajibisha wezi wa Kagoda EPA, Richmonduli na Downs nako kunahitaji shahada yarabi?

Hivi kujua kuwa kupeleka wagonjwa ugabacholini wakati tuna wataalamu na hospitali ni aibu nako kunahitaji shahada? Kama ni hivyo basi mie sina haja na shahada za namna hii ambazo zinatolewa kama njugu ukiachia mbali kughushiwa kila uchao.

Narudia. Mimi Mpayukaji Nkwazi Mhango Nkuzi Msemahovyo sitaki shahada za namna hii. Sihitaji shahada za heshima wakati ni za dharau wala za kughushi kama za wale jamaa ambao walipotajwa wakaweka mkwara kuwa wangemshitaki Keinerugaba wakaishia kunywea. Shitakini mvuliwe nguo hadharani. Kwani nyie si vihiyo hata kama mko kwenye ulaji mliopewa na vihiyo wenzenu?

Kabla ya kusahau, inabidi niwaeleze ukweli kuwa ukiniondoa mimi, ima wanafunzi wa mwalimu Mchonga walikufa au kama wapo kiroho ni wafu. Kama wapo basi ni wale ambao hawakumwelewa.

Kama wapo ni aina ya kina njomba Tunituni Denjaman Ben che Makapu aliyeishia kumtia aibu mzee Nchonga pamoja na kumbeba tena kwa lawama lukuki.

Hawa ni wengi. Kimsingi, hata kama waliingia kwenye darasa la mwalimu hawakuelewa na kama walielewa ni wakati ule siyo sasa. Nionyeshe mwanafunzi wa Nchonga aliye hai kimaadili zaidi ya mimi nitajinyonga ni mfuate kuliko kuendelea kushuhudia anavyodhalilishwa na kila mchumia tumbo na mpenda sifa kama Pio kuandika mitabu ya kujisifu wakimhusisha.

Ningekuwa na mamlaka mwaka huu ningenyonga mtu kutokana na kuendelea kuwapo wezi wanaotaka kuchuma kupitia mgongoni mwa mzee wetu Musa.

Komeni na kama hamna la kufanya basi kauzeni nyanya badala ya kuuza uchafu wenu kwa kuuficha nyuma ya mzee Musa Mungu amweke mahali pema peponi gwiji huyu.

Ngoja kwanza nilie kidogo nikimlilia gwiji huyu anayedhalilisha na kila kinyamkera kwa kudai eti ni wanafunzi wake. Mngekuwa wanafunzi wake mngelala kitanda kimoja na genge la mafisadi waitwao chama cha mafisadi?

Mngekuwa wanafunzi wake mngejaza watoto wenu kwenye kazi nzuri ughaibuni kwenye balozi za kaya? Shame on you all. Kwa uchungu na majonzi niliyo nayo siwezi kuendelea. Acha niendelee kulia nikijililia kwanza kwa yatakayowakuta watu wa mzee Nchonga.
Chanzo: Tanzania Daima Februari 15, 2012.

Tuesday 7 February 2012

Wabunge wa CCM wanamdanganya nani?

KATIKA kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodama wabunge wa Chama Cha Mapinduzi wamekuja na mpya-eti kuikosoa na “kuikomalia” serikali yao! Kioja hiki cha aina yake kilianza pale mbunge wa kwanza kuonyesha ‘usanii’ alikuwa Charles Tizeba aliyesema, “Kwanza waziri (Mkulo), angetuambia kwa nini alikaidi ushauri wa kamati na hasara ambayo taifa limepata, wenzangu wamesema ni usikivu, lakini mimi sioni zaidi ya ukaidi, huu si mwenendo mzuri. Ushauri wa wabunge unakuwa na nia nzuri,”

Je, Tizeba anaishi wapi huyu asiyejua tabia ya chama chake cha kupongeza kila upuuzi? Tukija kwa Mkulo na ‘sanaa’ zake za eti kupunguza ushuru wa maji ya kunywa ya chupa kwa kuwaonea huruma watu wa kawaida, ni vituko mtindo mmoja.

Tangu lini makapuku wakanywa maji safi ya chupa iwapo wengi hasa wale wa Dar es salaam wanakunywa maji ya mitoni wayanunuayo toka kwa wauza maji wanaoweza kuchota maji popote bila kujali afya ya mnunuzi? Kama Mkulo hajui basi aambiwe kuwa makapuku wengi hunywa maji ya visima au ya Sumaye na Makamba ambao waliwahamasisha kuchimba visima ambavyo kimsingi si visima kitu bali maji ya chooni yanayonywewa kwa kusingizia kuwa yanatoka visimani wakati huko chini ya ardhi mtandao ni mmoja.

Niliwahi kulalamikia suala hili kwenye mwaka 2001 kiasi cha kukosana na Yusuf Makamba wakati ule akiwa Mkuu wa Mkoa na Frederick Sumaye akiwa Waziri Mkuu. Je, Mkulo amewahurumia watu wa chini au amepewa chochote na wauza maji? Je, maji ya chupa ameona bora kuliko kulanguliwa umeme huku wizara ya Mkulo ikiongoza kutoa misamaha ya kodi kwa wafanyabiashara wakubwa wakubwa?

Aliyefuata kwa vituko ni William Mgimwa (Kalenga) aliyesema, “Kama TRA inakusanya asilimia 102 na kuna upungufu wa fedha, basi kuna tatizo na tunahitaji maelezo maana tuna takwimu za makusanyo, lakini hakuna maelezo ya matumizi,” Je, mkipewa maelezo au kutopewa maelezo mtafanya nini iwapo mnapojifanya kupinga huitwa na kukalishwa chini kama kamati ya chama na kuminywa mbavu kiasi cha kukaidi viapo vyenu?

Je, mmesahau kuwa wananchi wanajua usanii wetu na ushirika wenu na serikali yenu? Kuko wapi kutelekeza dhana ya kujivua gamba ambao kimsingi ndiyo chanzo cha maafa yote ya Watanzania?

Hebu turejee kwa Tizeba tena. Alikaririwa akisema, “Punguzo hilo halitamsaidia mlaji wa kawaida zaidi ya wenye viwanda kama waziri alivyokiri ameandikiwa na wenye viwanda… kwa hiyo itanufaisha wenyewe.”

Je, kama mbunge na wabunge wengine wanajua ukweli kuwa alichotaka kufanya Mkulo ni kufanikisha ‘deal’ lake, wanamchukulia hatua gani kwa mamlaka waliyo nayo? Maana yake ni kwamba Mkulo analidanganya Bunge jambo ambalo ni kosa linalopaswa kumwajibisha. Lakini nani atamwajibisha nani iwapo na wabunge nao wanawadanganya waliowachagua na kuishia kulala kitanda kimoja na serikali pamoja na mazabe yake yote?

Wabunge wetu hasa wa CCM ambao mara nyingi hutumika kutia mhuri kila upuuzi wa serikali wangekuwa wanamaanisha wanachosema, wezi wa Richmond wangekuwa gerezani ukiachia mbali kufuta mikataba ya kijambazi kama ile ya IPTL, Aggreko, Dowans na mingine mingi.

Wangeweza kuja na hoja na miswaada ya kufumua uwekezaji upya na kuusuka upya kwa masilahi ya taifa. Lakini nani anajali iwapo wanapewa ujumbe kwenye kamati na bodi mbali mbali na kupata ulaji wao? Nani anajali iwapo wote wanatenda dhambi ile ile na wana sharubu kama samaki wengine hasa mapapa?

Wabunge wetu hasa wa CCM wangekuwa wakweli na wawakilishi wa kweli wa wananchi wasingesumbuka kutaka maelezo ya kuridhisha wakati serikali inayojidai kukusanya kodi kwa asilimia 102 ikidai haina pesa ya kulipa malimbikizo ya mishahara na stahiki za walimu.

Wasingeelewa kitu wala kudai maelezo bali uwajibikaji kwa serikali yenye kukusanya kodi kwa 102% lakini ikashindwa kuongeza mishahara ya watumishi wake hadi madaktari kugoma nchi nzima.

Ni ajabu kwa serikali hii inayoweza kukusanya kodi kwa asilimia zaidi ya mia kupata pesa ya kugharimia safari za watawala nje zisizo na umuhimu lakini ikashindwa hata kupeleka huduma kwa wananchi!

Maana kwa wanaojua maana ya kulipa kodi, watakubaliana nasi kuwa wananchi hulipa kodi kwa serikali ili iweze kuwaletea huduma wasizoweza kuzitoa mmoja mmoja. kazi ya kodi siyo kuwalisha watawala na kuongezeana hata posho za makalio bali kurejesha hiyo kodi kwa wananchi waliochanga ili kujiletea maendeleo.

Ni bahati mbaya kuwa kwa Tanzania kodi inahimizwa kulipwa ili kugharimia maisha aghali ya watawala na wapambe wao na familia zao. Ni kodi ya kujihudumia na si kodi ya maendeleo kama inavyoitwa. Wananchi wangejua haki zao vilivyo, wangegoma kuilipa kodi serikali isiyo tekeleza ahadi na wajibu wake. Yako wapi maisha bora kwa watanzania yaliyoahidiwa na CCM kwenye uchaguzi?

Wabunge wa CCM wangejishughulisha na hili wangeleta maana zaidi ya kutafuta sifa. Mwenye kubisha na kunikosoa na kuonyesha udhaifu wa hoja zangu kama anaona upo. Ni mara ngapi wabunge wa CCM wanaikamia serikali na kuwekwa sawa kwenye kamati ya chama na kunywea?

Je, wabunge wa CCM wanamdanganya nani na nani anaweza kuwa ‘chizi’ awaamini? Tunawashauri waendelee na biashara yao ya kupongezana badala ya kuuhadaa umma kuwa wanaujali.


Chanzo: Tanzania Daima Februari 8, 2012.

Mpayukaji aidhinisha posho na kuzikana

NI makosa ni vibaya mnafanya wazazi
Ni aibu ni huzuni iyo yoyoo
Iwapo mzazi humpendi mwanao,
Nasi wa pembeni tutampenda vipi?

Uchungu wa mwana aujuaye mzazi
Ni wazi mwaelewa lakini mwafanya hivyo

Ni makosa ni vibaya mnafanya walaji
Ni aibu ni huzuni iyo yoyoo
Iwapo mkuu huwajali watibu
Na wagonjwa watawaheshimu vipi?

Uchungu wa kodi aujuaye mlaji eehe
Ni wazi mwaipata lakini mwafanya hivyo

Mkuu wajua kila kitu ni hovyo
Lakini wajifanya hamnazo bure
Siku utakapokuja uona ukweli
Utakuwa uso kwa uso na pilatoee

Huwezi kuamini mzee Maneno aliingia kijiweni akiimba wimbo huu kunitupia vimondo asijue mie ndiye bingwa wa mipasho na vimondo. Alipoendelea kuimba bila kujali mie nilikuwa pale na namuona na kumsikia niliamua kuuliza ni kwanini alikuwa akinikosea adabu. Mzee huyu mshenzi kweli si alijitetea kwa kusema, ‘No’. ubeti wa pili nimekosea. Nilitaka kumaanisha wazazi na watoto na si wakuu, walaji na wa tiba na wagonjwa. Kwani nani mgonjwa hapa. Anyways, unayesoma, zingatia yote isipokuwa ubeti wa pili. Mzee huyu alipayuka msameheni hajui alilokuwa akifanya. Wakati mwingine njaa yaweza kusababisha kichaa. Hayo tuyaache. Kwanza huu muziki wa Les Wanyika wa zama zetu ushanitibua nyongo. Ngoja niachane na mambo ya kuimba niingie kwenye mada ya rero. Tulimalizanaje na mzee Maneno? Hayakuhusu. Acha umbea.

Baada ya kurejea na hangovers za Davos, nilijikuta nikishauriana na mshirika wa Bedroom kuongeza posho za makalio za wanywa kahawa. Msianze kuhoji kama mimi ni fisadi au fisadi mtoto. Jamani mimi si Rizikione wala sina uhusiano na ulaji wao. Najua matahoji huyu jamaa kapata wapi pesa ya kutoa hata posho ya makalio kwa wanywa kahawa. Msijihangaishe. Mshiko niliopewa kwenda Davos ulitafunwa wote kule. Ninachoiita posho hapa si kingine bali kahawa ya dezo kwa wanywaji kahawa hasa wale wanaowakilisha walevi.

Nikiwa nimetoka zangu kuosha macho kule Davos nilikopiga picha na wazito kama sina akili nzuri, sikujua kuwa kumbe nilikuwa nimerejea Uswekeni kwenye matatizo ya kujitakia na kutakiwa. Sikujua kuwa kumbe Davos ilikuwa ni kisingizio cha muda. Sikujua kumbe matatizo niliyokuwa nimekimbia yalikuwa yamezaliana na kuongezeka kiasi cha kunitia majaribuni. Huwezi kuamini. Niliposhuka toka kwenye pipa na kuwasili nyumbani, nilikuta malalamiko hasa kutokana na wambea waliosoma habari zangu kwenda Davos. Nilijilaumu kwa nini sikuwaonya kuwa baada ya kusoma hawakupaswa kuwaambia watu!

Kwanza, nilikuta mshirika wangu wa bedroom amenuna baada ya kuambiwa kuwa nilikwenda kule kujivinjari na totoz na si kujifunza jinsi ya kuwa na nidhamu ya matumizi kama nilivyoeleza kwenye taarifa yangu ya wiki jana.

Kwa vile mie ni bonge la mjanja, hili halikugeuka tatizo. Kwani nilikuwa nimemfanyia shopping ya viwalo ya kuua mtu. Michuchumio na mi-gold nilivyotoka navyo Paris nilikopitia toka Davos vilimlainisha kiasi cha kusahau madai yake. Kilichonikera ni wanoko wa kijiweni kutojali kuwa nilikuwa nimetoka kutumia. Hivyo nilipaswa kupewa muda wa kupumzika.

Kumbuka, nilipoondoka kwenda zangu Davos, niliacha mgomo wa wanywa kahawa waliotaka waongezewe nyongeza ya posho ya makalio yaani vikombe na kashata ili kuendelea kuchangia kijiwe. Kadhalika niliacha minung’uniko ya waonja kahawa na mabwana usafi kijiweni.

Ajabu kina mgosi Machungi niliokwenda nao kutanua Davos wao hawaulizwi kitu isipokuwa mimi kwa vile ni mkuu wa kijiwe. Nasikia hata wapishi wa kahawa nao wana mpango wa kugoma wakidai kuongezewa ujira wao. Watashindwaje kudai iwapo sisi wanywaji tusiofanya chochote tunaongezeana posho na marupurupu ya makalio na makoo hata kuuchapa kijiweni?

Sikujua kuwa kumbe kukurupuka ni ugonjwa na tabia mbaya sana. Baada ya mshirika wangu wa Bedroom kunishauri kuwa lilikuwa jambo jema kuwaongezea motisha na posho wanywa kahawa, niliona ni jambo bora sana. Niliamua kuandika kimemo na kumpa mzee Machungi atangaze tena bila kupindishapindisha kama yule jamaa wa kupinda anayecheza makidamakida na yule Ana Makimba. Jamaa bila ajizi likatangaza kuwa mzee mheshimiwa Dk Mpayukaji ameongeza posho na ulaji wa wanywa kahawa! Lololo! Kama nilikuwa nimeingiza kidole kwenye kichuguu! Walevi walivyohanikiza kunipinga na kunilaani na wengine kuniita kilaza sina mfano.

Nilipoona maji yamezidi unga nikaamua kumruka mgosi Machungi kwa kusema kuwa nilimshauri yeye na mshirika wa bedroom watumie busara kuona kama kulikuwa na haja ya kuongeza ulaji wa wanywa kahawa ambao kijiweni hupenda kuuita posho ya makalio kama ya wale waheshimiwa wanaoongoza kuuchapa usingizi kwenye njengo.

Brother Wahasira upo? Ila jamaa zako wa Chakudema wanachapa kazi nzuri wakati wewe ukiutononoa na kupewa posho ya makalio, usingizi, kupayuka, koo hata kuongopa. Kwanza niseme. Genge lenu limeniponza. Kwani walevi waliposoma kwenye magazeti kuwa nanyi mmeongezewa mshiko wa makalio na mkuu wenu nao si wakaanza kudai mshiko au posho ya makalio ingawa wao wanalipwa kahawa na kashata!

Nasikia hata mkuu wenu amejifunza kuchomoa toka kwangu. Tofauti ya kijiwe nanyi ni kwamba nyinyi mna fweza nyingi ila hamna akili nzuri ya kuitumia zaidi ya ufisi na ubinafsi wenu wa hovyo.

Hiyo pesa mnayotanulia na kuingiza kwenye mifuko binafsi ingeletwa kijiweni tungeweza kuachana na kunywa kahawa na kunywa mvinyo tena ule wa champagne ambao wachovu wengi wameujua kupitia kwenye harusi basi. Hata hivyo mimi niliubwia sana nilipokuwa Davos ndiyo maana nikarudi na hangovers kama mia na ushei hivi. Hayo tuyaache mtamalizana wenyewe na mazabe yenu.


Chanzo: Tanzania Daima Februari 8, 2012.

Senegal: Is Wade Waiting for a Revolution ?


When I heard octegenerian Senegalese president, Professor Abdulaye Wade, saying that he wants to stand in the coming elections for the third time in order to complete his “projects”, I got confused and appalled. My first question was: Whose projects, between president and taxpayers, are they? I was simply confused due to the fact that it's become a norm for presidents to use same words conmen and women use to dupe their clients when it comes to fortunes.

Let's face it. Ironically, the man who wants to complete his “preojects” is but a beggar in an expensive suit as it is for the case of other African rulers! Another question was: Does it mean that Senegal is Wade and family’s personal estate? Interestingly, rumours are rife that Wade is even older than his official age of 86. What can such an old man do differently? If anything, Wade and Robert Mugabe are likely to enter the Guiness book of wonders for striving to die in power. It is even disgusting to learn that such educated oldmen behave goonlier than illiterates. Such a cabal of rulers has become another blow to our continent. Here we are talking of the oldmen who behave like boys. There are those who still believe that without them being in power nobody else can rule their countries. We have the likes of Yoweri Museveni, Meles Zenawi, Theodoro Nguema, Denis Sassou-Ngwesso, and many more who think that they were created to rule.

The far-fetched to-cling-unto- power- to- finish- unknown- and- dubious –projects reason has become another moniker of democracy many dictators use to get away with it. Do these selfseekers spend their personal fortunes on the so-called their projects or use the said projects to swindle people’s money? Developing infrastructure? Who told him that others cannot develop infrastructure? Others go as far as saying that they want to remain in power to see to it that their revolutions are not tarnished or being booted down as it has always been the case in Uganda. But for how long will Africa remain a captive of hungry individuals in power?

Analysits agree that Wade was grooming his son Karim to inherit his presidency as it was the projects in Libya and Egypt before Jasmeen revolution shattered such dreams. Moreover, when Senegalese openly opposed this plus what happened in Libya and Egypt, Wade decided to bite the bullet and stand himself to save his face. Given that he had not prepared anybody except his son to succeed him, Wade found himself caught between a rock and hard place. So with this vaccum, Wade decided to succeed himself by standing for a third time. Interestingly, Wade was able to manipulate the judiciary and get away with it. Once again, this exposed the weakness of judiciary made of presidential appointees instead of vetted judges as it is in Kenya and South Africa.

Wade has maintained that he wants to remain in power in order to advance his agenda of development. Many Senegalese do not subscribe to this given that when Wade came to power promised democratic and transparent changes that he did not do. He still maintains that he needs time to change the system. Again, Jonathan Jansen in his book Knowledge in the blood said, “The master’s tool can never demolish master’s house.” Therefore, it is an open secret that Wade still wants to take Senegalese for a ride once again. Will he succeed under all this pressure? Will he end up like Bakili Muluzi (Malawi) and the late Fredrick Chiluba (Zambia) that were stopped by the people or triumph just like Yoweri Museveni (Uganda) and Paul Biya (Cameroun) who got away with it after manipulating their constitutions and electoral bodies?

After being democratically propelled to power in 2007, Wade promised Senegalese that he won’t appoint anybody minister who did not win elections. His son Karim lost mayoral elections. This forced Wade to lick his vomitese to appoint his son a powerful minister jaggling from ministry to another from State for International Cooperation, Urban and Regional Planning, Air Transport to Infrastructure!

The guy is approaching ninenty. Many people say that he faked his age in order to cling unto power. Suppose his “projects” are not completed in his third term in office when he actually will e approaching a hundred year, will he run for the fourth term in order to do the same business of project completing? Does this make sense really?
Ironically, Wade a professor of Law does not honor the law he taught for many years. It becomes even murky to note that Wade came to power under the banner of democracy as it was in the case of Muluzi, Chiluba and many others who ended up becoming even more despotic than those they unseated. If anything, this has become another obstacle for Africa’s democratic transition. A few academics enter politics to end up creating more shame than even the less educated they unseated. We will discuss this next time in the need of signing a new social contract in Africa. Suffices to sum up asking Mr Wade: Is Senegal your private estate mr president?

Source: The African Executive Magazine Feb., 8, 2012.

Monday 6 February 2012

Kujivua gamba CCM tushike la nani au ndiyo mwanzo wa mwisho?


“Haiwezekanitukaendelea kuwa na watu wa hovyo, lazima chama kijipange na kujiweka sawa ilikisipoteze sifa kwa jamii,” Jakaya Kikwete akiwa Mwanza jana. Anaongeza, "Hivi karibuni nikiwana NEC hapo Dodoma, nilitumia kauli ‘Nyoka Kujivua Gamba’. Usemi huo ulienezwatofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameonaazimio moja tu la kujivua gamba.”


“Hatuwezi kuwa nachama imara kama hatukuondoa magamba, mwenyekiti wetu wa chama taifa lazimatuyaondoe magamba yanayokipaka chama matope.” Fredrick Sumaye akiwa Pangani mkoani Jana.


“Hata Waingerezawanatabia moja. Wakiona jambo linawasumbua, wanaunda Royal Commission, jambo hilolitachunguzwa kwa muda mrefu. Wakimaliza, watu wameshasahau,” Wilson Mukama katika mahojiano maalum na gazeti la Mwananchi wiki jana. Aliongeza,“Kufukuzana siyo dawa, si unaona jinsi jamii ilivyowageuka NCCR Mageuzi kwa kumfukuza David Kafulila au kufukuzwa kwa Hamad wa CUF. Sisi tumesema, kufukuzana siyo suluhisho.., utakuwa unashughulikia tu dalili wakati ugonjwa wenyewe haujaufikia,”

Kwa kauli hizo hapo juu tutegemee nini?

Thursday 2 February 2012

Angalia posho zenu zinavyopaswa kupatikana


Angalia mheshimiwa mbunge anavyotengeneza posho ya makalio. Hata hivyo posho hiyo ya makalio haitoshi kiasi cha mheshimiwa kulala na kuota posho ya kuuchapa usingizi. Hawa wanaoidhinisha na baadaye kukanusha sijui kama wana nia nzuri na wananchi.Hata hivo wanakosa nini iwapo mambo yao siku zote yakwenda kama ilivyopangwa?

Wednesday 1 February 2012

Leon Mugesera Deportation: A Notice to Impunity


Mugesera: The end of the road? Photo courtesy
When Rwanda faced genocide in 1994, it was betrayed and forgotten by the international community. However, Rwanda emerged from the ash, true to what Joseph Sebarenzi wrote in his piece God Sleeps in Rwanda, when he quoted 1 Samuel 2:8, “He raises the poor from the dust and lifts the need from heaps of ash…..”

Leon Mugesera, a long time Rwandan fugitive, was recently extradited from Canada after losing a lengthy legal battle to stay in Canada. A former linguistic professor at Laval University in Quebec, Mugesera is a very controversial figure. Educated as he is, many thought his knowledge would be the fountain of humanity and justice. Unfortunately though, he allegedly made a speech that acted as a precursor of Genocide.

Mugesera was able to juggle the law his way for 16 years before the long arm of justice caught up with him. Mugesera’s legal acrobatics created a headache for Canadian and Rwandan governments. He lost the battle when the government of Canada, after exhausting all legal venues and options, decided that the game was over and time up for Mugesera to be deported and face justice back home. At Montreal's Pierre Elliott Trudeau International Airport where Canadian authorities saw Mugesera off, his family and friends wept.

Mugesera’s deportation was not an easy stuff for the government to chew. On the one hand, Rwandan authorities asked Canada to deport Mugesara so that he could be tried back home where he allegedly committed the offences he is charged with. On the other hand, Canadian authorities were under pressure from Human Rights activists, Mugesera’s friends and sympathizers not to let him be deported. The weak reasons the pro-Mugeseras gave is that he would be tortured.

Mugesera’s ordeal stated in 1992, when he gave the hate speech to his party’s members that later acted as a button that triggered genocide in Rwanda a year after Mugesera fled Rwanda. Addressing 1,000 party members, Mugesera allegedly told the crowd to kill Tutsis and "dump their bodies into the rivers of Rwanda." And truly this happened in the shortest time so as to go even beyond Rwanda. Refer to how Tanzanian authorities became aware of the pogrom after people in Rwanda’s neighboring region of Kagera reported to have spotted so many corpses floating in the river.

When the father of five arrived in Canada, he concealed his past so as to be issued with a permanent residence status on top of securing a teaching job at Laval University. After two years, Canadian authorities got wind of Mugesera’s lies and henceforth stripped his permanent resident status off. His tribulations started right away thence so as to cost Canadian taxpayers’ money for 16 years.

Mugesera’s deportation though was received with mixed reactions by Canadians. Those who thought Mugesera deserved to answer his call congratulated their government for doing justice for the people of Rwanda. This was seen on the responses online when Yahoo reported the last ditch for Mugesera. Some Canadians who don’t know what actually transpired in Rwanda in 1994 are blaming their government for deporting Mugesera. Those in Quebec where he used to attend mass and sing in the church think Mugesera was an innocent and ideal person. “I personally think that it’s very unfortunate that Canada appears to have washed its hands and is sending Mr. Mugesera to a country which, according to the United Nations and the United States, practices torture,” said Allison Turner, a Montreal lawyer and former defence lawyer at the United Nation’s International Criminal Tribunal for Rwanda (ICTR).

Ironically, the pro-Mugeseras seem careless about the rights of those that were butchered in 1994. Instead they care a lot more for the rights of Mugesera. To them, Rwanda is not mature enough to try a fugitive! Again, such people do not dispute the fact that Rwanda has proved many wrong after emerging from genocide to become one of the fastest developing countries in the world! Let us face it. Rwandan government, if anything, has won international recognition after deciding to forge ahead instead of living in the past. Therefore, this can assure us that justice is going to be done in Rwanda as far as Mugesera’s allegations are concerned.

What is interesting is the fact that neither Mugesera nor his lawyers have ever disputed the charges he is facing. Instead their concerns have always been that Mugesera is going to be tortured. Apart from this, Rwandan authorities assured Canada that they will treat Mugesera according to the letter of the law. Rwandan Prosecutor General Martin Ngoga says: “We are prepared to follow the law to the letter and honour the guarantees we gave the Canadian government.” Ngoga continues, “Everyone is welcome (to observe).” To show how prepared and just the government is, Ngoga assured the international community of due diligence and accountability in dealing with this high profile case.

At last justice is closing in on Mugesera. Those who commit heinous crimes against humanity with impunity in Africa ought to be put on notice. Justice will one day close in on them.

Source: The African Executive Magazine Feb., 1, 2012.

Jakaya anajifunza nini davos kila mwaka?


Kwa mtu anayejua uchumi wetu unavyoharisha huku toboatoba ya mafisadi ikizidi kuuzamisha, anashangaa uwezo wa rais Jakaya Kikwete kujifunza. Tunasema hivi kutokana na mazoea yake ya kwenda Davos Uswisi kuhudhuria mkutano wa kiuchumi wa dunia wenye lengo la kutoa mikakati na mbinu za kuimarisha uchumi duniani. Tunasema hivi kutokana na kutoona tofauti kiuchumi.

Kila unapofanyika mkutano wa uchumi duniani kule Davos Kikwete na walaji wenzake huwa hawakosi. Inaonekana hii tabia aliirithi toka kwa mtangulizi wake Benjamin Mkapa aliyesifika kwa kupenda kusafiri na kuhutubia mikutano ya kimataifa kuliko hata ya ndani kama alivyowahi kutuhumiwa na akaamua kujibu kwa ubabe. Hii siyo hoja leo. Hoja ni kutafakari nini anachotufanyia na kutuletea Kikwete kwa kwenda Davos kila mkutano huu unapofanyika. Sisi si wa kwanza kuuliza. Gazeti hili lilihoji na ikulu ya Kikwete ikatoa majibu ya kitoto kubwa likiwa ni kutafuta udhaifu wa kitaaluma zaidi ya hoja husika.

Swali muhimu na kubwa linalotusumbua ni: Je Kikwete hujifunza nini iwapo uchumi wetu ndiyo wa hovyo kuliko zote katika eneo la afrika mashariki? Hebu itazame sarafu yetu. Utazame mfumko wa bei na kupanda gharama za maisha. Kwa wanaokumbuka, wakati Mkapa akiondoka mfumko wa bei ulikua ni asilimia tano. Leo tunaambiwa ni 20%. Sarafu yetu inabadilishwa kwa takribani shilingi 1,500 kwa dola moja wakati mkapa akiondoka ilikuwa ikikaribia kufikia dola moja kwa shilingi 800. Je hapa tatizo ni nini? Je ni muarobaini gani Kikwete anaendea Davos? Je inakuwaje mtu aende kuogelea kisimani asitoke na tone hata moja la maji? Je tatizo hapa ni kisima au mhusika? Haya ndiyo maswali yanayopaswa kujibiwa na hao wanaomjibia rais kwa kutoa majibu ya kitoto. Wakati mwingine huwa tunashangaa watu kama hawa wanalipwa kwa lipi iwapo hawawezi hata kusoma hoja na kuzitolea majibu yanayoingia akilini! Je ni ile hali ya kupatikana kwa wahusika kwa mbinu chafu kiasi cha kuwa genge la kulipana fadhila?

Kitu kingine kinachomuweka Kikwete msalabani ni ile hali ya kuwa nchi yetu inaongoza barani kwa kuombaomba kiasi cha kuwa nyuma ya Afghanistan na Iraki kutokana na nchi hizi kusumbuliwa na vita. Swali jingine muhimu ni: Anajifunza nini iwapo tunaongoza katika bara la afrika kupewa misaada ambayo mwisho wake ni kufujwa?

Sitaki nionekane namkejeli Kikwete. Acha niulize :Je kikwete huenda kujifunza uwekezaji wa kijambazi wa mtangulizi wake ambaye naye alikuwa shabiki wa Davos? Kwa uchumi wetu, hii Davos siyo divorce jamani? Je kama uchumi wetu haufanani na Davos, ina maana Kikwete na wenzake anaoandamana nao wanakwenda kule kutanua kwa kufuja kodi zetu? Nakumbuka jamaa mmoja toka Sudan ya Kusini aliyerejea nchini mwake baada ya kupata uhuru. Msimuliaji wa kisa hiki ambaye ni rafiki yangu toka huko anasema kuwa siku ya siku kijana aliyekuwa amekaa Marekani kwa zaidi ya miaka kumi aliporejea kwao katika mji mkuu Juba, aliitwa na wazee. Wazee hawa walikuwa kumbe wamemuandalia bonge la ofisi na cha mno kulikuwa na kompyuta. Kwa vile nchi hii ni change na ina kiu ya maendeleo, wazee hawa walidhani kijana wao kwa kukaa nchi iliyoendelea naye alikuwa amepata angalau ujuzi hata uzoefu unaofanana nayo. Hivyo walimpeleka ofisini na kumpa kumkabidhi ofisi yake.

Jamaa alifurahi sana. Lakini kabla ya wazee kuondoka walitaka kijana awaonyesha atakavyotumia ile kompyuta. Bila kujua kuwa katika wazee wale kulikuwapo mmojawapo mtaalamu wa kompyuta, jamaa aliwasha kompyuta na kuanza kubabaisha huku na kule. Mara yule mzee mtaalamu alimwambia kuwa angetaka afungue programu ya Power Point ambayo si ngumu. Kijana alianza kutoa toa macho. Kufupisha kisa hiki, wale wazee waliamua kumpa kipigo cha mwizi.

Somo la kisa hiki ni kwamba lazima mtu afanane na mazingira anayoishi au aliyokwenda kujifunza sawa na rais wetu kuja na mikakati inayofanana na mkutano wa Davos badala ya kuja na picha alizopiga na viongozi mbali mbali mashuhuri duniani. Watanzania hawahitaji kuona sura za viongozi mashuhuri bali kuona mabadiliko katika uchumi na maisha yao. Hili kwao ni muhimu kuliko hizo picha na stori za mara tuliomba hili au tulijadili hili. We need actions not words and photo gallery from Davos.

Ni jambo la hatari kwa mfano rais kutumia shilingi zaidi ya 300,000,000 kwenda kufanya vitu ambavyo hata haviingii akilini. Tunasema hivi si kwa sababu ya uchochezi au chuki. Tuna sababu. Hivi kulikuwa na mantiki gani kwa mfano kwa rais kwenda zake Davos huku makamu wake akijichimbia mikoani (Lindi na Tanga) akifanya ziara za kupanda miti wakati madaktari wakiwa wamegoma? Je kupanda miti na kuhudhuria mkutano wa Davos ni muhimu kuliko afya za watanzania? Je ni watanzania wangapi walipoteza maisha wakati wa mgomo wakati viongozi wao wakiwa wanatanua nje ya nchi na mikoani? Mbona rais kwa mfano Mwai Kibaki wa Kenya hakwenda kule na badala yake alimtuma waziri mkuu Raila Odinga kutokana na kutaka kusikia wakenya walikuwa wanatafakari vipi hukumu ya Mahakam a kimataifa? Kwani kila mkutano lazima uhudhuriwe na rais au ni ile hali ya kupenda kusafiri na kukimbia matatizo ya msingi nyumbani? Tunamshauri rais Kikwete kubadili tabia na mapenzi yake ya kujali mambo ya nje kuliko ya ndani. Yeye si waziri wa mambo ya nchi za nje tena bali rais. Je kwa kukimbia matatizo ya msingi ya nyumbani, rais Kikwete amekuja na kipi cha mno kwa uchumi wetu uliko chumba cha wagonjwa mahututi (ICU)?
Chanzo: Tanzania Daima Februari 1, 2012.

Mpayukaji aenda kutanua Davos

NAJUA wasomaji wengi wanaona kama stori hii ni kamba za kawaida wasijue ni ukweli mtupu. Kwanza mimi si msanii wala mjingamjinga kujipinga au kufanya vitu vinavyoweza kunitokea puani.

Kwa taarifa yenu ni kwamba nimeanzisha NGO ya ulaji ambayo iliniwezesha kupata wafadhili kwenda kuhudhuria mkutano wa kiuchumi na ulaji matanuzi na mambo mengine kule Davos Uswisi. Chunga sana ni Uswisi si Uswazi wala Sweden kama baadhi ya magazeti yalivyoandika hivi karibuni. Hivi hata neno dogo Swiss nalo linawashinda waandishi wa siku hizi?

Wanaobisha kuwa sikuwa Davos ngoja niwape vipande. Mkutano wetu wa ulaji wa waliwaji ulifunguliwa na dada yangu na mwanafunzi mwenzangu Dk. Angela Merkel, ambaye alinipongeza sana na kusema kuwa huwa ananikumbuka nilivyokuwa kipanga darasani. Tulipiga picha pamoja na kubadilisha business card na kila mtu akaenda zake. Niliandamana na marafiki zangu kama kumi na watano hivi, akiwamo mfotoaji wangu binafsi, Mwidini Michozi
Hayo tuyaache.

Baada ya wafadhili kunipa yapata dola kama 250,000 kwa ajili ya matanuzi yangu na watu wangu, tulijitoma kwenye pipa la Katari na kutua zetu kule kwenye kiwinta na kula mikuku na mitotoz. Jina la kampuni iliyonifadhili naweka kapuni kuogopa Matonya wetu wakubwa na wadogo kwenda kule kubomu na kututilia kichumvi. Si unawajua tena Waswahili walivyo na mitima nyongo.

Katika msafara huu ingawa nasema nilikwenda na watu 15 totoz zangu zilikwenda kivyake ili wanoko wasinishtukie na kumpa taarifa bi mkubwa ingawa hawezi kufanya kitu ikichukuliwa kuwa naye ananichuna kwa kutumia mamlaka yangu kijiweni. Kwani yeye hana washikaji wake wanaonilia vyangu? Anadhani sijui?

Hakuna kitu kilichonifurahisha kama kwenda kwenye ma fauna na kwa wataalamu wanaoitwa chiropracticians au madaktari wa kuchua mwili. Najua wale washenzi wakisikia neno kuchua wanaanza kufikiri upuuzi. Hapa namaanisha kukandwakandwa na kunyooshwa kila kiungo. Kitu kimoja sitawaambia ni kwamba wale wadada wanaofanya udaktari huu lazima wawe bila ngu… we koma! Wakati jamaa zangu madaktari wamegoma, niliamua kwenda kule kula upepo na kujitibia kwa kukandwakandwa. Kitu kingine, kule Davos hakuna dini wala ushehe. Unakata kilaji kama huna akili nzuri. Hayo tuyaache.

Kule Davos nimejifunza mikakati mipya ya kukuza uchumi wa kijiwe hasa kuhakikisha kuwa kila tone la kahawa inayochemshwa linaingizwa kwenye kitabu cha mapato.

Mbali na la usimamizi wa mapato, mengine niliyojifunza Davos ni kama ifuatavyo:

Mosi, kuondoa au hata kupunguza ofa za hovyo hovyo kwa wale ninaowalipa fadhili kutokana na kunisaidia kuukwaa ukuu. Hapa akina Silvia Rweyependekeza nadhani wananipata.

Pili, kufanya kampeni kuhamasisha watu kunywa kahawa na siyo gongo na upuuzi mwingine.

Tatu, kupunguza au kufuta ushikaji na kujuana kwenye kijiwe ambapo watu wamekuwa wakija na kunywa kahawa bila kulipa hata kukopa pesa za kijiwe kwa vile eti wananijua mimi au ni ndugu au marafiki zangu. Huu ni ukupe lazima ufe mara moja.

Nne, kumnyang’anya gabacholi Kanji mraji wa makaa kutokana na kuutumia kuibia kijiwe kwa kuanzisha ujambazi wa mkaa almaarufu Richmonduli, Downs, APITIELO na mwingine.

Tano, kuchemsha kahawa kwa umeme badala ya mkaa. Maana naona mkaa licha ya kuchafua mazingira umechafua hata maadili kutokana na kashfa tajwa hapo juu.

Sita, kupambana na mgawo wa umeme ili kuwepo na nishati ya kuchemshia kahawa. Hapa najua lisirikali litanichukia kwa vile nataka kuingilia ulaji wao kwa maslahi ya wana kijiwe changu. Hata hivyo nitajaribu. Maana mie simuogopi mtu awe Njaa Shibe au Kapinda mie namvaa tu.

Saba, kupandisha bei ya kahawa na kuhakikisha wanywaji wanalipwa kwa dola. Hii ni kutokana na madafu kuporomoka kila uchao kama mabua.

Hatua ya nane ni kuhakikisha nampiga stop bi mkubwa kuacha kuchota fweza za kashata. Kinachokera sana ni kwamba anachukua na mashoga zake nao wanakuja kuhomola nikimuuliza naye aniuliza kwani watu wangu si walaji? Kitu kingine kinachonitia shaka ni ile ya bi mkubwa kutaka kutumia vita yangu ya kuhakikisha kuna uadilifu kuwa chanzo cha kuvuruga u-house wetu.

Hapa kusema ukweli amenishika pabaya. Hata hivyo napanga kumpa laivu kuwa kama anaona u-house wetu unashikiliwa na kumruhusu kuwa fisadi basi nitaoa mwingine ambaye atakubaliana nami. Mbona mchonga aliishi hadi kufa na mama Mary? Najua wanawake wote si kama Anna Tamaa au Shari Salima wa Njaa Kaya.

Anyway hilo nitalishughulikia nikipata time baada ya kutafakari mikakati yangu ya Davos.

Ukiachia mbali hiyo mikakati hapo juu na matanuzi mengine, kule Davos kulikuwa na party ya kupiga picha na wakubwa wa dunia hii. Nakumbuka. Hakuna kilichonifurahisha kama kupiga simu na Devil Kameruni, Go- down Brauni, Yakobo Zumaa wa Sauzi ambaye kwa totoz anaonekana kunitoa jasho. Kuna kipindi niliambiwa nikapige picha na wakuu wa kaya kama Hafkanisheitani na Pakasheitwan nikakataa kwa kujua walivyo matapeli na magaidi. Kama wingi wa picha ungekuwa fweza basi kijiwe kingekuwa tajiri kuliko kaya zote ulimwenguni.

Najua mijitu mingine isiyo na adabu inaposoma ujumbe huu inasema moyoni kuwa ni kamba. Kama mnadhani ni kamba nenda kawaulize wote waliohudhuria ulaji huu wakwambie kama hawakuniona tena nikijinoma mipicha ya madingi wa ulaji wa mataifa mbalimbali.

Unajua? Acha niishie hapa niende kutekeleza mipango kemkemu kutoka Davos. Basi nanyi waulize wakubwa zenu waliounguza kodi zenu kwenda kule wawaeleze walifanya nini na wamekuja na nini cha mno kama mimi. Kama watawadanganya njoo kwangu niwape siri zao. Maana kamera yangu ilikuwa ikimulika kila mchovu aliyekuwa Davos akijinoma.

Nauli yangu na watu wangu kwenda kule Uswisi ilitolewa na Baraka Obamiza. Ila hii ni top secret ya confidential tell nobody except yourself. You know what?

Chanzo: Tanzania Daima Februari 1, 2012.