The Chant of Savant

Friday 30 December 2011

Je taifa linahitaji kuambiwa au kuombewa?




Kuna mchezo wa ajabu umeanza hivi karibuni ambapo wajanja fulani huaandaa eti mkesha wa kuombea taifa. Hivi kweli inahitaji kuombewa au kuambiwa ukwelinaviogozi wa dini na wale wote wenye udhu kusisitiza uwajibikaji na ku-deliver. Kwanini watu wengi wanatumia njia ya utapeli ya kujifanya wanalipenda taifa hili wakati wanakwepa ukweli? Tatizo la Tanzania si mikosi wala nini bali ufisadi, ukosefu wa maadili na uongozi wenye visheni. Yeyote anayetaka kujificha nyuma ya Mungu anajindanganya na kudanganya na kupoteza muda. Hivi kupambana na ufisadi kweli kunahitaji miujiza au utashi? Mjengwa, najua unachukia ufisadi na umekwenda shule, kama siyo kutoa nafasi kwa kila mtu kutoa mawazo yake, kweli namda kama hii ingeona jua la leo? Hawa kwanini hawasemi kuwa ni wasanii wanaotumia mateso ya jamii kujiweka karibu na watawala? Nawashauri wasome kitabu changu cha Saa Ya Ukombozi.

No comments: