The Chant of Savant

Thursday 17 November 2011

CCM kuzikwa au kufufuliwa Dodoma?









Habari zilizofikia vyombo vya habari ni kwamba kwenye vikao vijavyo vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), (NEC) na Kamati kuu ya CCM (CC) ambavyo vitaongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete vitawavua uanachama makada wake sita kutokana na makosa mbali mbali makubwa yakiwamo kujivua gamba na kuvuruga chama.

cha Hakika hii ni kesi ya mfalme Suleiman. Kikwete na NEC wanapaswa kuwa makini wasije wakakiua chama kilichokwishagawanyika vibaya. Kimsingi, kinachopaswa kufanywa siyo kuongeza namba ya watu wa kufukuza. Maazimio ya kikao kilichokuja na falsafa ya Kikwete ya kujivua gamba yalilenga kuwavua uongozi wanachama watatu yaani Rostam Aziz aliyejivua na Edward Lowassa na Andrew Chenge. Hawa wanne wanaozushiwa tuhuma mpya za kukigawa chama wakati chama kimegawanywa na ufisadi wanatoka wapi? Yetu macho kushuhudia CCM ikiuawa na wale walio wake.
Si vibaya kwa CCM kuongeza idadi ya mafisadi kwa vile inao wengi hata hawa wanaosimamia vikao. Lakini kuwafukuza wale wanaopinga ufisadi itakuwa ni kujipalia mkaa. Upinzani uombe Mungu sana hili litokee unufaike na kuichukua nchi mwaka 2015 ili yale niliyotabiri kwenye vitabu vyangu vya SAA YA UKOMBOZI na NYUMA YA PAZIA yatimie.
Upinzani pia ujitahidi sana kama hili litatokea kuwakataa magamba wanaojulikana. Maana kama watafukuzwa chamani upinzani ukawapokea utakuwa umeruka mkojo na kukanyaga manonihino.

No comments: