The Chant of Savant

Thursday 22 September 2011

CCM ijifunze toka Zambia



Hayawi hayawi huwa! Rais aliyeko madarakani nchini Zambia Rupia Banda amebwagwa vibaya na kiongozi wa upinzani Michael Sata baada ya jaji mkuu wa Zambia,Ernest Sakala kumtangaza mshindi . Ingawa watawala wa kale na wapya wa Afrika hawatabiriki, huu ni ushindi kwa upinzani barani Afrika.

Kushinda kwa Sata ni somo jingine kuwa hata kama Afrika imeshindwa kuwapindua maimla wake kama walivyofanya waarabu wa Afrika, inaweza kutumia sanduku la kura. Wengi wa watawala wezi na wababaishaji wamekuwa wakiwekeza kwenye hongo na wizi wa kura kusalia madarakani kama ilivyotokea Tanzania, mambo yanazidi kubadilika.
Kuna jambo moja la kuwapongeza Zambia kwalo. Wazambia siku zote wamekuwa mbele kwenye kuleta mageuzi huku na watawala wao wakiwa wakweli ikilinganishwa na wezi wenzao kwenye nchi nyingine.

Rais wa kwanza wa Zambia Kenneth Kaunda mnamo mwaka 1991 aliahidi uchaguzi huru na wa haki na akatimiza ahadi yake kwa kushindwa na kukubali kushindwa. Historia ina tabia ya kujirudia. Rais anayeondoka madarakani Banda amerudia alichofanya Kaunda. Tunawapongeza wazambia huku tukiwaomba watanzania kujifunza toka Zambia. Kwa watawala mafisadi wa Tanzania, ni wakati wa kutia maji pale mwenzao anaponyolewa. Hongera Satta na Hongera Zambia. Muhimu tusingetegemea uoza wa Fredrick Chiluba kujirudia. Tusingetegemea aibu ya Bakili Muluzi, Bingu wa Mutharika au Abdulaye Wade kutokea. Kila la heri Zambia. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

No comments: