The Chant of Savant

Monday 29 November 2010

Je Kikwete ameamua kufa na watu wake?








































Baada ya minong'ono, umbea na kila aina ya bunia hatimaye rais Jakaya Kikwete ameunda serikali yake. Amefanya kitu ambacho wengi hawakutegemea. Pamoja na kulalamikiwa kwa muda mrefu kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, amelipanua. Haijulikani kama hii inatokana na kiburi, kulipa fadhila au mahitaji ya wakati.

Wengi wanaona kama hapakuwa na sababu ya kupanua baraza la mawaziri sambamba na kuanzisha mikoa na wiliya nyingine mpya. Maana kufanya hivi kunazidisha zigo kwa walipa kodi wetu maskini. Bahati mbaya si rais wala washauri wake walioliona hili kutokana na ukweli kuwa hata kila kijiji kingekuwa mkoa wao bado wanapata marupurupu yao. Rejea pesa nyingi ya bajeti kuishia kwenye kuendesha serikali kubwa isiyo na ulazima badala ya kutumika kwenye shughuli za jamii na maendeleo.

Leo tunathamini nafasi za kisiasa kuliko hata elimu afya na ustawi wa watu wetu? Je hawa ni watu wetu kweli?

Kimsingi upanuzi wa serikali na mikoa haulengi kuwanufaisha wananchi zaidi ya wale walio karibu na bwana mkubwa ambaye amejenga mazingira ambapo karibu kila mtu anajipendekeza kwake ili akumbukwe kwenye karamu hii ya kuuangamiza umma.

Ukiangalia baadhi ya wateule wa rais unashangaa mantiki ya kuwateua hata kama ana mamlaka kikatiba. Ni juzi juzi aliukatisha umma wa watanzania kiasi cha kutaka kumuadhibu kwa kumnyima kura kabla ya kuokolewa na tume yake ya uchaguzi. Aliushangaza na kuuchokoza umma alipowapigia kampeni watuhumiwa wa ufisadi ulioliingizia taifa hasara kubwa sana.

Kana kwamba hii haitoshi, juzi amewateua baadhi ya watuhumiwa wa kughushi vyeti vya kitaaluma pamoja na umma kupigia hili kelele. Hii maana yake ni kwamba rais anatoa taarifa kuwa kwake kutenda ufisadi si tatizo pale autendaye anapokuwa mtu wake.

Hivi inaleta picha gani kwa rais kuteua watu kama Mary Nagu, Makongoro Mahanga, William Lukuvi,Emanuel Nchimbi ambao hawajawahi kujisafisha kutokana na kashfa ya kughushi vyeti vya taaluma? Je hii si kuhalalisha kosa la kughushi hasa linapotendwa na watu wa karibu yake? Je hii haipingani na utawala bora na wa sheria?

Kwa kuangalia jinsi rais alivyoendelea kuwabeba watu wake, ni dhahiri kuwa Kikwete ameamua kufa nao liwalo na liwe.

Kwa upande mwingine rais ametumia udhaifu wa watu wetu wasioshinikiza kufanyika kitu kuendelea kuwalinda watuhumiwa ambao kama kungekuwa na utawala wa sheria, walipaswa kuwajibishwa katika ngwe iliyopita. Lakini nani atamwajibisha nani iwapo rais naye alitajwa kwenye list of shame na hakukanusha wala kutoa maelezo na anaendelea kudunda baada ya kushinda kwenye uchaguzi wenye kila aina ya utata na hakuna anayeingia mitaani kumpinga?

Je umma utaendelea kuwa mashahidi wa mateso na kudhulumiwa na kikundi kidogo cha watu hadi lini? Je kwanini hatumbani rais akatupa sababu za kuwabeba watu wenye tuhuma nzito za jinai? Je rais wa namna hii licha ya kupatikana kwa utata yuko ofisini kwa ajili yetu au watu wake?

Ingawa rais Kikwete hupenda kujionyesha kama mtu msikivu, rahimu na aliye karibu na watu, matendo yake yanamwonyesha kama mbabe na asiyejali umma unasema nini ukiachia mbali kuwa mugumu wa kujifunza na kubadilika.

Je rais kuendelea kuwateua watu wenye madoa, anaandaa mazingira, huko tuendako, kuwarejesha na wengine walio karibu naye kwenye uteuzi ili waweze kuendelea na harakati zao za kuwania ukuu baadaye? Maana ukiangalia umma unavyoendelea kunyamazia jinai hii ya kuteua watuhumiwa wa kashfa za jinai, unagundua kuwa kama rais ataamua kuwarejesha marafiki zake waliotimuliwa kutokana na ufisadi na rushwa, umma utaendelea kulalamika bila kuchukua hatua.

Japo hili laweza kuonekana kama uvumi na hofu tu, kama rais ataruhusiwa kuendelea na ubabe na kiburi hiki, tusishangae wale tuliokwisha wasahau wakafufuliwa na kurejeshwa kwa hadhira na hata baadaye kututawala.

Ukiachana na watuhumiwa wa kashfa ya kughushi, rais amewarejesha baadhi ya mawaziri walioonyesha kushindwa kwenye awamu iliyopita. Kwa mfano, mawaziri Jumanne Maghembe, Shukuru Kawambwa, Hussein Mwinyi, Hawa Ghasia, George Mkuchika, Mathias Chikawe, Benard Membe na William Ngeleja waliboronga.

Maghembe alivuruga kiwango cha elimu huku Kawambwa akipwaya kwenye wizara ya Uchukuzi. Mwinyi atakumbukwa kama waziri wa ulinzi aliyekataa kujiuzulu baada ya kutokea uzembe wizarani mwake na kusababisha milipuko ya mabomu huko Mbagala ambapo raia wasio na hatia waliuawa.

Ghasia , Mkuchika na Membe walipoteza muda mwingi kwenye malumbano ya kisiasa badala ya kufanya kazi huku Ngeleja akiendesha wizara iliyojaza manung'uniko tokana na mgao wa na kupanda kwa gharama za umeme. Orodha haiwezi kukamilika bila kumtaja Sophia Simba bingwa wa kuvuruga utawala bora.

Kwanini rais hakuyaona haya mapungufu? Hakuyaona kwa vile hawa watu walionyesha utii kwake badala ya umma. Hapa ndipo dhana nzima ya rais Mungu-mtu au sultani wa kiswahili inapochimbuka.

Kimsingi, watajwa hapo juu wanaendelea kuwa mzigo kwa bosi wao. Na inaonekana Kikwete ameamua kwa hiari yake na sababu azijuzo kufa na watu wake. Je ana faida gani nao? Jiulize na kutafakari. Je tutaendelea kumruhusu ajifanyie atakavyo kwa gharama ya kodi na ofisi zetu? Ni kutafakari zaidi.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Novemba 28, 2010.

Saturday 27 November 2010

Kilichomwangusha Kikwete hiki


KUNA mambo mengi yaliyosababisha kuanguka vibaya kwa Rais Jakaya Kikwete na chama chake katika uchaguzi uliopita.

Kikwete ameanguka kutoka asilimia 80.2 mwaka 2005 hadi asilimia 61 katika uchaguzi wa mwaka huu.

Kwa ufupi, alishindwa kukidhi matarajio na mahitaji ya umma katika miaka mitano ya utawala wake; hasa kutimiza ahadi kuu ya “Maisha bora kwa kila Mtanzania.”

Kikwete ameshindwa kukuza uchumi; kusimamia urejeshwaji wa mali za serikali ikiwamo nyumba zilizoibwa wakati wa utawala wa rais aliyemtangulia, Benjamin Mkapa. Kikwete aliahidi kurejesha nyumba hizo mikononi mwa umma.

Aidha, Kikwete ameshindwa kuachana na baadhi ya marafiki zake, wakiwamo watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini. Alivunja rekodi kwa kutoa msamaha wa jumla kwa wezi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya taifa (BoT).

Hadi anamaliza kipindi chake cha kwanza cha miaka mitano, karibu watuhumiwa wote wakuu wa ufisadi, akiwamo swahiba wake – Rostam Aziz ambaye anatajwa kuwa ndiye mmiliki wa kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, iliyokwapua zaidi ya Sh. 40 bilioni, bado wanaendelea kupeta.

Jingine ambalo lilimfanya Kikwerte kushindwa vibaya, ni hatua ya chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM) – kuzuia mchakato wa kidemokrasia.
Katika kinyang’anyiro cha kutafuta mgombea urais, CCM hawakuruhusu Kikwete kupata mshindani. Alisimama pekee huku nguvu ya ziada ikitumika kuwatisha na kuwanyamazisha walioonyesha nia ya kugombea.

Mfano hai, ni hatua ya Sheikh Yahya Hussein kutisha wanaotaka kumpinga Kikwete. Ikulu ilibariki unajimu wake, badala ya kumkaripia. Jambo hili lilipunguza utamu wa uchaguzi na lilichangia kupunguza kura zake.

Licha ya kutonadi sera zake katika mikutano yake ya kampeni, hakushirikisha chama chake. Kampeni ziliendeshwa na familia na baadhi ya marafiki zake.
Hatua hii ilipunguza kwa kiwango kikubwa kura zake kwa kuwa wengi waliona kuwa mgombea huyo wa urais, anataka kugeuza Ikulu kuwa mradi binafsi wa familia.

Hadi kampeni zinamalizika, Kikwete hakuwahi kutaja mali zake. Kwa baadhi ya watu, hili lilimuondolea umakini na kuaminiwa, hasa wakati huu ambapo ufisadi serikalini umeshika kasi.

Akiwa katika mbio zake za kuusaka urais, Kikwete alipigia debe baadhi ya watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini. Wengine aliwamwagia hata sifa kwa kuwaita, “Jembe la kale” ambalo lingali na makali.

Miongoni mwa waliopigiwa debe na kusifiwa na ambao bila shaka walipunguza kura zake, ni Edward Lowassa, Basil Mramba, Andrew Chenge na Rostam.
Sababu nyingine ni ukweli kuwa licha ya kuwakatisha tamaa wapiga kura, serikali na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), walishindwa kuandaa na kusimamia uchaguzi wenye sifa na viwango vinavyotakiwa.

Angalia idadi ya waliojitokeza kupigakura. Ni pungufu kwa asilimia 30 ya waliojiandikisha.

Jingine ni hatua ya rais kunyamazia shutuma nyingi za wazi na kweli zilizoelekezwa kwa serikali yake.

Vilevile, hatua ya Kikwete kushindwa kueleza vyanzo vyake vya fedha ilipunguza sehemu ya ushindi wake.

Pamoja na kwamba Kikwete na chama chake walizindua kampeni ya kuchangia chama chao, lakini kila mwenye akili timamu aliona kwamba fedha zilizotumika, haziwezi kupatikana kwa njia ya michango ya “karata tatu.”

Kitu kingine kilichomwangusha ni kutokemea wazushi waliotumia baadhi ya vyombo vya habari na waandishi wa habari mmojammoja.

Kwa mfano, hatua ya gazeti la serikali, HabariLeo, kushupalia maisha binafsi ya mshindani wake mkuu katika kinyang’anyiro cha urais, Dk. Willibrod Slaa, kilipunguza kura za Kikwete.

Sababu nyingine ni matumizi mabaya ya vyombo vya dola na shutuma dhidi ya idara ya usalama wa taifa, kwamba imepanga kuchakachua kura. Haya pia yalipunguza kura zake.

Pamoja na kwamba watuhumiwa walijitahidi kukanusha, lakini maelezo waliyotoa hayakuaminika.

Pia rais aliridhia watu waliokamatwa wakitoa rushwa kupitishwa na chama chake kugombea nafasi za ubunge na udiwani katika maeneo mengi nchini.
Kesi zilizolistua taifa ni pamoja na ile iliyomhusu Magreth Sitta na Betty Machangu. Vigogo hawa waliendelea kuwa wagombea na kuruhusiwa kukipigia kampeni chama chao. Haya yalipunguza kura za rais.

Sababu nyingine ni matumizi ya fedha za umma kwenye kampeni zake. Rejea shutuma zilizotolewa dhidi ya mke wa rais, Mama Salma Kikwete ambaye alituhumiwa kutumia ndege na magari ya umma.

Hii ni nje ya tuhuma kwamba asasi yake ya WAMA ilitumika katika kumpigia kampeni mumewe na chama chake. Yote haya yaliupunguza kura za Kikwete.
Hadi sasa, mke wa rais, watoto wake – Ridhiwani Kikwete na Miraji, wanaonekana ni sura ya utawala bila kuchaguliwa na yeyote wala kutajwa popote katika katiba.

Hili liliwachukiza wapigakura wengi kiasi kutoona sababu ya kumrejesha Kikwete madarakani.

Haya ni nje ya tuhuma za rais kutumia fedha nyingi kwa safari za nje, badala ya kutatua matatizo ya nchi.

Ongezeko la deni la taifa; mfumko wa bei; kudhoofika kwa sarafu ya Tanzania kulinganisha na dola ya Marekani na kuongezeka kwa pengo kati ya walionacho na wasionacho, vyote hivyo vimechangia kutaka kumuondoa ikulu.

Kushindwa kwa rais kukabiliana na wahafidhina waliotaka Samwel Sitta anyang'anywe kadi ya CCM, ni sababu nyingine ya Kikwete kuambulia asimilia 61 ya kura. Kuna waliomwona ama ni dhaifu au anabeba mafisadi.

Sababu nyingine kubwa ni Kikwete kuendelea kuzuia kuandikwa kwa katiba mpya ambayo ingekuwa muarobaini wa kukabiliana hasa na ufisadi.

Kimsingi mambo mengi yaliyosababisha Kikwete kugeuka “chukizo la wananchi” na si chaguo na kipenzi chao, japo ataendelea kuwa rais.

Ni vema yeye na chama chake wangeziangalia ili achukue hatua ya kukabiliana nazo kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015.
Chanzo: Mwanahalisi Novemba 24, 2010.

Friday 26 November 2010

Siku Mungu aliponyang'anywa jua, ujanja au uchizi?

Tusishangae siku moja akatojea kichaa au mjanja akasajili kuwa waafrika wote ni mali zake. Je tufanye nini kuepuka hali hii inayozidi kuhalalisha wizi kupitia sayansi na teknolojia?





Angeles Duran, 49, told the online edition of daily El Mundo she took the step in September after reading about an American man who had registered himself as the owner of the moon and most planets in our Solar System.

There is an international agreement which states that no country may claim ownership of a planet or star, but it says nothing about individuals, she added.

"There was no snag, I backed my claim legally, I am not stupid, I know the law. I did it but anyone else could have done it, it simply occurred to me first."

The document issued by the notary public declares Duran to be the "owner of the Sun, a star of spectral type G2, located in the centre of the solar system, located at an average distance from Earth of about 149,600,000 kilometres".

Duran, who lives in the town of Salvaterra do Mino, said she now wants to slap a fee on everyone who uses the sun and give half of the proceeds to the Spanish government and 20 percent to the nation's pension fund.

She would dedicate another 10 percent to research, another 10 percent to ending world hunger -- and would keep the remaining 10 percent herself.

"It is time to start doing things the right way, if there is an idea for how to generate income and improve the economy and people's well-being, why not do it?" she asked.

Thursday 25 November 2010

Nchimbi ni kihiyo au genius?





Maelezo yaliyochapishwa na gazeti la Mwananchi la Novemba 24 juu ya historia hasa elimu ya waziri Emanuel Nchimbi yanaacha maswali mengi kuliko majibu.
Ukiangalia hapa chini unagundua kuwa Nchimbi alisoma shahada mbili yaani ya uzamili na ya uzamivu kwa kipindi kimoja yaani mwaka 2001-2003!
Si hilo tu, hata hicho chuo anachodai kupatia shahada ya uzamivu ukikichunguza kinatia shaka. Kina wafanyakazi wasiozidi 30 na masharti yake ndiyo usiseme. Je umefika wakati wa kumfichua Nchimbi huku tukimbana Jakaya Kikwete ambaye amefumbia macho tuhuma za kughushi vyeti vya kitaaluma za Nchimbi na wenzake?
Je hakuna watanzania wengine wanaoweza kuwa mawaziri hadi rais ang'ang'anie vihiyo na watuhumiwa wa jinai? Na hii si mara ya kwanza kwa Kikwete kujionyesha kama mvunja sheria. Aliwapigia kampeni watuhumiwa wa EPA na Richmond ukiachia mbali naye kutajwa kwenye list of shame. Je huu ndiyo ushirika wa mafisadi ambao wapinzani wamekuwa wakiupigia kelele? Je kama jamii tunapaswa kuendelea kunyamazia jinai hii?
Tafakari.


Jina: Emmanuel John Nchimbi
Nafasi: Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo
Tarehe ya Kuzaliwa: 24 Desemba, 1971
Jimbo la Ubunge: Songea Mjini (2005-2010) na ametetea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu

Nafasi nyinginea alizowahi kushika:
Naibu Waziri: Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (2008 – 2010), Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana (2006-2008) na Habari, Utamaduni na Michezo (Januari 2006 – Oktoba 2006).
Mkuu wa Wilaya: 2003 -2005
Afisa Tawala, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC, 1998 – 2003)

Elimu:
CommonWealth Open University PhD (Management) 2001 2003 PHD
Shahada ya uzamili katika masuala ya fedha na benki (MBA), Chuo Kikuu Mzumbe, (2001 -2003)
Stashahada ya Juu ya Uongozi, Chuo cha Uongozi wa Maendeleo Mzumbe (IDM) (1994- 1997).
Je Nchimbi ni kihiyo au jiniasi wa kawaida?

Monday 22 November 2010

Je mbunge wako ni mwizi?


Odongo Otto Mtunzi na mbunge wa Uganda





























Wabunge wanatumia nafasi zao kinyume cha sheria kujilimbikizia utajiri. Hivi ndivyo kitabu kipya kilichotungwa na mbunge wa Aruu Odongo Otto kinavyodokeza.

Kitabu cha “Theory and Practice of Parliamentary Democracy (Dhana na utekelezaji wa demokrasia ya Bunge- tafsiri ni yangu, kinaonyesha jinsi wabunge walivyotelekeza wajibu wao na kukimbiza pesa.

“ Warsha zinafanyika kwenye mahoteli ya kitalii kujadili bajeti ya wizara, na ajabu warsha hizi hugharimiwa na wizara.” Hii haina tofauti na ujambazi unaofanyika Tanzania. Rejea warsha elekezi kule Ngurdoto iliyoishia kuzamisha pesa ya walipa kodi wetu maskini na kisifanyike kitu zaidi ya wakubwa kujazana mapesa.

Kitabu kinaendelea “Kawaida warsha hizi huanza ijumaa na kila Mbunge hurejea nyumbani na posho ya mafuta hata kama warsha yenyewe imefanyika jijini-eneo la kawaida la kazi la wahusika..”

Akizidua kitabu chake Bungeni ijumaa Otto alisema: “ Najua kitabu hiki kitakwenda sambamba na bunge. Lakini wananchi wana haki ya kujua nani anawaangusha katika mapambano dhidi ya ufisadi. Naweza kuitwa na kamati ya nidhamu lakini watu wanapaswa kujua ukweli.”

Naibu spika, Rebecca Kadaga, alisema kuwa atatoa maelezo yake baada ya kukisoma kitabu husika.

Kwa ufupi Otto anajenga hoja kuu ya msingi kuwa bunge lazima lijipambanue na ufisadi na kuonyesha kwa vitendo jinsi linavyopambana nao badala ya kuushiriki kama yalivyo mabunge yetu.
Tanzania inapaswa kusoma kitabu hiki kutokana na kuwa na wabunge wengi wafanyabiashara ya haki za umma ukiachia mbali kuongoza kwa kuingia mikataba ya kiwizi na kusababisha umaskini wa kunuka.
Je mbunge wako ni moja ya hawa? Tafakarini.

Sunday 21 November 2010

“Kudos Jammeh shall you live up to your words”


Many things have been said and written about Gambian strong man Yahya Abdul-Azziz Jemus Junkung Diliu Jammeh. He was listed among the horrid and stinking dictators Africa has ever had. He’s renown for his iron fist when it comes to manning a tiny west African country. So too, he likes honours, braggadocios and titles even where he does not deserve. You can see where a string of his fickle titles like “Professor, Doctor, El Hajj” and other emanates.

Despite all above, he recently stole thunder shall his promise not end up being a mere confabulation or something near.

The media recently reported that he is intending to stand down. What a big heart that does not need to be recanted! He won’t seek a fourth term in office after lapsing the third one, the media has reported. This, by all standards, is good and welcome news. Shall he willingly quit, this is but a boost for democracy shall he live up to his words. And indeed this puts him in the group of nobles and statesmen.

We need to congratulate and encourage him for seeing the light. We need to tell him that he should live up to his words as we say go Jammeh go!

Things have changed. Dictatorship does nary pay. In future, thanks to the establishment of the International Criminal Court (ICC), dictators and vote riggers won’t have a place in Africa, thanks to its prosecution of violence and crimes that dictators have always used and relied upon to cling unto power.

Other dictators need to read from Jammeh new scriptures shall they want to go down nobly. What they’re required to do is read and honour the signs of the time and changes accompanying them, shall they want to live as free bin-Adams after abdicating from office.

Strictly speaking, shall Jammeh live up to his words, he’s likely to beat many so-called democratically-elected rulers whose power was obtained by evil means of bribery, intimidation, scheming, lying , rigging and what not, as it recently happened in Tanzania. Thus, this makes more sense to rulers like Jakaya Kikwete, Mwai Kibaki, Yoweri Museveni, Paul Kagame, Dennis Sassou Ngweso and Meles Zenawi.

Others that have to deeply and aggressively dive into Jammeh’s scriptures and take a leaf are Robert Mugabe, Theodoro Obiang Ngwema, Blaise Compaore, Muamar Gadaffi, Joseph Kabila, Hosni Mubarak and other many more.

Africa won’t forge ahead without getting rid of a corrupt kit and and caboodle of ramp-fed ronyons and election thieves-in-chief. This cabal of criminals are causing more harm and mayhem for Africans than other enemies such as ignorance, globalization, neo-colonialization and so forth so to speak. The money they are spending on consolidating their power suffices to bring about positive changes to our people. The army of major domos and praise singers they keep and finance won’t help them any more. The money they steal and squander suffices to create harmonious and healthy environment for them and their people to live peacefully and securely instead of living behind fears and arrogance.

Jammeh goes down in history books as the man that saw the light and tomorrow at the right time, shall he not become a turncoat as always politicians, especially rulers have been. The good thing about Jammeh’s new take is the fact that the citizenry almost everywhere in Africa has always been ready and able to forgive. Refer to how Kibaki is currently emulated and honour for ushering the new constitution in and taking on corruption head on.

It is, thus, not too late for the rest to emulate Jammeh’s stance with regards to the future of democracy in his country and Africa in general.

If Jammeh who came to power in 1994 can truly and practically contemplate about leaving the office, what of those that came before him? What of those that messed even more than him? If Jammeh would see his failure, what of others that have even messed a great deal more than him?

Methinks, the reward for those messing up for a long time should be to stand down. Rulers and leaders come and go, but the nation remains and it will remain ad infinitum.

History shows that military rulers who relinquished power willingly have since lived respected and good life altogether. Those enjoying and commanding exemplary lives thanks to ushering democracy in are Mathieu Kerekou (Benin), Abdulsalami Abubakar (Nigeria), Olusegun Obassanjo (Nigeria) and Jerry Rawlings (Ghana). Soon Sekouba Konate of Guinea will proudly come into the big picture shall he keep his zeal and promises. So too, Niger’s military junta can win accolades shall they do what they have been saying with regards to returning democratic elected government in the country.

In a nutshell, shall Jammeh’s vow be put in actions, it needs to be recommended.
Source: AfroSpear Nov. 21, 2010.

Bai bai Samm Sixx ndiyo uchakachuaji huu ati

Niliposema kuwa mimi ni mtafiti na mvumbuzi wengi walinicheka na kunikejeli bila kujua.

Maskini hawakujua. Hawakujua kuwa nimevumbua mbinu mpya ya kuwa mkuu wa kijiwe! Kabla sijazama kwenye thesis yangu lazima niseme: ukitaka kuwa mkuu lazima ujenge ufalme wa familia. Bila hii, ukuu utausikia kama Dokta Silaha au Sammy Sixx na usipika.

Baada ya kuona walionizunguka kijiweni ni wasaka ngawira na vyangu wanaoweza kumtumikia yoyote kama toilet tissue niliamua kuunda ufalme wa familia ili kuukwaa ukuu wa kijiwe.

Japo nilimtumia mgosi Machungi wa Makambale na mwanae, hawakunishawishi kutokana na tabia ya mgosi kupayuka hovyo. Hata hivyo tusimlaumu sana. Shule, shule bwana. Hamkuona akina Tambo Hizo walivyochemsha wakitaka kunifurahisha kwa kuwaongopea walevi?

Baada ya kugundua udhaifu wa kambi yangu, nilijipanga upya na kuja na mpya.

Hatua ya kwanza ya kufikia ufalme huu japo uchwara na wa muda ilikuwa ni kuwamotisha bi mkubwa na kitegemezi changu.

Hatua ya pili ilikuwa ni kuwaamrisha vijana wangu wa usalama kuhakikisha nakuwa mkuu tena.

Bila wao zengwe la Zenj lingeninyotoa roho. Maana kama si wao kunishauri nimbebe huyu daktari Blaah Blaali huenda pangechimbika bila jembe. Pia walifanya jambo la maana kunishauri kumtosa wa Kusheini ili asijeharibu dili hapo 2015 kwa kuwa maarufu zaidi ya mshikaji ninayemuandaa kunilinda baada ya kuachia ngazi.

Ilibidi nijipange kweli kweli mimi na nyumba yangu ili kunusuru ulaji na madili yetu ukiachia mbali kuhofia kuja mtu mwingine akatutupa lupango.

Hapa ndipo nilipogundua sayansi ya karne hii ya kuukwaa yaani kuchakachua. Hata hivyo, inabidi niwashukuru waliovumbua uchakachuaji orijino. Nichukue fursa hii kuwashukuru wachakachuaji wa wese walioniwezesha ku-modify kanuni ya uchakachuaji na kuweza kuchakachua kula za kura.

Na bila hii nisingeshinda kuongoza sorry kuibia kijiwe kwa kishindo cha uchakachuaji. Kishindo cha uchakachuaji kilikuwa kikubwa kuliko hata Tsunami. Na niliposema nitashinda kwa kishindo nilimaanisha uchakachuaji.

Sasa wale maadui zangu wakuu wakae mkao wa kuliwa. Hamkuona nilivyomwaga manonihino Sammy Sixx aliyetaka kuangusha ulaji wangu siku za nyuma hadi akasababisha swahiba zangu kama Eddie Ewassa kutimliwa kama kibaka hata kama alikuwa kibaka?

Walipomshauri ahame chata yetu na kujiunga na wapingaji wetu alidharau asijue nilikuwa namlia timing. Maskini Sixx. Hakusoma alama za nyakati na kujua jinsi mambo ya mitandao yanavyokwenda. Hata hivyo, ashukuru Mungu. Bila shinikizo la walevi tungemwengua mapema na akawa anausikia mjengo magazetini kama Selelii na wale wote tuliowaengua kutokana na kufuatilia ulaji wetu.

Hapa inabidi nitoe onyo mapema. Yeyote atakayejifanya kuingilia ulaji wetu ajue atapata cha mtema kuni. Maana kipindi hiki nitakuwa bonge ya dikteta bila kujali lolote. Maana baada ya lala salama hii sina mpango wa kuwania ulaji zaidi ya kutafuta kibaraka wa kunirithi na kunilinda mimi na Tuni Tuni.

Tuendelee na masahibu ya Sixx. Kwa wajuzi wa kiarabu watanielewa. Ukitaka kumla panya huwezi kumuita panya. Unamwita Hamaam al wadi au hua wa wandani. Hata nasi tulipotaka kummaliza jamaa ili asitorokee kwenye ukinzani tulimtisha na hatimaye kumpitisha ili ajidanganye kuwa tu kwenye safari moja. Pia tulimsifu asijue alikuwa anameza chambo! Sasa atakaa benchi na akija na michango yake ya kutaka kuharibu ulaji mtu wetu kwenye kiti kikuu anampiga stop.

Kwanini kukaa na mtu anayepata umaarufu kuliko hata mimi? Sumu yangu ni mtu kujulikana kuliko mimi. Nikiona unaanza kujenga umaarufu na kukubalika lazima nikusukie zengwe uishie bwana. Hata bi mkubwa akijitia kujua kujua na biashara zake na kukaribia kunizidi umaarufu namwacha na kuoa mwingine. Na ngwe hii sitamruhusu kunifuatafuata kila niendako ughaibuni kutanua. Kwanini awe na mtima nyongo wakati ulaji wake nimempa wa kutosha? Nami aniachie nitanue na dogo dogos bwana. Maana maisha ni nipe nikupe.

Kijiwe kimechoka na aibu ya kufichuliwa maulaji yake tena hili likiwezeshwa na mtu aliyedhaminiwa na chata letu la Uchakachuaji. Kwanini mtu anayevunja sera yetu ya kulindana na kujuana asipatilizwe badala ya kuwapatiliza mashujaa kama Ewassa na Chenga? We can't let our kijiwe go to dogs even if we are dogs. But we are big dogs not skinny ones. Samahani nikipandisha mwenembago huwa kiingilishi kinapanda pia.

Pia nichukue fursa hii kuwaonya wapingaji. Nasema. Mtajijeijei mna dola nyie?

Sasa baada ya kuushikilia mjengo wale wapinzani wangu ndiyo wajue nimewamaliza. Maana walipata umaarufu wao kiasi cha kutaka kunitimua kukuu kutokana kupewa nafasi na Sixx. Sasa hamtawasikia tena na lazima uchakachuaji ujao chata langu lazima lipete kama kawa.

Baada ya kuchakachua kula na sasa nafasi ya microphone, ngoja muona washirika wangu ama watoto zao watakavyojaa kwenye baraza langu la wezi sorry mawaziri. Washikaji wangu wawe wa kike au wa kiume lazima wapete na kupetuka wakati nyie mkiteseka. Hata hivyo msikonde. Nshasema: raha jipe mwenyewe usingoje kupewa.

Na kwa wale waliotaka kuingilia mbio zangu za kurejea kwenye ulaji wajue sitawasamehe. Wasidanganywe na bashasha zangu. Mie ni katili kuliko mnavyoniona au kunidhania. Anayebisha akawauliza akina Babu Seya na hata Sixx.

Msichachawe na kuchanganyikiwa bure. Bado sijamaliza majadiliano na bi mkubwa na kitegemezi changu kuamua nani aingie na nani atemwe.

Utemaji wa Sixx haukufanywa na bunge langu kuu yaani bi mkubwa na kitegemezi changu. Huu ulifanywa na kina Ewassa, Roast Tamu, Endelea Chenga na Mgosi Machungi Makambale. Kawaida ya chama chetu ni kumruhusu anayemaliza muda kugombea tena. Lakini kwa kesi ya Sixx hatukuwa na jinsi. Ilibidi kuukiuka huu utaratibu wetu. Najua wengi watasema mimi ni mnafiki kwa vile niliwazuia waliotaka kugombea ulaji wakati mie ndiyo nilikuwa bado incumbent kama Sixx.

Hata hivyo mgosi Makambale asiwatie hofu. Licha ya kudhoofu kiakili na kiafya, nshamchoka kutokana na kuniletea matatizo kutokana na kupayuka kwake kusiko na mantiki wala maana. Kwanza amenitisha. Mie nimesotea ulaji na ukuu. Hivyo, ninastahili kuwaingiza kwenye ulaji wangu bi mkubwa na kitegemezi changu. Bila kutoa jasho lolote eti naye analeta kitegemezi chake kuunda ufalme mwingine ndani ya ufalme wangu. Lazima muhura huu nimtimue ikiwezekana nichukue kifaa toka Somalia.

Hata hivyo, lazima nitafakari. Kifaa toka Somalia kina nongo nyingi hasa kugundulika kuwa kinajihusisha na utoroshaji nyara. Lakini hata hivyo nani anajali iwapo mimi ni yote katika yote na juu ya yote? Hapa ni kuwashawishi washirika wangu yaani bi mkubwa na kitegemezi wakikubali na wasikwaruzane nacho kutokana nao kuwa na dili zao. Hivyo kwa mtu mwenye kusaka ngawira kama wao lazima kuwepo na mgangano nisipokuwa makini.

Naona shangingi la Mr Sixx likipita! Acha nimmpe pole kwa kulipiziwa kisasi Njaa Kaya bin Mchakachuaji.
Chanzo: Tanzania Daima Nov. 17,2010.

Friday 19 November 2010

Kumbe na miamba hutikiswa!



Simba anapogeuka mbwa!






Laiti wengi wangejua kuwa lengo la Maalim Seif Shariff Hamad ni kutafuta utukufu na ulaji binafsi, wasingemwanga damu zao kule Zanzibar. Sijui hii inajenga picha gani ambapo Seif amegeuka kiraka cha CCM nyongeza ya Augustine Mrema? Je ni wangapi watafuata matumbo yao na kutelekeza vichwa vyao ukiachia mbali nadhiri? Je kuna uuaji wa demokrasia wa kutisha kama huu? Kila wafanyapo dili zao wanasingizia amani na mshikamano. Je twaweza kuwa na amani na mshikamano vya kweli bila kutenda haki? Je amani na mshikamano vyaweza kushamiri sambamba na ufisadi wa wazi wazi na utawala wa kujuana,familia na kulipana fadhila? Je amani na mshikamano vyaweza kuletwa na watawala walioingia kwa uchakachuaji badala ya kura halali? Je kutanua au kulikwepa tatizo siyo kujipalia mkaa? Mbuni ana tabia moja ya kihayawani. Pindi amuonapo adui hufutika kichwa chake kwenye mabawa yake. Je hulka hii yamfaa mwanadamu tena aitwaye kiongozi? Tafakarini na jadilini.

Thursday 18 November 2010

Msaidieni Vladimir Putin jamani

Kumbe mbwa kwa watawala ni mali kuliko umma!
Je angekuwa mtawala wako ungemshauri nini?

Je hili ndilo wanalohitaji Warusi?







The three-month old Karakachan dog was a gift from Mr Putin's Bulgarian counterpart after Moscow and Sofia signed a series of accords to boost the South Stream gas pipeline.

A government statement on its official website said anybody could send in a suggestion for the dog's name.

News of the contest received a mixed reception from people on the streets of Moscow.

One commuter said: "I won't be taking part in the contest because I am not concerned about the President's dog. There are many more serious things to ask the people of this country. I won't be taking part."

The puppy will have to share the spotlight with Putin's beloved black Labrador Connie, who is 11.

Wednesday 17 November 2010

Wananchi wanapouchoka utawala mfu




Picha hii inaacha maswali mengi kuu likiwa, kama tumefikia hapa nani atamtetea na kumlinda mwananchi? Je hawa polisi wanamlinda nani na anawalipa nani? Je hapa mwenye makosa kati ya mwenye rungu dola na bunduki ni nani? Je ni kwanini mwanamme mzima ameamua kuchukua sheria mkononi tena dhidi ya dola lenyewe? Je kwa namna hii bado kuna kondoo wa kuchinja au punda wa kutwisha kila uchafu kama ilivyotokea kwenye uchakachuaji hivi karibuni?
Hivi jamaa huyu wa Uganda angepandikiziwa mbunge kama ilivyotokea Danganyika, huyo mbunge nyemelezi na pandikizi angepona masumbwi ya jamaa huyu? Je wabongo hapa tunapata somo gani hasa wakati huu tunapotawaliwa na serikali fisadi itokanayo na EPA NEC na zoezi zima la uchakachuaji? Je namna hii mlipa kodi ana haja ya kuendelea kuwalipa mishahara watesi wake ili wamtese?
Jibu unalo wewe unayesoma.

Kikwete aendelea kuwalipa fadhila waliofanikisha EPA


-------------
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete,amefanya uteuzi wa Wabunge watatu(3)kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1)(e)ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa na kupewa mamlaka ya kuteua Wabunge 10.

Wabunge walioteuliwa ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha,Prof.Makame Mnyaa Mbarawa na Ndugu Zakia Hamdan Meghji.

Rais atateua wengine waliosalia siku zijazo.

Rais Kikwete ameshawasilisha majina ya wateule hao kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Anne Semamba Makinda(Mb)kwa ajili ya hatua zipasazo.

MWISHO

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dodoma
17 Novemba, 2010

Sunday 14 November 2010

Siku rais alipopewa ofa ya ngono!

Je angepewa ofa hii rais wako ungemshauri nini?
Soma habari mwenyewe uamue.








Author's sex-for-nuclear-veto offer to German president
German writer Charlotte Roche offered in an interview Sunday to spend the night with President Christian Wulff if he votes against government plans to extend the lifetime of Germany's nuclear reactors.
ADVERTISEMENT

"I am offering to sleep with him if he does not sign," the 32-year-old anti-nuclear activist told the weekly Der Spiegel.

"My husband agrees. Now it is up to the First Lady to give her consent," she said. "I am tattooed."

Roche, British-born author of the sexually explicit 2008 bestseller "Wetlands", took part in major demonstrations last week against the transport of radioactive waste that underlined unease in Germany over nuclear power.

Wulff has to decide this year if a law prolonging the lifetime of the country's 17 nuclear reactors by up to 14 years should be enacted without the consent of the Bundesrat, the upper chamber of parliament that represents the regions.

The hotly disputed plans were approved by cabinet in September and will postpone by more than a decade to around 2035 the date when Europe's biggest economy abandons nuclear power.

Saturday 13 November 2010

Je waweza kuamini ghorofa 15 kujengwa ndani ya juma moja?


As the United States and China battle over the finer points of currency manipulation at the G-20 summit, American negotiators may want to take note of this startling testimonial to the productivity of Chinese workers: A construction crew in the south-central Chinese city of Changsha has completed a 15-story hotel in just six days. If nothing else, this remarkable achievement will stoke further complaints from American economic pundits that China's economy is far more accomplished in tending to such basics as construction.

Hongera maalim Seif na Lipumba kurejea CCM




Wengi wanajiuliza kama siyo kushuku. Je usuhuba na ushirika wa mwenyekiti wa CUF na katibu wake na CCM una tija kwa taifa kwa namna yoyote?. Je usuhuba huu utadumu? Je ushirika huu utaikuza au kuiua demokrasia nchini? Je kupewa kipande cha utawala visiwani kutalinufaisha taifa au kuliweka msambweni? Je CUF kama TLP ndiyo imerejeshwa CCM?

Kwanini serikali ya umoja wa kitaifa upande mmoja na si nchi nzima? Je ushikaji huu ni kwa maslahi binafsi au ya wanachama? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Wednesday 10 November 2010

Tanzania Elections a Shame

Though Tanzania has always been regarded as a strong and peaceful country in the region, this no longer holds water thanks to what transpired in the just ended elections. Marred by violence, allegations of bribery, and other irregularities, the elections left the country paralyzed and tarnished.

The presidential candidate who secured the second position, Dr. Wilbrod Slaa of Chama cha Demokrasia na Maedeleo (CHADEMA), has nary conceded defeat claiming that the rigging was done by the National Intelligence Service. The elections were not free and fair by all standards. How could it be with the turn out of just 8,398,394 equivalent to 42.8% of the 20,137,303 registered voters?

Kikwete scooped 5,276,827 votes equivalent to 61.17% as opposed to the landslide of over 80% he enjoyed when he first came to power in 2005. Dr. Slaa came second with 2,271,941 votes equivalent to 26.34% whilst the third Pro-CCM contender Professor Ibrahim Lipumba of Civic United Front (CUF) did away with 695,667 equivalent to eight percent. Other four contenders from small parties shared the rest.

The low turnout was reportedly a plot by the NEC whereby many young voters did not find their names at polling stations. Much affected areas involved opposition strongholds in big cities. Apart from that, there were delays and logistical handicaps almost everywhere.

Sensing the danger after Dr Slaa asked Pro-CCM National Electoral Commission (NEC) to stop announcing doctored results, Mr. Kikwete was hurriedly sworn in a day after NEC declared him a winner with a slim winning margin though.

The ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM), despite all massive rigging saw over 50 of its MPs lose including five ministers, prominent being that of Home Affairs Lawrence Masha, a friend and partner of Kikwete's son.

Violence was reported in various places whereby people were injured and houses set on fire. During and after the campaigns, five people were attacked by machetes in Mara and many more in Busanda. Over ten houses were set on fire in Shinyanga not to mention chaos in Mwanza, Mbeya, Kagera, Morogoro, Kigoma and Dar es salaam where Field Force Unit (FFU) used tear gas to curb demonstrators.

Tanzania used to broker peace for other countries in the region such as Kenya and Zimbabwe, bringing about Governments of National Unity (GNU). Recently the same thing was reached in Zanzibar, not under the efforts of Kikwete, but the fear of The Hague.

In the just ended dirty campaigns, religion, nepotism and tribalism took a fore stand. Dr. Slaa was accused of being a Christian who was sent by Vatican despite quitting from the cloak many years ago. Muslims campaigned openly for Kikwete a Muslim. Another undemocratic anathema was the use of paid-up tabloids to unleash abuses and fabrications against Kikwete's arch foe namely Dr Slaa. The police force too was used to intimidate people.

Kikwete’s government has been accused of many wrong doings including mega scandals such as robbing over $ 100, 000, 000 from Central Bank under the External Payment Arrears (EPA) account whose money went to the campaigns of Mr Kikwete. Another shocking scandal that saw former Prime Minister Edward Lowassa booted out is Richmond. In this scandal, billions of schillings were stolen under the pretext of providing emergency power utility that never was.

In a nutshell, CCM is slowly and gravely losing its wand that saw it rule the country since independence. Tanzanians are vehemently agitating for changes after being tired of status quo. Like Kenyans, they badly want a new constitution. One eminent question still remains unanswered: Is Tanzania, yet again, going to dogs?

Source: The African Executive Magazine Nov. 10, 2010

Umma umetoa onyo kwa vigogo CCM

HAKUNA shaka kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilishiriki uchaguzi kikiwa na matokeo.

Kilishaandaa uchakachuaji baada ya watanzania kutohongeka kwa ahadi na upuuzi mwingine. Kilishajua walivyokichoka kiasi cha kutegemea nguvu ya ziada ambayo nayo haitasaidia kama umma utaendelea kusimama imara.

Na kama si kuogopa kufikishwa The Hague kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), kwa kichwa ngumu na ukatili wa watawala na polisi wetu, tungeshuhudia makubwa kuliko haya tuliyoshuhudia.

Kura zingeibiwa sana ukiachia mbali watu wengi kuuawa au kujeruhiwa. Maana tamaa ya mali ya watawala wa sasa na genge lao inajulikana fika.

Nani alijua kuwa nyasi zingeangushwa vigogo? Wako wapi kina Lawrence Masha aliyekuwa amekaririwa akijisifu kupita bila kupingwa asijue atapigwa chini? Wako wapi kina Basil Mramba, Monica Mbega, Diodorous Kamala, Nazir Karamagi, Baltilda Baruan bila kuwasahau kina John Malecela na vigogo wengine wenye nafasi zao?

Kushindwa kwa CCM kulianzia ndani mwake kwenye zoezi la kuchagua wagombea wake pale rushwa na vitisho viliposhindwa kufua dafu ingawa vilitawala matokeo.

Bahati mbaya CCM ilizidi kujipa moyo ikitegemea majimbo yake makuu ya ushindi yaani Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na makuadi wengine waliopenyezwa kwenye zoezi zima la uchaguzi lililoishia kuwa uchakachuaji na wizi wa kutia aibu.

Nani alitegemea CCM yenye wagombea wengi wenye tuhuma za ufisadi na kughushi kushinda? Nani alitegemea Kikwete kushinda kwa kutoa ahadi zaidi ilhali hajawahi kutekeleza hata moja?

Nani angebariki siasa na sera za ubadhirifu, utapanyaji, kujuana, udugu, ukosefu wa sera na dira na vitu kama hivyo? Nani angebariki rushwa na mawazo mgando yaendelee kututawala ilhali kulikuwa na mbadala yaani CHADEMA?

Umma si haba umetoa onyo na tangazo kuwa umechoka na upuuzi wa kurudia kuchagua watu wasio na sifa wala uwezo wa kuongoza bali kuiba.

Tunaambiwa imepoteza majimbo kama 50 pamoja na kutokea wizi wa kura wa kutisha. Je, haki ingetendeka zaidi ya kubaki kwenye vitabu vya historia chafu, CCM ingekuwa wapi?

Kuna watu waliishajibinafsishia ubunge hata uwaziri. Walishajiona kama wao ni kila kitu na bila wao nchi haiwezi kutawalika. Nani angeamini kuwa watuhumiwa wakuu wa ufisadi wangeruhusiwa na chama kinachojinakidi kuleta ukombozi kusimama kwenye uchaguzi?

Pamoja na wengine kupigwa panga la umma, wengi wamerejeshwa na uchakachuaji. Ni aibu na hasara kwa taifa. Ni mwanzo wa kiama chake kama hatutaanzisha kiama chao.

Nani aliamini kuwa mgombea wa CCM rais aliyemaliza muda wake angesimama bega kwa bega kuwashawishi wananchi waathirika wa ufisadi wawachague mafisadi?

Pamoja na kutajwa kwenye ‘list of shame’ na kuuchuna, kwa kusimama na mafisadi naye amejidhihirisha alivyo mmoja wao.

Kuna kitu kimoja ni wazi na kinafurahisha. Kama CCM itaridhiwa itawale kwa ushindi wa kuchakachua, ijue fika 2015 kitakuwa kiama chake taka usitake. Na kwa mtaji wa watu wachafu walioshinda kutegemea jinai, CCM haitabadilika wala kujirekebisha. Imeishachafuka kiasi cha kutosafishika.

Ingawa wakubwa wetu wamepoteza macho na masikio hasa kuiona haki na kusoma alama za nyakati, tunahitaji kuvunjilia mbali tume ya uchakachuaji na kuliweka chini ya uangalizi Jeshi la Polisi. Maana wamethibitisha wasivyo pale kututumikia bali kutumiwa na kundi dogo la waharifu.

Ingawa baadhi ya waangalizi wa kitaifa waliusifia uchaguzi kutokana na kudanganywa na utulivu wa siku ya kwanza, uchaguzi haukuwa huru. Rejea vitisho kabla ya uchaguzi ukiachia mbali uchakachuaji uliofanyika baada ya zoezi zima la uchaguzi.

Rejea kucheleweshwa matokeo bila sababu zaidi ya kuyapika na kuwapitisha wateule wa CCM.

Wananchi kimsingi walifanya uchaguzi wa amani tume ya uchaguzi ikawaletea fujo kupitia uchakachuaji na ucheleweshaji matokeo ili kuchakachua kama tulivyoona.

Baya zaidi, kama alivyodai mgombea urais wa CHADEMA, Willibrod Slaa, wanaofanya hivi ni usalama wa taifa.

Hawa kama tungekuwa na uongozi hata utawala adilifu walipaswa walinde demokrasia na siyo kuwa maajenti wa ufisadi na uchakachuaji. Hawa si usalama wa taifa bali uhasama na zahama na aibu ya taifa.

Kilichotokea baada ya uchaguzi yaani uchakachuaji wenye kila baraka za CCM, unabadili maana ya jina lake na kuwa Chama cha machakachuzi.

Inatisha na kukatisha tamaa. Watawala wanaotokana na uchakachuaji na si ridhaa ya wananchi hawafai na ni waharifu tu. Uchakachuaji licha ya kuwa uhuni ni jinai na utalipeleka pabya taifa. Licha ya kuilaani jinai hii, tunapaswa kuipiga vita kwa gharama zozote. Tusitishwe na kudanganywa na amani mawenge ambayo hutegemea ukondoo na si utendaji haki. Hatuwezi kuishi kama taifa la kondoo tukafika ilhali tukitawaliwa na fisi na mbwa mwitu.

Kuna haja ya kusimamia haki zetu kwa namna yoyote bila kutishwa wala kudanganywa. Tusiogope mabomu. Watatupiga mabomu lakini si risasi. Nani anataka kwenda kunyea debe The Hague?

Na bila ya The Hague vurugu tulizoshuhudia zingeondoka na watu kwa kifo cha risasi za moto. Hii ndiyo siri ya mafanikio yetu.

Na ndiyo maana Slaa kugomea matokeo hajachelewa wala kupoteza. Alluta continua na Mungu ibariki nguvu ya umma dhidi ya nguvu ya mafisadi.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 10, 2010.

Uchakachuaji kila pahala, tunapelekwa wapi?

BABA yangu mzee Msemahovyo kumbe alinidanganya! Si alinifundisha kuwa mvumilivu hula mbivu! Maskini hakujua mambo yangebadilika na mvumilivu kuishia kupigwa mibomu ya machozi na kuchakachuliwa kura na kula yake!

Mie nitamfundisha kijogoo wangu Kapayukaji kuwa aliyeko juu mpandie kama ambavyo Silaha atawapandia Nambari chakachua wahedi.

Hivi kaya hii inapelekwa wapi? Mama akienda mwanamanyala kujifungua anachakachuliwa mtoto na kubambikiziwa asiye wake.

Ukienda polisi unachakachuliwa na kubandikiwa kesi za madawa na upuuzi mwingine. Ukienda banki kubwa watu wanachakachua na kutoka na EPA! Tukubaliane. Hii kaya ya Danganyika sasa imeongeza sifa. Ni kaya ya Kuchakachua. Sijui tuiite Chakachua au Fisidika? Mie sijui.

Baada ya kushuhudia kufuru, uonevu, jinai na mazabe mengine ambayo sikutegemea kuona kwenye uhai wangu, nilikaa pembeni na kutafakari nini cha kufanya kuepuka kurudiwa. Nafanya hivi kuepuka kujidanganya kama kaya na wanadamu. Nafanya hivi si kwa kumuudhi wala kumfurahisha yoyote bali Mungu na taifa.

Hii yote inatokana na walevi kupiga kura kwa ufanisi na amani vya hali ya juu lakini uhasama wa taifa wakazichakachua ili kumbeba msukule wao. Simtaji jina. Kwani hata kuku wanamjua. Kama humjui basi utajiju mwenyewe.

Tusipojiangalia vizuri, tutaiweka kaya njia panda na kuitapakaza damu bila sababu. Kwanini uroho wa kikundi kidogo cha waharifu utufikishe huku? Lazima watu wenye akili na udhu kama mimi waonye na kuonyesha njia. Acheni jinai hii Njaa Kaya na wenzako. Mtaipeleka kaya kuzimu kwa tamaa na upogo na upofu wenu.

Kutokana na taaluma yangu ya utafiti na upayukaji, nimegundua kuwa kaya yetu ina matatizo mengi, kubwa likiwa ni waharifu wachache kugombea ulaji hata kwa gharama ya damu ya walevi wasio na hatia.

Watu wako tayari kuwanyotoa wenzao tena wasio na hatia roho ili waendelee kuinyonya na kuinajisi kaya. Wameigeuza kaya mateka wao kiasi cha kudhani bila wao haiwezi kuwepo wala kutawalika. Huu ni upuuzi na kujidanganya vya hali ya juu. Na anayeamini katika jinai hii ya uchakachuaji ameisha na kuishiwa na hatufai hata alazimishe vipi.

Hili halikubariki wala kuvumilika ingawa kuna wapuuzi wanatushauri tuvumilie wakati tunapukutishwa kama majani. Kwanini hawa watanguliza matumbo wasivumilie. Kwanini sisi kuwavumilia watu wasiotumilia kwa miaka yote waliyotuguguna?

Kuondokana na adha ya niliyoshuhudia wakati wa harakati za uchakachuaji ili kuwezesha misukule na marehemu kuwala walevi, nimegundua kanuni rahisi. Japo wanafiki ambao kimsingi ni madikteta na wezi wa kawaida hawapendi waambiwe ukweli kuwa ni waharifu na wanafiki, kuna haja ya kujikaza kisabuni na kutangaza ufalme kwenye kaya yetu ili kuepusha vita ya mibomu na mibunduki niliyoshuhudia.

Nani angeamini kuwa watu tusio na hatia tungepigwa mibomu ya michozi ili kuachia wezi waibe kura zetu? Nani angeamini kuwa walevi wangekatana mapanga na kuchomeana nyumba kutetea haki zao?

Nani angeamini kuwa, kwa upande wa pili, kuna walevi wendawazimu na vyangudoa ambao wangeweka maisha yao hatarini kuwatetea majambazi wa kisiasa kama ilivyotokea kule Musoma, Buzwagi, Shinyanga na kwingineko?

Ajabu na aibu ni ukweli kwamba kuna wenzetu ambao wako tayari kuwaumiza wenzao wakiwatetea mabwana zao wanaowalipa makombo yatokanayo na jinai ya kutusaliti na kutuchuuza!

Nani angeamini kuwa kodi ya walevi ingetumika kununua mibomu ya michozi na kuwalipa wahuni waliotupiga mabomu badala ya kununua madawa na vifaa vya elimu?

Nani angeamini kuwa deni la nje la walevi lingeumka kugharimia upuuzi huu? Halafu wanaotenda jinai hii bado wanajiaminisha na kutuaminisha kuwa wanafaa kututawala! Thubutu! Hatukubali kutawaliwa na wezi na wachakachuaji hata watutishe vipi. Hapa ndipo tunapopaswa kumuunga mkono shujaa Silaha aliyeamua kuwekea ngumu jinai hii hadi kieleweke.

Kama tutashindwa kusimama na kuondosha jinai hii na genge hili basi tufanye jambo moja kieleweke. Kuondokana na hili japo ni aibu, nashauri: tutangaze ufalme ambapo mfalme Njaa Kaya na malkia zake wa uharibifu kina Shari Salima na Rahma Kasigasiga wawe malkia.

Njaa mwenyewe aende kwa shoga yake Mswati kujifunza jinsi ya kutawala kifalme badala ya kutegemea mafisadi na majambazi waitwao uhasama wa taifa.

Mambo hayaishii hapa. Lazima mwana wa mfalme Riziki Njaa Kaya awe mwana mrithi wa mfalme. Mambo namna hii yatanoga na kuepusha hujuma za kipuuzi kwa watu wasio na hatia.

Ingawa sipendi wafalme kutokana na kuwa madikteta na wanyonyaji wa kawaida wasio na lolote la maana zaidi ya kujikweza na kuvuna wasipopanda, kwa hali iliyojitokeza sina namna. Badala ya kuwa na rahisi aliyezalishwa na uchakachuaji wa kina Kivuitu Kiravuuu na Louis wa Ukame, heri tuwe na mfalme na washauri wake kina Ewassa, Endelea Chenga na wengine.

Najua wasomaji wangu wengi watashangaa kwanini shujaa na jabali kama mimi nabwaga manyanga. Sijabwaga manyanga.

Naona huruma jinsi walevi wanavyoteswa. Nawatukana kwa kutaka tuwe na mfalme ili wachukie na kukataa na kusimama na kupata haki kwa njia ya kidemokrasia.

Baada ya wahusika kukataa zoezi la uchaguzi basi tutumie lile kali la migomo na maandamano tuone kama hawatang'oka na tukawa huru. Tena nataka hapa nieleweke. Sifanyi uchochezi.

Wanaofanya uchochezi ni wale wanaotuchokoza kwa kufanya uchakachuzi na matumizi ya maguvu tena kwa vyombo vyetu vya umma wa walevi.

Najua fika kuwa kuwa na mfalme ni matusi ingawa tulishatukanwa sana tusi hili kwa kisingizio cha uchaguzi. Nani hajui kuwa walevi, kwa miaka mitano iliyopita, walitawaliwa na ufalme wa familia fulani iliyojificha nyuma ya chama?

Nani hajui kuwa kwa sasa mkuu wa kaya hajulikani kati ya mwanae yeye na mkewe ukiachia mbali wafadhili wake ambao ni mafisi na mafisadi?

Nani hajui hili nimjuze vilivyo? Nani anabishia hili aje na hoja za kupiga na si mizengwe ya kutishia waandika magazeti ilhali wao waliwatumia wale wale kuwachafua wenzao japo hili halikufua dafu?

Nani hajui kuwa tuna watu wachafu patakatifu pa patakatifu wakifanya kila aina ya uchafu? Nani hajui kuwa hawa wezi waliingia huko kwa pesa ya HEPA na Richmonduli? Nani hajui kuwa hawana lolote zaidi ya ajenda ya siri ya kutufanya shamba la bibi kwa ajili yao na vimada wao?

Ni upuuzi watu wazima kufanya mambo ya kitoto. Ngoja niondoke hapa karibu na ofisi ya kuhesabia kura wasijenipiga mibomu mingine.
Chanzo: Tanzania Daima Novemba 10, 2010.

Tuesday 9 November 2010

Hongera maalim Seif na Lipumba kurejea CCM kinamna




Wengi wanajiuliza kama siyo kushuku. Je usuhuba na ushirika wa mwenyekiti wa CUF na katibu wake na CCM una tija kwa taifa kwa namna yoyote?. Je usuhuba huu utadumu? Je ushirika huu utaikuza au kuiua demokrasia nchini? Je kupewa kipande cha utawala visiwani kutalinufaisha taifa au kuliweka msambweni? Je CUF kama TLP ndiyo imerejeshwa CCM?

Kwanini serikali ya umoja wa kitaifa upande mmoja na si nchi nzima? Je ushikaji huu ni kwa maslahi binafsi au ya wanachama? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Monday 8 November 2010

Uchakachuaji, amani gani inaletwa na dhuluma?




Watanzania tuna tabia ya kujisifia upuuzi hasa watawala wetu. Huwa tunaona fahari hata kusifiana upuuzi na ujinga. Utamsikia mtu akisema Tanzania ni nchi ya amani wakati haina haki! Hivi amani inaweza kuwapo wapi bila kuwapo haki?

Hali hii imejitokeza baada ya watanzania kujihimu na kupiga kura kwa wingi ingawa ziliishia kuchakachuliwa kiasi cha kupachikiwa washindi ambao kimsingi walishindwa.

Hakuna kitu kilinifurahisha na baadaye kunisikitisha kama jinsi uchaguzi (uchakachuaji) ulivyoendeshwa na hatimaye kuharibika.

Kwa aliyefuatilia, siku ya kwanza ya uchaguzi, licha ya kuanza kwa vituko hapa na pale na wapiga kura na umma kuvivumilia, angalau wananchi walipiga kura kwa amani. Uchaguzi ulionekana kuwa uchaguzi kiasi cha kutia moyo. Lakini baada ya tume ya uchaguzi kuanza mizengwe na uchakachuaji, maana nzima ya uchaguzi ilikufa hapo hapo na kuzaliwa dhana chafu ya uchafuzi na uchakachuaji. Baada ya hapo, usalama wa taifa kama inavyodaiwa, wachakachuaji wenyewe wanaotaka kurejeshwa madarakani wameuharibu uchaguzi kiasi cha kuwa vurugu ujuha na jinai nyingine.

Hii imepelekea chama kikuu cha upinzani Chadema kusema wazi kuwa hakitatambua matokeo ya kupikwa na watawala wa kupachikwa na kundi la wasaka ngawira na wateule wa yule yule anayebebwa bila hata chembe ya aibu na kujali mstakabali wa taifa.

Tumekuwa tukionyana kuepuka yaliyojiri nchi jirani kama Burundi Kenya hata Rwanda bila kujingalia vizuri tabia na mienendo yetu! Ni unafiki kiasi gani?

Sikutegemea mtu ambaye aliingia madarakani akiitwa chaguo la Mungu, kugeuka ghafla na kuwa chaguo la wachakachuaji na mafisadi. Sisemi haya kumkejeli mgombea wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete. Nina sababu nuzuhu.

Kwanza, ukiangalia hata namna alivyofanya kampeni kwa kutegemea mke na mtoto wake na genge lenye kutia shaka hasa pesa iliyomwagwa bila kuelezwa ilikotoka, inatosha kukuonyesha ni kiasi gani maji yalishazidi unga. Ukirejea nyuma kutathmini aliyofanya angalau nusu ya aliyoahidi, huoni kitu. Ukiangalia namna kampeni zake za kutumia magazeti nyemelezi na wachumia tumbo kuwachafua wenzake, unagundua ni kwanini madai kuwa ameiba kura yana mashiko tu.

Pili, ukiangalia ahadi za wazi za uongo alizotoa tena lukuki unajua fika kuwa jamaa alikuwa akitafuta kupata ngwe ya pili ikulu kwa kila namna bila kujali kama alichokuwa akifanya kinawezekana.

Tatu, ukiangalia chama chake kinavyozidi kuunga mkono kila upuuzi wa tume ya uchaguzi, unagundua fika jinsi ambavyo wako nyuma ya kila kinachofanyika kiasi cha kushindwa kuelewa nani mwenye mamlaka nchini kati ya chama na tume ya uchaguzi.

Na hata ukiangalia matamko na uendeshaji wa nchi, hutashindwa kumaizi kuwa CCM ina nguvu na ushawishi kuliko serikali. Reja CCM kuamrisha benki kuu kuruhusu ujambazi wa EPA ambao kama ambavyo imekuwa ikidaiwa bila kukanushwa ni mtaji uliomwingiza madarakani Kikwete anayetuhumiwa kuvuruga uchaguzi na kuiba kura na chama chake kisikanushe.

Inashangaza kusikia watawala wa CCM na hata washirika zao toka Ulaya wakiwahimiza watanzania kukubali matokeo yaliyochakachuliwa eti kwa kisingizio cha kulinda amani na mshikamano wa taifa. Kwani mwenye dhamana ya kuwezesha kuwepo amani ni wananchi na wapinzani tu? Kwanini CCM waibie watu wasiogope amani itatoweka? Na ni wapi kunaweza kuwapo amani ya kweli bila kutenda haki?

Anayelitakia amani taifa hili ni yule atakayetenda haki. Na kutenda haki katika uchaguzi ni nguzo ya amani na mshiamano lakini si kuwavumilia waharifu fulani waendelee kufanya uharifu. Kinyume cha hili wa kulaumiwa ni hawa hawa wanaolalamikiwa ambao wanaweza kutumia raslimali za taifa ukiachia mbali kuiba ili waweze kuendelea kuwa madarakani. Huku ni kuishiwa kwa kila hali na watu wa namna hii hawafai kukaa madarakani hata kwa nukta moja?

Rais atokanaye na wizi wa kura ni mwizi na fisadi wa kawaida tu na atakapokuwa madarakani atawajali na kuwatumikia waliomwezesha kuchakachua na si wananchi waliomnyima kura hadi akategemea uchakachuaji. Hivyo,

kumruhusu mtu wa namna hii ainajisi nchi kwa miaka mitano ni upumbavu ambao hata kuku hawezi kufanya. Katiba yetu inasisitiza haki. Maadili yetu yanatufundisha kuifia haki. Sasa ni wakati wa kuyaweka haya kwenye matendo ili liwe somo kwa dunia.

Hivi inaleta picha gani kusema eti wapinzani wapokee matokeo hata kama wanachoambiwa wapokee ni matusi kwao na hujuma kwa taifa? Je kwanini wananchi walipoteza muda wao kwenda kupiga kura ilhali matokeo yalishajulikana? Kweli kulikuwa na haja ya kupoteza pesa na muda kwenda kupiga kura ambazo zisingezingatiwa na uamuzi kuzitegemea? Tujalie wapinzani wajifanye mabwege wakubali kuibiwa na kupokea matokeo ya kupikwa. Je hii haiwezi kumaanisha kuwa wapinzani ni wapuuzi, mataahira, waongo na matusi mengine kama hayo? Kwanini wakubali kuibiwa kirahisi hivi na mchana kweupe tena haki yao ya kikatiba? Je huku si kuwachokoza na kuwaangusha watanzania? Kwanini watu, hasa hawa wanaojitia kuwa wafadhili na wasimamizi wetu, hawataki kusikiliza madai ya upande wa pili? Je wanataka kutupandikizia rais kama walivyotupandikizia magavana wakati wa ukoloni? Watanzania tusikubali kudanganywa wala kutishiwa nyau. Maana hii nchi ni yetu sote kwa sawa. Kwanini amani yetu itegemee woga badala ya misingi yake?

Inshangaza kuona uchaguzi unaharibiwa nasi tunashauriwa tukae kimya na kubariki wizi na uchakachuaji! Anayetushauri hivi hatutakii mema hata kidogo. Hata hivyo ulitegemea nini kampeni kusimamiwa na watu wenye rekodi chafu za uovu ambao hata ndege anaujua?

Nani alitegemea wapiga kura wa Tanzania wawe majuha kuchagua mtu aliyebariki wizi wa EPA. Bila aibu hata kuchelea kuwa wanachosema kina walakini, wanatushauri tukubali kuingizwa mkenge kwa mara ya pili! Nani anatulazimisha kuwachagua watu wanaowastahi wezi wa EPA ambao waliitikia wito wa rais wa kurejesha fedha hizo kabla ya Novemba 31 mwaka juzi.

Je serikali ambayo, kimsingi, ni Kikwete aliyewahi kusema eti aliwashauri wezi wa EPA warejeshe pesa ya wizi, ilifanya hivyo kama nani na kwa msingi gani kama siyo kulea na kuficha ufisadi wanakosema wapinzani? Hili ndilo watanzania walipinga kupitia sanduku la kura.

Mambo yaliyowaudhi wananchi hadi wakatoa adhabu ni mengi. Walizingatia yafuatayo na kuyatolea majibu kwa kutoichagua CCM.

Hawakusahau maneno ya rais aliyemaliza muda wake. Rais aliwaambia warejeshe pesa kama nani wakati kazi hii ni ya mahakama kama yeye si mshiriki na mnufaika wa wizi wa EPA-kama wanavyodai wapinzani? Je kwa kufanya hivyo, licha ya kuvunja katiba na sheria, rais hakusaidia mafisadi kuendelea kuiba wakijua hakuna wa kuwagusa-kwani, ama wapo juu ya sheria au kuna mtu wao aliye juu ya sheria wa kuwalinda kwa sababu azijuazo? Je huu si ushahidi tosha kuwa Kikwete hajapambana na ufisadi kama anavyojidai?

Kwanini rais aingilie mamlaka na uhuru wa mahakama huku akipindisha na kuvunja sheria kama hakuwa na maslahi au kuwa mhusika kamili? Je huu si ushahidi tosha kuwa rais na chama chake hawafai na hawako pale kwa manufaa ya umma bali ya mafisadi wanaowakingia kifua? Je kwa ushahidi huu wa mazingira haitoshi kusema kuwa Kikwete hafai na amewaangusha wananchi vibaya? Je mtu akisema Kikwete Toka anamkosea adabu au kumuonea? Kikwete toka hii inatosha. Na tuseme tena kwa kupaza sauti sana.

Kuthibitisha ushiriki na unufaika wake, licha ya kuvunja sheria, rais alificha hata majina ya hao mafisadi na wezi waliorudisha hiyo pesa. Kwanini na anaogopa nini? Je mtu au wapinzani wakisema kuwa rais aliamua kuwaokoa watuhumiwa kwa vile ni washirika na wawezeshaji wake atakuwa anadanganya? Kama kusema hivyo ni uongo, ukweli ni upi zaidi ya huu?

Kama rais wetu na serikali yetu wamegeuka mabwana na mabibi huruma, mbona hatuioni hiyo huruma kwa vibaka tena wa kutengenezwa na serikali yenyewe iliyomo kwenye kitanda kimoja na mafisadi?

Nani angemchagua rais kama huyu ambaye hata aliogopa kushiriki midahalo ukiachia mbali kutofanya lolote la maana kwa miaka mitano? Hawa wanaotwambia tukubali matokeo bila kuzingatia haya ni maajenti wa maafa ya taifa.

Hata kama CCM 'imeshinda' uchaguzi huu kama mazingira yanavyotengenezwa, haitakaa iwe salama zaidi ya kuwa kongwa na aibu kwa taifa. CCM haiwezi kupitisha watuhumiwa wote wa list of shame kugombea urais na ubunge ikawa salama. Hebu watetezi wa uchakachuaji huu watueleze. Watuhumiwa wa list of shame waliotajwa wazi wazi wako wapi zaidi ya kuendelea kuhifadhiwa na CCM na serikali yake? Je kwa kuendelea kuwahifadhi na kuwapitisha kugombea na hatimaye kuwawezesha kushinda ili kuongoza nchi yetu siyo ukweli kuwa CCM inaongozwa na list of shame? Ziko wapi kesi zilizotishiwa kufunguliwa na watuhumiwa akiwamo rais Kikwete ambaye aliamua kukaa kimya? Je huu nao ni uongo na lugha ya matusi? Je vitu hivi havitoshi kuvuruga amani?

Kuna haja ya kuacha kuogopana na kuongopeana. Tuwaeleze wahusika (watuhumiwa) waache urushi, visingizi, utoto na uhuni. Waeleze wanachojua kuhusu tuhuma zinazowakabili. Kutokuwa tayari kueleza haya ndiyo uongo wa mwaka unaofanywa na CCM ambayo, siku zote, imewachukulia watanzania kama mataahira, majuha na shamba la bibi la kufanyia madili yao ili kuendelea kuwa madarakani ingawa siku zao zinazidi kuhesabika.

Kama CCM inakanusha kuwa haikutumia pesa ya wizi wa EPA kuingia madarakani mwaka 2005, mbona haijawahi kueleza vyanzo vya pesa yake iliyotumika kununulia madaraka? Kwanini kila wakitajwa wawezeshaji wa wizi huu mfano Kagoda CCM na serikali hupata kigugumizi kama hakuna ukweli?

Hata hivyo, akiwa Morogoro, mgombea urais wa Chadema, Wibrod Slaa alimshukia Mwenyekiti wa kampeni za CCM, Abdulrahaman Kinana ambaye amekuwa mstari wa mbele kutuaminisha CCM itashinda kwa haki, akimtaka aleze jinsi alivyo na mkono mchafu kwenye biashara ya makampuni ya meli. Inaonekana Slaa alikuwa akimbipu ili kumvutia pumzi na kuona atakavyojitetea badala ya kupoteza muda kupaka rangi upepo kwa kuwaandama wapinzani wakati anayepaswa kuandamwa ni yeye.

Tumalizie kuwataka wasomaji wajiulize swali moja kuu. Kwanini tukubali matokeo tusiyoridhika nayo na ambayo hayatokani na utashi wetu kikatiba? Pia Kinana aulizwe. Ni kwanini Kinana anapata muda wa kuwatetea wenzake kabla ya kujitetea mwenyewe? Je anafanya hivyo ili kufaidi ulinzi wao kama rais mstaafu Benjamin Mkapa?

Kwa waangalizi wa kimataifa wanaotushauri upuuzi, waambiwe waache. Maana mwenye stahiki ya kuamua hatima ya Tanzania ni watanzania wenyewe na si watawala na mawakala wao wala wageni.

Chanzo: Gazeti la Dira ya Mtanzania Novemba 8, 2010

Friday 5 November 2010

"Ushindi" wa Kikwete ni mea maxima culpa na aibu

Kibaraka wa Kikwete, Luis Makame mwenyekiti wa Tume ya Uchakachuaji akimkabidhi bosi wake cheti cha kuwaibia urais watanzania



Japo Jakaya Kikwete, chama chake na waramba viatu wake hasa mafisadi, watajiridhisha kuwa ameshinda kuwa rais wa Tanzania, ni aibu na matusi kwa demokrasia kwa utawala mchovu kurejea madarakani. Ni hatari na balaa. Hatutaki kuwa watabiri. Watanzania ndani ya kipindi kifupi watagundua kosa lao kuvumilia uchakachuaji uliorejesha utawala huu wa kifisadi usio na lolote la kuwafanyia bali kuwaibia.

Tusitoe madai bila ushahidi. Nani alitegemea kuwa watuhumiwa wa ufisadi kama Andrew Chenge, Edward Lowassa,Nimrod Mkono, Rostam Aziz na wengine wangerejea? Nani alitegemea watuhumiwa wa kughushi vyeti vya taaluma kama Emanuel Nchimbi, Makongoro Mahanga, Mary Nagu, Victor Mwambalaswa na wengine wangerejea bungeni? Nani angeamini kuwa mtuhumiwa kama Chenge angediriki hata kugombea ubunge. Ili alitumie kufanya nini zaidi ya kuwalinda na kuwapa ulaji mafisadi wenzake? Haya ndiyo mauzauza ya mfumo mbovu na mchafu wa Tanzania.

Japo watu wengi wakiwamo wasimamizi wa kimataifa wameshauri Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakubali matokeo yaliyochakachauliwa, ni jinai namna gani? Kisingizio na sababu uchwara inayotolewa eti AMANI. Amani gani bila kutenda haki? Amani gani kuwavumilia wezi wa kura na mafisadi? Amani gani ndani ya jinai kila aina na ufisadi ukiachia mbali ukosefu wa visheni na sera bila kusahau uadilifu? Huu ni upuuzi.

Wanaoshangilia ushindi wa CCM wanashangilia ufisadi na maangamizi yao wenyewe ima kwa makusudi au bahati mbaya.
Ushindi wa Kikwete, CCM na waramba viatu wake si chochote wala lolote bali MEA CULPA.
Tungekuwa na watu wanaojali mstakabali wao na taifa, watu kama Kivuitu Kiravu na Luis Makame na Kikwete wao wangetafuta sehemu ya kujificha pale People's power ingeanza kuwasulubu. Natamani watanzania waamke toka kwenye usingizi huu unaowafanya makondoo na kuku. Je ukuku na ukondoo vinalipa. Majirani zetu ambao tulizoea kuwacheka wanatucheka kwa ukondoo wetu.Heri wao tuliwaita mbwa mwitu na mafisi lakini wanatuzidi wamejikomboa ikilinganishwa nasi tulio kwenye kongwa za mafisadi na mabwana zao. Je tutaendelea na kitanzi hiki hadi lini? Tafakarini.

Thursday 4 November 2010

Hata majina ya marehemu yalikuwapo vituoni

BAADA kumaliza ligi ya uongo na ahadi hewa wa kuusaka uongozi, kuna jambo sikulitarajia ingawa lilitokea. Nikiwa na hamasa ya kuchagua ukombozi na kuuzika upuuzi na ufisadi, siku ya tarehe 31 Oktoba nilidamka kwenda kupiga kura nisijue nitapigwa na butwaa na kuishiwa kuliwa na kubambikiziwa wezi wa kunila zaidi!

Kuna kipindi ukiiangalia hii dunia unaweza kuichukia wakati si mbaya bali walimwengu. Sijui ni wangapi yaliwakuta kama haya yaliyonikuta kaya nzima.

Je, huu nao si mtaji wa kurejesha wachovu ambao wengi wao wanaweza kupeta wakiwamo hata wale mafisadi papa na wanaonuka? Kwa mtu ambaye nguvu zangu na akili zangu zinajipa imekuwa hivi. Je, hao vikongwe na wenye welewa kidogo ilikuwaje?

Siku moja kabla ya kipute chenyewe nilikwenda kwenye kituo changu cha kupigia kura cha kwa Mfuga Mbwa ingawa siku hizi nimehamia Kigogo Mwisho. Nilijilaumu. Kwani licha ya kulipa nauli na kupoteza muda wangu jina langu halikuwapo.

Ajabu majina ya marehemu yalikuwapo yote. Walipiga vipi kura na kumpa nani kula usiniiulize na unajua kilichotokea. Hivi huyu atakayeshinda kwa kutegemea kura za maiti naye atajisifu na kujiona ni kiongozi halali wakati ni haramu?

Baada ya kutokuta jina langu, nilipiga mguu kwenda kwa wakubwa wa uchakachuaji (National Electoral Counterfeiters (NEC) na kuulizia kulikoni hata jina langu silioni.

Majibu waliyotoa hata kuku hawezi kufikiri kuyatoa achia mbali kuyatoa. Ajabu bado wapuuzi hawa wanalipwa njuluku zetu! Yaani tunawalipa waongo kutuongopea na kutuwekea misukule yao!

Hakuna kilichonikera nusu kujinyotoa roho kama kusikia wapuuzi fulani wakijisifu upuuzi eti wamekuza demokrasia wakati wameidumaza na hatimaye kuiua kabisa ukiachia mbali kuidhalilisha.

Demokrasia au ghasia? Mara utawasikia na kuwaona mitaani wakijinyevuavua-'wamechukua wakaweka tukachukua na kuchakachua waa'.

Demokrasia gani watu tunakatwa majina na marehemu wanabakizwa ili kutumiwa kuchakachua na kuula kwa kuiba kura? Demokrasia gani kampeni zinaendeshwa kwa wizi na matumizi ya udugu, ufamilia, udini, usanii, uongo, mamluki, makanjanja na ufisadi?

Hata hamuogopi Mungu ingawa mliwahi kujipachia kuwa chaguo lake msijue ni la mafisadi na shetani mwenyewe? Hivi kuwatumia marehemu si kuwadhalilisha ukiachia mbali kujidhalilisha? Anayewatumia marehemu kufikia malengo yake naye ni marehemu ambaye alipaswa kuzikwa tu.

Bahati mbaya tunatawaliwa na marehemu kisiasa kwa sera zao mfu na mgando, bila kusahau ufisadi wa kunuka! Je, tuendelee na ibada hizi za sanamu?

Leo watu wazima hata kama tu walevi tunaambiwa eti uchumi umekuwa simply because fisadi mkuu na familia yake wanashiba wakati si kweli?

Anayebishia hili aende vijijini aone watu wanavyoishi kwenye mbavu za mbwa huku wezi wachache wakitanua na vimada wao.

Madame Rahma Haruusi Kharous wa Kissie upo japo unajificha kwenye ufadhili wa michezo na kujifanya mtafiti wa mawese wakati tunajua wewe nesi. Du! Ona sasa ulevi ulivyo balaa. Naona nimevuka mipaka. Badala ya kujadili uchakachuaji najadili u hovyo! Hata hivyo nondo imefika na wahusika wameipata hata kama hawatajibu. Wajibu nini wakati nao ni marehemu wa ndoa?

Turudi kwenye uchakachuaji na uchafuzi. Hakuna kinachozidi kunikera kama kuona wezi na majambazi wa ufisadi na kura kujisifu eti wamepata ridhaa yetu.

Ridhaa gani wakati hatukupiga kura? Je kosa letu ni kuwaacha kufanya ufisadi wao hadi kufikia kunadiana hadharani tukiwa mashahidi? Je, walevi wataendelea kuvumilia huu upuuzi hadi lini?

Kana kwamba madhambi na dhuluma walivyowatendea walevi havitoshi, wameongeza na hili la kuiba haki yetu ya kupiga kura kwa kuhofia tungewaangusha.

Je, umma wa walevi utajitendea dhambi ya kujitia kitanzi kwa kusamehe upuuzi huu? Je, huu nao ujanja au kuishiwa? Je watawala wazalishwao na jinai hii waharifu wa kawaida? Je, namna hii walevi hawajatawaliwa na genge la mafia?

Je, tutaendelea na usanii huu wakati tukijua waathirika wakubwa ni sisi hadi lini? Ni swali ambalo kila mlevi anapaswa kujiuliza.

Kwanini tusitumie ulevi wetu unaotuwezesha kuzungumza kiingereza ambacho huwa hatuwezi kabla ya kulewa, kuondoa balaa hili la kujitengenezea? Hakika hii ni kucheza na mauti.

Lazima tukubaliane. Watu wanaoshinda kutegemea misukule, maruhani, marehemu na upuuzi mwingine kama huu nao ni maruhani, misukule, wafu na waharifu wa kawaida wasiopaswa kuwa kwenye ofisi za umma. Je, ni wangapi wanaona hivi ili wawatoe mkuku?

Ndiyo maana kaya yetu inachezewa na wachukuaji na mafisadi. Hii ni kutokana na kuongozwa na marehemu, misukule, maruhani na upuuzi mwingine.

Ruhani aweza kuwa mtu anayetumia familia kama nguvu yake ya kisiasa. Msukule aweza kuwa yeyote anayetegemea nguvu na pesa za mafisadi kupata maulaji ya utawala.

Marehemu aweza kuwa yule anayeendesha kijiwe kwa sera marehemu na mambo mengine kama hayo. Je, hawa na haya hawapo miongoni mwetu? Je ni marehemu gani anaweza kumkomboa aliye hai wakati ameshindwa kujikomboa mwenyewe?

Ni uongo kiasi gani kwa marehemu kuamini atamkomboa aliye hai sawa na aliye hai kuamini atakombolewa na marehemu?

Ama kweli Yesu mwana wa seremala alijua. Alisema waache wafu wazike wafu wenzao. Je, nasi umefika wakati wa kuwaambia tuwaache wafu wawatawale wafu wenzao?

Je, wale ambao si wafu watapata wapi ukombozi? Je wataendelea kujitoa huku mambo yakizidi kuharibika au watachukua hatua mujarabu?

Je, chanzo cha haya yote ni nini kama si watu kuogopa kufa hadi kutawaliwa na marehemu? Heri kufa ukipambana kuliko kuishi kama punda kihongwe bingwa wa kubeba kila mizigo.

Juzi tumewaona marehemu wengi wakiwapigia debe marehemu wenzao. Tumewaona makanjanja na wasomi nepi wakijivua nguo kuhakikisha marehemu wenzao wanapita ili wapete nao. Tumewaona wengi tena ambao ungedhani walikuwa hai kumbe walijifia zamani.

Marehemu hawa wanawauza walio hai kwa vile wao hawana hasara. Wafe mara ngapi? Waweza kuwa hai kimwili lakini ukawa mfu kimaadili. Na hawa ni wengi sina mfano.

Wapo kila mahali kama majani yaliyopukutika. Wapo maofisini, makanisani, misikitini, vyuoni na kwingineko.

Wako vijijini na mijini. Wako nawaona kila mahali. Wamezagaa kama uchafu kwenye mitaa ya Bongo. Ukichanganya na mainzi mafu yaliyowazunguka hicho kinyaa Mungu ajua.

Turejee kwenye uhalisia na ukweli bila kuugopa wala kuupindisha. Hivi mtu anayewanyima haki walio hai akajificha nyuma ya usanii wa kuwatumia maiti hajaishiwa kiasi cha kutostahili hata kuishi kufanya kile anachofanya?

Je, huu si ushahidi kuwa kumbe kaya inaweza ikatawaliwa na waharifu huku walevi wakitegemea waharifu hawa wauondoa uharifu wakati wao ni tunda lake? Je, namna hii kaya kuna siku itafika huko Kanani au Golgotha?

Ngoja nivuke barabara haraka kabla ya mataa kuzima na hawa wehu wa dala dala kuninyotoa roho.
Chanzo: Tanzania Daima Novemba 3, 2010.

Monday 1 November 2010

Je na hawa walichagua au CCM au mchakachuo?











Picha kwa hisani ya Masangu Matondo Nuzulilima wa CHAKULA KITAMU.

Kwa matokeo yanavyotoka ni wazi kuwa uchakachuaji hasa kwenye kura za urais umefanyika. Kuna maswali mengi ya kujiuliza kuu likiwa ni kwanini matokeo yacheleweshe ukiachia mbali watu wengi (hasa wanaosadikiwa kuwa ngome ya upinzani kutokuta majina yao kwenye vituo)?
Japo CCM inaweza kujipa matumaini kuwa imshinda, imefungua pazia la kuporomoka na hatimaye kutoweka kwenye ramani ya Tanzania.
Je hao juu nao waliichagua CCM au Kivuitu Kiravu aliwachagulia?je hayo tuonayo ndiyo maisha bora aliyowaahidi Kikwete na akaahidi zaidi ya hapo? Je matawala anayechekelea na kuitumia hali hii kama mtaji wake si fisadi wa kiroho wa kutupwa? Tafakarini jamani.