The Chant of Savant

Thursday 30 September 2010

Ona watawala wetu walivyo vipofu na washirikina

HARARE

A witchdoctor who misled Zimbabwean President Robert Mugabe’s entire Cabinet into believing that petroleum was oozing from a rock has been jailed for 27 months.

President Mugabe went to the extent of setting up a Cabinet committee to investigate how the country could benefit from the “discovery” after Rottina Mavhunga claimed to have discovered refined diesel at a mountainous area.

Mavhunga hosted several ministerial delegations at her shrine and was paid thousands of dollars as she sent the government on a wild goose chase. She cleverly exploited a fuel shortage that had gripped Zimbabwe for more than five years.

A magistrate in Chinhoyi, about 100km from Harare, said the witchdoctor deserved a custodial sentence as the government had channelled money to her fake project and which was now lost.

“The court cannot be faulted for saying that the offences were premeditated and diligently executed.

“Many people became gullible owing to the crisis the country was under and accepted an unknown phenomenon.

“The accused lied to the nation for self-actualisation and personal benefit. Your trickery brought despondency in the nation during a dry period,” the magistrate said while passing sentence.

Mavhunga blamed the diesel claim on spirit possession. She said she does not know if the diesel exists.

The government later discovered that Mavhunga and her accomplices were drawing diesel from tanks left by a white commercial farmer who lost his farm during President Mugabe’s controversial land reforms.

Mugabe’s close ally and Zimbabwe’s registrar-general, Mr Tobaiwa Mudede, who allegedly sheltered Mavhunga when she was being sought by police, was also criticised.

Mavhunga faces another charge after she allegedly exchanged a stone weighing 18kg, claiming it was gold, for a cow.

Source: Daily Nation Kenya

Wednesday 29 September 2010

Tumepata KAPAYUKAJI


Baba akiongea na mwana
Mama akimhusia mwana
Wapendwa wasomaji wangu,
Naomba nichukue fursa hii kuwataarifu kuwa familia yetu imepata mtoto wa kiume (pichani) aitwaye NKUZI (Kapayukaji) mnamo tarehe 25 majira ya saa 2:51 za Manitoba. Kwa Tanzania ilikuwa saa ilikuwa ni saa 11:51 alfajiri. Kichanga chetu kilizaliwa Boundary Trails Medical Centre, MB.
Mama mzazi, Nesaa Nkwazi Mhango na kichanga wanaendelea vizuri.
Nimeona niwafahamishe kutokana na ukaribu uliojengaka baina ya wasomaji wangu nami na bila shaka na familia yangu.
Chanzo: Mhango Family Libarary.

Kikwete, Lowassa ni mchapakazi?!!!!!!!



Akiwa mkoani Arusha wilayani Monduli alikokwenda kufanya kampeni, rais anayemaliza muda wake Jakaya Kikwete alitonesha tena vidonda vya watanzania hasa wapinga ufisadi.

Alikaririwa akimmwagia sifa mgombea wa CCM mbunge aliyemaliza muda wake na waziri mkuu aliyetimuliwa (siyo kustaafu kama anavyopambwa), Edward Lowassa.

Kikwete sijui kuwa kusahau, makusudi au dharau alikaririwa akisema: “Lowassa ni mchapakazi hodari, hana mfano wake. Wananchi tusahau yaliyopita tugange ya sasa na yajayo, namuombea kura.”

Huku ni kufuja maneno. Wamezoea kufuja pesa ya umma hadi wanafuja maneno ya kutushawishi tufuje haki na akili zetu! Ni dharau na kuishiwa kiasi gani?

Ni ajabu na aibu. Kwani vyombo vya habari na watanzania kwa ujumla hawakulaani kauli hii ya kuwadhalilisha na kuwangopea. Kikwete alipaswa abanwe aombe umma msamaha kwa kutonesha vidonda vyake. Kwanini tusahau yaliyopita wakati tunaendelea kuuguza vidonda vyake? Huwezi kuganga yajayo bila kurejea yaliyopita. Kufanya hivi licha ya kuwa upogo ni kushindwa wazi. Maana kesho hutengenezwa na jana.

Tuache utani na usanii. Je kweli Lowassa ni mchapakazi kama alivyosema Kikwete au ni upotoshaji na jitihada za wazi kumsafisha na hatimaye kumrejesha rafiki na mshirika wake huyu ambaye rekodi zake ziko wazi kuwa si mchapakazi bali mtu aliyeliingiza taifa kwenye hasara na mateso makubwa kutokana na kuwa kizani kwa mwaka mzima ukiachia mbali ubinafsi na tamaa? Je huu ndiyo uchapakazi usio na kifani wa Lowassa?

Rekodi gani za Lowassa zinaweza kumvutia mpiga kura yeyote mwenye akili? Madai kuwa amejilimbikizia mali lukuki zisizo na maelezo na zitokanazo na ufisadi kama alivyowahi kudai baba wa taifa marehemu mwalimu Julius Nyerere? Ajabu, kwa kufuru na upotoshaji wa namna hii, utamsikia Kikwete akimsimanga Nyerere kuwa anamuenzi!

Inashangaza rais kutoa maneno kama haya hasa wakati huu anapokabiliwa na kibarua kigumu kurejea madarakani bila kufanya lolote la maana ukiachia mbali shutuma nyingi za ufisadi zilizomkabili rais binafsi na serikali yake!

Je bado watanzania kweli wanamhitaji Lowassa ambaye alilazimika kuachia ngazi baada ya kubainika alikuwa nyuma ya kashfa iliyotugharimu mabilioni ya Richmond? Je hii si dharau kwa bunge lililomtimua na wananchi kwa ujumla? Je mtu huyu analo jipya la kuwafanyia wananchi kiasi cha kuwaaminisha wamchague tena aendelee kuwakingia kifua marafiki zake?

Leo kasema Lowassa ni mchapakazi. Jana alisema waziri wake wa fedha wa zamani mwenye kesi ya matumizi mabaya ya madaraka Basil Mramba ni mtu makini! Mtu gani makini anaweza kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka na ofisi? Je Kikwete hajui kiswahili hivi au anatuchezea shere? Usishangae kesho kusikia Kikwete kaenda Shinyanga wilayani Bariadi na kusema mgombea wake wa jimbo la Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, aliyeripotiwa na mashirika ya kijasusi ya Uingereza kuficha kiasi cha zaidi ya shilingi 1,000,000,000 nchini humo ni mchapakazi. Kazi ya kuhujumu na kufilisi umma!

Kesho kutwa utamsikia akiwa Igunga kumpigia kampeni Rostam Aziz akimnadi kama mtu mwaminifu na mfanyabiashara wa kupigiwa mfano!

Je huu si mshikamano wa kifisadi, uongo na matusi ya nguoni kwa waathirika yaani watanzania?

Ni Kikwete huyu huyu ambaye serikali yake imekuwa ikiuibia umma kwa kumtambua na kumlipa marupurupu ya ustaafu Lowassa wakati alitimuliwa na Bunge baada ya kamati teule ya Bunge kumkuta na kashfa ya ufisadi ulioteketeza mabilioni fedha ya umma.

Tuutazame ukweli bila makengeza. Je ni kweli kuwa Lowassa ni mchapakazi na waziri mkuu mstaafu au rafiki wa rais aliyenusurika kufikishwa mahakamani kutokana na kukingiwa kifua na rafiki yake?

Kwa kumtangaza Lowassa kama mchapakazi asiye na mfano, Kikwete, kwanza analidhalilisha bunge lililomkuta na hatia ukiachia mbali kuwakatisha tamaa wachapakazi wa kweli.

Ukiangalia alivyosimama bega kwa bega na Mramba, utagundua kuwa hata kesi inayomkabili ni changa la macho. Maana kama Kikwete kweli angekuwa na nia ya kumshughulikia vilivyo na si vunga, angejitahidi angalau kuepuka kuwapigia kampeni watu kama hawa ambao mbele ya watanzania ni machukizo na alama ya mshikamano wa kinafiki na wa kifisadi.

Sifa za Kikwete kwa swahiba yake Lowassa zimethibitisha tambo za Lowassa kuwa urafiki wao na Kikwete si wa barabarani na hivyo hauwezi kuvunjwa na vyombo vya habari. Je hii kwa mpiga kura mwenye uchungu na nchi yake inaashiria nini zaidi ya kuwa taarifa kamili kuwa wawili hawa na wenzao wanaotuhumiwa kushiriki uhujumu wa taifa maslahi yao na urafiki wao ni zaidi ya maslahi ya taifa? Je huu si ushahidi wa mazingira kuwa kashfa iliyomuondoa Lowassa ilikuwa na kila baraka za Kikwete na kutimka kwake kulimnusuru Kikwete na serikali yake kiasi cha kuwa tayari kwa lolote ilmradi mtu wake asiguswe?

Je huku si kutumia sheria na madaraka kibaguzi na kwa upendeleo? Rais anayejali urafiki, udugu, unyumba, kujuana, ushirika, mitandao na mengine kama haya hatufai. Rais wa Tanzania anapaswa kuwa ofisini kwa ajili ya watanzania na si marafiki au jamaa zake. Anayebishia hili aangalie mke na mtoto wa Kikwete wanavyokata mbuga kumpigia kampeni wakifuja mali na fedha ya umma. Je tunataka Kikwete atukwaze na kutuangusha mara ngapi jamani?

Ingawa watanzania hasa vyombo vya habari havikulaani upotoshaji na mshikamano huu wa kifisadi, nichukue fursa hii kama mtu binafsi kulaani jinai hii. Nitafurahi kama nitasikia watu wengine wakijitokeza kulaani upotoshaji huu. Nitafurahi zaidi wapiga kura kama watatumia upotoshaji huu kama sababu mojawapo, kati ya nyingi, kuinyima kura CCM.

Na niseme wazi. Kama Kikwete na CCM wataendelea na mshikamano na upotoshaji huu hawataachwa kuendelea kuitwa Chama Cha Mafisadi na majina mengi yasiyopendeza.

Ni vizuri wakumbuke. Tanzania si mali ya CCM, Lowassa, Kikwete wala mitandao ya kifisadi bali ya watanzania. Kuna siku umma utaamka na wanaotukoga watakosa pa kujificha. Nani alijua kuwa majambazi kama Mobutu Seseseko (Zaire), Jean Bedel Bokassa (CAR), Ferdinand Marcos (Ufilipino), Fulgencio Batista y Zaldívar (Cuba) na wengine wengi wangelidondoshwa tena kwa aibu na people's power?

Dalili za kuoza kwa mfumo wowote wa maisha ni pale watu fulani wanapojiona watukufu kuliko wengine kiasi cha kukufuru na kutetea uoza watakavyo kana kwamba hakuna kesho. Swali linabaki pale pale. Je kweli Lowassa ni mchapakazi au?

Chanzo: Dira ya Mtanzania Septemba 27, 2010.

Tuesday 28 September 2010

“Madness and self seeking in the name of God”


Recent stand-off-cum-threat by American quack Terry Jones to enflame 200 copies of Koran gave us many lessons. The biggest lesson we got is some Muslims and politicians proved to be mad and awkward thanks to their lush and myopia. For many people in various “Muslim” countries took to the streets to protest the kindling of the Koran.

Jones succeeded in using and abusing goofy Muslims to reach his nugatory goal-fame. So too, he unearthed another anomaly in that many people are idolatrous and blind. For they value a book (material) more than humans, as opposed to spirituality. Refer to the deaths of two demonstarors in Afghanistan or deaths of many people who memorized the whole 114 chapters (Surat) of Koran (Hafidh al Qur’an) in Darfur, Sudan.

One wonders how people could die for something material, the thing that even Muhammad (SAW) himself did not authorize its application and compilation? To know what this means, refer to the genesis of the Koran that was authorized by Caliph Othman. That’s why there are many versions of the same such as Othmanic codex, Othmanic recension, Samarkand codex, Samarkand manuscript and Tashkent Qur’an. Also one can refer to the fact that the Koran was compiled after the death of prophet Muhammad. He left it as scripta defectiva, incomplete and instructed his disciples (Ṣaḥābah ) to memorize it and not to write it as they contrary did.

Interestingly though, many Somalis took to the streets to condemn this stupidity-cum-insanity. One, however, wonders. How can Somalis that have, for long, been hijacked by warlords (they’ve nary demonstrated to condemn), do this?

This reminds me of Sudanese who in 2007 blindly took to the streets to condemn, whilst others wanted the neck of English teacher Gillian Gibbons, simply because she scribed the name Mohammed on a bear toy that she gave as a gift to her student whose name is Mohammed. This act was wrongly and maliciously taken as blasphemy to prophet of Muslims, Mohammed. Many still wonder. When Sudanese were baying for the blood of an innocent teacher with machetes and clubs for the blood of poor Gibbons, they’re protecting Ahmad Harun who was implicated by the International Criminal Court (ICC) for committing genocide in Darfur. It is sad and shameful for Sudanese and Middle East so-called Muslims to not take to the streets condemning Sudanese government that is butchering poor and innocent Darfuris among whom there are many Hafiz. Where does Khartoum get money to run its day-to-day business and financing janjaweed if not the Middle East? Refer to many countries in the region to not sign international instruments or honour and meet their obligations thereby enabling swift movement for Sudanese butcher Omar Bashir as he once boasted when he visited Qatar. Even other Africans are to blame for this. For after warrant to arrest Bashir was issued he was able to visit Egypt, Libya, Eritrea, Kenya, and Ethiopia without being arrested.

More so, how many Muhammads’ are rotting in prisons for committing rape, robbery, drug trafficking, theft and what not? Why don’t those “Muslims” demonstrate to condemn the parents of these criminals with the name Muhammad, for naming them after the prophet? Why didn’t we see these good Muslims demonstrating when US invaded Iraq, where many copies of Koran were burned or destroyed when mosques and homes were bombed? Isn’t demonstrating against the burning of Koran only hypocrisy and shirk?

There is no need for humans to lose or endanger their lives just fighting for something material. Koran is a concept. Nobody can burn or destroy it. Now look. After the dust of the attempt to burn the Koran settled, one Australian lawyer Alex Stewart smoked two pages one from the Koran and another from the bible.

Suppose, were copies of the Koran torched, would the sun fall down or the world come come to an end? Nothing would happen given that those that wanted to torch the Koran used it to get cheap popularity. And indeed, they succeeded in hoodwinking Muslims and politicians who goofed and fell in the trap easily and blindly.

Given that the source of all fracas was the intention of building a memorial mosque at ground zero, this thing should be given much thoughts. Why building the mosque there? To commemorate the terrorists that brought down WTC?

Another madness we witnessed is the torching of American flag that was done by demonstrators. Why should one defend his rights by abusing those of others? If the Koran is holy for Muslims, US flag is the symbol of the nation. It is holy to them too.
Source:Afro Spear Sept 27, 2010.

Thursday 23 September 2010

'Dodoma Locuta Est Causa Finita Est' mwisho wa CCM

KWA wanaokumbuka majivuno, kiburi, mitandao, usanii, uzembe na manjonjo ya utawala wa zamani wa Kirumi, bado wanakumbuka ujanja ujanja ulivyojiangamiza baadaye na ikabakia historia.

Himaya hii iliyoishi zaidi ya miaka 500 ilianza kusambaratika baada ya kugawanyika katika vipande wiwili- mashariki na magharibi, baada ya kifo cha Theodosius mwaka 395.

Mwaka 476 upande wa Magharibi, ulianguka chini ya utawala wa Romulus Augustus ambaye alilazimishwa kuikimbia Odoacer.

Upande wa mashariki ambao kwa kiasi fulani ulihimili mikiki na kufanya marekebisho mbalimbali ulisambaratika baada ya kifo cha Constatine IX. Trajan aliyechukua madaraka baadaye alishtukia akitekwa na Waturuki chini ya kiongozi wao Mehmed II huku akiwa amejigeuza mungu mtu juu ya ardhi.

Alilewa madaraka huku wasasi wa ngawira wakimramba miguu hadi kujisahau asijue wanafiki watupu ambao wangemkimbia baada ya taji kumtoka!

Chanzo kikuu cha kudhoofika hadi kutekwa na kutoweka ni ufisadi uliokuwa ukiendeshwa na wapambe wa mfalme (Praetorian Guards) na migongano baina ya seneti na mfalme huku Roma ikishikilia usanii wake wa Roma Locuta Est Causa Finita Est yaani ‘Roma Ikiishasema, Kesi Imefungwa’.

Hapa hatujagusia ukosefu wa kazi na maisha duni kwa wafanyakazi, kuporomoka kwa uchumi, matumizi makubwa, kutoweka kwa maadili, utumikishaji au unyonyaji wa umma na mengine mengi hadi ikavamiwa na kuangushwa kirahisi.

Histori ya Roma ni ndefu sana kiasi cha kuhitaji vitabu si makala. Nimeanza nayo kuonyesha ni jinsi gani kila kitu, hasa tawala, huwa ni cha msimu.

Nataka kuwapiga kijembe wajinga na wahuni wanaosema eti Chama cha Mapinduzi (CCM) kitatawala milele. Pia napenda kupiga upatu kuwa hata huu Muungano unaweza kufa tukawa na nchi mbili huru yaani Zanzibar na Tanganyika na maisha yakaendelea kama hautaboreshwa kwa matakwa ya umma badala ya watawala.

Kitu kingine ni kutaka kuonyesha kuwa ufanisi wa kupita kiasi huzaa maanguko. Karibu himaya zote zilizopita zilipanuka hadi kupasuka sawa na CCM ambayo imefanikiwa kutandawaa nchi nzima kiasi cha kujenga vijimitandao vya kimaslahi vinavyoanza kuipasua kidogo kidogo huku ikishikilia kuwa iko imara wakati siyo.

CCM imekuwa kama yule mama wa Kigiriki wa kutisha Medusa ambaye macho yake yakikulenga ilitosha kukugeuza jiwe.

Tumeona wengi waliogeuka mawe baada ya macho ya CCM kuwalenga kwa hasira. Tunawakumbuka kina Edward Sokoine na Horace Kolimba waliogeuzwa mawe waliposema CCM imekosa mwelekeo au kutaka kuirekebisha. Kosa lao kubwa kwa CCM ilikuwa ni kusema ukweli huu au kutaka kutenda haki. Na kwa wao binafsi ni kuendelea kubaki ndani ya CCM ilhali wa kijua hasira za Medusa binti Pholcys na mkedada Ceto na matokeo yake.

Siri mojawapo ya ufanisi wa himaya ya Roma iliyokuwa imetawala yapata eneo la ukubwa wa kilometa 6,5000,000 ilikuwa ni kauli mbiu yake ya Roma Locuta est causa finita est yaani kilichoamriwa Roma huwa hakina mjadala tena. Kilichofunguliwa au kufungwa Roma ndiyo kimefungwa au kufunguliwa hakuna wa kufunga au kufungua.

Ukiangalia mazingaombwe na usanii wa hivi karibuni huko Dodoma, utakubaliana nami kuwa kilichofungwa Dodoma, hakiwezi kufunguliwa na yeyote.

Sitapenda kuongelea vituko, kuzushiana, kumalizana na kuoneana kulikoripotiwa ambapo kada mmojawapo Hussein Bashe alipigwa kibuti kwa madai kuwa si raia. Maswali mengi yameishaulizwa na hayajajibiwa ni kwa nini sasa na si juzi kabla ya kutaka kugombea ulaji mkuu?

Awe raia au vinginevyo, Dodoma Locuta est causa finita est, Bashe kama rafiki yake Yusuf Masauni anayoyoma. Bahati mbaya kwa vijana hawa wote wameangushwa na sumu ile ile. Maana wengi wa wachambuzi wanasema eti walikosana na mtoto wa Rais Jakaya Kikwete yaani Ridhiwani ambaye ametokea kuwa King Maker kwenye Umoja wa Vijana wa CCM.

Roma kama himaya iliaminika kwa maajabu yake ambayo kimsingi hayakuwa maajabu kitu bali usanii ambao hatima yake uliisambaratisha Roma yenyewe.

Ni maajabu haya haya tumeyashuhudia juzi kule Dodoma yakiwapitisha watuhumiwa (Praetorian Guards) wa kashfa mbali mbali na kuwakata wapambanaji dhidi ya ufisadi mmojawapo akiwa Lucas Selelii mbunge wa Nzega anayemaliza muda wake ambaye nafasi yake baada ya kumtosa Bashe ilikwenda kwa Hamis Anderea Kigwangala ambaye naye anadaiwa kuwa Mrundi.

Maajabu ya Roma yanaendelea. Huko Kigoma kuna minong'ono kuwa mgombea aliyepewa baraka za CCM aliwahi kutajwa kwenye kura zilizoendeshwa na serikali ya CCM yenyewe dhidi ya wauaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi, kuwa ananunua viungo vya watu. Lakini kwa vile ni mwenzao, nani atamgusa? Dodoma locuta est causa finita est.

Na haya ndiyo maajabu ya watu kama Basil Mramba na Andrew Chenge wenye tuhuma na kesi mbichi kupindishiwa sheria na kupeta. Ni maajabu haya haya yaliyowawezesha waliotuhumiwa kughushi vyeti vya kitaaluma kama Emanuel Nchimbi, William Lukuvi, Mary Nagu, Victor Mwambalaswa na Makongoro Mahanga kupeta kana kwamba madai yao ni ya kutenda mema si kuvunja sheria.

Ni miujiza hii hii iliyowawezesha watu kama Rostam Aziz aliyedaiwa kuwa mmilki wa kampuni iliyodaiwa kuiba mabilioni ya EPA, Kagoda na Edward Lowassa aliyeachia ngazi kama ishara ya kukiri alishiriki uchafu wa Richmond kupeta. Ajabu maajabu haya haya yamemtupa nje Fredrick Mwakalebela kwa kutoa rushwa mbuzi siyo kuuza nchi!

Hata kina Diodorus Kamala na Samuel Chitalilo kama siyo kuasiwa na wapiga kura wangepeta.

Ni miujiza hii hii iliyowezesha watu kama Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, pamoja na kuvuruga chama na kuwa na mashikamano yenye kutia shaka, kuendelea kupeta.

Watu wengi wenye akili wanajiuliza. Nini mantiki ya serikali na TAKUKURU, kwa mfano, kukamata baadhi ya wana CCM na kuwaacha wengine? Vyombo vya habari viliwahi kuripoti kisa cha mgombea mmoja mwenye jina kubwa aliyewahi kushika nyadhifa za juu na baadaye kuchafuka na kutimka alivyokuwa akigawa simu tena miezi zaidi ya miwili hata kabla ya kura za maoni na TAKUKURU hawakufanya lolote!

Jambo muhimu la kuikumbusha Roma- CCM- ni ukweli kuwa mwenzake alitekwa na Waturuki kama ambayo siku moja CCM itajikuta imepinduliwa na mafisadi ambao tayari wameishaiteka na kuanza kuipeleka kuzimu taratibu.

Kwa ufupi ni kwamba kama ilivyokuwa Roma, kwa Tanzania, kila kilichofungwa au kufunguliwa Dodoma hakiwezi tena kufungwa au kufunguliwa na mtu. Ila Zanzibar wameanza kukifungua.

Uzuri wa ubabe na sanaa hii ni kuwa mbwembwe, manjonjo, kiburi, uzembe, usanii, ushufaa hujenga mbegu za uharibifu ambazo hatimaye husambaratisha genge zima kama tulivyoona kwenye himaya ya Roma.

Tuthibitishe kuwa wale wanaosema na kuamini kuwa CCM itatawala milele, licha ya kuwa hakifai, wanapaswa kusoma historia upya kama wanataka kuishi kwa usalama na ufanisi na vizazi vyao.
Chanzo: Tanzania Daima Septemba 22, 2010.

Utabiri wa shehe Asohaya Hoseni

MFUNGO wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan umepita salama.

Baada ya dhiki kuzidi kuongezeka na uwezo wa wadanganyika kufikiri kupungua, kiasi cha kuibiwa na kudhalilishwa na kila tapeli na msanii, nimegundua kuwa utabiri, usanii na utapeli vinalipa kweli kweli.

Hivyo, baada ya kuona maeneo ya Magomeni Mikumi, Mikocheni, Mwenge na Jangwani matapeli kujizolea sifa na ndururu, nami nimeamua nitie guu.

Kwanza nieleweke. Sitabirii njaa wala kujikomba wala kutafuta sifa uchwara bali mapenzi ya kaya yangu ya Danganyika inayogeuka kaya Juha. Pia sina ushindani na matapeli maarufu mnaowajua kuanzia kina Ka-Tortoise, Gamanyua, Rwakatarehe, mpiga ramli Shehe Ubwabwa Yaya na wengine. Wao ni vihiyo mie ni bonge la msomi tena mwenye PhD ya kusotea na si kupewa kama kilaza fulani asiye na kumbukumbu kama alivyosema msomi mwenzagu daktari Silaha hivi karibuni.

Wala mie si kihiyo kama mgosi Machungi wa Makambale. Mie ni msomi kama Shivji na gwiji kama Mchonga. Upo hapo mshirika? Mie siogopi mtu wala kitu bali kumwaga ukweli ili kuwakomboa wadanganyika wapumbavu ambao kila kitu kimewekwa mbele yao lakini bado wanaamini watapelekwa Kanani wakati ni motoni kwa kwenda mbele.

Nikiwa ndiyo najinyoosha kwenye sita kwa sita yangu na bi mkubwa akiwa anakoroma pembeni mwangu baada ya … we koma! Hili tuliache nimepata accident ya ajali ya ulimi. Maana nilitaka kwenda nje ya mpaka kama jamaa yangu anapokuwa akiwaongopea wadanganyika wakati wa kutoa ahadi. Utamsikia akisema: tutafanya tutafanya hadi anadondoka.

Nawaza kufanya kazi ya utabiri wa kweli siyo ramli za shehe Ubwabwa mtoto wa yaya mlea majini wa mitaa ya Migomigo.

Natabiri tena kwa kujiamini kuwa vigogo vitang'oka. Anayebishia hili au kuwa na wasiwasi nalo a jiulize ni vigogo vingapi vimeishaanguka wakati vingine vikingoja kunyofolewa? Sasa nasema mapema. Vile vigogo vilivyoko hatarini kuusikia ulaji magazetini vije kwangu haraka niwakinge na anguko hilo vinginevyo wataanguka tu. Hawana haja ya kwenda Bagamoyo wala Sumbawanga. Waje Manzese kwa Mfuga Mbwa. Namba ya nyumba sitaji wataulizia hadi wanipate.

Na kuhusu yule mgombea ninayemshabikia, nitampa kinga ya kuadhirika yaani kumshauri ajipumzikie asijeanguka hata kufa kama alivyomtabiri yule mhuni wa migomigo.

Aking'ang'ania nitamtengenezea zindiko ambalo huwezi kulinusa kwa pua na atakayejaribu kumchezea litakalompata asinilaumu. Mie siyo kama wale watabiri uchwara wanaotumia viungo vya majini na mazeruzeru kuwaibia wateja wao wapumbavu kwa kuwapumbaza na sifa na ahadi za kipuuzi kama wanazotoa kwa wadanganyika.

Mie nasema facts na I am more educated than all those goons calling themselves astrologers or preachers and whatnot. Looh! Nshachanganya na umombo utadhani niko kwetu mombo! Hata hivyo msinishangae. Siku hizi napandisha mwenembago wa kiinglish kutokana na kuwa rafiki mkubwa wa malkia.

Natabiri kuwa wale wote walioibia nchi ama kwa kushiriki MAEPA au Marichmonduli watakumbwa na aibu na magonjwa ya ajabu ajabu kama kupayuka, kuanguka, kuchezeana na kudhulumiana hata kukata roho.

Rushwa kwenye uchaguzi itaongezeka kiasi cha wale waliopaswa kusimamia kuiangamiza kuishiriki vilivyo wao wake na watoto zao bila hata chembe ya aibu. Maskini watumiao matumbo kufikiri watahongwa na kuahidiwa pepo ilhali wanao dhahiri wanavyoelekezwa motoni.

Neema za muda kama kuongezeana mishiko na uhuru mfu hasa kwa ndugu zangu wamachinga kuvunja sheria ya mgambo wa Kandoro zitaongezeka na kupotea baada ya kutangazwa matokeo yatakayotawaliwa na wizi mkubwa wa kura. Wauza gongo nao wakae mkao wa kula. Polisi waliozoea kuwapiga mabao wataamrishwa kusitisha zoezi zima la kuibiana hadi uchafuzi upite. Vyangudoa waliokuwa wakisumbuliwa na ndata kuwakamata uzururaji na kujiuza wanaweza kujiuza kwa sana hadi mwishoni wa Oktoba ambapo nyota zinaonyesha mambo yao yatabadilika kutokana bahari kuwa na mawimbi makali kutokana papa kuwa na njaa sana baada ya kukaa muda bila kula.

Pepo za vuli zitavuma kutokea Bagamoyo, Chalinze, Kangangani hadi Monduli lakini hazitakuwa na madhara yoyote zaidi kujifia kitambo si kirefu. Ngurumo zikisikika sana toka Karatu ikiwa ni ishara ya neema kwa wakulima. Maana baada ya hapo itanyesha mvua itakayosafisha uchafu wote uliokusanywa na pepo za vuli ambazo mara nyingi ni ishara ya uchafu.

Natabiri vurugu zitakuwapo kutokana na wezi wa kura kupambana na watakaotaka kuwaibia kiasi cha baadhi ya watu kufikishwa the Hague baadaye. Jamaa yangu madevu Mureno Okampo yuko anachekelea. Kama jamaa watatiana ngeu na kutoana roho kama ninavyoona kwenye utabiri wangu. Maana atakuwa na watu wengine wa kujaza kwenye sero zake karibu kabisa na Chaz Teila yule wa Liberia.

Natabiri kuwa atakayeiba kura na kushinda akaapishwa atakufa kabla ya kumaliza kipindi chake cha wizi. Pia natabiri kuwa wizi kwenye ofisi na mashirika ya umma utaongezeka kutokana na kufidia rushwa itakayohongwa kwenye uchaguzi. Natabiri kuwa wengi watapewa kakumba ya mipete ya ajabu ajabu kama kinga wakati ni kifo.

Nashauri hawa wajinga wajinga wanaodanganywa na wajinga wajinga wenzao waje kwangu niwape kinga ya kweli ambayo inaitwa UUUK yaani uadilifu, umakini, ubukuzi na kuongea lugha ya wananchi na kufanana nao kimatendo siyo kilongolongo kama wale wenye njaa kaya.

Kusikika ngurumo na radi ni ishara ya mababu kuchukizwa na utawala huu. Nasema wazi kwa kutumia utaalamu wangu wakitabiri kuwa mababu wa Danganyika hawana raha wala ladhi na yanayoendelea kwenye nchi yao walioipigania na kuifia.

Kwanza nisisitize. Mie sijikombi kwa gendaeka yeyote hata awe na maulaji kiasi gani. Kwanza sina appointment na daktari yeyote India kuhitaji kujidhalilisha na kujikomba ili gendaeka wenye madaraka wanilipe fadhila kwa kunilipia nauli na kugharimia matibabu kama shehe Ubwabwa bin Njaa Yaya.

Angekuwa anajua kutengenezea watu kinga si angejikinga badala ya kuhangaika na kujivua nguo ili apate pesa ya kwendea Inida? Kusum bin kusuru audhubillahi mina-shaitwan rajiim shehe Yaya Ubwabwa.

Pia natabiri kuwa bi mkubwa wa Njaa Kaya atafikishwa kwa pilato muda si mrefu asipoacha kujipendekeza na kufuja mali za walevi kwa kutanua na kupiga ndogo ndogo kwa ajili ya bwanaake. Juzi nimemuona hata Riziki naye akimpigia kampeni dingi wake. Kumbe tuna ufalme bila kujua!

Loh! Kumbe kumekucha!
Chanzo: Tanzania Daima Septemba 22, 2010.

Tuesday 21 September 2010

Salma Kikwete Imelda Marcos wa Tanzania


Ridhiwan akifanya mazoezi ya kuwa rais. Chini yake ni bi mdogo wa mzee akifuatiwa na Ridhiwan akikagua gwaride la machinga wa kesho ambao wametengenezwa na utawala wao na kufuatiwa na Imelda Marcos wa Bongo akilakiwa na mkuu wa mkoa wa Dodoma kabla ya kukagua vikundi vya ngoma kama mpendwa chaguo la Mungu mzee Marcos mwenyewe bila kusahau mauzauza (Risiti) za Kinana.




Mauzauza ya Kinana

Je risiti hizi ni halali?

Baada ya kuwa tunalalamikia matumizi mabaya ya pesa ya umma na madaraka hasa kuhusiana na jinsi mke wa rais Salma Kikwete anavyoliibia taifa, Chama Cha Mapinduzi, juzi, kilijikosha kwa kutoa risiti za kukodi ndege ya bi mkubwa.

Kama risiti, hata kama zinatia shaka, zinavyoonyesha, ndege ya bi mkubwa inalipiwa dola za kimarekani 3,000 kwa saa! Kwa kazi gani ya mno kama siyo ulimbukeni, upenda raha na kutafuta per diem. Ajabu mama huyu mpenda raha na pesa anapokwenda mahali hupokelewa kama mkuu wa nchi! Je ni yale ya mbwa wa mfalme kuwa mfalme wa mbwa wote?

Huyu ndiye mama aliyewahi kuwaongopea wanawake wa Tanzania eti aliwahi kunyanyaswa akijifungua bila kutaja lini wapi na nani walimdhalilisha eti wakati mumewe akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje. Hivi kweli huyu ana uchungu na wanawake wa taifa hili au kuwatumia kama majuha kupata mradi wake?

Hapa hatujaongelea pesa inayotumiwa kumkodishia ndege mtoto wa rais Ridhiwan Kikwete anayezurura kama mama yake kila uchao mikoani. Sasa kama Kikwete ameamua kutumia familia yake kupiga kampeni hii maana yake urais wake ni kwa ajili ya familia na si watanzania kama anavyowahadaa. Leo Ridhiwan akikuchukia chamani ujue utaondolewa taka usitake. Rejea yaliyowakuta Hussein Bashe na Hamad Yusuf Masauni walipotofautina naye. Interestingly, alimtuma baba yake kufanya kazi hii chafu. Je hapa rais kati ya Ridhiwan na Jakaya ni nani?
Je huu si ufalme wa nyuma ya pazia? Bahati mbaya hata mfalme mwenyewe yupo yupo kama kibonzo. Anatumiwa kwa remote control na kila aina ya wapuuzi kuanzia shehe Yahya, Lowassa, Rostam, Makamba na wengine! Je huyu bado anafaa kuwa rais wa nchi kweli? Jamani tuondolee hii aibu kwa kumnyima kura lau liwe somo kwa wababaishaji wengine.

Niliwahi kuhoji mantiki ya Salma kutambulishwa kama mwenyekiti wa shirika lake la ulaji la WAMA ilhali akipigia kampeni CCM. Nimekuwa na ugomvi na mama huyu muda mrefu kiasi cha kumuandikia mara kwa mara.

Haiwezekani kulala kitanda kimoja na rais kutumiwe kutufilisi. Hapa hatujaongelea nyumba ndogo ya Kikwete iendayo kwa jina la Rahma Kharoos.
Tufikie mahali tukatae upuuzi huu. Je muda ambao tumekuwa tukimuona Salma akizurura kila mahali ameishatumia dola ngapi na zingeweza kuwasaidia kina mama wajawazito au watoto wa kike wangapi? Ni unafiki na ufisi kiasi gani?

Monday 20 September 2010

Midahalo ya wazi itaiumbua CCM


INGAWA midahalo baina ya wagombea ni jambo jema, kwa wengine, hasa wasio na kitu cha kuonyesha wapiga kura, ni jambo la hatari.

Kupitia midahalo, chama hata mgombea huweza kuwashawishi wapigakura kwa kujibu maswali yao makuu. Kupitia midahalo, mipango, vipaji, sera, historia, weledi, uoza na hata umahiri wa wagombea na vyama vyao, huwekwa wazi mbele ya wapiga kura.

Kwa mgombea au chama ambalo kiliishachafuka au kutopea kwenye shutuma lukuki, tena za kutisha na kuchusha, midahalo ni sawa na moto, huku wao wakiwa wamejipaka petroli.

Kwa kutambua hatari na hali hii, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimewapiga marufuku wagombea wao kushiriki midahalo.

Hata hivyo, hii ni dhuluma na hujuma kwa demokrasia. Kwani kufanya hivyo ni kujiangalia binafsi na kuupuuzia umma ambao chama hicho kinadai kuupigania na kutaka kuuongoza.

Midahalo haijaanzia Tanzania. Hata nchi zinazotufadhili hutumia midahalo kuonyesha kufaa au kutofaa kwa wagombea wa nafasi za uongozi.

Hivyo kutoshiriki ni sawa na kuturejesha kwenye zama za kiza za chama kimoja. Ni aina fulani ya ubabaishaji na kushindwa kwa wazi.

Zuio hili lilianza baada ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete kuonyesha wazi kukacha midahalo kwa sababu anazozijua mwenyewe na chama chake.

Wengi hawakushangaa hili kutokana na kujua hali ambayo CCM na mgombea wake wanakabiliana nayo katika uchaguzi huu. Wameamua kufunika kombe mwanaharamu apite.

Hata hivyo tukirejea historia ya ugombea wa Kikwete, hatutashangaa kukacha midahalo hadi sasa kuingiza hata wagombea wengine wa chama chake.

Alianza mchezo huu mwaka 2005 alipopitishwa kwa kishindo na ushabiki baada ya wengi waliompinga kuchafuliwa vibaya.

Kwa wanaojua uwezo wa Kikwete na hali inayokikabili chama chake, hasa tuhuma za ufisadi, ingekuwa sawa na kujinyonga kama wangeridhia kushiriki midahalo.

Wangeshiriki na lipi la maana ambalo CCM wangewasilisha kwa wapigakura? Je, ingetokea wakaulizwa maswali muhimu na chokonozi, wangejibu nini?

Kwa mfano, kama wananchi wangemuuliza juu ya yeye na chama chake kunufaika na fedha za umma zilizoibwa na kampuni ya Kagoda, Kikwete angejibu nini?

Au, kama baadhi ya vyama vingekuja katika mdahaho huo na nyaraka zinazoonyesha majina halisi ya wakwapuaji wakiwamo vigogo wa serikali, Kikwete na chama chake wangesemaje?

Angeelezwa kwamba fedha hizo zilizoibwa katika fuko la madeni ya nje (EPA) zilitumika kumuwezesha kuingia madarakani chini ya jinai ya takrima, angeeleza nini?

Hivi Kikwete angejibu nini kama angeulizwa chanzo cha fedha zinazomwezesha mke wake kumpigia kampeni, ukiachia mbali madai ya matumizi ya mali na fedha za umma katika kufanya hivyo?

Bila shaka Kikwete angeulizwa mantiki ya mkewe, kwa mfano, kuanzisha NGO baada ya yeye kuingia madarakani. Angeulizwa kwa nini mke wake anayelindwa na fedha za umma anatumikia chama kimoja?

Swali jingine ambalo lingempiga chini na kumuacha uchi bila shaka lingekuwa juu ya ahadi zake za kuwapeleka Watanzania Kanani ambazo alitoa mwaka 2005 asitekeleze hata moja.

Pia swali juu ya ni vipi atatekeleza ahadi nyingine mpya lukuki anazozidi kutoa lingemuacha hoi mbele ya wapigakura kiasi cha kupunguza kura zake.

Hapa halijaulizwa swali moto kabisa kutokana na tukio la hivi karibuni la Shehe Yahya Hussein kuahidi kumpa ulinzi wa majini, tena katika karne ya 21 ya sayansi na teknolojia, ilhali anao walinzi wanaolipwa mabilioni ya shilingi.

Pia wengi wangetaka aeleze ni vipi alichezewa hadi kuanguka kama alivyodai Hussein bila kusahau kumbana aeleze ni kwanini Hussein amegeuka msemaji wake.
Angeulizwa kwa nini Yahya anaingilia mambo yanayopaswa kutolewa maelezo na yeye Kikwete au daktari wake na asimkemee, kama kweli hajamtuma kujenga hofu kwa Watanzania?

Hivyo basi, CCM imekataa kuweka shingo lake kitanzini na kufa ikijiona, ingawa hili si jibu mujarabu. Kwani wengi wamefanikiwa kuona woga wa chama hiki kiasi cha kushindwa kuiamini CCM-mwoga kuendesha taifa lao.

Kuna maswali mengine ambayo yangemsumbua hata kumuumbua Kikwete.

Kwa mfano, kama angeulizwa mantiki ya mwanae Ridhiwan kuwa na nguvu katika chama; unadhani angejibu nini?

Najua wanaohoji wasingekuwa na ubavu wa kumuuliza maswali makali kama haya. Bali wagombea wenzake hasa Dk. Willibrod Slaa angeyachomeka ili yapate majibu kwenye kadamnasi.

Kwa vile kugoma kushiriki midahalo kwa CCM kumewanyima wananchi haki yao ya kuchambua sera na mipango yao, kuna haja ya kuiogopa CCM kama ukoma.

Hakika kama chama hicho kimekosa hata mawazo ya kuwaeleza wananchi, kitapata wapi msuli wa kuwa na matendo ya kuwafikisha watakako?

Leo, Kikwete anajitahidi kuwaaminisha Watanzania kuwa atawavusha wakati pesa ya umma, licha ya kutumika vibaya, inaibiwa kila uchao?

Rejea kugundulika kwa wizi wa Sh.1,700,000,000 (trilioni moja na milioni mia saba) uliofichuliwa na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kuwa ulifanyika ndani ya mwaka jana tu.

Fedha hizi ni sawa na takriban moja ya tano ya bajeti ya Tanzania ambayo ni trilioni 11.

Kupitia midahalo, wengi wangetaka kusikia majibu ya Kikwete, hata wagombea wengine, juu ya mantiki, kwa mfano, ya kupitisha wagombea wanaotuhumiwa kwa kashfa mbalimbali, kama vile ufisadi na kughushi vyeti ukiachia kutoa rushwa ambayo inasemekana imetolewa na wagombea wengi, kama sio wote, wa CCM.

Aidha, wengi wangetaka kumsikia Kikwete akielezea mipango yake ya kuvunja urafiki na watuhumiwa wa ufisadi ambao wamekuwa wakijisifu kuwa urafiki wao hauwezi kuvunjwa na vyombo vya habari.

Wengi wangetaka kusikia tathmini binafsi ya Kikwete ya utawala wake ulioonyesha wazi kulegalega na kufumbia macho ufisadi kiasi cha imani kuanza kujengeka kuwa CCM inaendeshwa na mafisadi.

Kwa jumla, maswali ambayo yangemuweka Kikwete msalabani kama angeridhia kushiriki midahalo, ni gunia.

Hapa CCM imekiri wazi udhaifu na utupu wake. Hakika, imedhihirisha kuwa imeisha na kuishiwa, ukiachia mbali kuwa mshiriki wa jinai na kuendeshwa kwa mawazo mgando yanayopingana na mambo ya kisasa kama midahalo.

Je, kwa hili, hukumu ya wapiga kura itakuwa kali kiasi gani? Tungoje tushuhudie ambacho hatukutegemea. Kuna uwezekano watu wasiamini masikio na macho yao huko tuendako.
Chanzo: Mwanahalisi Septemba 15, 2010.

Wednesday 15 September 2010

Is Rwanda's Day of Reckoning Here?

There is bad blood between authorities in Kigali and UN thanks to a leaked report on genocide and crimes against humanity implicating Rwanda forces in DRC. The darling of UN, Rwanda, is now threatening to stop cooperating with UN.

Though Rwanda has the right to defend itself, it ought to consider what transpired in 1994. When UN hurriedly declared that the killings in Rwanda were genocide, the accused people-Hutu, were not given any chance to argue their case. If precedent is to be followed, Rwanda's denial does not help anything save to show the UN's double standard shall it bow to the pressure and stop publishing the report.

According to Rwandan government spokesperson Ben Rutasingwa, “It is immoral and unacceptable that UN, an organisation that failed outright to prevent genocide in Rwanda...now they accuse the army that stopped genocide of committing atrocities in DRC.” This is the 'big weapon' Rwanda has always used to intimidate the UN and the whole world.

The point at hand is not who stopped or failed to stop genocide in Rwanda. The issue is whether the Rwandan army committed genocide in DRC. The UN failed to prevent the Rwanda genocide from as it did in DRC. But shall UN failure be used as a pretext of burying the rights of those that were felled in DRC? This is a separate case that should not be used to deprive and trample on the rights of DRC. Two wrongs never make a right. Today, Kenya cannot intimidate ICC in defending its post-ballot warlords simply because ICC has failed to arrest Omar Bashir. These are two different cases with different merit.

If Rwanda sticks on its guns and UN cowers away, who then will prosecute the criminals that committed genocide in DRC? Shall individual countries institute cases against Rwandan authorities as Spain and France did? Will they be accused of sabotaging Rwanda and the development already realized there? The blood of the innocent people of DRC as it was for Rwandans cannot be spilled in vain. Invading DRC was illegal ab initio.

If it was possible for Rwandan authorities to come up with the numbers of those that were felled in the 1994 genocide ex-parte, what is wrong with the UN looking into what actually transpired in DRC when Rwanda and Uganda invaded and plundered DRC?

Shall UN withdraw this report or cower away just because Rwandan authorities have threatened to withdraw their army in Darfur, UN will end up in an awkward situation thereby losing its credibility before the eyes of the world. This should not be allowed to happen.
Source: The African Executive Magazine Sept. 15, 2010.

Mwaka huu tuelewane vizuri, ni ahadi kwa saana



BAADA ya kutambulisha chama changu cha FACCM rasmi, nataka niwaeleze wapiga kura kitu kingine muhimu. Wiki jana nilielezea sera zangu zenye sura nzuri kama mimi. Pia niliweka wazi hali yangu kiafya kwa kusema niko fit kichizi. Ingawa leo sitatangaza mali zangu, naahidi kufanya hivyo kabla ya kumaliza kampeni za uchafuzi huu.

Pia niseme wazi. Mie siungi mkono madai ya kipumbavu kama wizi wa wake za watu. Hivi kati ya 'mwizi' wa wake za watu, mbakaji na mwizi wa mabilioni ya EPA na mengine nani mbaya? Jibu mnalo na mtajaza kwa kunichagua mimi na kuwanyima wale wasile. Walichokula kinatosha kama hakitoshi waende lupango watakula huko huko.

Najua watani wangu hasa wale waliofukuzwa ualimu kwa kubaka wanakiita chama changu FARIKICCM au CCMFIRIA MBALI. Hata hivyo mie sijali. But beware. I'll yuk it up with these braggarts. Kama ulifukuzwa kazi kwa kubaka, jiandae. Sina urafiki na kujuana tena hata kama unaniabudia.

Ibada zako za masanamu haziwezi kunifanya nikupendelee au kukukingia kifua tena. Nitafufua kesi yako upya ili umalizie maisha yako lupango. Mgosi makambale upo hapo? Naja mwana mapinduzi kipenzi cha wadanganyika na walevi.

Kama unatumia hovyo mali za umma kumpigia kampeni mumeo nawe jiandae kunyea debe bila huruma. Na kweli nitawafunga. We ngoja wadanganyika wanichague uone.

Naomba niahidi kitu kingine. Nitapunguza nyumba ndogo kutokana na washauri wangu kunishauri kuwa wanakula pesa nyingi ya umma. Kwa vile nimeamua kupambana na ufisadi, nao nitawaweka kwenye kundi la mafisadi hata kama ni wapendwa wangu. Pesa nitakayookoa itatumika kununulia bajaj za kuwapeleka wajawazito zahanati.

Naomba mtege masikio na kupanua macho kama mnapokea roho mtakakitu- sorry mtakatifu. Kipindi kile nilipowaahidi maisha bora wengi walikosea. Walidhani maisha bora niliyomaanisha ilikuwa ni kwa wote. No. hapana. Nilimaanisha mimi, bi mkubwa, vitegemezi na marafiki zetu.

Kwa walio wengi nilichodhamiria kufanya si kuwapeleka Kanani bali motoni- sorry- peponi kimawazo. Nilishasema wazi. Raha jipe mwenyewe usingoje kupewa nami au siyo. Ila kipindi hiki, baada ya kuleta maisha bora kwa watu wangu, nadhamiria kuleta maisha bora kwa wote wote. Si sanaa. Niaminini.

Naahidi kuwa nchi nzima itaanza kubadilika kutoka kwenye nchi changa kwenda nchi tajiri.

Nitajenga magereza mengi ili kuwafunga watakaotaka kutusumbua. Pia nitajenga vyuo vikuu vingi feki na vya kweli ilmradi kila mtu apate digrii nyingi za heshima kama zangu. Hamjasikia nakijisifu kuitwa Dokta Mpayukaji ingawa sijawahi kusomea udaktari kutokana na kuwa kilaza?

Nazidi kutoa ahadi. Nataka nieleweke. Kipindi hiki nitanunua ndege nyingine kwa ajili ya wanakaya sorry bi mkubwa, I mean, wanakijiwe wote. Na hii si utani. Nitawanunulia ndege za kumwagilia maji na dawa za kuulia wadudu. Msiulize pesa itapatikana wapi.

Nimepokea mabilioni mengi kutoka kwa mafisadi niliowaomba warejeshe pesa hiyo kutokana na kuwastahi. Si mnakumbuka nilivyofungua kesi za kiushikaji-sorry- za kipiginaji dhidi ya akina Mbwamwitu, Pesatatu, Son of Jonah na Grace Mgonjwa.

Mwaka huu nitawafunga hata bi mkubwa kama atajiingiza kwenye ufisadi naapa haki ya mama. Sina mchezo na mafisadi. Nitahakikisha, kipindi hiki, hata misafara yangu ya magari na madege itapunguzwa.

Bi mkubwa aliyezoea kupokelewa kama mimi naye lazima alie. Ataruhusiwa kusafiria gari moja tena mkangafu siyo shangingi. Kwanini shangingi kupanda shangingi usawa huu? Je, hiki si kiherehere alichosema bi fulani wa kule Chakudema?

Wakulima wa kaya hii kwa mara ya kwanza wataona mimashine mikubwa ya kulimia kama vile tillers, hoes, machetes na mingine midogo midogo kama harvesters, sprinklers, hallows, milkers, splitters, tow-able diggers, crawling diggers, 12MTR hardi sprayers, Mercedes/claas OM422, sow bench na madude mengine yenye majina magumu.

Ile helikopta yangu ya kampeni nayo itatumika kusambaza mbegu za kisasa ili kuhakikisha tunakuwa na kilimo cha kisasa na si ufisadi wa kisasa na kisasi.

Uchumi wa kaya utakua kwa asilimia milioni moja niaminini. Kwa vile nimegundua sayansi ya kuchakachua, kaeni mkitarajia maajabu ya maajabu ambapo kila kitu kitachakachuliwa na kuzaa vingine vingi.

Wale ndugu zangu wa Kanda ya Ziwa wanaoteswa na ukosefu wa meli kwenye Ziwa Nyanza watulie. Kwani, nitakapoingia madarakani nina mpango wa kuwanunulia meli kumi zenye ukubwa zaidi ya lile meli la kitalii liitwalo Princess Kaguya.

Kwa vile wamekaa muda mrefu bila usafiri huu muhimu, kwa mwaka wa kwanza watasafiri bure ili kufidia madhara waliyopata hata kupoza hasira za kusahaulika. Waathirika hasa ndugu za marehemu wa ajali ya mv Bukoba, licha ya kusafiri bure maisha, watalipwa fidia na riba ya miaka mia kutokana na walionitangulia kulifanyia uzembe suala hili. Niamini. Hii si sanaa wala kamba ya kupata kula.

Pamoja na kuahidi kujenga daraja pale Kigamboni, nitaongezea vivuko vingine viwili vikubwa kuliko Colour Magic na Colour Fantasy ili kuchukua rekodi ya dunia ya vivuko bora na vikubwa duniani.

Wale vijana waliokuwa wakizungushwa na tume ya mikopo ya elimu ya juu wakae mkao wa kula. Kwa sasa ndiyo wakati wa kupata mikopo ili mnipigie kura ya kula kwangu ukoo wangu na mafriend zangu au siyo? Hamjasikia walichosema wahenga? Kufa kufaana ati.

Nasisitiza. Msitie shaka. Yule jamaa aliyewanyanyasa J4 Majembe hawezi kurudi kwenye ulaji. Mmeishashuhudia jinsi wasanii wanavyoniabudia hadi kunipiga kampeni. Hata hivyo najua. Hata kama hawanipendi zaidi ya pochi, tunatumiana hivyo hivyo. Huu ndiyo usanii.

Hamjaona waimbaji wa nyimbo za Bwana nao wameingia kwenye kipute cha kuninadi. Nisikose shukrani. Mie ni chaguo la God ndiyo maana waimbaji wa nyimbo za God money wananipigia debe. This is bongo usishangae hata kama ni sanaa.

Kwa upande wa Zenj nao nasema poeni. Nikishaingia kukuu nitahakikisha, licha ya kuwapa hadhi ya nchi, nitaigeuza Zenj kuwa Hong Kong ya Afrika. Huu ni ukweli si longolongo wala ndoto za mchana niaminini ama sanaa ama lugha ya kamapeni. Hakuna kuhangaishwa na tetesi za kuwapo wese.

Mie nitawageuza kabla ya wese hata kugundulika. Nimepania kuleta mapinduzi kichizi ya chama changu cha mafisadi. Nitafanya nitafanya tutafanya tutafa...

Aisee! Ntiiii! Mweleka. Kumbe shuga imepungua kwenye bode!
Chanzo: Tanzania Daima Septemba 15, 2010.

Tuesday 14 September 2010

Hivi hawa nao ni wanadamu au ?

Taarifa zilizopatikana kutoka London Uingereza ni kwamba daktari mmoja wa kiingereza mwenye asili ya kihindi na mwanae walimshikilia na kumtumikisha mama wa kitanzania aitwaye Mwanahamisi Mruke (46) tangu mwaka 2006.

nani anaweza kuamini kuwa katika karne ya 21 Mruke alikuwa akilipwa paundi kumi za Uingereza kwa mwezi? Nani angeamini kuwa jinai hii ingetendwa na mtu anayejiita mtanzania ingawa kwa sasa ana uraia wa Uingereza ambao ameupata kutokana na pasi ya kusafiria ya Tanzania sawa na wahindi wengine ambao huja kuzuga na kutumia pasi zetu?

Daktari Saeeda Khan (68) alimrubuni Mruke na kumvusha hadi Uingereza alikomshikilia mateka na kumtumikisha kama mtumwa huku akilala jikoni na shuka moja pamoja na baridi kali ya Ulaya. Ni unyama kiasi gani? Je mamlaka za Tanzania baada ya kupata habari za ushenzi huu zimefanyanini? Zifanye nini iwapo jamii hii nyemelezi ndiyo inadhamini wezi wapenda madaraka kuwa madarakani na kulipa fadhila? Rejea kushindikana kukamatwa kwa Rostam Aziz, Ketan Somaiya, Jeetu Patel, Shailesh Villani wa rada, Andy Chande na majambazi wengine wa kihindi wakishirikiana na majambazi wa kiswahili kama Andrew Chenge, Dk Idris Rashid, Nazir Karamagi, Edward Lowassa, Ridhiwan Kikwete na wengine kabla ya kuwataja majambazi wa kisomali kama Aden Rage, Abdulrahaman Kinana na wengine.

Kuhakikisha unyama na ushenzi huu unafanikiwa, Khan alikuwa akimvisha Mruke kisasa na kutomruhusu kutoka nje bila ya kuwa naye mumewe au mwanaye kiasi cha kuepa jicho la majirani. Hii imewashangaza majirani wengi. KWa miaka minne Mruke alikuwa akila mabaki yanayobakizwa na 'mabwana' zake waliomteka. Ni ukatili kiasi gani?

Leo utawaona kunguru nao eti wakigombea ubunge kupitia Chama Cha Mafisadi ili kuwatumikia lakini wabongo kwa makengeza na chongo huwaamini. Hata hivyo tuna mikoa yenye kukaliwa na mataahira na waroho wanaohongwa upuuzi wanaowapigia kura hawa kunguru Pamoja na India kuwa na watu weusi, ni wangapi wanaishi maisha mazuri au kuwa na fursa hata kuingia kwenye siasa? Kuna haja ya kubadilika. Kwani kila walipo kunguru huakikisha wanaweka mfukoni watawala mbwa na vipofu na kuondoka na utajiri huku nyuma wakiacha umaskini wa kutisha. Hivi karibuni imegundulika kuwa mtoto wa rais wa Afrika Kusini aitwaye Duduzane Zuma anatumiwa na kunguru kuhujumu nchi hiyo. Hii ni syndicate ya kuhujumu kila nchi ili kunufaisha ukunguruni.

Hili nimelijadili sana kwenye kitabu changu cha NYUMA YA PAZIA kitakachotoka hivi karibuni. Angalieni unyama huu wabongo muamue wenyewe.

Monday 13 September 2010

Karibuni tutashika bomba kwenye pipa



Hizo ndizo zana mpya za kushikia bomba kwenye pipa. Bado wapiga debe nao kuajiriwa.




Kampuni moja ya kitaliano iitwayo Avioninteriors imekuja na mpya ilipobuni siti za kusimama kwenye ndege ili angalau wale wachovu kama mie nao waweze kupanda pipa kwa bei nafuu. Hapo juu ni viti vya kusimama au tuseme kushika bomba au SkyRider kama wao waviitavyo.

Zana hizo za kushika bomba kwenye pipa zilionyeshwa juzi miezi michache baada ya mkurungezi wa Ryanair, Michael O'Leary kusema kuwa shirika lake lilikuwa na mpango wa kuanzisha huduma ya kushika bomba kwenye pipa.

Hata hivyo sijaelewa. Hivi kweli itawezekana kwa mfano mtu kushika bomba toka Bongo hadi Marekani au toka Ujepu hadi Kanada hii?
Yetu macho.

Sunday 12 September 2010

Tishio la kuchoma Qur'an ujuha na wendawazimu..






























Mwezi wa Ramadhan umeisha katikati ya kitatange cha mchungaji mmoja mchumia tumbo Terry Jones wa Gainesville Florida nchini Marekani alipotishia kuchoma nakala zipatazo 200 za Qur'an. Jambo hili lilizua maandamano kwenye nchi mbali mbali za 'kiislam' ikiwemo nchi iliyoshindwa ya Somalia.

Wengi walijiuliza mantiki ya wasomali kuandamana kupinga tukio hili huku wakishindwa kuandamana kuwashinikiza mabwana vita walioliteka taifa hili wafikishwe mahakamani. Hii imenikumbusha kisa cha kipumbavu kilichotokea nchini Sudan mwaka 2007 ambapo mama mmoja mwalimu wa kiingereza Gillian Gibbons alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la kuandika jina la Mohammad kwenye zawadi ya kinyago cha dubu alichompa mwanafunzi wake alyeitwa Mohammad.

Wengi wenye akili walijiuliza mantiki ya wasudan kuandamana wakiwa wameshikilia visu na mapanga kupinga 'kufuru' hii ilhali wasudan hao hao wakimkingia kifua ili asikamatwe na mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC) muuaji Ahmad Harun ambaye jina lake Ahmad pia ni jina la mtume Mohammad! Wengi walizi kushangaa wauaji wengi wanaoendesha mauaji ya kimbari jimboni Darfur kuwa na jina Mohammad!

Hivi ni kina Mohammad wangapi wanakula unga, vibaka, wabakaji na mengine mengi?

Mambo yalizidi kunoga na kubainisha wendawazimu pale waandamanaji walipochoma bendera ya Marekani. Inashangaza binadamu tumekuwa majnun na wehu kiasi hiki! Tumeshuhudia bendera ya Marekani ikichomwa na wehu waliokuwa wakiandamana kupinga kuchomwa kwa Qur'an. Yaani unapinga jinai kwa jinai? Hakika huwezi kufua nguo kwa maji taka ikatakata.

Hivi kweli kuna mtu anaweza kuchoma Qur'an yaani ujumbe au ni kuchoma vitabu tu? Huwa najiuliza kati ya aliyehifadhi Qur'an na tabu Qur'an ni ipi? Huu ni ushahidi kuwa wengi wanaojiita waislam japo si wote ni washirikina. Kwani wanaiona Qur'an kwenye maandishi wakishindwa kuijua kwenye mitima!

Hivi ni hafidhi wangapi wanapanda dala dala na kukaa karibu na vyangudoa, walevi hata mafisadi? Ni ajabu kidogo!

Hakuna anayeshabikia kuchomwa kwa Qur'an sawa na kuchomwa bendera ya nchi yeyote.

Wengi bado wanajiuliza mantiki ya kujengwa msikiti kwenye eneo la Ground Zero lilipokuwa jengo la World Trade Center (WTC) lililolipuliwa na kufutwa toka kwenye uso wa dunia hapo Septemba 11, 2001 ambalo, maadhimisho yake ndicho chanzo kikuu cha mgogoro wa tishio lililositishwa la uchomaji Qur'an. Wengi wanaona kujenga msikiti kama ni kuwakumbuka magaidi, na kwa kiasi fulani, kuwakweza kwa kitendo chao cha kishenzi. Wengi wanahoji, ingekuwa Makka wangeruhusu msikiti kujengwa kuwakumbuka magaidi wa dini nyingine?

Wengi wangejua kuwa Jones alikuwa anatafuta namna ya kujulikana na kukuza kanisa lake la kibabaishaji dogo, wasingepoteza muda wao na kuonyesha wendawazimu dhidi ya kupambana na wendawazimu. Let a fool hold his tongue and he will pass for a sage.  ~Pubilius Syrus
Somo kuu hapa ni kwamba: tapeli mmoja, sawa na wale wa viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam na kwenye luninga, amefanikiwa kuwatumia waislam wapumbavu kupata umaarufu na kufanikisha lengo lake. Nia aibu iliyoje?

Tumalize kwa kuhoji. Je kama Jones angechoma Qur'an ingekuwaje? Je jua lingesimama au kudondoka? Ni ajabu kuona kitu ambacho hata mtume Mohammad hakuacha kuwahangaisha watu wakasahau hata kufikiri! Je Qur'an ina maana kuliko binadamu wanaouawa kila siku ilhali ilishushwa kuwatumikia si wao kuitumikia? Tutafakari tena kwa sana.Je Qur'an ambayo ni kifaa ina thamani kuliko binadamu?

Kituko na wendawazimu zaidi ni pale mwanasheria mmoja wa Australia Alex Stewart alipochana Biblia na Qur'an na kutumia karatasi zake kutengeneza msokoto kuona ni kipi kinaungu vizuri. Hii maana yake ni kwamba matepeli wengi sasa watajitokeza, sawa na makundi ya kigaidi, kuvichoma vitabu hivi wakitafuta kujulikana!

Siku kunguni walipowanyima usingizi wakanada



Inaaminika kuwa kunguni ni adha na dalili za umaskini. Lakini hali si hivyo hapa Kanada ambapo kunguni wanaonekana kuwanyima usingizi wanasiasa kiasi cha kulalamika. Je hili lingetokea uswekeni wenye pesa zao wangesemaje? Tungeona ma-TX wa kutuhubiri juu ya usafi na mambo mengine kama hayo huku watawala wetu omba omba wakiomba misaada ya haraka kuteketeza balaa hili. Tungeambiwa huu ni ugonjwa wa maskini. Leo watasemaje jamaa zetu hawa? Maana kwa ujumla Kanada haina maskini kwa maana ya neno.
Michael Colle wa Chama cha Liberal alikuwa na haya ya kusema: "Inakatisha tamaa. Watu wananiambia kuwa hawawezi kulala na ni gharama na hawajui la kufanya na kipi kitawasaidia,"

Mamlaka za tiba za jiji la Toronto zimekiri kuelemewa na tatizo la kunguni. Kunguni jike, mdudu mwenye ukubwa wa milimeta sita asiyeruka ana uwezo wa kutaga mayai kuanzia 200 hadi 400 katika kipindi chote cha uhai wake. Kwa sasa kunguni ni tishio kwa wenye majumba na biashara kadhalika.

Tatizo haliko Toronto tu. Majimbo mengine kama Quebec na British Columbia yameishalalamika. Nashukuru Mungu kwenye jimbo langu hawajafika nami nikaipata fresh.

Thursday 9 September 2010

“Mr. Museveni, you can retire now”


Little bird confessed to me that Ugandan strong man wanted the retiring age to be suffocated from 60 to 55 years! What appalls so as to create amber of anger is the fact that the advocate who, in essence is a grand provocateur, is himself above 60 and he does not seem to think about retiring! This suggestion, though, did not augur well even with his own establishment leave alone Uganda. Is this better than thou or just blind arrogance? Help me out thither.

But how could Museveni bother or get it at all if his military regime has always depended on ex-rebels and their friends? To him the civil service that employs many does not affect his government and family. Museveni thinks he’ll create more jobs by curtailing the age of retirement. Many are baffled and annoyed altogether. Is this the only way of creating jobs? Youths have already urged him to retire a lot of his friends, cronies and compatriots in the rank whose age are above 60.

His heart in his mouth, at this time he’s grappling with trying to convince Ugandans that he’s healthy reason to stand for presidency after 24 years in power. Many would think he’d have heart not to take this suicidal direction. But what is he afraid if at all, is all, in all and above all?Ugandans however would like to have something new. They are tired of being under a state of emergency for decades that aims at cowing them not to dare touch power that Museveni and his cabal has cowered on. The power that has become Museveni’s and his family and cronies.

Though, legally a state of emergency is declared in the main, when there are some natural dangers and in this case, the danger is Museveni himself.

What I very much know about our mumbo jumbos is the fact that they are good at teaching what they failed in. They will forcefully tell you to pay tax so that they can squander whilst they actually don’t pay the same but stealing it!

They will tell you of trimming down expenditure whilst they squander and steal the same money you toil for in the name of oiling the cog of the government full of corrupt elements invited, dined and cloned by them.

They will tell you to take pride in your home education whilst they sent their kids abroad for the same, not to mention hospital and procurement.

They will tell you to invest in your country whilst they steal money and stash it in off-shore banks.

They will tell you everything whilst they do and love nothing as far as the country they advocate is concerned.

They will teach you how to love your country whilst they hate it by selling it to bogus investors which, in essence, are but their agents and business partners behind the curtains.

They will tell you die for your country whilst they put the same on crucifixion.

One thing is obvious. They preach water and drink water not to mention how they are actually double-faced nugatory creatures. Recently in Tanzania, the president was telling people to abide by rule of law. But at the same time, his wife, the first lady, is abusing his office than never before. His son is the “son president”, his wife a “wife president”. Presidency within presidency.

This reminds me of the current Rwandan regime that accused others for committing genocide. When its dirty linens in DRC came forth with true image of what it committed, the same genocide it has accused others of, it started swearing at whoever tells the truth. But remember. The same applauded the same UN it wanted to shun, when it hurriedly declared that genocide was committed against Tutsi that are ruling Rwanda and the same that are accused of committing genocide in the neighbouring DRC.

This reminds me of Gambian oddball Yahya Jammeh who came to power by way of coup d’ Etat but does not like to accept that he taught many the same.

It reminds me of King Mswati III who committed adultery so as to pay a bull. But when tables were turned against him, he wanted throats chopped! What a better than thou aggrandizement!

Museveni’s blindness reminds me of Zimbabwean strong man Robert Mugabe, who, in the name of fake patriotism and delivering on his promises he made over twenty years ago, destroyed his country by negative idealism and racism. So too, the butcher of Malawi, Hastings Kamuzu Banda, used to encourage Malawians to respect and love him whilst he hated and disrespected them. His successor, Bakili Muluzi suffered the same. He came to power under the banner of democracy. But he ended up a traitor that wanted to tamper with the very constitution that brought him in so as to remain in power.

Indeed, hypocrisy is like blindness and mania. It reminds me of the dilemma of Mwai Kibaki. He hated and fought Daniel arap Moi’s dictatorship so as to usher the new constitution, at whose promulgation he invited the dictatorship and genocide of the butcher of Sudan Omar Bashir.

So too, this reminds of the circus Jacob Zuma is now playing after duping the workers of South African who, in essence, drummed big support for him to come to power after toppling Thabo Mbeki. Currently Zuma is under fire thanks to workers unraveling his ploy.

To spice all this, news that the 84 years Senegalese neo-dictator is intending to standing for presidency again left many paralyzed. We used to wrongly think that Zimbabwean strong man Mugabe is the only centurion to cling unto power. Now we have another geek not to mention Egyptian one Hosni Mubaraka.

Unemployment, bad governance and corruption are the major anathema for Africa’s destitution. To curb them, our rulers must create job instead of slashing retiring age. If this is the must-have remedy, then they must retire themselves first before retiring others that are even younger than them.

Another thing to pull us out of this purgatory is nothing but to practically thwart corruption which, in the main, involves them, their cronies and members of their families.
Source: Afro Spear Think Tank September 8, 2010.

Salma Kikwete anapiga kampeni kama nani na kwa pesa ipi?

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT mkoa Dodoma Fatma Tawfiq alipowasili katika uwanja wa ndege Mkoa wa Dodoma jana.katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh. James Msekela. Tarehe 28 Agosti 2010.

JUZI niliona habari kuwa mke wa rais Jakaya Kikwete aliyetambulishwa kama mwenyekiti wa WAMA, Salma Kikwete, akimnadi mgombea wa ubunge CCM, jimbo la Mafia, Abdulkarim Shah.

Swali la kwanza lililonijia ni: kama WAMA ni asasi isiyo ya kiserikali ya kutetea wanawake wote wa Tanzania wakiwemo na wa vyama vya upinzani, inakuwaje mwenyekiti wake amnadi mgombea wa CCM?

Je, kweli WAMA iko kwa ajili ya maendeleo ya wanawake wote kama jina lake au kutumika kama chombo cha kukusanyia pesa kwa ajili ya familia ya Kikwete na chama chake? Je kwa kujiingiza kwenye siasa, bado WAMA inaaminika? Je WAMA si taasisi ya nyuma ya pazia ya ulaji ya CCM kwa mgongo wa ikulu?

Nikiri. Nimekuwa na picha mbaya ya WAMA si kwa sababu nina ugomvi nayo bali hali halisi. Nikikumbuka yaliyotokea kwa EOTF ya Anna Mkapa iliyoishia kuwa kichaka cha ufisadi kwa kutumia ikulu, sina imani na amani na WAMA.

Kuondoa utata basi WAMA iitwe WAMACCM yaani Wanawake na Maendeleo wa Chama Cha Mapinduzi. Hili likifanyika sitakuwa na ugomvi na WAMA ingawa kama mchezo wa kutumia mali za umma na serikali kufanya shughuli za kisiasa kama ilivyo utaendelea, vitanilazimisha kuwashukia tena. Huu ni wizi hata kama unafanywa na wakubwa. Wizi ni wizi na si mzuri.

Niliwahi kuuliza ingawa sikujibiwa. Kwanini kila shughuli ya WAMA inaonekana kuwa ya kidikteta kwa maana ya kusimamiwa na mtu mmoja-Salma kiasi cha WAMA kuwa Salma na Salma kuwa WAMA?

Kwa nini iote baada ya bwana mkubwa kuingia madarakani kama lengo si ulaji kwa kutumia mgongo wa ikulu kama EOTF?

Hata ukiangalia mpangilio wa watendaji wake unagundua kuchanganya mambo kiasi cha kuumbuka au kuufichua ukweli ulioko nyuma ya pazia. Kwa mfano kwenye watendaji wa WAMA kuna mtu aitwaye Anande Munuo ambaye ametajwa kama secretary to the first lady siyo to the chairperson. Hii ni nini kama siyo kufanyiana usanii?

Habari tajwa inaendelea kusema kuwa Salma alikuwa kwenye ziara ya siku moja kisiwani Mafia kuwahamasisha wanachama wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) kuwachagua wagombea wa CCM! Je hapa kuna swali tena? Je huu si ushahidi wa kimazingira kuwa asasi hii ni hatari kwa demokrasia kwa sababu kuu mbili:

Mosi kutumika kisiasa kwa manufaa ya Kikwete na CCM. Na pili kuanzisha katika wakati na mazingira yanayotia shaka ukiachia mbali shughuli zake kutia shaka vile vile. Mbona hatuoni taarifa ya ukaguzi wa hesabu za WAMA kila mwaka? Nani ataikagua iwapo hata mume wake amegoma kutaja mali zao na WAMA ikiwemo?

Hapa hujagusia mapokezi mazito anayopewa kama mke wa mkubwa kila anapokwenda m ikoani hata nje ya nchi anapokusanya pesa kwa mgongo wa ikulu. Bado hapa hujadodosa misafara mirefu ya magari anayoandamana nayo. Kama nani chini ya katiba yetu viraka? Je huku si kutumia vibaya madaraka kwa mumewe? Leo utasoma habari za Salma akifanya kazi ya CCM kesho mwanae wa kufikia, Ridhiwan akimnadi baba yake kabla ya baba mwenyewe. Je hapa si kutengeneza ufalme wa familia ya Kikwete jamani?

Najua Salma ni mwalimu. Wengi wangedhani, kama kweli angekuwa ana uchungu na watanzania, basi angewekeza kwenye elimu badala ya siasa za nyuma ya pazia. Asingepata muda wa kuwania nafasi chamani bali kutumia muda wake kama first lady kuhamasisha elimu iliyosahauliwa na utawala wa mumewe. Hata hayo maendeleo yasiyoonekana anayohamasishwa yanakwamishwa na serikali ya mumewe iliyokumbatia ufisadi na kujuana.

Tusiseme bila ushahidi. Wako wapi kina Kagoda ambao wanazidi kutesa huku wanaowapinga wakiteseka? Wako wapi kina Richmond wanaotukoga kila uchao kuwa urafiki wao na Kikwete si wa barabarani na hauwezi kuvunjwa na vyombo vya habari? Leo fisadi ananyea ofisi mchana anatimuliwa lakini anaitwa mstaafu! Tangu lini mharifu aliyekiri kwa kujiwabisha akawa mstaafu? Au ni kwa vile wastaafu wa kweli kama vile waliokuwa wafanyakazi wa Jumuia ya Afrika Mashariki tumewadhulumu na kubadilisha maana ya mstaafu? Kama Salma na WAMA yake wanapigania maendeleo kweli, kwanini asimwambie mumewe kuwa maendeleo hayawezi kupatikana katikati ya ufisadi na ubabaishaji?

Wakati Salma akiwatumia wanawake na ikulu kumpigia debe mumewe, mumewe naye anatumia magari ya umma kujipigia kampeni! Hivi nchi hii imerogwa na nani na itapona lini?

Je, kwa tabia hii na ufichi huu Salma anajitofautisha vipi na ma-first ladies mafisadi kama Grace Mugabe bingwa wa kufuja pesa ya umma, mareheme Stella Obasanjo aliyewahi hata kutoa amri ya kufungia gazeti, Lucy Kibaki aliyewahi kuwachapa waandishi wa habari bila kusahau, Nana Kanadu Rawlings aliyewahi kutajwa na mumewe kuwa ni binadamu pekee ambaye angeweza kumdhibiti Jerry Rawlings rais wa zamani wa Ghana?

Je, kitendo cha mke wa rais kutumia taasisi isiyo ya kiserikali kuwahadaa na kuwahonga kina mama hakitoshi kuwa ufisadi? Kwanini wapinzani wasichukue hoja hizi na kuwabwagia watanzania wajue nchi yao inavyoliwa kwa mgongo wa rais? Haya ni matumizi mabaya ya mamlaka yanayokinzana na utawala bora na wa sheria anaojisifia kutekeleza rais Kikwete. Wapinzani wakiuonyesha umma madudu yake, licha ya kufichua ubovu wake, watakomesha tambo na uongo wa Kikwete ambaye kwa miaka mitano hajafanya lolote la maana zaidi ya kulinda ufisadi na matumizi mabaya ya raslimali na fedha za umma.

Pia kwa kufichua hujuma ya WAMA angalau wananchi watajua siri ya kampuni hii kuundwa pindipo rais Kikwete alipoingia madarakani na si kabla. Kwa kuiandama hata kuifutilia mbali WAMA tutaepusha wake za marais wajao kuendelea kutuibia kwa kisingizio cha NGO na visingizio vingine ambavyo kimsingi vinaonyesha hizi NGO zinaanzishwa kwa minajili ya kujitajirisha na kuzitumia kupitisha rushwa kwa wapiga kura kama inavyofanya WAMA.

Ningeshauri WAMA iitwe MAWA au Maulaji ya Wake (za Wakubwa). Ukitaka kujua ninachomaanisha nenda uangalie wadhamini wa WAMA. Ni mke wa makamu wa rais na mgombea wa urais wa CCM Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, Zakhia Meghji waziri wa fedha wa zamani, Balozi Mwanaidi Majaar, Sophia Simba waziri wa Kikwete, Blandina Nyoni katibu wizara Regina Lowassa mke wa waziri mkuu aliyetimuliwa na wengine wakubwa tu. Hapa WAMA haijawa mradi wa ulaji wa wake za vigogo na vigogo? Je hawa hawajateuliwa kutokana na kujuana na bi mkubwa aliyempa ushauri mumewe awateue mashoga na washirika wake katika kusaka ngawira?

Hakika WAMA imeficha mambo mengi ambayo umma unapaswa kuyajua hata kuhoji.

Wapinzani na watanzania ibomoeni WAMA. Kwani inatumika kutuhujumu kwa mgongo wa ikulu na ni alama ya matumizi mabaya ya madaraka, ulafi, ufisadi na udhalilishaji wa taasisi ya urais.

Je, Salma anapiga kampeni kama nani na kwa pesa ipi?

Chanzo: Tanzania Daima Septemba 8, 2010.

Sera yangu ni ufisadi kwanza

NATOA tahadhari. Jakaya Kikwete na Dk. Wilbrod Slaa jiandaeni mgombea makini nakuja. Sina shaka. Msimu huu tutagawana kura mtake msitake. Wakati sera ya Kikwete na CCM yake ni Kilimo Kwanza, mie natoka na kitu Ufisadi Kwanza. Yeye anaendesha CCM nami nimeanzisha FACCM yaani Fight against a Cabal of Criminal Mafia.

Hii ni baada ya kugundua kuwa wakulima na wafanyakazi wanapozalisha, mazao yao yanaliwa na mafisadi. Hivyo kuliondoa tatizo hili nakuja na Ufisadi Kwanza.

Mkinichagua jueni. Nitawakamata mafisadi wote wawe na madaraka au wastaafu mie nafyeka tu na makazi yao ni lupango niaminini. Mie sina mshiko wa kuhonga kwani ni kinyume cha sheria na dhambi.

Pia sitaahidi kupandisha mishahara wakati huu wa kampeni. Kwani kufanya hivyo, hata kama tutajifanya kujirusha kimanga, ni rushwa ya wazi. Unaahidije kupandisha mishahara wakati huna mamlaka hadi uchaguliwe? Kwa wale waliomaliza muda wao, kwanini hawakufanya hivyo wakati wakiwa madarakani? Si ni hawa hawa waliowaambia wafanywakazi kuwa hawataki kula yao? Leo watu wazima wanakuja na upuuzi wa kitoto wa eeh unajua sikueleweka vizuri, unajua dokta Silaha ndiye anapinga kupandishwa mishahara wafanyakazi. Jamani, tufanye vitu kiakili na kisheria na si kitaahira kisanii na kipuuzi. Hili mkinichagua litabaki historia.

Nimeanzisha Chama cha Mafisadi si kwa maana ya kumilkiwa na mafisadi kama kile cha mafisadi bali kupamaba nao. Chama changu ni sawa na 'jeshi la wananchi' ambalo huwabonda hao hao wanapoliboa na kuendelea kuitwa la wananchi. Usiniulize maana ya hii ni nini. Sitaki matatizo mie ati.

Nasema mwaka huu uchaguzi utakuwa mtamu kutokana na kuingia kwa kidume mie kwa sababu zifuatazo.

Mosi, nimepima afya yangu na kuambiwa ni fit kichizi kiasi cha kuweza kuhimili mikiki mikiki ya kampeni na utawala bila kuanguka. Ili kujua nilivyo fit, nimepima kwenye hospitali za kawaida na kuweka wazi matokeo yangu na si kwa vigagula kama Yaya Hossein anayewadaa watu. Huyu jamaa mshenzi sana. Anaweza kukutabiria kuwa utaishi maisha mazuri wakati akimaanisha kinyume. Anaweza kukutabiria kuwa watakaokupinga watadedi kumbe akimaanisha wewe. Mie nimeamua kugombea bila kujali wala kuogopa vitisho vya shehe ubwabwa wa Migomigo aliyemuwangia jamaa hadi akadondoka dondoka kila mara.

Ifahamike. Hata mtakaponichagua kuwa rais, afya yangu haitakuwa suala binafsi la kifamilia na usalama wa taifa bali mali ya umma. Lazima mjua status ya afya na kiongozi wenu ili msiishie kuwa Nigeria na marehemu Oumaru Yar' Adua ambaye wapambe na waramba viatu wake walificha status yake hadi kumtesa akifa kwa mateso na kuwaumbua.

Hata ikitokea nikaukwaa au kuugua na kuanguka, sitaficha wala kudanganya umma. Nitawambia fika ninachoumwa hata kama ni ukimwi. Kwani mimi ni jiwe zaidi ya kuwa binadamu wa kawaida tena dhaifu? Hakuna ufisadi unaonuka kama kudanganya au kuficha afya ya kiongozi wa nchi.

Kitu kingine ambacho lazima nifanye ni kutangaza mali zangu. Nafanya hivyo ili kumpiku Kikwete ambaye amegoma kufanya hivyo. Hivyo kwa kutangaza mali zangu na afya yangu, nitakuwa nimemnyima uwezo wa kuchaguliwa na kura zake nitapewa mimi.

Mkakati mwingine ninaopanga kufanya na kunadi, ni kuuelezea umma ninavyomuenzi mzee Mchonga bin Musa bin Burito wa Mwitongo. Kama ambavyo hakuwatumia watoto au mke wake kwenye kampeni na uongozi wake, nami nitatangaza wazi kuwa mke na watoto wangu hawataruhusiwa kufanya shughuli yoyote ya kisiasa vinginevyo si kwa mgongo wangu. Kwa vile Kikwete anawatumia wanae, wapiga kura watamnyima kura na kunipa mimi.

Kitu kingine ambacho napanga kupigia debe ni kuwambia wapiga kura kuwa mke wangu mama Kidume, hataanzisha NGO baada ya mimi kuchaguliwa kuwa rais wa jamhuri. Sitamruhusu ili kuepuka migongano ya kimaslahi na kujiingiza kwenye biashara za ubuyu.

Nitawambia wapiga kura wazi kuwa wake za wakubwa wanapojiingiza kwenye NGO, licha ya kufuja madaraka ya waume zao, wanauibia umma. Hamjamuona mwizi mmoja anayezunguka huku na kule akimpigia kampeni mumewe kwa mwamvuli ya NGO iliyodhaniwa ni ya watoto wa kike kumbe hola? Kwa leo sitamtaja. Ila nikizidiwa nitamuanika ili mmjue na kumuepuka yeye na mumewe hata chama chake.

Kitu kingine, nikishachaguliwa mwaka huu, mwaka 2015 nitaunda tume huru ya uchaguzi na kukutana na vyama vya upinzani kuchagua mlezi wa vyama vya siasa. Sitafanya usanii kama wa wale wala kutumia asasi hizi kujineemesha kisiasa. Kwa vile sera zangu ni nzuri, sina cha kuchelea wala kuvunga.

Kitu kingine, nitaunda mamlaka huru ya kupambana na kuzuia rushwa siyo kuizua na kuipamba kama ilivyo. Nikiwa rais sitataka ofisi ya kupambana na kuzuia rushwa iwe chini ya ofisi yangu. Pia nitawawezesha polisi na vyombo vingine vya siri kuwachunguza tume ya kupambana na rushwa ili nao wasile rushwa kama ilivyo. Naamini hili litaondoa utata uliopo ambapo wala rushwa huwakamata wala rushwa wenzao. Lazima kuchunguzana na hakuna cha kuaminiana kienyeji.

Jambo jingine muhimu wapiga kura kujuzwa ni ukweli kuwa katibu mkuu wa chama changu si mpayukaji wala vuvuzela kihiyo. Ni msomi mkata tamaa. Nadhani wengi mnamfahamu. Nilimteua baada ya kuona katibu wa chama wa zamani mgosi Machungi wa Makambale,
kwanza kuwa kihiyo na pili vuvuzela aliyekuwa akitumiwa na akina Ewassa, Kanji na Mbwamwitu kuibia kijiwe. Hivyo naingia kwenye uchaguzi na kitu kipya tena kifaa kilichokwenda chuo siyo lile vuvuzela zilipendwa bingwa wa ufisadi mgosi.

Pia nawafahamisha wapiga kura kuwa mie sitachangiwa wala kudhaminiwa na magabacholi ili hapo baadaye niwalipe fadhila. Tegemeo langu ni wananchi wenye uchungu na kaya yao inayoendelea kunajisiwa na gendaeka wale muwajuwao ambao lazima mwaka huu niwakomeshe kwa ushindi wa kiatomiki siyo ule wa wizi wa kitsunami. Hivyo nawashauri wapiga kura wasikilize sera na kuzizingatia badala ya sura na longolongo. Maana kura yako licha ya kuwa kula ya mwingine ni taslim wal tasalum yaani ikienda hunyakwa na hairejei. Hivyo epuka kuwapa kura yako sharmutah na habithi wajao na uongo wa mchana.

Hakuna kitu kilinikera kama wezi fulani kuambiwa ukweli kuwa waliiba njuluku ya kaya halafu eti wanalalamika wametukanwa na lugha iliyotumika si ya kistaarabu. Hivi kweli hawa wanaujua ustaarabu? Kwani siri? Mlikwiba na mnaendelea kupanga kukwiba kula ili mshinde isitokee nikaukwaa nikawashindilia lupango bila huruma. Akina Ewassa na Roasttamu na Endelea Chenge, Nimmy Mkonongo na wengine mpo? Nyinyi na baba yenu ni mijizi tu hata kama kuna wajinga wanawaita waheshimiwa wakati hamna heshima. You are but thugs by all accounts. Samahani. Huwa nikipandisha mwenembago huwa naongea kimombo hata kilatini wakati mwingine Kijerumani.

Wakati mwingine huongea kwa lugha lakini siyo kama wale wezi wanaotangaza kwenye luninga kuwa wanafanya miujiza wakati miujiza yenyewe ni kuwaibia maskini na kujitajirisha.

Ngoja niwahi kwa msajili mshikaji kumwekea pingamizi Njaa Kaya kwa kutotangaza mali na afya yake.

Chanzo: Tanzania Daima Septemba 8, 2010.

Sunday 5 September 2010

Slaa anachumbia mtalaka na huyu wa Kikwete ni nini?

Rahma Al Kharoos mkurugenzi wa kampuni ya mafuta na madini ya RBP Oil anayesemekana kuwa mke wa pili wa rais wenu.
Bila shaka watanzania wengi wanajua kuwa rais wao aliyemali muda wake Jakaya Kikwete ni Toboatoboa au tuseme Chovyachovya kuanzia Makongo Sekondari, Chuo Kikuu cha Dar es salaam,Sinza Kijiweni hadi nje ya nchi.

Ingawa CCM wanaona kama wamegundua silaha ya nyuklia ya kummaliza Dk Wilibrod Slaa kwa sababu aliachana na mama aliyezaa naye, jambo ambalo hafichi, wajue mtu wao, katika hili la ndoa, hana salama.
Tutaanza kuwaletea nyumba zake ndogo na baadaye tutaleta hata vyangudoa wa mitaani ambao amewahi kuparamia.

Tukimaliza hili, tutakuja na mgogoro wa kuanguka ambao ni ushahidi tosha kuwa afya yake ni ugogoro mtupu ingawa yeye na waramba viatu wake wanaficha.

Tuanze na hawara yake Kikwete anayejiweka weka kwenye udhamini wa mambo fulani fulani huku akimuigiza Salma Kikwete kumpigia kampeni mtu wake.

Hata Salma hatanusurika. Waliofundisha naye wako na wana data zake zote hata na alivyokutana na JK kwenye mazingira ya kutia kila shaka. Hapa bado hatujaenda kwao umakondeni na kuja na data nyingine nyingi tu. Hapa bado hatujagusia vimada waliojazwa kwenye ukuu wa wilaya na sehemu nyingine nyeti serikalini. Hapa bado hatujakuletea aliozaa nao na wanaharamu wake. Hapa bado hatujavinjari kila kona inayojulikana. Na CCM wajue. Tunapata data zake sawa na tulivyopata za EPA-wanaomjua wengi wako tayari kujitolea kuanika uchafu wake.
Hapa hatujagusa biashara zake na mambo mengine machafu kuliko hata hayo.
Inzi ana hekima moja kuu. Anasema. Ukijua huu naujua ule.

Thursday 2 September 2010

UFISADI WA SALMA KIKWETE



MIMI NILITOBOA, DK SLAA SASA AMEPASUA HUENDA WATASIKIA
HII MAKALA NILIANDIKA JANUARI 3, 2010. BAHATI MBAYA HAIKUCHAPISHWA. NILIMTUMIA EVARIST CHAHALI ILI ACHAPISHE KWENYE BLOGU YAKE ILI KUZIDI KUSAMBAZA SUMU. BAHATI NZURI, ALIICHIPSHA KWENYE BLOGU YAKE. HATA HIVYO, NILIFANIKIWA KUBOMOA MANENO THE OFFICE OF THE FIRST LADY OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AMBAYO YALIONDOLEWA KWENYE WAVUTI WA WAMA BAADA YA KUWATUMIA KOPI WAMA IKIWA NI MARA YA PILI KUWASILIANA NAO NIKIANZIA SEPTEMBER 9, 2009.

NAKALA YA UJUMBE NILIOWATUMIA WAMA NI HII HAPA:
Kama mzalendo, nimejaribu kukusanya baadhi ya maoni kuhusiana jinsi ufisadi unavyoingia ikulu kiasi cha kututatiza. Kwa sasa Anna Mkapa mke wa rais wa zamani na mumwe wako msambweni. Ukiangalia kinachofanywa na WAMA hakina tofauti na Fursa sawa kwa Wote (Wake za wakubwa).
Kuondoa aibu, nimejitolea kuwasiliana nanyi ili angalau mjue tunavyojihisi kwenye wimbi hili la ufisadi wa kutumia madaraka ya waume zenu. Mama Salma NGO yako ni ulaji mtupu kusema ukweli. Acha kuna kesho. Ni uamuzi wako kuamua. Kuna kesho wakati madaraka yatakuwa mikononi mwa wengine. Hasa nikizingatia kilichompata Regina Chiluba ambacho kinapaswa kumpata hata Anna Mkapa, nimeona bora niseme hata kama nitapuuziwa. Ila najua ujumbe utafika. Someni alama za nyakati na mjue kuwa madaraka yana mwisho na yanalevya. Kuna siku mtakumbuka mchango huu.
Kila la heri,
Mpayukaji Msemahovyo

Je mama Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe?


na Nkwazi Mhango

Siku hizi mke wa rais, Salma Kikwete, anaonekana kwenye kurasa za mbele za magazeti karibu kila siku akiwa mikoani akihamasisha hili na lile. Wengi wanahoji. Kwanini sasa na si tangu mwanzo mume wake alipoingia ikulu? Na kwanini asiseme wazi kuwa anampigia kampeni mumewe? Maana, inajulikana alivyo mwana CCM damu damu tena mjumbe wa vikao vyake?

Watetezi wake wanaweza kusema anafanya kazi ya shirika lake lisilo la kiserikali la WAMA. Haiwezekani mumewe akawa mkuu wa serikali naye akawa na shirika lisilo la kiserikali kusiwe na mgongano wa kimaslahi kisheria. Uzoefu tulioupata toka kwa Anna Mkapa ungetosha kumsaidia rais Jakaya Kikwete kuondokana na aina hii ya ufisadi sugu na unyemelezi kwa kutumia mgongo wa ikulu kama angekuwa ni mtu wa kujifunza na kudhamiria kutenda haki kwa taifa.

Ngo yake ni ya mashaka-kwanini ianzishwe baada ya mumewe kuwa rais? Kuanzisha NGO baada ya mume kuwa rais ni ishara tosha ya ufisadi na usasi wa ngawira. Mbona hatuoni wake wa viongozi wa vyama vingine wakiwa na NGOs? Hata wakiwa nazo nani atazichangia iwapo wanaochangia NGOs za wake wa marais wanatafuta kuwa karibu na ikulu ili waihujumu nchi kwa kupata upendeleo kama ilivyokuwa kwa EOTF ambayo ilitumiwa na watu wengi kuliibia taifa? Mke wa Kaisari hapaswi kutenda tendo lenye kuweza kutia shaka au doa utawala wa mumewe.

Tuliishi na kumuona baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Mkewe-mama Maria-hakuwahi kujihusisha na upuuzi mdogo mdogo wa kutafuta pesa kwa mgongo wa mumewe.

Niliwahi kuwaandikia barua EOTF na WAMA kuwaonya juu ya hatari ya kuitumia ikulu. Hawakuwahi kunijibu zaidi ya kufumba macho na kuendelea kutengeneza pesa kwa mgogo wa ikulu. Ila nafurahi. WAMA wamefanya jambo moja (la maana la kuondoa aibu)-kuondoa maneno yasemayo WAMA Foundation the office of the First Lady of the United Republic of Tanzania kwenye wavuti wao. Niliandika baruapepe ifuatayo kwa WAMA tarehe 3 Septemba 2009:

Kama mzalendo, nimejaribu kukusanya baadhi ya maoni kuhusiana jinsi ufisadi unavyoingia ikulu kiasi cha kututatiza. Kwa sasa Anna Mkapa mke wa rais wa zamani na mumwe wako msambweni. Ukiangalia kinachofanywa na WAMA hakina tofauti na Fursa sawa kwa Wote (Wake za wakubwa).
Kuondoa aibu, nimejitolea kuwasiliana nanyi ili angalau mjue tunavyojihisi kwenye wimbi hili la ufisadi wa kutumia madaraka ya waume zenu. Mama Salma NGO yako ni ulaji mtupu kusema ukweli. Acha kuna kesho. Ni uamuzi wako kuamua. Kuna kesho wakati madaraka yatakuwa mikononi mwa wengine. Hasa nikizingatia kilichompata Regina Chiluba ambacho kinapaswa kumpata hata Anna Mkapa, nimeona bora niseme hata kama nitapuuziwa. Ila najua ujumbe utafika. Someni alama za nyakati na mjue kuwa madaraka yana mwisho na yanalevya. Kuna siku mtakumbuka mchango huu.
Kila la heri.

Bahati mbaya sana , hata wavuti wa Kurungenzi ya habari Ikulu unaonekana kutangaza biashara ya WAMA badala ya wizara za serikali! Ajabu hakuna anayestuka wala kupiga kelele!

Kama umma ukishupaa NGO hii inaweza kufutwa hata na mahakama kutokana na mgongano wa maslahi ukiachia mbali kuwa kichaka cha ufisadi kutokana na uwezekano wa kuchangiwa pesa chafu kutokana na kutokuwapo sheria makini ya kuchuja na kutangaza wafadhili wa WAMA.

Hata hivyo nimefarijika kuwa sauti yangu imesikika na fedheha imeondoka. Maana neno Jamhuri ya Muungano, kisheria, halipaswi kutumiwa na mtu au taasisi yoyote isipokuwa mihimili mitatu ya dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala. Cheo cha Ofisi ya First lady hakimo katika katiba yetu.

Kwanini mapenzi kwa wanawake na watoto yaanze baada ya kuupata urais kama siyo gea ya kuitumia vibaya ikulu? Ina maana rais na washauri wake hawalioni hili au wameridhia kwa sababu NGO ya mke wa rais inaweza kutumika kama kivuli cha kuanza kampeni hata kabla ya tume kutanganza hivyo? Inabidi tustuke. Ajabu hata wapinzani hawajaliona hili!

Tanzania inaweza kuwa nchi pekee ambapo rais na mkewe wote ni marais. Kikwete ni rais wa jamhuri huku mkewe akiwa rais wa WAMA. Ukitaka kujua hili jikumbushe mapokezi anayopewa na coverage anayopata Salma kwenye vyombo vya habari. Ajabu ukitafuta uhalali wake kikatiba haupo!

Hata kama anajulikana kwa ubabe na upayukaji wake, bado mke wa rais wa Kenya Lucy Kibaki hana mamlaka kama aliyo nayo Salma ambaye anaweza kuingia mkoa wowote kwa kisingizio cha NGO yake na kufanya shughuli za kisiasa kama kulakiwa na viongozi wa mikoa na kukagua miradi ya maendeleo ukiachia mbali kutoa kauli mbiu zinazoonyesha wazi kumpigia debe mumewe.

Salma anchomzidi Lucy ni ile hali ya kufanya kitu waitacho waingereza one woman show. Kwani kila lilipo jina WAMA yupo yeye. Hii maana yake ni kwamba yeye ni dikteta na mpenda madaraka anayetaka kufanya kila kitu peke yake. Kwanini hatuoni makamu wake au hata wasaidizi wengine wakifanya shughuli za WAMA kama kweli ni ya umma kama anavyodai? Kuthitibitisha hili, tembelea tovuti ya WAMA uone ukweli huu. Hii haiwezi ikawa taasisi ya wanawake na watoto wa Tanzania .

Kuonyesha kuna namna ya kampeni na kutumia mamlaka ya mume wake, hivi karibuni, Mama Kikwete amewahi kutoa namba yake ya simu ya mkononi ambayo ni 0754-294450 kwa wanawake mkoani Singida ili waweze kumpigia au kumtumia ujumbe mfupi wa maneno pindi waume zao watakapowanyanyasa kutokana na kitendo cha wao kwenda kupima kwaajili ya kujua afya zao. Japo kwa juu hili linaweza kuonekana ni jambo bora, kwa mtu anayejua mipaka ya mamlaka yake na utaratibu wa utawala kisheria, angeshauri wahusika waelekeze madai yao kunakohusika-polisi, vituo vya kutetea haki za binadamu hata wizarani.

Licha ya kuwa ubabe, hii ni kampeni ya wazi kuonyesha wahusika wanawajali wananchi jambo ambalo si kweli. Kwanini hasira zake zisielekezwe kwenye kumshauri mumewe kupambana na ufisadi kama ana uchungu na nchi hii? Yaani hajui kuwa ujinga na umaskini ndivyo vyanzo vya haya yote? Sijui hata kwenye kupokea misaada anauliza usafi wa mtoaji.

Kwa nijuavyo upenzi wa sifa wa watawala wetu na watu wao, kama utafanyika uchunguzi huru juu ya matumizi ya MAWA, ushingae pesa inayotumiwa kwenye ziara ikawa kubwa kuliko hiyo inayowafikia walengwa. Bahati mbaya sijwahi kusoma popote taarifa ya mahesabu ya mwaka ya si WAMA wala EOTF.

Wengi wanaweza kuona kama tunamuandama mke wa rais au kutotambua umuhimu wa kupigania haki za akina mama. Kwanini mke wa rais wakati tuna wizara yenye watendaji wanaolipwa pesa ya kodi yetu? Kwanini misaada hiyo anayopokea isipelekwe wizarani au kwenye mashirika huru kama kweli ana uchungu na walengwa na si kujipatia umaarufu, pesa na kubwa zaidi kutumia ikulu kwa manufaa binafsi yawe yake au mumewe na marafiki zake?

Je Salma Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe hata kabla ya kipenga kupulizwa? Je akina mama wa Tanzania wataingia mkenge wake huku waume na kaka zao wakizidi kuteswa na sera za Kikwete za kuvumilia mafisadi? Je atawalainisha wasahau kuwa Kikwete hajatimiza ahadi hata moja? Je watahoji uhalali wa NGO yake na kumwambia ukweli kuwa ni ya mashaka na ulaji?

“The day Kenya was born”



No doubt. The overwhelmingly passing of the new constitution in Kenya can be termed as the rebirth of a new true Kenya that had nary existed. This, if anything, I believe, will bury the demons of tribalism, self seeking, land grabbing, dictatorship, corruption, irresponsibility and unaccountability that marred the history of Kenya.

Now that the new constitution has been promulgated, it remains to be seen when it comes to putting it to exercise. Kenya I used to know before the new one was but a loose amalgamation of tribes and other groups of interests, but not a nation though Kenyans used to believe they were a nation whilst they actually were not.

In totality, there has nary been a nation of Kenya but a country of Kenya. This needs the whole article to discuss. I, thus, will hang it hither and soldier on with the birth of the new constitution that surely will make a Kenyan nation for the first time in history.

The new constitution is not only an impetus for development and prosperity of Kenya but also the precedent for other nations in the region even in the continent. By attaining this very milestone, Kenyans, for yet another time, have led the world to a new world order based on mature and true democracy. I comfortably believe that other east African countries that are under the yoke of one-man- or one-party abracadabra such as Burundi, Rwanda, Tanzania and Uganda, will borrow a leaf from Kenyans. It is time for kicking old constitutions out. They’re and they have nary been ours at all. Most of them were made in Lancaster house as proxy means of elongating British colonial rule. These constitutions created vampires that have exploited our countries to the bone. We need home-made-and- grown and progressive constitutions such as those of Kenya and South Africa.

I once noted that whilst some Kenyans, especially the “NO” camp and the clergy, were hoodwinking the majority that the new constitution was hogwash allowing abortion. In other countries in the region, their constitutions are nothing but a writ of a cabal of mediocre swindlers that can tamper with them when they deem fit. Now that the new dawn’s unfold and verily it is hither with us, let us forget our differences and build a new nation steered by our views and wishes. That a new baby is born, let us stand together to see to it that the light is shinning in its life as well as ours. Let us reconcile the country and forge ahead.

Against all odds, that Kenyans have raised to the occasion, we need to congratulate them on this leap forward as we borrow a leaf from them. I understand. Kenya has been the country in big crises thanks to be manned by thieves, killers and tyrants that were empowered by archaic constitution. Refer to the grisly killings that occurred soon after disputed 2007 elections and being under one tyrant for over two decades. I, so too, understand that Kenyans lost a lot of their rights, such as true freedom to economic well-being, land, peace, security, democracy and what not. Many Kenyans were killed and tortured under the former constitutions and their rights were pushed under the carpet. Refer to the assassination of Tom Mboya, Josiah Mwangi Kariuki, Robert Ouko and many more others. Refer to the infamous Nyayo house sacrilege that left many Kenyans dead or tortured.

By ushering the new constitution in, I am sure, the buried cases of grave violation of human rights will be unearthed and being dealt with accordingly, so as to give a reprieve and redress to the families of those that were butchered or in anyway affected by blood dripping former regimes. I am sure too. The land that was grabbed since Jomo Kenyatta, Daniel Moi and their cronies will be retaken and be redistributed the landless Kenyans. What’s more, vampiric corruption scandals such as Goldenberg, Anglo-Leasing and others will be dealt with transparently and accordingly. More so, those who authored post-elections killings will now be urgently dispatched to The Hague, so that another precedent can be set where Kenya leads others.

Though there won’t be a quick fix of the rust Kenya has gone through for decades, it is upon Kenyans to patiently and united start to put the whole goodies in the new constitution in practice. Moreover, the Kenyan referendum was regarded as something normal, it was not. It is only South Africa that once attempted and successfully did this. Other African countries are still in slumber. Tanzanians, just on the next door, need a new constitution so badly that they can recapture their mojo. Ugandans, just like Rwandans, are in dire need of the same. The constitutions of the mentioned countries are just mere documents that thievish rulers can manipulate as they deem fit, at any time they deem fit, for their personal gains.

Kenyans have created a constitution that frees them from all evils of the past as it guides them to the future. Shall this being emulated by other countries in the region, even the union of the region will be easier and possible to attain even tomorrow.

I must call upon the citizenry of the countries in the region to start agitating for new constitutions. They should fear nothing when it comes to repression. No ruler can now resort in archaic means of beating protesters thanks to the fear of being delivered to The Hague. This being the year of elections in Rwanda and Tanzania, the people there should get prepared to refuse to accept cooked results resulting from the charade known as elections. We have already seen how the just ended Rwandan elections were marred by killings and detention of opposition leaders and journalists. This proves beyond doubts that the said elections was not be free and fair by all standards. The era of one-party-cum-one-man show is over.

In Tanzania, Chama Cha Mapinduzi (CCM) just like the National Resistance Movement (NRM) In Uganda, has always manipulated elections thanks to appointing a kitchen Electoral Commission. These three countries mentioned above need to have Independent Interim Electoral Commissions (IIECs) in place to facilitate the transition. On this, Kenya can offer expertise thanks to her experience.

To cut the story short, it should be noted and appreciated that what Kenyans voted for is actually not only their constitution but also ours in the region. For the precedent they set is second to none. Importantly, we must face this challenge and vote ourselves out of tyranny be it of one party of one man. Bravo Kenyans once again for showing and leading the way.

The worst thing that tarnished the promulgation of the new constitution is the presence of Sudanese killer- Omar Bashir. This indeed, either by mistakes or calculations, showed Kenyan rulers as improbable. Now this being the case, will they deliver the suspects of post-election killings to The Hague as they are required by the law? This is another tough home work for ICC and UN.

Source: Afro Spear Think Tank.