The Chant of Savant

Tuesday 25 August 2009

Is Justice closing in for Muluzi?

The President of Malawi, Bingu wa Mutharika, did something beyond and above the call of duty. Many people thought that he would not deal with his predecessor, Bakili Muluzi over graft scandals such as allegedly diverting over $ 10, 000,000 from donor monies to his personal accounts. Many wrongly thought that Mutharika would cower before Muluzi as happened in neighbouring Kenya and Tanzania where current potentates allied with their predecessors to cause harm to their economies in lieu of bringing them to book.

As per Anti Corruption Bureau (ACB) Public Relations Officer, Egrita Ndala, some 44 vehicles out of 149 Muluzi is believed to own, Keza Office Park and all bank accounts were seized. Among the accounts ACB seized, is account number 0141035074200 at Zomba National Bank where some 23 organisations and individuals deposited various amounts during Muluzi’s tenure of office.

Muluzi’s lawyers are tirelessly fighting to stop this purge against their customer to no avail. In his attempt to get away with it, in April this year, he chose his wife as his party presidential candidate after his attempt to stand again was foiled by the court. Recently ACB attempted to seize more of Muluzi’s properties. But it hit a snag, for, it came to light that some properties had already changed hands or being registered under other people's names. This took the ACB officials by surprise. The fleet of posh vehicles at Muluzi’s BCA residence that include, Range Rover, Land Rover Discovery, Lexus Cruiser, Bentley, several Mercedes Benz cars and Nissan Patrol among others for example, are registered in former first lady Dr. Patricia Shanil Muluzi’s name. Surprisingly, Muluzi’s wife seems to own many more vehicles than her husband-but again, will Mr. and Mrs. Muluzi substantiate how she acquired this massive wealth ?

Once again, one can see how Africa’s carbuncular and thieving rulers use their wives, relation and foreign criminals to hide their wealth. Muluzi used Mohamed Munif Al-Nadhi just like Daniel Moi used Kamlesh Pattni; Mkapa used Sailesh Vithlani; Jacob Zuma used Schabir Shaik; Yoweri Museveni used Mahendra Mehta or Jakaya Kikwete used Rostam Aziz to rob public coffers.

Will ACB also seize Lonrho buildings standing on plots LE 212, LE 459, LE 371 and LE 211A, in Limbe formerly owned by Muluzi as they did with Keza office park? In a twist of events, Muhomed Munif Al-Nadhi claims to be the owner of Keza Office Park that is said to have been sold off by Muluzi but without disclosing when the same was sold.

ACB must seize more of Muluzi’s hidden properties. A little bird confided in me that there are some properties hidden in Tanzania. One MP and Muluzi’s confidant, John Komba mans two of Muluzi’s secondary schools of which one is named after Muluzi himself. Some Tanzanian newspapers once asked the rationale for Muluzi to build schools in affluent Tanzania whilst he ignores to do so in Malawi that needs those schools the most. Given that the Tanzanian media is not independent, the story died after a reprimand.

To easily hoodwink Malawians and donors, Muluzi established Malawi Social Action Fund (MASAF) that was later aped by Mkapa so as to become Tanzania Social Action Fund (TASAF). This outfit was closely manned by Muluzi’s consigliore and confidants something that enabled him to easily swindle public money as it happened with Mkapa in Tanzania where he’s currently facing calls for prosecution alongside his wife for robbing public funds and properties chief one being Kiwira Coal Mine in south Tanzania. Much of MASAF money ended up benefiting the president’s strong hold. The case is the same in Tanzania where TASAF invested heavily in the southern region where Mkapa hails from and North where the former PM, Fredrick Sumaye hails from.

Muluzi and Mkapa ought to accept a legal process as happened in Zambia where former ruler Fredrick Chiluba stood the test of time by being duly exonerated in lieu of stonewalling himself behind far-fetched immunity. This, apart from proving democratic maturity, sets records straight despite the shock as to how Chiluba’s conspirators would be jailed as he was set free. Chiluba ceases to be a reference point as far as corruption in power is concerned. However, many questions still beg answer regarding the amount he actually stole on top of his wife’s conviction that still taints his reputation.

As for corrupt African former thieves-in-chief, it is time for them to face the consequences. Today, you may indifferently sit on your predecessors’ cases. But tomorrow, somebody will make sure that no stone will be left unturned.
Source: The African Magazine August 26, 2009.

CCM yetu na vioja vya ufisadi


NIMEFARIJIKA kusoma habari kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeunda mkakati wa kuwanyamazisha makada wake wapinga maovu! Hongera CCM. Kwani wanaopinga ufisadi wanapinga sera ya chama na wanatishia amani ya matumbo yetu wakubwa. Hawana mapenzi mema na taifa letu.

Vikao vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC), vilivyomalizika hivi karibuni, kwa kujipiga kifua na “kusoma alama za nyakati”, vimetoa karipio na onyo kwa wanaochukia ufisadi. Hapa wananchi, ambao ndiyo wanufaika wa maendeleo haya, wanapaswa waandamane kuunga mkono msimamo huu.

Wapo walioota ndoto za mchana wakatumia Bunge wasijue nalo ni mali yetu.

Hebu kwanza soma nukuu hii toka kwa mtu ambaye namheshimu sana na kumuona kama mzalendo, John Chiligati, “Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele. Wanaoropoka hovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge.”

Lazima vizabizabina wapashwe. CCM ina wenyewe na wenyewe ni wale mnaowaita mafisadi. Mafisadi ni nani kati ya nyinyi msiokubali kuunga mkono sera za mafanikio za Rais Jakaya Kikwete ambaye ameishatekeleza ahadi zake zote? Japo ni lugha ya kitapeli, siku hizi hata dua kufika lazima uwe tajiri kama alivyosema jambazi mmoja ajifichaye kwenye majoho.

Soma nukuu hii kuhusu CCM kumuenzi rais mstaafu Benjamin Mkapa kama shukrani kwa kuridhia mradi wa kupigiwa mfano ulioingiza serikali ya sasa madarakani chini ya uzalendo wa EPA.

Chiligati, tena bila wasiwasi anawapa, “Mkapa anastahili pongezi si kejeli! Anastahili heshima si dharau! Na anastahili kuenziwa si matusi!”

Hebu nimuulize, kwa nini tusimpongeze Mkapa kwa kujitwalia machimbo yenu ya makaa ya mawe ya Kiwira na kuidhinisha pesa yetu itunufaishe Benki Kuu? Kweli tunastahiki kumheshimu Mkapa. Alitufundisha kuufaidi urais na familia zetu na nyumba zetu ndogo.

Wanaosema alifanya biashara haramu Ikulu; wajinga hawa. Hawakujua: rais huwa hakosei na nchi yote ni mali yake? Tumuenzi Mkapa kwa kuwasahau akina Nyerere waliotuwekea mtima nyongo hadi tukachelewa kuula. Acheni roho mbaya, bila ufisadi nchi haiwezi kwenda popote. Muelewe. Tunaposema nchi tunamaanisha sisi. Nchi ni sisi na sisi ni nchi.

Lazima kaka Chiligati atetee hata kama mtasema ni upuuzi. Soma hii upasuke, “Hayo yote ni mambo mazuri, lakini bado Watanzania wanaona kuwa alichokifanya Mkapa kilikuwa ni kazi bure, jamani sisi ni watu gani tusiokuwa na shukrani, yaani kila jambo kwetu ni baya, tukumbuke kuwa nchi hii ilikuwa katika hali ya kuwa mufilisi; ilikuwa haikopesheki, lakini sasa tunakopesheka.”

Je, kauli hii haimuenzi mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye alitoa taarifa ya utendaji wa serikali yake wakati akiondoka madarakani? Mzee Mwinyi kafurahia sifa hizi kiasi cha kushiriki kwenye kigwena chetu.

Nakumbuka. Alieleza alivyokuta nchi bila vitu madukani wala akiba na akaacha ziada. Hakuna aliyewahi kukanusha. Kuthibitisha hili Mkapa aliondoka hata bila kuaga achia mbali kutoa taarifa kama alivyofanya mtangulizi wake. Kwa maana kila kitu kilikuwa bomba. Mkapa alikuta “muflisi” akaacha ujasiriamali.

Aliuminya mzunguko wa shilingi huku uchumi ukinawiri baada ya kukabidhiwa mikononi mwa wawekezaji “waaminifu” kiasi cha Jakaya Kikwete kutoa ahadi ya kurekebisha mikataba aliyoingia Mkapa ili iwe bora zaidi. Hamkuona alivyotekeleza hili haraka na kwa ufanisi? Asiyeona hili basi hana macho.

Tuache matusi. Kila Mtanzania anapaswa kumuenzi Mkapa kuanzia mkewe na watoto wake waliochuma utajiri haraka haraka kwa njia halali, Kikwete aliyeweza kuingia madarakani kwa madai ya kutumia pesa ya EPA, Chiligati na wengine wengi walionufaika na neema za Mkapa. Watanzania hawana sababu hata moja ya kutomuenzi mtu aliyewafundisha jinsi ya kutumia mali zao huku wakiendelea kuwa matajiri kama alivyowazidishia utajiri Kikwete.

Wengine wanaopaswa kumuenzi Mkapa ni wawekezaji wa kupigiwa mfano kama Net Solution Group, IPTL, Kagoda, wezi madini yetu, Fosnik, DevConsult, Tanpower na waheshimiwa wengine.

Tukirejea CCM kutaka kuwanyamazisha wanaopinga ufisadi, huu ni mwito na onyo kwao kuwa hawana chao ndani ya CCM. Hivyo, watafute mahali pengeni wanakofaa ambako wanajiona kuchukia na kupambana na ufisadi, wakati si mbaya.

Karipio hili la jumla linawalenga Samuel Sitta, John Malecela na mkewe Anna, Dk. Harrison Mwakyembe, Lucas Selelii, Aloyce Kimaro, Christopher ole Sendeka, William Shelukindo na wengine walioonyesha wazi kuchukia ufisadi. Je, watafyata mkia au kuchukua hatua kuiadhibu CCM kabla haijawapatiliza? Watajijeijei.

Kwa wanaojua historia ya CCM, tukubaliane; hata mwanzilishi wake Mwl. Nyerere alitabiri kuwa atakayeisumbua, sorry, atakeyeijenga CCM atatoka CCM. Je, wakati wa utabiri huu kutimia umetimia ambapo vigogo wanaojulikana kwa kuchukia ufisadi watajitoa au kuendesha upinzani mkali ili kuipa changamoto ya kuimarika zaidi?

Je, haya ni madhara ya lile ombwe la mawazo na visheni lililosemwa au kutamalaki kwa mafisadi kwenye nyadhifa za juu chamani? Sisi hatuchukii wala kuogopa upinzani ili mradi usitake kutia kitumbua chetu mchanga. Hivi unategemea nini unapokuwa na vihiyo, sorry wasomi kama Tambwe Hiza, kama wasemaji wa chama?

Hakika CCM ni chama cha matajiri tena mnaowasingizia kuwa mafisadi kama alivyowahi kuonya Mwalimu. Wanakisaidia chama kupeta. Hivyo, si wabaya mnavyodhani. Wanachama wetu wote ni mafisadi na matajiri kwa mujibu wa wakosoaji. Unadhani umma ungetuzimia ingekuwa vinginevyo? Hauwezi kukubali kuendelea kutumika kama nepi kusafisha uchafu wa walafi wachache wenye madaraka nje ya chama wanaowataka ama kuachana na CCM. Kwani CCM ni mama au baba yao? Tokeni msitusumbue. Tuache tule vyetu kwa amani. Msitujazie mbu.

CCM ina haki ya kidemokrasia kufanya uamuzi wowote, hili la kuhalalisha nyenzo hii ufisadi na kuwanyamazisha wanaouchukia linatufariji na lipaswa nalo kuenziwa ukiachia mbali wapiga kura kuchukua hatua ya kuipa zawadi CCM kama ilivyotokea nchi jirani kwa chama cha KANU.

Je, Watanzania wataendelea kujirahisi na kukubali kutumiwa na kuteswa na manyang’au wachache hadi lini? Waguswe wapi na vipi ili washtuke? Kuonyesha CCM inavyowaheshimu, inadiriki kutoa mipasho ilhali tangu ichaguliwe haijawahi kushindwa kutimiza ahadi hata moja ukiachia mbali kutenda mema kuliko hata ya rais aliyetangulia. Je, hawa wasioona mema haya si kuwageuza wananchi majuha na mataahira wa kutupwa?

Badala ya wachukia ufisadi, kuiandama CCM, wanapaswa waienzi kwa kutimiza ahadi yake kuona kuwa ufisadi hauwi tatizo nchini mwetu. Wanafahamu. Maanguko yao hayatatokana na kupinga ufisadi bali upofu wao wa kutoona neema na matendo mema ya serikali inayoendeshwa na watu wema wanaoitwa mafisadi wakati mafisadi ni wale wanaoupinga ufisadi.

Dawa si kuandamana na kupatilizana, bali kuachana na jinai na ubabaishaji wa kuandama ufisadi wakati ni mfumo mzuri kwetu. Mmesahau wosia wa Mkapa kuhusu uwekezaji?

Je, ukweli ni upi? CCM imeishiwa na inapaswa kupumzishwa haraka iwezekanavyo? Maana ni hatari na aibu kwa nchi. Sorry, namaanisha ni imara na inapaswa kuongoza vipofu milele. Hakika, CCM sasa ni chama cha Mafisadi rasmi.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 26, 2009.

Ukapa + Ukwete = Ufisi na Ufisidunia


HAYAWI hayawi; yamekuwa! Tulisema na kulonga bila kukoma kuwa kuna siku nyoka atajivua ngozi. Hata ajivue ngozi mara elfu bado nyoka ni nyoka na dawa yake ni kumpondaponda bichwa lake na kumteketeza.

Siku nyingi walevi walikuwa wakiniuliza sera ya lisirikali letu ni ipi. Niliwahi kujibu; ubangaizaji, usanii, ujambazi mbuzi, ufisi na ufisadi. Wazushi waliita mzushi huku wasanii wakiniita msaliti wasijue wao ndiyo.

Hakika Mungu si Mpayukaji. Wale wale waliokuwa wakikana hata kwa kutishia kulamba pua zao hata kutishia kuonyesha makaburi ya Adam na Eva, sasa Wamejiumbua kwa kubariki na kutia ubani maneno yangu kuwa sera yetu kijiweni hakika ni ujambazi, ufisi na ufisadi.

Hakuna dhambi isiyostahili msamaha kama kuulaani ujambazi na ufisi huu. Ukitaka kujua nimaanishacho, muulize kipaza sauti Sam Six au Joni Machela. Juzi nasikia walilazimika kulamba viatu vya kaisari kwa kosa la kusema yu uchi. Nasikia walidhalilishwa kiasi cha kutamani ardhi ipasuke. Lakini adui yako muombee njaa.

Matumbo yaliwazuia kutema ulaji wa masimango na masharti utadhani kiama ndiyo mtoa riziki pekee. Huku nako ni kujidhalilisha na ubabaishaji hata usanii ukiachia mbali kuwa uchumia tumbo.

Nasikia majambazi kama Luwasha, Makorongo, Roast Tamu na wengine waliangusha bonge ya pate huku Joni Chilyagt akizidi kujivua nguo na kuonyesha alivyo mtupu kama Tambo Hizo (Mrundi ajiitaye Mgosi), kihiyo na changudoa wa kisiasa aliyeridhia kutumiwa.

Tambo Hizo, Chilyagt, Kimdunge Mwehu na Makorongo wamepayuka. Bado namsubiri shangingi wa kihaya. Naye lazima ataropoka kumfurahisha Bwana.

Kuna ngedere mmoja toka Idodomya aitwaye Kuzila. Huyu ndiye hana maana kabisa. Eti anasema kina Sam Six na Machela wafunguliwe mashtaka ya uhaini. Hivi ngedere huyu anaujua uhaini au anaota?

Zamani nabii Mpayukaji nilihubiri na kutabiri kuwa muandae maziko ya Genge la Gwagu na Majambazi (GGM). Nilionekana naota mchana. Juzi shehe Njaa Ubwabwa, Haya naye alitia guu kwenye unabii wangu ingawa alitumwa na njaa baada ya kuona ngedere wenzake wamemzunguka.

Turejee kwenye gwena la juzi. Ingawa GGM sasa inaanza kuonja joto ya jiwe kiasi cha kuanza kulamba matapishi yake-kukanusha, ukweli ni kwamba ni genge la mafisadi. Hebu jiulize; kwa nini wanamchukia Sam Six wa kijiwe cha Idodomya? Ni simpo. Aliruhusu Eddie Ewassa kusulubiwa kwa niaba ya Njaa Kaya.

Hawa wawili kama alivyotahadharisha nabii Mchonga ni hatari kwa usalama wa kaya. Wana tamaa kama fisi kiasi cha kulala kitanda kimoja na mafisadi wakila kwa miguu na mikono bila kunawa. Ushahidi? Tazama wanavyokufuru kusema eti tumuenzi Denjaman Makapu bin Tunituni kwa kutuibia!

Kama kuna wa kumuenzi si mwingine bali Anna Tamaa, Njaa Kaya, Joe Makombo, Dani son of Jonah, wachukuaji waitwao wawekezaji kina Richmonduli na ndegere wenzake walioiba mahindi ya watoto huku wakiwaacha wafe njaa.

Kama tutamuenzi Tunituni na Mchonga tutamfanya nini? Acheni matusi ya rejereja. Jamaa mmoja alinitonya kuwa Sam Six anachukiwa kutokana na kuanza kuandaa mazishi ya Njaa Kaya na Salama Kikwekwe wa MAWA watakapokuwa wamekitoa.

Maana kama Regina Chiluwa anapaswa kunyea debe Keko au Ukonga huku Anna Tamaa akihukumiwa kunyongwa maana ndiye aliwaletea kina Salama pepo la kupenda pesa utadhani wanatokea karibu na mlima Nonihino. Pesa babangu. Pesa lasima ujenge nyumba ati. Kimaro umekataa kuiba utakula mafi yako. Niliwahi kumsikia jamaa mmoja akitania jamaa hawa.

Kimsingi, kilichofanyika ni GGM kuwaonyesha Wabongo inavyowachukulia kama mataahira ambao hata ikiamrisha wale viungo vyao wanaweza kama wawafanyiavyo mazeruzeru huku wakidai amani na ustawi. Huu ni uchokozi usio na kifani kama walevi wetu watatia akilini.

Njaa Kaya na genge lake wamedhihirisha walivyo wa kuogopwa kuliko hata ukoma au ukimwi. Kimsingi, vikao vilivyokwisha vimezika matumaini na Tanzia. Kilichobaki ni tulie na kusaga meno ndugu zanguni.

Kwa ufupi kilichofanywa na vikao vya GGM licha ya kumvua nguo Mchonga, ni msiba kwa kaya. Tunyoe nywele, kujipaka majivu na kuvaa magunia. Tuomboleze kifo cha mkabala wetu na kaya yetu.

Ajabu genge hili bado linawadanganya walevi kuwa linaheshimu uhuru wao. Thubutu. Utamheshimuje mtu wakati unamfunga mdomo hata asikwambie ukweli baada ya kugwaya kukuzaba vibao? Hawa ni wa kuchomwa moto kama vibaka, kama walevi wasingekuwa woga. Lakini yana mwisho na mwisho wenyewe unakaribia. Maana wahenga walisema: ujanja ujanja mwishowe huzua janga.

Kwa wenye akili baada ya kuondoka, Mchonga tulijua msiba mkubwa unaandaliwa. Hakuna siku tulianza kuvaa magunia kama siku alipopitishwa Njaa Kaya eti kugombea ukuu. Tulijua. Ewassa atamtumia kabla ya wengine kumtumia. Maana jamaa ni mtupu hakuna mfano.

Laiti angekuwa kinara wa miziki na mipira si haba. Ajabu na msiba mkubwa, baada ya wendawazimu kama Kimdunge Ngumbaru Mwehu kuwa wazee wa gwena tulijua mambo kwisha. Ukitaka kujua nimaanishacho, jiulize Kimdunge na nkewe wamefanya nini pale mabung’o.

Babu linafanya mambo ya kitoto kuogopa lisiumbuliwe kwa ufisadi wake. Mwl. Mchonga alisema: ogopeni wehu wanaotumiwa na wake zao na wakatumia ushauri wa kitandani kufanya mambo ya umma. Yuko wapi Tunituni? Ameponzwa na Delila sawa na Njaa Kaya atakavyoumbuliwa naye siku si nyingi.

Hivi ulitegemea nini kama wachenza mdumange kama Joe Makambo kuwa kinara wa gwena? Hivi unategemea nini kutoka kwa vihiyo kama Mkukuchikaji? Unategemea nini kutoka kwa walu walu kama Joe Masahauni au kibaka kama Makorongo?

Kama kuna jinsi ya kulinganisha gwena la juzi, basi kwa kukopa maneno ya rafiki yangu wa kichina aitwaye Xian Cham, kilikuwa ni cha manyani na ngedere.

Kwa ufupi huu ndiyo ukapa kujumlisha ukwete uliozaa ufisi uliojukuu ufisadi.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 26,2009.

Thursday 20 August 2009

Darfur: Are Muslims a Betrayal?


“Brother, to me, there are no Muslims in this world presently except Darfuris. Since the Arab-backed illegitimate regime under Omar Bashir started butchering my people, all we mistook to be Muslims- especially Arabs-, became infidels (kaffirs) for not acting.” These are sarcastic words by Salih Fur whom I met on plane on my way to Winnipeg from St. John’s early this year.

He goes on: “I came to Canada from Egypt where I was called ‘slaves’ and other bad names, simply because I am black.”

Salih was on his way to Toronto and we coincidentally shared a seat. He sadly told me: “Can you believe? Sudan still has black people who regard themselves to be Arabs and discriminate against fellow Africans!”

His cry is clear. Muslims, the world over, have betrayed their colleagues in Darfur. This betrayal, according to Salih, has rendered them kaffirs.

I wanted to know further why this was his take. He has good Quran-based reasons. He told me that his people goofed thanks to being referred to as ‘Ahal Quran’ or ‘the people of book’ by Bashir. Little did they know it was a ploy he used to fool them as they refrained from pursuing modern education! They heavily regret his lie.

Salih seems to be good at this holy book of Muslims thanks to verses he gave me. When I arrived home, I touched base with another friend from Darfur, a Mr. Etahir. This guy -I met also in Canada-, hates everything Islamic and Arabic. He was born and raised a true Muslim till 2005, when he survived beatings in Cairo simply because he was black, and thus, slave, as per Arab take of black people. Therefore, was not supposed to attend prayers. Infuriated and badly injured at heart, he kissed Islam good-bye.

[49:11] O you who believe, no people shall ridicule other people, for they may be better than they. Nor shall any women ridicule other women, for they may be better than they. Nor shall you mock one another, or make fun of your names. Evil indeed is the reversion to wickedness after attaining faith. Anyone who does not repent after this, these are the transgressors.

James, a Darfur Christian convert, too was born and raised Muslim. But when Arab-sponsored Janjaweed started killing his people as they uttered "Allah Akbar!" (God is great), he reverted to Christianity. There are many such incidents reminiscent to Darfur people.

Going back to Salih, he gave me some verses from the Quran to justify why he has lost faith in all believes all Muslims except his Darfur people. Before delving the whole fiasco and betrayal as per Salih, I must admit. This is not my take though.

Now let us face it. As per Islamic tenets, all Muslims are brothers and are connected like cogs on the wheel. If this is so, (and indeed it is) it is ordered that when one Muslim is offended, all Muslims should come to his aid.

[49:9] If two groups of believers fought with each other, you shall reconcile them. If one group aggresses against the other, you shall fight the aggressing group until they submit to GOD's command. Once they submit, you shall reconcile the two groups equitably. You shall maintain justice; GOD loves those who are just.

Why didn’t this happen to Darfur? One thing makes one an infidel; going contrary to Islamic teachings and Quranic-and-Allah’s commandments. [49:1] O you who believe, do not place your opinion above that of GOD and His messenger. You shall reverence GOD. GOD is Hearer, Omniscient.

Why did the Arab League become the first Islamic outfit to vehemently support Bashir -the African that calls himself an Arab- after he is water-tightly implicated by the ICC? Where is the Organization for Islamic countries? Why are Arab countries openly supporting genocide of Muslims by inviting Bashir to their countries and being his lifeline financially?

Where were African Muslims that are renowned for taking to the streets when Arab Muslims are touched? Refer to many demonstrations when US attacked Iraq and Afghanistan not to mention the support for Hezbollah when Israel pounded on its stronghold in Lebanon. We don’t see them doing the same for Somalia or Darfur! Isn’t this self-discrimination as seen in Sudan where African tribes like Al-Shygya, Al-Jalya and Misriya discriminate colleagues? Why did Africans not support their colleagues in the first place? Doesn’t this put them in the same bag as other Arab infidels -to loan words from Salih-that turned their backs to those supposed to be their brothers and sisters in faith? How could they remain Muslims whilst their hands are full of Darfur’s blood ?

Interestingly, although the West is always accused of being anti-Islam by Islamic fundamentalists, what it is doing in Darfur proves otherwise. The West is assisting the Darfur refugees whilst Arab countries shy away, exploit and torture them. Refer to Cairo killings and beatings of Sudanese refugees when they took to the streets to make their case so as -for some- to be housed by Israel. They reached this stage after being discriminated against, killed, exploited and insulted by Egyptians simply because they’re black. As usual, Arab and so-called Muslim states failed to condemn this brutality!

Let’s face it. Arabs north of Sahara (Maghreb) call themselves Africans under AU or whenever there’s anything of benefit for them under African preference. This happened IN 1991 when an Egyptian, Dr. Boutros Boutros-Ghali, was appointed UN General Secretary on Africa’s ticket. However, Egyptians abuse, and hate to be referred to as Africans. And to prove Arab's indifference and disregard of Africans, the same "African" did not take any action during the Rwanda Genocide.To Egyptians and other Arabs every black person is a slave. Remember. These people calling blacks 'slaves' are the same people whose ancestors sold Africans to slavery. Therefore, slavery still exists in their mindset. That’s why redressing Africa for miseries slavery caused is sine quo non shall we want to deter such barbarism.

[49:13] O people, we created you from the same male and female, and rendered you distinct peoples and tribes that you may recognize one another.The best among you in the sight of GOD is the most righteous. GOD is Omniscient, Cognizant.

Surat al Hujurat or walls put more emphasis on brotherhood and equality for Muslims. It insists on reconciliation especially during conflicts like the one we’re evidencing in Darfur in which Muslims all over the world have shied away. Hereunder are more verses about the same.

[49:10] The believers are members of one family; you shall keep the peace within your family and reverence GOD, that you may attain mercy.

[49:14] The Arabs said, "We are Mu'mens (believers)." Say, "You have not believed; what you should say is, `We are Muslims (submitters),' until belief is established in your hearts." If you obey GOD and His messenger, He will not put any of your works to waste. GOD is Forgiver, Most Merciful.

[49:15] Mu'mens (believers) are those who believe in GOD and His messenger, then attain the status of having no doubt whatsoever, and strive with their money and their lives in the cause of GOD. These are the truthful ones.

Having mused upon above verses, is it unfair for Darfuris to regard other Muslims the world over as kaffirs for betraying them?
Source: The African Executive Magazine August 19, 2009.

Nina usongo na damu ya mtu

BAADA ya munene wa nguvu na raismali kuhalalisha ujambazi kwa kutangaza kuwa Beni Njaa Makapu, nkewe, vitegemezi na washirika zake wangezawadiwa bilioni mia tano, nilijisikia kupandisha mwenembago kiasi cha kutamani kunywa damu ya mtu, nikishushia nyama yake.

Bill Ngurumbili Ngereza, bosi wake na sirikali kwa ujumla waliamua kumzawadia mjasirimali ulaji kwa kuonyesha mfano katika kujasrimali akiwa ikulu.

Si siri. Baada ya kusikia upuuzi huu nilitamani nikutane na jamaa hawa kwenye mitaa ya giza nikiwa nimejihami na zana za maangamizi kama vile sime na mikuki, nondo, bisbisi na panga ili lau niwafanyie kweli.

Hivi ulijisikiaje uliposikia kufuru hii ambapo majembuzi badala ya kupelekwa lupango yanazawadiwa njuluku za apache alolo kama wewe nami?

Mie sikuamini kama viumbe hawa hayawani watu wana akili timamu. Pendekezo langu ni wapelekwe Mirembe wakachunguzwe bongo zao kabla hawajaleta madhara zaidi.

Pili sikuamini kama jamaa hawa mafisi wa mafisidi walisoma na kuelewa somo la uzalendo wakati wa Mchonga. Sijui kama walielewa hata dhana nzima ya kujitegemea na kujenga taifa.

Kama wangeielewa vilivyo wasingejitegemea kwa kuibia makapuku wa kaya hii huku wakilijenga kwa kulibomoa. Hakika upuuzi na ujambazi unaoendelea unanikumbusha wimbo maarufu wa zamani wa bomoa tutajenga kesho.

Tatu, sikuamini gendaeka hawa waliumbwa na chembe ya aibu. Watakuwa nayo vipi iwapo wanayofanya hata mbwa na kunguru wanawazomea na kuwacheka? Maskini hawasikii wala hawaoni. Wakisikia neno utajiri au pesa, basi utu huwatoka na kuvaa ufisi kiasi cha kuendekeza ufisadi.

Hayawani watu hawa bila shaka. Hivi ni akili gani hata kama ni mbovu kwa jizi hata kama heshimiwa kuiba mali ya walevi likazawadiwa mara mia badala ya kulambwa bakora na kuozea lupango? Au ni kwa vile walio na madaraka leo hawana tofauti na majizi wayalindayo ukiachia mbali kuwa nao ni matokeo ya majizi haya haya?

Natamani ninywe damu mtu hasa hawa mafisi fisidi. Hawa waibakao kaya wanapaswa kubakwa pia. Ndiyo. Sikio kwa sikio, jino kwa jino. Mwenye masikio na asikie ipo siku itakuja.

Hivi akili gani kwa jizi hata kama jiheshimiwa kuiba mali ya walevi halafu likazawadiwa mabilioni badala ya kula mboko na kuozea lupango? Bado nina usongo na kiu na damu ya fisadi heshimiwa. Laiti Musa angerejea leo na torati si haba tungewatia adabu fisi watu hawa fisidi.

Eti, jitu linatumia vibaya patakatifu pa patakatifu na makahaba zake halafu linazawadiwa njuluku za makapuku hata kama walevi! Kwanini kondoo wafe njaa ilhali chui na fisi wakinenepeana kwa nyama ya kondoo?

Ajabu fisadi jingine bado linajichekesha chekesha kama changu likiwahadaa walevi litawaletea maziwa na samli nao wanaliamini!

Hali ni mbaya hadi Shehe Ubwabwa anatabiri maangamizi na misiba kwa mafisadi. Ingawa Shehe Ukoko huyu haaminiki kwa sanaa zake za utabiri, kuna jambo. Hapa pamoja la laghba zake amelenga. Lazima tuchenjiane kieleweke tena na mapema.

Siamini pamoja na ulevi wao, kama walevi wataendelea kukubali kunajisiwa mchana hivi. Sikutegemea miaka mitano ingeyoyoma kabla ya nyumba za kaya zilizoibwa na Tunituni na mbweha wenzake hazijarejeshwa.

Ajabu, pale Tanisico tunasikia wezi wakikarabati majumba kwa mabilioni na kujiuzia kwa malaki! Uwiii! Najisikia kunywa damu ya fisadi na kushushia na nyama yake.

Sikutegemea kama hata lile jambazi la CPB eti lingeonywa badala ya kukatwa shingo na mali lilizojilimbikizia kurejeshwa kwa walevi. Kwanini tusilivue nguo hadharani na kulifanyia ufilauni ili liwe somo kwa wengine?

Hakika sikutegemea kama Mwana wa nyika naye angeendelea kupeta ilhali yu kibaka wa kutupwa. Jamani hamkusikia ya bwana microfoni Sam Six na kujaza vinyakuzi kwenye ofisi za pale Idodomya?

Kuna ajabu la maajabu. Yaani omba omba wanazawadiana bilioni 50 kama njugu na walevi wasisituke na kufanya kweli lau kwa siku moja! Je huu mchezo ni kutafuta pesa ya kuchangiana kwenye uchafuzi wa uchaguzi baada ya EPA na Richamondu mpya kustukiwa au namna gain?

Yaani hadi hapa walevi hawajaambua hadi mzee nipasue koo!

Jana nilijisikia vibaya nusu kujinyotoa roho. Si ndege walinicheka na kunizomea nilipopita jirani ya mti walipokuwa wametua wakitanua na kuvuta sigara na bangi zao.

Niliwasikia kwa masikio yangu wakitujadili na kudai tumo kwenye fungate na pepo ya mabwege ambapo mabwege wakubwa wanawageuza mabwege wadogo na mabwege wadogo wanakubali ubwege wa mabwege wakubwa.

Katika ndege wote, hakuna aliyenikera kama Kunguru au Indian crow ambaye alilinganisha kaya yetu na kundi la maizi yakipiga kelele huku mafisi yakiufaidi mzoga.

Hakuna kilichiniudhi hadi nizidi kutamani kula nyama ya nyang’au hawa fisidi. Nilitamani niwadonye na kutoa macho lau wasione hizi bilioni hamsini.

Ajabu hadi niandikapo majambazi watukufu wanazidi kuombana ulinzi huku vibaka wakiendelea kuteketezwa na walevi hawa hawa woga wa kuwapa dispilini majambawazi-heshimiwa. Hivi tumeingiliwa na nini? Mbona hapo nyuma hatukuwa hivi?

Nirejee kisa cha kuzomewa na kunguru. Walinizomea sana huku mafisi yakicheka na kuzidi kunitishia niache kuingilia mzoga wao. Mafisi yaliniamba nikapimwe akili nisiyeona neema iliyonizunguka badala yake nikashikilia kulaani. Yaliongeza kuwa wa kupimwa akili si mimi peke bali ukoo mzima wa walevi!

Mafisi walishangaa kuona nagombea ubinadamu ugeuzwe sera badala ya ufisi huku siku zikizidi kuyoyoma. Je hizi sera za ufisi zitatumika wakati wa kutupa vijiti? Kama zitaendelea kutumika, je walevi watafanya ufyongo waendelee kuridhia ufisi badala ya utu na maendeleo? Mie simo kusema ukweli.

Baada ya kuvuka kunako ule mti wa kunguru nilianza kutafakari. Ya kweli. Kweli eti! Hawa gendaeka wanatuona mazezeta wa mazumbukuku kiasi cha kututembezea ufisi na ufisadi tena hadharani kwa namna ya dharau na wazi wazi.

Kama si hivyo wangechelea lau kiama siku si nyingi. Lakini ajabu hawachelei chochote zaidi ya kuzidi kukwapua! Wangehofu wangesema siku ile inakuja ambapo kila fisadi atapewa adhabu yake. Wangechelea wangeandaa mapito badala ya kufanya madudu. Wasagaliwa hawa wanazidi kuiba mchana tena bila aibu!

Kila siku litajwapo jina la jamaa mwenye Njaa kwenye Kaya na Beni Njaa natamani nikutane nao kwenye sehemu za kiza totoro nikiwa na zana zangu za kazi kama vile panga, nyundo hata bunduki nitoe taarifa kwa kufanya kweli.

Natamani nikutane na gendaeka hawa wakiwa wawili bila walinzi tena wamelewa ili nitoe fundisho kwa dunia.

Nikiwapata umma utajua nilivyo na damu ya morani na laigwanani haki ya nani. Natamani nitenganishe viwili wili vya watu hawa mchana kweupe na mizoga yao niwape fisi na mbwa wale bila hata ya chembe ya huruma.

Nina usongo wa damu na nyama vya watu.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 19, 2009.

Friday 14 August 2009

Arican Union: Has it Lost Relevance?

Africa must unite. Those are introductory words on AU's website. They're cool to read but sour to implement. They are verbally practicable but viably impracticable as far as AU is concerned.

May 25, 1963 was seen as Africa's new era. For it's the time the Organization of African Unity (OAU)-the mother of AU, was born. This milestone was thought to be the sine quo non for the total emancipation of Africa. However, it slowly ended up becoming a white elephant.

The sixties saw many post colonial Africans aspiring for a more autonomous united Africa. As the time lapsed, the dream of unifying Africa became a hoax thanks to the machination and manipulation of African countries spearheaded by the West and East. Slowly, dictators cropped up not to mention military juntas. Togo was the first African nation to be overthrown. Sadly though, OAU did not step in to foil the coup d’Etat that later gave birth to many more military juntas.

After many decades of stillness, on 9.9.1999, in Sirte Libya, African heads of state issued a Declaration (the Sirte Declaration) calling for the establishment of an African Union, with a view, inter alia, to accelerating the process of integration in the continent to enable it play its rightful role in the global economy while addressing multifaceted social, economic and political problems compounded as they are by certain negative aspects of globalisation.

The Sirte declaration, that created AU, was the realization of the failure of OAU. The main objectives of the OAU were, among others, to rid Africa of the remaining vestiges of colonization and apartheid; to promote unity and solidarity among African States; to coordinate and intensify cooperation for development; to safeguard the sovereignty and territorial integrity of Member States and to promote international cooperation within the framework of the United Nations.

In its all objectives one was already met. That's to get rid of apartheid in South Africa. Nobody knows why African rulers included this objective whilst it was already deja vu. When AU was dreaming of ridding Africa of apartheid in Sirte, the first post-apartheid president Nelson Mandela had five months in retirement! Did African rulers insert this objective knowing it would be the only success they'd boast of whilst others were mere impossible?

Looking at the map of Africa today, after OAU, one sees a nightmare. Ethiopia that used to be one split into Ethiopia and Eritrea. Somalia, too, went under thanks to having Punt land and the failed state of Somalia. The loose confederation of Senegambia survived for only seven years. Tiny Islands of Comoro or Juzur al-Qumur are still in tussle between Anjoun and Mohéli that declared their independence from the Comoros in 1997.

Generally speaking, the AU is a club of dictators that meet annually to do shoptalk and spend the tax of their paupers. It's totally failed in solving impending crises in Africa. Refer to its failure in Rwanda during genocide, Liberia, Sierra Leone, Somalia, Zimbabwe and DRC. The dreams of its founder no longer exist.

Many wonder. How can one unify Africa amidst stinking dependence and dictatorship? If AU has ever brought any reprieve for Africa, it’s been for rulers only that can congregate annually to do shop talking and chest beating. The recent shame-cum-blow to AU was its alliance with those that committed genocide in Sudan and African supremacists in Zimbabwe not to mention bloodsucking regimes like those in Congo, Equatorial Guinea, Gambia and Gabon.

AU, since its inception, has nary barked on rampant corruption in African regimes. When it comes to democratization, AU has totally failed. Museveni in Uganda, Abdoulaye Wade (Senegal), Robert Mugabe (Zimbabwe) and Paul Kagame (Rwanda) were comfortably able to tamper with their countries' constitutions so as to illegally remain in power. Meles Zenawi (Ethiopia), Denis Sassou Ngwesso (Congo), Teodoro Obiang Ngwema (Equatorial Guinea), Yahaya Jammeh (Gambia), Idris Derby (Chad), Francois Bozize (CAR), Muamar Gadaffi (Libya), Hosni Mubarak (Egypt), Zine El Abidine Ben Ali (Tunisia) and Omar Bashir (Sudan) have always terrorised their citizens as AU sits idly by!

Regarding the economy, AU has proved to be a liability incurring even more pangs to the African paupers. The East African Community that aims at creating a regional economic power house is still struggling, thanks to every country guarding its interests. How can they be united whilst they lack rule of law and democratically elected governments?

In Rwanda and Uganda, dictators have been tampering with the constitutions to remain in power whilst in Kenya and Tanzania, the potentates have always rigged elections. Can such carbuncular rulers unify their countries really? If they do, it will be for their interests- not those of the people.

Africa under AU is the only continent with large-but-doing-nothing governments. They've become another hole in which Africa's wealth sinks.These superimposed-corrupt regimes are but the veins through which African resources are siphoned thanks to playing a middlemen role in ruining the continent.

Despite all the mentioned failures, AU, a cup-in hand begging outfit still chest beats that it can unite Africa! Can it usher in any union?
Source: The African Executive Magazine August 12, 2009.

Thursday 13 August 2009

Kikwete, lini utatangaza mali zako?


HII ni mara ya tano namkumbusha Rais Jakaya Kikwete kutangaza mali zake, mkewe na familia kwa ujumla kama alivyoahidi kwenye kampeni za uchaguzi mwaka 2005.

Mara ya mwisho nilifanya hivyo pale mwenzake wa Urusi, Dimitry Medvedev, alipotangaza azma yake ya kuweka wazi utajiri na mapato ya familia yake, ikiwa ni kuthibitisha dhamira yake safi ya kupambana na ufisadi.

Moja ya sababu kwa Watanzania kumchagua Kikwete, ni ahadi zake za kupambana na ufisadi, ambao kimsingi kwa sasa nadhani umemshinda.

Rejea kuibuka kwa wizi wa kutisha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) pale Benki Kuu ya Tanzania (BoT), na ule mkataba wa kampuni hewa ya Richmond, ambao amejitahidi kujitenga nao bila mafanikio.

Rejea serikali yake kushirikiana na watuhumiwa wa ufisadi kama ilivyotokea hivi karibuni ilipompa onyo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hosea badala ya kumwajibisha, kumchunguza na kumfikisha mbele ya sheria.

Rejea kuendelea kumkingia kifua Rais mstaafu, Benjamin Mkapa mkewe, marafiki na washirika wake, ukiachilia mbali kutaka kuwazawadia sh bilioni 50 baada ya kujitwalia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, kinyume cha sheria.

Rejea watendaji na watumishi wa karibu na rais wanaonuka na kutia kila aina ya shaka kama washauri na wasaidizi wake, mfano Kingunge Ngombale Mwiru anayetuhumiwa kwa ufisadi na uhujumu kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo.

Hakuna ubishi. Kikwete alichaguliwa kutokana na ahadi alizotoa wakati wa kampeni ambazo sasa zimegeuka kuwa sanaa kama wasemavyo watani wake.

Ni wazi Kikwete kashindwa kuwakamata mafisadi kutokana na ukweli kwamba, wengi wao ni watu wake wa karibu. Hata kutangaza mali zake nako ameshindwa! Hivi mwakani wakati wa uchaguzi atawaambia nini Watanzania wamwelewe? Je, Kikwete anaogopa nini kutangaza mali zake?

Pamoja na tuhuma zinazomwandama Mkapa, angalau alitangaza mali zake ingawa nayo ilikuwa kama danganya toto. Kwani baada ya kuchuma, hakufanya hivyo alipokuwa akiondoka madarakani.

Naamini kwamba, mtu anayeshindwa au kuogopa kutangaza mali zake na familia yake, hawezi kuwa safi. Hivyo hafai katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Kitu kingine ambacho kinanipa wasiwasi, kwamba rais anaelekea kushindwa kupambana na ufisadi, ni ile hali ya mke wake kuwa kile Wazungu waitacho 'typical replica' ya Anna Mkapa, mke wa rais anayetuhumiwa kwa ufisadi na upindishaji wa sheria.

Hakuna ubishi. Mzee Mkapa sasa yumo msambweni kutokana na tamaa za mkewe na nduguze. Nahisi hili litajirudi kwa Rais Kikwete. Mkewe, anaendesha NGO iitwayo WAMA. Nimewahi kumwandikia kuonyesha kutoridhika na biashara hii ambayo kwangu ni ufisadi wa kutumia vibaya ofisi ya rais. Bahati mbaya hadi naandika makala haya, hajanijibu.

Kwa nini Salma Kikwete hana tofauti na Anna Mkapa? Kwanza, ameonyesha wazi anavyopenda kutumia madaraka ya mumewe. Soma logo ya WAMA kwenye wavuti yake ya wamafoundation.or.tz. Kuna maneno yasemayo WAMA Foundation the office of the First Lady of the United Republic of Tanzania.

Kisheria, hakuna ofisi ya First Lady of the United Republic of Tanzania. Ukifungua katiba yetu, pamoja na udhaifu wake haina mamlaka haya. Je, yanatoka wapi na kwa nini rais anaridhia yawepo kama hana faida nayo?

Nimeona kwenye sakata la kashfa zinazomkabili Mkapa. Naamini kwamba nyingi zimeasisiwa na kutekelezwa na mkewe. Ninashangaa kwa nini Kikwete hataki achukuliwe hatua. Je, anaogopa na mkewe baadaye yasimkute ambayo yanapaswa kumkuta Anna Mkapa? Je, mtu wa namna hii anaweza kupambana na rushwa?

Hata ukisoma 'pre-amble' ya WAMA hukuti popote iliponukuliwa sheria iliyoanzisha WAMA! Hata ukiangalia wavuti ya EOTF ya Anna Mkapa, ambayo ni eotfz.org hakuna kitu kama hiki. Huu ni ushahidi kuwa NGO hizi zilizoanzishwa baada ya waume zao kupata madaraka, hazipo kisheria na zipo kama ofisi za kujineemesha. Anayepinga hili anipe ushahidi kisheria. Je, madaraka ya rais hapa hayajatumika vibaya tena dhidi ya wale waliomchagua?

Huu ndiyo utawala wa kienyeji aliosema Hassy Kitine, ingawa hakufafanua. Mie huuita utawala wa kilevi, yaani ulevi wa madaraka na njaa ya utajiri. Huu ndiyo upogo na kile Wazungu huita myopia kama si mania. Kuna haja ya kuliangalia suala hili kwa makini.

Muasisi wa taifa hili, Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kumkaripia aliyemfuatia zilipoibuka shutuma kuwa mkewe, alikuwa anatoa vimemo kwa watu kwenda kuchukua mikopo benki.

Hii ilimkera sana Mwalimu kiasi cha kuonya; 'msipende kusikiliza ushauri wa wake zenu. Mambo ya chumbani yasitumike kuamua au kuendesha mambo ya taifa'. Kweli, Mwalimu kwa kipindi chote cha urais wake, hakuruhusu madaraka yake yatumiwe vibaya na familia yake.

Leo, tuna watu wamewajaza watoto na wake zao kwenye 'ulaji' ndani ya chama tawala, BoT na NGO halafu watu hawa watuhadae wanaweza kupambana na ufisadi. Huu ndiyo usanii wanaosema watoto wa mjini.

Kisaikolojia, taifa linaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwakani. Je, kama Kikwete ameshindwa kutaja mali zake kwa miaka mitano akitegemea kugombea tena, atafanya hivyo kwenye ng'we ya mwisho ambayo mara nyingi hutumiwa kwa watawala kusimama tena kwenye uchaguzi?

Rejea Mkapa alivyochapa kazi vizuri kipindi cha kwanza, akaivuruga nchi kwenye lala salama ambapo ujambazi kama EPA, Tanpower, ANBEN, Fosnik na mwingineo uliasisiwa. Je, Watanzania bado tunakubali tena kumpa Kikwete ng'we ya pili atufanyie aliyotufanyia mtangulizi wake?

Mpumbavu ni yule awekaye mayai kwenye kapu moja. Je, tu wapuuzi kiasi hiki? Kuna kashfa zinazohusisha chama tawala, yaani CCM, kutajwa kwenye kashfa karibu zote zinazohusisha wizi wa mabilioni ya pesa.

Hakijatoa utetezi kwa vile ushahidi ni kile wanasheria wanachokiita 'water tight'. Hii ikiongezewa na ukimya wa Rais Kikwete na hali ya familia yake. Je, kuna haja ya kuirejesha CCM iliyoshiriki kwenye Kagoda, EPA, Meremeta, Deep Green Finance na hata Richmond?

Leo sitasema mengi. Natoa changamoto kwa Rais Kikwete kutangaza mali zake kabla ya kumaliza muhula huu ili hata atakapogombea angalau tujue kama ni safi ama la! Hili la mke wa rais kuwa na NGO halimsaidii zaidi ya kuwa kishawishi. Ni kipofu kiasi gani kuanguka alipojikwaa jana Mkapa? Kwa wananchi, uchaguzi wa mwakani agenda kuu iwe ni nani anafaa kupambana na ufisadi.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 12, 2009.

Richamundi, Kitwitwi na maji ya shingo

ZA mwizi huwa arobaini. Na malipo ya uovu huwa ni hapa duniani, walinena wahenga. Pamoja na kulipa wapambe na walamba viatu wake wamtetee, jamaa yangu Njaa Kaya, kama Ben Njaa Makapu, anaanza kuadhirika.

Na kweli ataumbuka, aminini nawambieni. Arobaini yake inazidi kukaribia huku akizidi kuchanganyikiwa na kujichanganya. Leo, walamba matapishi yake wanakuja na hili; kesho na lile, ili mradi sanaa tupu.

Wengi wanajiuliza: Je, yule mbuzi wa kafara wa Richamundi, Eddie wa Ewassa, ameamua kumwaga mtama ili kila mtu abebe furushi lake? Je, huu ni mwanzo wa mitandao uchwara kuraruana na kulipuana? Japo sipo nyuma ya pazia, ni kwamba hakukaliki na mambo si mambo.

Je, walevi wataendelea kubugia sanaa na longo longo, ghiliba na utetezi uchwara au wataamua kumtia Yuda msalabani kweupe? Liwalo na liwe. Lazima asulubiwe mtu hapa.

Zile saa za kuwika majogoo alizosema mwana wa Adamu Nabii Mpayukaji kwenye unabii wa Tanzia punde yatatimia na ang'aaye atachafuka na kufichuka uchafu wake uliofichwa nyuma ya utukufu na utukutu.

Saa ya Yuda kupandishwa majili kupata malipo yake ya usaliti karibu itawadia na wenye macho wataona huku wenye masikio wakisikia, wasiamini kuwa kumbe walimfuga nyoka kwenye unga! Itakuwa aibu, kilio na kusaga meno kwa Yuda na salata wenzake wajilishao upepo.

Hakuna siri chini ya jua. Kila jiwe litafunuliwa na msaliti atawekwa wazi mbele za walevi na kuumbuliwa bila huruma. Je, walevi watamtia adabu gendaeka huyu mkuu wa machukizo na maangamizi katika uso wa nchi?

Mpayukaji alipotabiri alionekana mbaya. Je, mbaya hapa nani? Asemaye Kaisari yu uchi au walamba viatu na wala makombo wajipendekezao ili waambulie makombo kama malipo ya aibu, uchafu na usaliti wao?

Jamani, wakati wa kumfichua mwovu, salata, fisadi aliye tunda la ujambazi na jinai ya ufisadi umewadia, jiandeeni kumdhihaki na kumnnywesha siki huku akivikwa taji la miba.

Walevi wana hamu ya kuwaona kina Kagoda, Richmond, EPA na wengine wakiumbuka na kutiwa adabu kwenye majili ya umma. Wamehanikiza na kusema patakatifu pa patakatifu pamechafuka na si patakatifu tena.

Pamevamiwa na majambazi, vinyama vya mwitu na makahaba wa matumbo yao. Panahitaji kufukizwa ubani na kutoharishwa huku Yuda wa Nabkadnezzar, akiwambwa msalabani, nyumba yake na washikaji wake.

Japo Yuda kajitahidi kuwatoa kafara wahalifu wenzake, hajafanikiwa. Tazama. Naona kina Pesatatu Nusurupia, Dan na Mgonjwa wakitolewa kafara kumwepusha Yuda bila mafanikio. Kitafutwacho ni matumaini na imani vilivyopotea.

Hakika, walevi wanataka baba wa jinai ya ufisadi na ujambazi ajitiaye utukufu apatilizwe ili liwe somo kwa wengine. Imeandikwa. Aishie kwa upanga, atakufa kwa upanga. Achumaye asipopanda ni mwizi astahikiye kunyongwa.

Yote katika yote, akweaye kwa uchafu na jinai atashushwa navyo. Je, hayakutimia aliyotabiri nabii Musa? Hakika walevi wanataka ule ushirika mchafu uliojivisha utukufu uangamizwe na wana wa Aliye juu, wakombolewe kutoka kwenye makucha na ukahaba wa Kaisari Nero.

Wakati wa kuita kulego kwa jina lake halisi umewadia na kila mtu ajifunge mshipi tayari kuukabili ukweli na mapigo yake. Hakika amini nawambieni. Wana wa Musa watauvua ukondoo na kuuvaa usimba huku wakifanya ambacho hakikutarajiwa kwa namna ambayo haikutarajiwa.

Yashikeni maneno haya ya unabii wa Mwovu Yuda kuumbuka na kusulubiwa mchana. Tazama. Wana wa Musa watauvua umbwa, ukuku na ulamba viatu wakipania kujikomboa na kuitangazia dunia iwatambue na kuwaheshimu. Watamkabili kidhabu na genge lake kama vile chungu chungu wamkabilivyo nune.

Hakika kidhabu huyu aliyetabiriwa na manabii kuwa atageuka shubiri badala ya sukari, akakwezwa na walevi kutokana na ulevi wao wasijue ni mauti yao, atatiwa adhabu na kuondolewa kwenye uso wa dunia ya ulaji.

Mwana wa yule mwovu lazima apatilizwe na mapema. Lazima magenge yote na vinyamkera na vitimbamkwiji waliomzunguka nao wateketee naye kwenye bahari ya moto uchomao fisidi na hasidi.

Pakuu pa pakuu patatayarishwa na kurejeshewa kilicho chake huku somo la milele juu ya adili na idili likifundishwa kwa dunia ya wapenda haki na maendeleo.

Tunahitaji kuvaa silaha zetu za kivita ambazo ni kujiamini, ushirikiano, uwazi, uthubutu na ukweli, tayari kumkabili mwovu salata na watu wake. Kwa silaha hizi, hatutamwogopa mtu wala magenge yake ya makenge watu. Tutamkabili yeyote kwa mustakabali wetu na vizazi vyetu.

Karibu minara, vinara na mihuri ya wizi, ufisadi, ujambazi na kila jinai itadondoshwa na uovu utaporomoka huku walevi wakijitambua na kufanya mapinduzi ya kifikra ili kutorudia kosa.

Alianza yule aitwaye Asi wa Ewassa na sasa atafuatia yule aitwaye Njaa Kaya, mwenye makeke kama Kitwitwi hadi akaitwa Kitwitwi. Atafuata yule mwanzilishi wa salata aitwaye Makapu na mama watoto wake. Huyu zake zazidi kwisha asijue maskini.

Baada ya hapo kishindo kikubwa kitasikika huku baragumu ikipigwa na mwovu mkuu atawekwa ugani akiwa uchi wa mnyama tayari kuipokea hukumu ya umma. Natamani siku hii kila mmoja asilale na awepo kushuhudia kushindwa kwa fisidi na hasidi mkuu.

Siku hiyo ikitimia vigogo vingi vitaporomoka kama unyoya kwenye mgongo wa ng'ombe ambaye huwa hauhisi unyofolewapo. Tuandae mapito ya kaya mpya yenye kila kitu kipya na walevi waliojitambua walioitwa Danganyika wakadanganyika kwa uongo wa kila jizi.

Tumaini jipya na mwelekeo mpya vitaonekana siku hiyo kuchukua mahali pa kiza, ulafu, salata, ukahaba na ujambazi. Hakika imeandikwa. Heri kijana maskini mwenye busara kuliko mfalme tajiri mpumbavu ajilishaye pepo asijue ni kuni za maangamizi yake. Aaminiye wamlao akidhani wanamhami asijue wanahami matumbo yao. Atumiwaye akadhani atumia asijue anapaa mkaa kama pweza mpumbavu.

Sikizeni enyi Tanzia. Yule habithi aliyetiwa muhuri wa uovu atatiwa hatiani siku si nyingi huku wapambe wake wakiasiwa na kunyofolewa ndimi ziwapazo kiburi na majisifu.

Hakika wote watatupwa gerezani aminini nawambieni ili yatimie yaliyotabiriwa na kuandikwa kwenye kasri la nabii Mpayukaji mwana wa Msemakweli aitwaye Msemahovyo.

Hakika imeandikwa. Kila jambo lina mwisho wake, ingawa uongo huaminika kuliko ukweli. Lakini ukweli hauuawi na ukweli huweka huru.

Tuufie ukweli kwani utatuweka huru. Umefika wakati wa kuwazika majambazi wa Richamundi, ambapo wataumbuka ambao hatukutegemea.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 12, 2009.

Saturday 8 August 2009

Why East Africa heads cannot be trusted


TANZANIA is a hard nut to crack. It has trashed some proposals made in a meeting for the unification of East African countries and stated clearly that it would never allow East Africans to enjoy the right of movement and permanent residence on its soil as proposed by other countries in this loose outfit.

To prove Tanzania's muscle, the just-ended summit of East African Heads of State issued a communiqué to the effect that the draft on the Common Market shall not contain provisions which authorise overriding of national policies and laws. The communiqué further stated that 'the granting of related rights to access to land and establishment should not be automatic, but should lay a basis for eligibility.'

This, if anything, is the last nail in the coffin for the right of permanent residence. If anything, this is a slap in the face on Kenya and Uganda that felled the former East African Community (EAC).

Being a Tanzanian, I have always supported some of my country’s stances on land matters. Other countries, especially Kenya, must first harmonize their land policies before prevailing upon Tanzania (the only East African country with a vast land) to let go of its land. Kenya (a country with many landless citizens) as well as Rwanda and Burundi have never taken this as a pressing issue!

Tanzania should, however, stop being hypocritical. I have concluded that she is hypocritical owing to the fact that President Jakaya Kikwete has invited Saudis to come and invest in agriculture – with a view of feeding the Saudis!

Why is Tanzania, a country that’s portrayed itself as the model of good land policies, cascading into the same sin it’s been castigating others like Kenya and Sudan for? What hypocrisy!

This means that our rulers are not eyeing the unification of our countries for the good of their people. How can Tanzania commit such a sacrilege – and still have moral authority to deny other access to its land?

Isn’t this racism whereby Africans from Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi are regarded as a danger to Tanzania’s land but Arabs aren’t? Isn’t this enough hypocrisy and double standards to let Tanzania go solo with its new Arab partners?

What transpired between Kenya and Uganda over a tiny and barren island of Migingo demonstrates how myopic and short-term minded our rulers are. Who’d think such tail wagging would consume a lot of time and resources?

One would think conventional wisdom would prevail, with one of the protagonists knuckling under and setting a precedent in the interests of unification. But nay! What’s all this furore
about if the tax and income obtained from Migingo is not at par with the expenses of bargaining and scheming?

Our rulers are breathing fire to show their ‘passion and fire’ for the good of their countries whilst they’re the same creatures stealing from them.

Why should neighbouring countries live under suspicion and differ over a tiny island? Isn’t this an assault on unification and prosperity? How genuine is this unification project?

When the Rwandese were bearing the brunt of genocide, where were these 'good' neighbours? They did not help. They did not even bother to hold to account the current Rwandan regime that’s alleged to have perpetrated it. Sadly, East African countries condoned it. And now they’ve already incorporated those behind it!

Kenya never bothered to ask Uganda's Yoweri Museveni and Tanzania why they supported Rwandan Paul Kagame to ascend to power. Why make noise on unification without enhancing democracy? How can you unite people ruled by dictators and poll riggers?

It is not bad to ape the European Union on unity. But, we should not forget one thing: that union was enhanced by democratic leaderships that listen to the people. We still remember how the French and Dutch voters smashed the referendum in 2005. They did. For, the union is theirs, not their leaders.’ Those emulating the EU do not want to face this!

Let us face it. If we need unification of the East African countries, we must play our part instead of leaving all decision-making powers to our failed gluttonous and myopic rulers. Their interest has always been flocking to East African capitals or other cities to get per diem as they do their shoptalking.

The proposed East African Federation will never materialize as long greed rules over concerned partners. Recently, for example, there were rumours that oil reserves had been discovered in the Indian Ocean on Zanzibar’s side – and they were enough to threaten to tear down the union between Tanganyika and Zanzibar!

The islanders started agitating for the removal of oil matters from Union jurisdiction.

For over forty years, Zanzibar has been breastfed by Mainland Tanzania. But it now wants to break away from the Mainland on the basis of rumours of oil wealth. If Zanzibar cannot share oil with Mainland Tanzania, how will it share its resources with other East Africans?

If East African countries cannot contain the internal wrangles within themselves, how ca they effectively handle regional matters together?

In a nutshell, either Tanzania should be left to remain solo as the other countries seek advice from their people to see to it that whatever is reached at must come from the hoi polloi instead of the cabal of myopic pretenders.
Source: Business Time August 7, 2009.

Wednesday 5 August 2009

Strongmen or Strong Institutions: Which Way for Africa?

Those are my catch words from president Barack Obama's stunning speech in Ghana although he dwelt on many issues reminiscent to Africa's endemic and systemic problems. Unlike other past American presidents, Obama seems determined to face the reality by giving African potentates a bitter pill to swallow.

Before becoming US president, many African strongmen such as Paul Kagame (Rwanda), Yoweri Museveni (Uganda) Meles Zenawi (Ethiopia) and Teodoro Obiang Ngwema (Equatorial Guinea) were darlings of the US, thanks to enhancing the exploitation of Africa's resources. Things seem to have taken a new turn with Obama’s promise of change. His ‘Yes We Can’ slogan seems to have started working. Yes. Africa can be a good and prosperous place without thieving dictators at the helm. Yes. We can kick dictators out of Africa's political landscape.

"No country is going to create wealth if its leaders exploit the economy to enrich themselves, or police can be bought off by drug traffickers," Obama says. He speaks as if he lives in our streets where the police force protect and promote crime. He speaks as if he lives in our state houses where thieves-in-chief steal public money.

Tanzania, my own country, is the fifth giant when it comes to mineral abundance but interestingly, the country is fifth on the tail as far as poverty worldwide is concerned. Small countries with fewer resources like Kenya, Rwanda and Uganda outshine Tanzania.

“Development depends upon good governance. That is the ingredient which has been missing in far too many places, for far too long. That is the change that can unlock Africa's potential," Obama adds. Many African mumbo jumbos cannot like this. It is like carpet-bombing them. They have always preached rule of law and good governance even when they govern tyrannically.

Telling African chronic thieves to stop stealing by their volition is as good as telling the monkey to stop stealing maize. What needs to be done is to categorize crimes involving rulers and their cronies stealing from public coffers as crime against humanity. Most Africans lose their lives to corruption than wars. Genocide in Rwanda claimed over 800,000 lives. In Darfur, it has claimed over 200,000. Malaria, that is curable shall our rulers stop stealing from the public, is killing many more people than all genocides put together.

An April 2009 report by the World Health Organization (WHO) says that malaria is responsible for 30% of childhood mortality and 11% maternal mortality in Nigeria. In Zambia, the figure stands at 66%. Malaria kills more than a million people worldwide each year—90 percent of them in Africa; 70 percent being children under the age of five.

Being the 12th producer of oil on earth, one would think Nigeria's economy and people would look like it. Alas! Its rulers and their whiz kids are super rich whilst the hoi polloi live in abject poverty. What's this if it is not crime against humanity?

The president of America is the most powerful and influential person on earth currently. So too, is his non-bendable writ -if he stands for it. We saw it in Iraq despite all blunders. Obama's regime brought Swiss banks and others to their knees thanks to sheathing tax evaders and thieves in power. Soon they'll be duty-bound to open their books. The time of criminal secrecy is over thanks to Obama's new take on them. Suppose Obama stands for making theft of public moneys by rulers a crime against humanity? Truly, this will add up. The ICC should be vested with powers to indict anybody that commits this crime. This way, Africa will forge ahead. Her resources will benefit citizens suffering in the hands of its all time thieving regimes.

Many analysts, nonetheless, blamed Obama for not coming to Africa with money or promises of dishing money out. Giving money knowing it'll be embezzled has nary become a solution to our problems but a problem in itself. Obama's new approach is a reminder that Mr. Moneybag America is no more. Why did Asian tigers manage to blast off from poverty whilst Africa is still sinking even more? Good-and-responsible governance is the only vehicle behind.

To jump-start Africa's economy, among others, rule of law and good governance based on accountability and democracy must be emphasized. African people are ready to bring their development. The only barrier they encounter is nothing but corrupt and irresponsible regimes supported by west.

Africans have fed thieving and begging corrupt regimes for long. Transparency International says, "The combination of abundant natural resources, a history of autocratic and unaccountable government, as well as conflict and crisis throughout the continent have posed particular challenges to governance and the fight against corruption in Africa to the point that several countries have become virtually synonymous with graft."

TI adds that the development challenges faced by sub-Saharan Africa are enormous: It is the only region of the world where poverty has increased in the past 25 years and half of the continent’s population of 840 million people lives on less than 1 USD per day. Thirty-two of the world’s 38 highly indebted poor countries (HIPC) are in Africa. In addition to corruption, protracted armed conflict, the HIV/AIDS pandemic and declining terms of trade for non-mineral primary products continue to exacerbate the many challenges facing the region.

To know how perilous the situation is in Africa, think of Sani Abacha;s $ 550 million fortune. Remember other thieves such as Mobutu Seseseko, Felix Houphet Boigny, Jomo Kenyatta, Daniel arap Moi, Fredrick Chiluba, Jean Bedel Bokassa, Denis Sassou Ngweso, Teodor Obiang Nguema, Omar Bongo,Charles Taylor and others. How much did they rob from their countries?

Some analysts agree that the amount of money robbed by ruling thieves in Africa is even bigger than all foreign aids put together. Recently I hollered about current scandals in Tanzania alleged to have been perpetrated by the current and former regimes. Over $ 1,000,000,000 is believe to have been stolen by Tanzania's rulers. To get away with it, they instituted fake charges against a few sacrificial officers so as to win people's confidence. Recently, Prof. Ibrahim Lipumba CUF chair, linked president Jakaya Kikwete with External Payment arrears account that sank over $ 200,000,000 and Richmond scams. The president did not comment on or deny these damning accusations.

Many African rulers, apart stealing and stashing money abroad, steal in order to bribe voters and buy loyalty from military and other influential figures. So to fell this malady, democratic institution especially opposition must be fully supported without forgetting financing civil education to the general public. This way, we'll be able to break the back of graft.

Astonishingly, Tanzania's pro-government media still have the guts of reporting that Obama praised Kikwete for taking on graft whilst he is himself the custodian of it! Sadly, even the American embassy in Dar es salaam does not repudiate such naked lies that show Obama as a double standard person or ignorant! What arrogant and corrupt pro-media is doing in Tanzania is telling their readership lies. In Africa, Obama only praised praised Ghana.

Africa needs strong institutions manned and headed by people of probity, responsible and accountable to the people. To enhance this, Africa’s constitutions need to be amended or re-enacted. The current ones shamelessly and expressly provide for much discretionary power that strongmen use to rob the hoi polloi. Almost all African potentates and their families are above the law.

Something needs to be done urgently to do away with this anathema. Those that have already ruined their countries should be held accountable. Truly Africa does not need strongmen but strong institutions.
Source: The African Executive Magazine August 5, 2009.

Ngeleja, Mkapa na usanii wa Kiwira


TAARIFA zilizotolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuhusiana na mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kurejeshwa serikalini kinyemela haziwezi kupita bila kulaaniwa na kupingwa.

Pia uzushi kuwa ANBEN, Kampuni ya Anna Mkapa na Benjamin Mkapa ilijitoa mwaka 2005, haziwezi kupita bila kushutumiwa na kukalipiwa.

Kwanza ifahamike, waziri anataka kuuhadaa na kuupotosha umma kwa kudai kuwa Mkapa na mkewe walijitoa kwenye mradi wa kuhujumu Kiwira. Waziri anataka kumgeuza nani bunga? Mkapa na mkewe watajitoaje iwapo watoto wao na Kampuni yao la Fosnik wamebaki?

Je, walijitoa kwa sababu gani, tena ndani ya kipindi kifupi cha kuasisi dili hili huku Mkapa akiwa bado yu madarakani? Je, ni kweli walijitoa au ni danganya toto na mazoea ya usanii wa watawala wetu waliopo madarakani?

Kuonyesha habari hizi zilivyo sanaa na ujambazi wa mchana, eti waziri anasema serikali itawafidia wezi waliojitwalia mali ya umma kinyume cha sheria! Hawa ni watu wa kufikishwa mahakamani na kuitwa wahujumu wa uchumi moja kwa moja hata kama wana madaraka.

Wanalipwa kwa jema gani iwapo mradi mzima uliibiwa kutoka mikononi mwa umma kwa bei ya kutupwa? Je, waziri anadhani umma umesahau jinsi Mkapa na wenzake walivyojitwalia mgodi wa Kiwira kwa bei ya karibu na bure?

Hebu fikiria mali ya 4,000,000,000 inauzwa kwa bei ya shilingi 70,000,000. Huu ni wizi na uhujumu uchumi hata upakwe mafuta vipi. Na huu ni ushahidi kuwa utawala wa sasa ni fisadi na mshirika mkuu wa jinai hii.

Mkapa na mkewe wanaweza kuwa wamejitoa vipi iwapo maswahiba wao bado wanaendelea kushirikiana na watoto wao katika dili hiyo?

Je? serikali imeamua ‘kuitwaa’ Kiwira ili kumuepusha Mkapa kupambana na hasira ya umma na kumkingia kifua kama alivyoahidi Rais Jakaya Kikwete au kuna namna wakubwa wa serikali ya sasa walifaidika na mradi huu au ufisadi huu? Je, watawala wetu wanalipa fadhila kutokana na Mkapa kuidhinisha benki yetu kuu ivunjwe ili kupata mtaji wa kuingilia madarakani?

Je, wanaamua kufanya hivyo kwa kuogopa Mkapa asiwafichue kuwa nyuma ya wizi na ujambazi wa EPA na Richmond? Hivyo wanaona wamuhifadhi kabla hajawaumbua? Je, kwa serikali kama hii inayoshirikiana na wahalifu kweli tunaweza kupamba na ufisadi unaozidi kugeuka donda ndugu nchini?

Je, wakuu wa serikali ya sasa wana mpango wa kufanya kama alivyofanya Mkapa, mkewe, watoto na marafiki ili baadaye wajilipe fidia kama wanavyopendekeza kwa Mkapa? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Ikumbukwe. Kabla ya Ngeleja kuja na dili la kurejesha Kiwira serikalini, aliwahi kulihadaa Bunge na taifa zaidi ya mara nne akisema angefichua wamiliki wa Kiwira. Sasa badala ya kutimiza ahadi yake anakuja na sanaa nyingine za kumuokoa bosi wake Mkapa! Je, umma wa Watanzania wenye mali watakubali kugeuzwa majuha na kuchezewa mahepe mchana kweupe?

Hebu angalia sanaa za waziri kama alivyonukuliwa na vyombo vya habari. Inatia kinyaa na inatisha kama wananchi wenye mali wataukubali upuuzi huu ambao kimsingi ni wizi wa mchana.

“Januari mwaka 2005 (siku 13 tangu kuanzishwa kwa TPR), ANBEN iliondolewa kuwa miongoni mwa wamiliki wa hisa kwa vile haikuweza kulipia hisa ilizokuwa imechukua wakati wa usajili wa TPR, hivyo wamiliki wa TPR waliobaki walikuwa wanne.”

Haiwezekani Rais Mkapa na mkewe washindwe kulipia hisa zao lakini watoto wao waweze. Huu ni uongo wa mchana na waziri hakufanya ‘home work’ yake vizuri katika kutunga uongo huu unaolenga kuhalalisha uhujumu wa taifa.

Tuambizane ukweli bila kumung’unya. Ukweli ni kwamba dili hili linaihusisha Serikali ya Awamu ya Nne moja kwa moja na ndiyo maana Mkapa na wenzake wamekuwa na kiburi cha kutotaka kutoa maelezo. Kwani wanajua nyuma yao kuna nani. Na ndiyo maana Rais Jakaya Kikwete aliamua wazi wazi kumkingia kifua bosi wake wa zamani na mshirika wake zilipofumka tuhuma za uhujumu na ufisadi.

Kwani katika maelezo ya Ngeleja kuna ukweli usiopingika kuwa mwizi mkuu hapa si Mkapa pekee, bali hata serikali. Alibainisha kuwa, mkataba wa kuendeleza mradi wa Kiwira kati ya serikali na Kampuni ya KCML, uliingiwa Machi 24, 2006 kwa kutia saini makubaliano ya makusudio (Agreement of Intent-Aol) na mikataba ya Power Purchase Agreement (PPA), Implementation Agreement (IA), Escrow Agreement (EA), Transmission Line Facilities Agreement (TLFA) na Facility Transfer Agreement (FTS), ilitiwa saini Agosti 2006.

Je, serikali iliingiaje mkataba na kampuni ya kijambazi huku umma ukipiga makelele kama si mhusika mkuu? Je, serikali iko tayari kutoa maelezo kwanini imekuwa ikiwakingia kifua mafisadi kila wanapobainika?

Rejea kuendelea kugeuka muujiza kwa kampuni dokozi la Kagoda, kuendelea kutoshitakiwa kwa waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa na wenzake, kutokana na kubainika walishiriki ufisadi, kutofikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wa ufisadi wa EPA na wengine na yote katika yote, kutaka kulipa fidia kwa wezi wa Kiwira.

Je, serikali ya namna hii si fisadi wa kutupwa? Ingawa Ngeleja, bosi wake, Mkapa na wengine wanaweza kujiridhisha kuwa wametua mzigo, ukweli ni kwamba mzigo bado ni mbichi na historia itawahukumu kwa ukali wote siku moja.

Nani alijua kuwa mtawala mbabe kama Mkapa angetiwa adabu kiasi cha kutegemea kulindwa na rais huku akiendelea kuishi maisha ya aibu? Tunaitaka serikali iwafungulie mashitaka wezi wa Kiwira badala ya kuwazawadia pesa yetu.

Baada ya kugundua kuwa kisingizio cha Mkapa kuwa na kinga hakiwezi kuwaokoa mkewe na wanawe, sasa serikali imeamua kuua ushahidi kwa kuutwaa mgodi wa Kiwira huku ikitenda kosa moja ambalo siku moja italijutia-kuwafidia kwa unyakuzi wao.

Ngeleja, mwakani unakabiliwa na uchaguzi. Kama umma utaweka nukta, Mkapa amekutoa kafara, kwani huna sababu ya kurejea bungeni kuendelea kuwatetea mafisadi huku ukiwatelekeza wananchi.

Ukistaajabu ya Musa utaona ya Filauni. Hakika huu ni usanii wa Ngeleja, Mkapa na serikali kuendelea kuuibia umma bila aibu. Na hakika, huu ni ushahidi tosha kuwa serikali yetu haina nia ya kupambana na ufisadi ambao mazingira yanaonyesha inautenda tena bila aibu.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 5, 2009.

Nina usongo na damu ya mtu Kiwira


Baada ya munene wa nguvu na raismali kuhalalisha ujambazi kwa kutangaza kuwa rahisi mstaafu Ben Njaa Makapu, nkewe, vitegemezi na washirika zake wangezawadiwa bilioni mia tano, nilijisikia kupandisha mwenembago kiasi cha kutamani kunywa damu ya mtu nikishushia nyama yake.

Bill Ngurumbili Ngereza, bosi wake na sirikali kwa ujumla waliamua kumzawadia mjasilimali ulaji kwa kuonyesha mfano katika kujaslimali akiwa ikulu. Si siri. Baada ya kusikia upuuzi huu nilitamani nikutane na jamaa hawa kwenye mitaa ya giza nikiwa nimejihami na zana za maangamizi kama vile sime na mikuki, bisibisi, nondo na panga ili lau niwafanyie kweli.

Hivi ulijisikiaje uliposikia kufuru hii ambapo majembuzi badala ya kupelekwa lupango yanazawadiwa njuluku za apache alolo kama wewe nami?

Mie sikuamini kama viumbe hawa hayawani watu wana akili timamu. Pendekezo langu ni wapelekwe Mirembe wakachunguzwe bongo zao kabla hawajaleta madhara zaidi.
Pili sikuamini kama jamaa hawa mafisi wa mafisidi walisoma na kuelewa somo la uzalendo wakati wa Mchonga. Sijui kama walielewa hata dhana nzima ya kujitegemea na kujenga taifa. Kama wangeielewa vilivyo wasingejitegemea kwa kuibia makapuku wa kaya hii huku wakilijenga kwa kulibomoa. Hakika upuuzi na ujambazi unaoendelea unanikumbusha wimbo maarufu wa zamani wa bomoa tutajenga kesho.

Tatu, sikuamini gendaeka hawa waliumbwa na chembe ya aibu. Watakuwa nayo vipi iwapo wanayofanya hata mbwa na kunguru wanawazomea na kuwacheka? Maskini hawasikii wala hawaoni. Wakisikia neno utajiri au pesa basi utu huwatoka na kuvaa ufisi kiasi cha kuendekeza ufisadi.

Hayawani watu hawa bila shaka. Hivi ni akili gani hata kama ni mbovu kwa jizi hata kama heshimiwa kuiba mali ya walevi likazawadiwa mara mia badala ya kulambwa bakora na kuozea lupango? Au ni kwa vile walio na madaraka leo hawana tofauti na majizi wayalindayo ukiachia mbali kuwa nao ni matokeo ya majizi haya haya? Natamani ninywe damu mtu hasa hawa mafisi fisidi. Hawa waibakao kaya wanapaswa kubakwa pia. Ndiyo. Sikio kwa sikio, jino kwa jino. Mwenye masikio na asikie ipo siku itakuja.

Hivi akili gain kwa jizi hata kama jiheshimiwa kuiba mali ya walevi halafu likazawadiwa mabilioni badala ya kula mboko na kuozea lupango? Bado nina usongo na kiu na damu ya fisadi heshimiwa. Laiti Musa angerejea leo na torati si haba tungewatia adabu fisi watu hawa fisidi.

Eti jitu linatumia vibaya patakatifu pa patakatifu na makahaba zake halafu linazawadiwa njuluku za makapuku hata kama walevi! Kwanini kondoo wafe njaa ilhali chui na fisi wakinenepeana kwa nyama ya kondoo?

Ajabu fisadi jingine bado linajichekesha chekesha kama changu likiwahadaa walevi litawaletea maziwa na samli nao wanaliamini!

Hali ni mbaya hadi Shehe Ubwabwa anatabiri maangamizi na misiba kwa mafisadi. Ingawa Shehe Ukoko huyu haaminiki kwa sanaa zake za utabiri, kuna jambo. Hapa pamoja la laghba zake amelenga. Lazima tuchenjiane kieleweke tena na mapema.

Siamini pamoja na ulevi wao, kama walevi wataendelea kukubali kunajisiwa mchana hivi.
Sikutegemea miaka mitano ingeyoyoma kabla ya nyumba za kaya zilizoibwa na Tunituni na mbweha wenzake hazijarejeshwa. Ajabu, pale Tanisico tunasikia wezi wakikarabati majumba kwa mabilioni na kujiuzia kwa malaki!

Uwiii! Najisikia kunywa damu ya fisadi na kushushia na nyama yake.
Sikutegemea kama hata lile jambazi la CPB eti lingeonywa badala ya kukatwa shingo na mali lilizojilimbikizia kurejeshwa kwa walevi. Kwanini tusilivue nguo hadharani na kulifanyia ufilauni ili liwe somo kwa wengine?

Hakika sikutegemea kama Johansenia Mwananyika naye angeendelea kupeta ilhali yu kibaka wa kutupwa. Jamani hamkusikia ya bwana microfoni Sam Six na kujaza vinyakuzi kwenye ofisi za Jumba pale Idodomya?

Kuna ajabu la maajabu. Yaani omba omba wanazawadiana bilioni 50 kama njugu na walevi wasisituke na kufanya kweli lau kwa siku moja! Je huu mchezo ni kutafuta pesa ya kuchangiana kwenye uchafuzi wa uchaguzi baada ya EPA na Richmonduli mpya kustukiwa au namna gain? Yaani hadi hapa walevi hawajaambua hadi mzee nipasue koo!

Jana nilijisikia vibaya nusu kujinyotoa roho. Si ndege walinicheka na kunizomea nilipopita jirani ya mti walipokuwa wametua wakitanua na kuvuta sigara na bangi zao. Niliwasikia kwa masikio yangu wakitujadili na kudai tumo kwenye fungate na pepo ya mabwege ambapo mabwege wakubwa wanawageuza mabwege mabwege wadogo na mabwege wadogo wanakubali ubwege wa mabwege wakubwa.

Katika ndege wote hakuna aliyenikera kama Kunguru au Indian crow ambaye alilinganisha kaya yetu na kundi la maizi yakipiga kelele huku mafisi yakiufaidi mzoga.
Hakuna kilichiniudhi hadi nizidi kutamani kula nyama ya nyang’au hawa fisidi. Nilitamani niwadonye na kutoa macho lau wasione hizi bilioni hamsini.

Ajabu hadi niandikapo majambazi watukufu wanazidi kuombana ulinzi huku vibaka wakiendelea kuteketezwa na walevi hawa hawa woga wa kuwapa dispilini majambawazi-heshimiwa. Hivi tumeingiliwa na nini? Mbona hapo nyuma hatukuwa hivi?

Nirejee kisa cha kuzomewa na kunguru. Walinizomea sana huku mafisi yakicheka na kuzidi kunitishia niache kuingilia mzoga wao. Mafisi yaliniamba nikapimwe akili nisiyeona neema iliyonizunguka badala yake nikashikilia kulaani. Yaliongeza kuwa wa kupimwa akili si mimi peke bali ukoo mzima wa walevi!

Mafisi walishangaa kuona nagombea ubinadamu ugeuzwe sera badala ya ufisi huku siku zikizidi kuyoyoma. Je hizi sera za ufisi zitatumika wakati wa kutupa vijiti? Kama zitaendelea kutumika, je walevi watafanya ufyongo waendelee kuridhia ufisi badala ya utu na maendeleo? Mie simo kwenye usenge huu kusema ukweli.

Baada ya kuvuka kunako ule mtu na kunguru nilianza kutafakari. Ya kweli. Kweli eti! Hawa gendaeka wanatuona mazezeta wa mazumbukuku kiasi cha kututembezea ufisi na ufisadi tena hadharani kwa namna ya dharau na wazi wazi. Kama si hivyo wangechelea lau kiama siku si nyingi. Lakini ajabu hawachelei chochote zaidi ya kuzidi kukwapua! Wangehofu wangesema siku ile inakuja ambapo kila fisadi atapewa adhabu yake. Wangechelea wangeandaa mapito badala ya kufanya madudu. Wasagaliwa hawa wanazidi kuiba mchana tena bila aibu!

Kila siku litajwapo jina la jamaa mwenye Njaa kwenye Kaya na Ben Njaa au mwenye para kama Heathrow international Airport natamani nikutane nao kwenye sehemu za kiza totoro nikiwa na zana zangu za kazi kama vile panga, nyundo hata bunduki nitoe taarifa kwa kufanya kweli.

Natamani nikutane na gendaeka hawa wakiwa wawili bila walinzi tena wamelewa ili nitoe fundisho kwa dunia. Nikiwapata umma utajua nilivyo na damu ya morani na laigwanani haki ya nani.

Natamani nitenganishe viwili wili vya watu mchana kweupe na mizoga yao niwape fisi na mbwa wale bila hata ya chembe ya huruma.
Nina usongo wa damu na nyama vya watu wa Kiwila.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 5, 2009