The Chant of Savant

Wednesday 7 November 2007

Jicho la Kijiweni

NIMEZINYAKA za Idodomya mjini mkuu usio mkuu ila wenye makuu.

Ndipo kigwena cha ulaji na usanii cha nambari wahedi kinakutana kulamba njuluku zetu na mkuu kuonyesha ufalme na mazingaombwe yake. Naelekea ulabuni nikitafakari kila sanaa, mizengwe, rushwa za kuombea kura ya kula na ujidhalilishaji wa waliowahi kuwa waheshimiwa.

Namuona mkuu akichomoa mvinyo wa kale na kuuweka mezani. anumwaga wa kale. Ni mvinyo aina ya Peas Msukwa. Ule wa Johnnie Machelani unamwagwa kwenye jalala!

Kuishi kwingi kuona mengi! Mivinyo wenye tofauti ya miezi 12 hakuna tofauti ya umri.

Kibaya walevi wamedanganyika. Wanashangilia kugeuzwa majuha!

Abishae ajikumbushe walivyomshangilia msanii kutoa mvinyo wa kale aliouita mpya.

Nilijua mkuu hatataka tena mvinyo aina ya Johnnie. Ulijitia ukali kama Butuku ukapayuka huku nao ukitokota usijue uko kwenye chupa ya mwenyewe!

Tuache mambo ya ulevi. Nampongeza babu Pius Msekwa kuukwaa umakamu na daraja la ujana. Nampa pole kijana wa zamani John Malecela kwa kutupwa nje, lakini kubaki na heshima kubwa. Ndiyo siasa hizo ndugu yangu hasa za mizengwe kujuana na kulipana fadhila. Usikonde John vuka pazia kama akina Mtei kama utaona namna gani vipi.

John nilikuonya kuwa maneno uliyotamka kuwa Jakaya asafishe nyumba yake ashughulikie mafisadi yatakurudi. Hukujua kuwa naye alitajwa? Shauri yako.

Baada ya kumaliza kuwapongeza na kuwapa pole wahusika sasa natoa tathmini ya maajabu ya mwaka huu wa machungu.

Mosi ni ajabu ahadi ya Kanani kugeuka ya motoni na wadanganyika wasiasi!

Pili ni ajabu waheshimiwa kukesha wakiwanga wakisaka kura za kula. Freddie sumaiye na Dk. Haribu Bilhali mpo?

Tatu ni ajabu kijana wa fomu wani kuwa na akili na busara kuliko Luwasha kiasi cha kumtwanga swali akashindwa kulifuta. Siyo chuku yalitokea Ukara.

Ni ajabu ya pekee mkuu kupendekeza kuunda kamati ya kushughulikia madini wakati Buzwagi zilishahitimisha zoezi.

Je, ni sanaa mpya ya kutia moyo na kukwepa ili kufunika madai ya sasa? Silaha upo? Je utaukwaa huo mkenge kama wadanganyika? Mie simo! Nakushauri umbane kwanza awawajibishe wanaosababisha kuhitajika “marekebisho” haya. Wapo. Kuna Chwenge Anderea na Niziro Kadamage.

Ajabu jingine ni mkuu kutovunja baraza zigo la mawaziri. Kisa? Linachapa mzigo sana . Limefanikiwa kuvuka hata malengo kwa kuwa na kashfa lukuki ndani ya kipindi kifupi.

Ajabu la maajabu ni mkuu kuendelea na ziara ughaibuni. Alituvunga kwa kupunguza kidogo. Sasa ameanza kwa kasi mpya na staili mpya ya kufungua mikutano ya kimataifa! Lakini pesa inayopotea si ni ile ile?

Huu ni wakati wa maajabu jabu jabu! Ajabu jingine? Mkuu kufunga ndoa na wafanyibiashara. Ndoa hii ilifungwa mjini Nyunyoko kwa rais Joji Pori Kichaka.

Usichoke. Maajabu yanaendelea. Kaya kugeuka Tierra del Fuego au nchi ya mioto. Tandahimba wanyonywaji walichoma hekalu la mbaya wao. Bi’mulo kituo cha usalama hakikuwa salama. Kilitiwa nari! Mwe! Amani ipo hapa kweli? Je huu siyo mwamko mpya kwa kasi mpya na zari mpya?

Moto ukitesa, chinga waliamua kuuongezea kinono kwa kuchoma beramu ya nambari wani Iringa! Kipute hiki kikiendelea, wazomewa ndiyo usiseme huko madongo poromoka! Mmoja alizidiwa na hasira hadi akaitungua kopta kwa jiwe si RPG! Huyu akipata bomu, atakuwa mwanachama safi wa mradi wangu hapa chini. Ajabu la mwisho? Kukua uchumi kwa takwimu za kupika! Haya we! Uchumi umekuwa wakati shida zikikua, bei ndiyo usiseme? Bado ufisadi.

Ngoja niende kupata kwanza. Baada ya kuutwika, nakurubia home. Uchache nimeunguza. Ngoja niimbe kumsifia mama Kidume kumlainisha.

Nembogha eee X2
Nembogha ee Nembogha nitakufa.

Nitakufa aaa nitakufa mama,
Nitakufa nitakufa nitakufa bila wewe.

Danganyika aaaX2
Danganyika aa Danganyika nitakufaaa,
Danganyika nitakufa nitakufa kukulinda.

Nitaua eee X2
Wee! Stupid bastard we! Koma hujui huo uchochezi
kutishia walaji waliobarikiwa?

Kama mbaya mbaya. Mweleka! Jasho linabubujika ka’ maji!

Najisemea: Boha la leo si bomba, kajaza maji mama Sheki. Ngoja nimpake. We mama Shekimweli, hujui nina mpango wa kuanzisha kundi la Al-Kayada (kirefu Al. Kayadanganyika), kuwalipua wanaowadhulumu wenzao! Jina langu ni Musama bin Laban. Upo hapo?

Nakwenda chini tena!

Najikusanya na kupiga mbinja na kuendelea: Baada ya kuona kuwa kuanzisha dini ni utapeli tena wa kumchezea mzee mwenyewe huko juu, sasa nalianzisha potelea kote.

Naanzisha kupambana na magaidi wa kiuchumi na kisiasa.

Gaidi Joji Pori Kichaka hatahangaika nami. Sipiganii mafuta na dini. Kichaa changu ni Kaya yangu Danganyika.

Sitahubiri ufufuko wa wokovu. Nitahubiri kifo. Ukifa ukipigania Danganyika: peponi moja dairekti. Utapata utajiri kama Magabacholi na kufaidi ngo… we koma!

Naona kama mshirika yupo dirishani. Ngoja nimpambe.

Naanza kuimba.

Nembogha weeX2
Shetani na mbuyu nami na wewe.

Kama akina nanihino wa kule Idodompya,
Mimi na Nembogha.

Lisirikali na Magabacholi,
Mpayu na Nembogha. Ninihiiii nonohoo!

Nikimfunga kamba haninyimi kitu. Chajio, chausiku na hata ngo…. We stoooopu! Hapo hapo; don’t cross the line. Nikipasha umombo unapaa kichizi!

Nimekumbuka. Siri ya magabacholi kutajirika na wasionekane kwenye madudu ya akina Richmondu, Deep Green, Tangold ni nini? Je hawaparuri? Mzigo mzito mtwishe Mnyamwezi?

Mbona walihonga wakaingia kijiwe cha uheshimiwa wakati siasa yao ni pesa siyo chama wala nchi?

Nani anamdanganya nani? Juzi walitaka kuniitia polisi wanibambike kesi. Nitawakomesha. Nikianza mchezo wa kujial-qaida watanishitaki kwa nani?

Sitanii nitakufa na watu. Kuzomea cha mtoto shurti nifanye kweli kieleweke.

Ngonja niimbe. Pwaa chini!

Hakuna Mungu kama wewe Mfumo eee eeeX2
No nimelewa sistahili kumtukuza Mungu kama wale jamaa wa majoho wanaomtia midole machoni kuhubiri maji wakanywa mvinyo.

Hakuna mwizi kama wewe Kwekwe aaaa
Hakuna mwizi kama washa aaa aaa
Unakomba aaa.

Hii sasa siasa. Nimeachana na siasa na kuanzisha ugaidi mtakatifu. Najua vimbelembele watanilaani kuwa nahatarisha amani ya Kaya. Kuna amani hapa iwapo tunageuza mafala mchana kweupe? Mijitu inakwiba njuluku zetu inakuja kutunafiki itatupeleka kwenye maulaji! Ulaji gani: mnakula bila kunawa mkinya humo humo kama mainzi?

Mandhani sisi ni kama wale fisi mnaowatupia uchafu wenu wawasaliti wenzao? Hatuna roho ya mbweha bwana.

Hatuna roho mtakakitu wala mtenda chafu kama nyinyi.

Hata kama ni walevi tuna roho mtakatifu wa kuikomboa kaya.

Naona hilo nalo na kitambi mimba chake linanishangaa badala ya kujishangaa na kujisikitikia! Kuna nini humo tumboni kama si rushwa?

Ngoja nilisogelee nilipashe. Wewe nakujua. Baba yako alikuwa kibaka na babu yako muwindaji wa ndezi. Leo una mijumba na mgari wako mkubwa! Ngoja nitakula nanyi kia-Al-qaida Al-qaida ndiyo kieleweke. Ngoja niengoee kwa kimombo kuonyesha namaanisha siriyasi. My main and only target is the Gang of Self-serving Goons (GSG).

Unapandisha vioo: mie mvua! Mnaogopa hata mvua ya maneno mbwa nyie! Ku.. ndigisi, kumbaff na wenzako.

Eti linajiita mwanaume! Ungekuwa mwanaume ungewekwa kinyumba na waliokuhonga cheo? Mngekuwa wanaume mngetetemeshwa na washitiri wanaowatumia kama nepi? Linajiita heshimiwa! Heshimiwa au laaniwa! Mbona linaishi kwa haramu kama shimo la choo?

Lione. Ngoja nikupayukie hata kama umefunga vioo. Nyinyi na mfalme wenu wote hovyo kabisa. Mnawaibia wana kaya halafu mnajichekesha chekesha! Ala! Pambaff.

Nyie sawa na mbwa wa kizungu. Nawalisha kwa jasho langu. Ni sawa na mbu. Nawalisha kwa damu yangu.

Ohoo! Ngoja……

No comments: